Hasara itokee isitokee mambo aliyofanya Magufuli hata vipofu wameyaona

Acha upotoshaji mkuu,kwa uchache tu hiyo miradi ya interchange za Ubungo na TAZARA ilianzishwa uongozi wa awamu ya 4 nikimaanisha kuanzia kutafuta wahisani hadi kuwekwa jiwe la msingi n.k.
 

Huko mtaani hata hotuba za kina Hitler ukiuza zitanunuliwa. Hizo za Magu za watu kutokujana na mavi mjini tutaachaje kununua kukumbuka kejeli zake?
 
Usingekuwa na jina la kiume kwenye username yako, ningedhani wewe ni Hadija Koppa, Malkia wa Mipasho! Bara na Visiwani.
 
Mungu alituletea muuaji, mtekaji, mtesaji, ?
Kama Mungu alimleta shetani atashindwa kumleta Magu? Grow up, ni mtawala gani katika ulimwengu huu hajawahi ua na kutesa watu?

Pamoja na madudu yake yote huyu mwamba alithubutu kiasi chake kwenye baadhi ya mambo.
 
Hitler aliijenga sana Ujerumani kaburu akaijenga South Afrika, wakoloni waliijenga sana Tanzania ila wako wapi marehemu ni Hitler mixer kaburu mixer mkoloni.
 
Ukumbuke wakoloni walijenga

Maendeleo ni watu sio vitu

Yani mradi wake wa maana huo mmoja, na ni hasara kwenda mbele ndio unataka kutuambia nini?
 
kama mungu alimleta shetani atashindwa kumleta magu? grow up, ni mtawala gani katika ulimwengu huu hajawahi ua na kutesa watu?

pamoja na madudu yake yote huyu mwamba alithubutu kiasi chake kwenye baadhi ya mambo.
Mwamba alithubutu kwa ukatili wa hali ya juu
 
kama mungu alimleta shetani atashindwa kumleta magu? grow up, ni mtawala gani katika ulimwengu huu hajawahi ua na kutesa watu?

pamoja na madudu yake yote huyu mwamba alithubutu kiasi chake kwenye baadhi ya mambo.
Alithubutu mambo gani
 
kama mungu alimleta shetani atashindwa kumleta magu? grow up, ni mtawala gani katika ulimwengu huu hajawahi ua na kutesa watu?

pamoja na madudu yake yote huyu mwamba alithubutu kiasi chake kwenye baadhi ya mambo.
Hah hah haa. Utawala dhalimu kamwe hauwezi kutoka kwa Mungu.
Shetani ni mungu wa dunia hii, naye pia hugawa vyeo na mamlaka na utajiri na fahari za dunia. Nakushauri tu uache dharau na kuwaambia wenzako "grow up"
 
Samahani kama umekwazika kwa kauli hiyo bt muda ni mwalimu mzuri utatufunza kitu soon.
 
Afazali hapa mtaani kwangu Vijiwe vya Kahawa vimeanza kumuongelea waziwazi hakuna uoga tena

Tena ndio wameanza na Fisango word kuhusu Hayati, confidence imeanza kurudi kitaale hahaha
Hata Kahawa sasa inashuka muruwaa kabisa bila ya kuogopa

Asante Mama

Trust me Watanzania hatujaumbwa kutawaliwa na Dikteta

Kama CCM unataka kutusimkia Dikteta, kwanza iwaingize Warundi hadi watuzidi kwa uwingi ndio isimike Dikteta,sisi haiko kwenye DNA yetu unasikia Polepole ?
 
MATAGA ndio mmeamua hivyo
 
Hata hivyo hakufanya maendeleo kwa ajili ya wanaoona.

Hii ndio sababu waonao wasubiri wamtakae yu aja wampokee kwa shamrashamra.
 
Hakuna jambo gumu kuficha kama UKWELI.

Hata ufanyaje, kuna wakati ukweli utakuwa wazi tu.

Vinapita hata vizazi kisha ukweli unajulikana. Kama mtu ni mwovu wakati wake utafika, hata serikali yote na nchi ikaamua kumpamba ila wakati utafika ukweli utajulikana.

Kama ni mwema hata akichafuliwa vipi wakati utafika UKWELI utashinda.
 
Kaka mbona hasira hivyo? Hiki ni kipindi cha Kwaresma!!
 
Nilichojifunza ukiwa madarakani hata ufanye nn ila ukifanya kosa la kuminya uhuru wa watu kukosoa na kupata uhuru wa habari basi siku utakapotoka madarakani legacy yko inaweza zidiwa na maneno ya watu waliokuwa wakishindwa kukosoa wakati upo hai...mzee kazikwa juzi tu ila maneno yaukosoaji ni mengi mno hata angali ajaoza...JK na mwinyi waliacha uhuru wa kukosolewa na habari, walipostafu watu hawakuwa na mengi yakukosoa maana vifua vilikuwa vyepesi madudu yte watu waliyakosoa wakati wakiwa madarakani sahvi wamestafu kwa amani
 
Haina upinzani hii mkuu
John Pombe Joseph Magufuli amefanya mengi makubwa, na sio rahisi kumfuta kwenye historia ya nchi hii kwa kuyatangaza mabaya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…