Hasara ya kuvunja mikataba ni baada ya kupuuzwa ushauri wa Tundu Lissu

Hasara ya kuvunja mikataba ni baada ya kupuuzwa ushauri wa Tundu Lissu

Sina mashaka na uzalendo wa Tundu Lissu kwa Taifa. Kinachomponza ni kuwaambia watu tusikombe mboga ili tushibe wote. Kuna watu hawataki kuambiwa usikombe mboga, wanachofurahia ni wao wakombe peke Yao wengine mle ugali kwa kuchovya tongue au mle bilà mboga kabisa.
Ukweli mtupu.

Tundu Lissu ni mzalendo kweli kweli
 
Kwa hili la mikataba kuna aspect ya ukweli , hata hao wazungu wenyewe wanatushangaa , inafika sehemu mtu anaingia makubaliano ya hovyo kisa tu anapata vijisenti yeye na familia yake anasahau kwamba kuna watu wengine zaidi yake na familia yake .Kwa ufupi suala na mamikataba na makubaliano ya hovyo kama tungekubaliana wote kama taifa kuyafumua na kuanza upya tungekua mbali sana
Nchii hii mambo ni shaghala nagala.
 
Sina mashaka na uzalendo wa Tundu Lissu kwa Taifa. Kinachomponza ni kuwaambia watu tusikombe mboga ili tushibe wote. Kuna watu hawataki kuambiwa usikombe mboga, wanachofurahia ni wao wakombe peke Yao wengine mle ugali kwa kuchovya tongue au mle bilà mboga kabisa.

Tundu Lissu aliwaonya watu kuhusu ubaya wa kuvunja mikataba bila kufuata Sheria za kuvunja mkataba uliofungwa kisheria. Lakini aliambuli kile alichokiambulia. Sasa tunaambiwa taifa limeingia hasara inayotugharimu sisi wote na akiwemo Tundu Lissu.

Nashauri deni hilo lilipwe na waliohusika kuvunja mkataba wa symbion na mikataba mingine iliyovunjwa kwa njia hizo kama wenyewe watashinda kesi. Tushikilie Mali zao popote zilipo ndani na nje ya Nchi na kuzipiga mnada kulipia gharama hizo, na deni litakalobaki basi ndio sisi wote kwa shingo upande kabisa tulilipe.

Hii ni kuonyesha kuwa CCM imeshimdwa kuisimamia serikali yake, wajitafakari.

Tuliambiwa hakuna watumishi hewa mbona CAG amesema wapo wengi TU? Tulidanganywa? Kuna watumishi hawakupandishwa vyeo Wala kuongezewa mishahara Yao kwa kisingizio kuwa wanashughulika na watumishi hewa kwanza, mbona wapo?

Kwa hiyo ruksa kuingia mikataba mibovu huko mbeleni tukiogopa kuivunja kwa kuhofia hasara? Ungekuwa na rational thinking ungesema waliosababisha kuingia mikataba mibovu wawajibishwe kabla ya waliovunja q
 
Kaka CCM inatawala nchi hii ki magumashi.

Hayo madeni yote watayalipa watoto na wajukuu zetu hatuna namna na kibaya zaidi ukiwakosoa kama lissu alivyokuwa anafanya wao wanasema wewe si mzalendo umetumwa na mabeberu - kwao mzalendo ni yule anayekubali kuyala matango pori bila kuyamenya.

Ni kweli Lissu alikuwa sahihi na bado yupo sahihi.
 
Kwa hiyo ruksa kuingia mikataba mibovu huko mbeleni tukiogopa kuivunja kwa kuhofia hasara? Ungekuwa na rational thinking ungesema waliosababisha kuingia mikataba mibovu wawajibishwe kabla ya waliovunja q
Kuingia na kutoka kwenye mkataba kuna taratibu zake, aliyekosea kuingia na kutoka kwenye mikataba wote wana makosa. Chaajabu kwenye taifa hili la CCM kwa miaka 60 watu wote hawa wako salama usalimini, wenye hatia na wanaostahili kunyongwa hadi kufa ni akina Lissu ambao wanaosema tulikosea kuingia na tunakosea kutoka kwenye mikataba hii. Akina Lissu walipiga kelele sana bungeni wakati wa kuingia na walipiga kelele sana wakati wa kuivunja lakini walionekana wanatumiwa na mabeberu. Mnyonge mnyongeni lakini iko siku kilio chake kitaturudia watanzania wote. Lissu anapigwa risasi kwaajili ya watanzania lakini lakini watanzania hawaithamini damu ya Lissu iliyomwagika, wanaendelea na kazi zao kama kawaida as if nothing happened, iko siku tutailipa wote damu yake kwa gharama kubwa sana.
 
