Inasemekana matajiri wengi wakubwa wa level ya Forbes akiwemo Bill Gates na watu mbalimbali mashuhuri duniani walihudhuria.
Kwa mujibu wa mtangazaji wa runinga nchini Kenya, ndugu Jeff Koinange, anasema hata mzee wetu kipenzi Rais mstaafu wa Tanzania mzee Jakaya Kikwete alihudhuria.
Picha kwa msaada wa mtandao wa Instagram.
--------
TAARIFA ZAIDI..
Sherehe ya kifahari ya binti wa Bilionea namba moja Afrika, Aliko Dangote aitwaye Fatima Dangote, yazua gumzo nchini humo kutokana na kuhudhuriwa na watu mashuhuri kutoka sehemu mbalimbali duniani akiwemo Bilionea kutoka Marekani, Bill Gates.
Naye Rais Mstaafu wa Tanzania, Jakaya Kikwete alikuwa ni miongoni mwa wageni wa heshima waliohudhuria katika sherehe hiyo ya kihistoria.
Wengine walioudhuria ni pamoja na mke wa Rais wa sasa wa Nigeria, Hajiya Aisha Buhari; Makamu wa Rais, Osinbanjo; Spika wa Bunge, Magavana na Watu wengine mashuhuri wakiwemo wasanii na wafanyabiashara wakubwa.
Davido na Wizkid waliangusha show moja kali sana mpaka mzee Dangote mwenyewe ikambidi ayarudi magoma.
Tafrija hiyo ya mapokezi baada ya ndoa (reception party) kati ya Fatima na mumewe ambaye ni mtoto wa Mkuu wa Jeshi la Polisi mstaafu, Jamilu Abubakar, ilifanyika jana Ijumaa katika Jiji la Lagos.
View attachment 724020View attachment 724021View attachment 724022View attachment 724080