Hapo ndipo mnakwama watu wa sampuli yako.Ushauri ulitolewa.Na ikawa hiyari kuupokea au kuukataa kama ulivyokaza mishipa ya kiuno.Muwe mnasikiliza maneno tu na kama mtu "unajidai" humpendi kausha.
HALAFU:
Ukiona mtu anapenda sana kuuongelea ushoga bila shuruti ujue ni muhanga wa kubakwa kuanzia utotoni.Kumbukumbu za kimaandishi ndivyo zinavyoonesha.
Umemlipua asante sana,huyo kweli ni shoga ndiyo maana anamsingizia Lissu kisa yuko Ubelgiji.
 
Sina mashaka na uzalendo wa Tundu Lissu kwa Taifa. Kinachomponza ni kuwaambia watu tusikombe mboga ili tushibe wote. Kuna watu hawataki kuambiwa usikombe mboga, wanachofurahia ni wao wakombe peke Yao wengine mle ugali kwa kuchovya tongue au mle bilà mboga kabisa.

Tundu Lissu aliwaonya watu kuhusu ubaya wa kuvunja mikataba bila kufuata Sheria za kuvunja mkataba uliofungwa kisheria. Lakini aliambuli kile alichokiambulia. Sasa tunaambiwa taifa limeingia hasara inayotugharimu sisi wote na akiwemo Tundu Lissu.

Nashauri deni hilo lilipwe na waliohusika kuvunja mkataba wa symbion na mikataba mingine iliyovunjwa kwa njia hizo kama wenyewe watashinda kesi. Tushikilie Mali zao popote zilipo ndani na nje ya Nchi na kuzipiga mnada kulipia gharama hizo, na deni litakalobaki basi ndio sisi wote kwa shingo upande kabisa tulilipe.

Hii ni kuonyesha kuwa CCM imeshimdwa kuisimamia serikali yake, wajitafakari.

Tuliambiwa hakuna watumishi hewa mbona CAG amesema wapo wengi TU? Tulidanganywa? Kuna watumishi hawakupandishwa vyeo Wala kuongezewa mishahara Yao kwa kisingizio kuwa wanashughulika na watumishi hewa kwanza, mbona wapo?
Tundu Lissu ukimpuuza utaumia mwenyewe.

Mifano tunayo
 
Ndio maana mimi namshauri mama mama mama yetu Samia Rais wa JMT kuwa haya mamiradi uliyoachiwa na mwendazake achana nayo kabisa au yafanyie modification kubwa sana, badala yake jielekeze kwenye miradi inayogusa watu wengi sana kama vile kupeleka maji, umeme, zahanati, shule, barabara vijijini kote. Ukipeleka maji ambapo hakukua na maji tangu wakati wa mkoloni hadi uhuru utakumbukwa milele na watu wote kuliko ukimalizia ujenzi reli mpaka uganda, rwanda, kongo na burundi. Mradi wa reli jenga tu hadi Tabora baaasi na kutengeneza bandari kavu pale ili watu wa mwanza, uganda, rwanda, burundi, congo, musoma, na kagera waje Tabora kufuata mizigo yao ili uokoe fedha za kuboresha maisha ya watanzania wote. Anaekuja ataendelea na ujenzi kama ni muhimu. Mwandazake ametuachia balaa kubwa ambalo tutangaika nalo kwa zaidi ya miaka 50 ijayo.

Sasa hivi taifa haliambiwi ni mkakati gani ulioko wa kupunguza adhali za kupanda kwa bei ya mafuta kwa kutumia natural gas yetu tuliyonayo nchini. Mfano, nilitamani kusikia kuwa kuanzia mwezi Mei mabasi yote ya DART na serikali yatatumia gas yetu badala ya petrol/dizeli.
Hadi hapa ushajionesha upo kwenye chuki fulani, ni mwendo uleule wa kumkashifu aliyetangulia. Post kuu uozo wote ulifanyika awamu ya nne hasa hiyo Symbion, ila sasa unahusisha awamu ya tano.

Yaani mtu keshapumzika ila bado anawasumbua akili zenu, mnahangaika kuzima legacy yake. Hii nguvu kubwa mnayotumia ndiyo mnajulisha watu nyinyi ndiyo wenye tatizo
 
Hadi hapa ushajionesha upo kwenye chuki fulani, ni mwendo uleule wa kumkashifu aliyetangulia. Post kuu uozo wote ulifanyika awamu ya nne hasa hiyo Symbion, ila sasa unahusisha awamu ya tano.

Yaani mtu keshapumzika ila bado anawasumbua akili zenu, mnahangaika kuzima legacy yake. Hii nguvu kubwa mnayotumia ndiyo mnajulisha watu nyinyi ndiyo wenye tatizo
Hajapumzika la hasha,bado yuko kuzimu anajutia mateso aliyokuwa akiwafanyia Watanzania wasio na hatia.
 
Back
Top Bottom