Hasira za Gen Z ya Kenya; Chanzo Chake ni Umaskini Uliotopea

Hasira za Gen Z ya Kenya; Chanzo Chake ni Umaskini Uliotopea

Slums ipo kwenye majiji yote makubwa yenye population density kubwa kama Nigeria ipo Makoko Slum pia Johannesburg slums ipo pia. Lakini maisha ya watu wanaoishi kule yana nafuu kuliko wanaoishi Manzese, Mbagala na kwingineko. Mathare kule wapo wasomi wengi tuu.
Hivi Manzese na Mbagala unazionaje? Zile siyo slums kama za Nairobi
 
Kenya mpaka uwe na hali ya ahueni aisee lazima umepigika mno, Kenya kukuta vijana ni matajiri au viongozi wa ngazi za juu serikalini au kwenye organizations ni ngumu sana, Tanzania ukienda maeneo ya Iringa kule matajiri wengi sana ni vijana wadogo from early 20s wamepata pesa kwenye miti, avocado's etc

Ukienda kanda ya ziwa vijana wengi sana ni matajiri wamepata pesa kwenye madini, uvuvi, wtc

Ukienda kaskazini utakutana na vijana wengi wanamiliki expedition companies na tour operators wametajirika ni vijana wadogo yaani kila eneo Tanzania kuna fursa ya mtu yeyote kufamikiwa tofauti na monopolised Kenya, waliofanikiwa ndio wataendelea kufanikiwa na maskini wanazidi kua fukara.
Naunga mkono hoja yako.
Angalau Tanzania kuna fursa kwa kada mbalimbali kutajirika tofauti na ilivyo Kenya.
Kenya ardhi yote imetwaliwa na watu wachache wenye uwezo, ni ngumu kwa jamii nyingine kupata chochote kupitia ardhi hiyo.
Tanzania ni jitihada zako ndizo zitakufanya uwe lofa milele au usogee hatua kadhaa mbele.
Kuna ardhi ipo ipo tu kuanzia Lindi mpaka Ruvuma, Itigi mpaka Tabora.
Kariua mpaka Uvinza.
Sikonge mpaka Mlele.
Hata kabla hatujafikiria kilichomo chini ya ardhi hiyo, kilimo tu kinaweza kubadilisha maisha ya watu wetu.
 
Usichukue slum kama kigezo tuu cha kutathmini umaskini, je Watanzania wengapi hapa Dar hawana hata pa kulala wanalala barabarani na kwenye vituo vya mabus.
Slam kwenye jiji kama Nairobi ni kielelezo cha kwanza kutambua umasikini wa nchi hiyo.
Nairobi au Dar ni kioo cha nchi.
Mji unapokuwa na makazi machafu wanayoishi masikini wa mji kama Kibera huwezi kukwepa ukweli wa umasikini wake.
Tuonyeshe eneo kama Kibera jijini Dar.

Suala la watu kulala vituo vya basi au sokoni ni hali ya kawaida kwenye miji mingi Duniani.
 
Naunga mkono hoja yako.
Angalau Tanzania kuna fursa kwa kada mbalimbali kutajirika tofauti na ilivyo Kenya.
Kenya ardhi yote imetwaliwa na watu wachache wenye uwezo, ni ngumu kwa jamii nyingine kupata chochote kupitia ardhi hiyo.
Tanzania ni jitihada zako ndizo zitakufanya uwe lofa milele au usogee hatua kadhaa mbele.
Kuna ardhi ipo ipo tu kuanzia Lindi mpaka Ruvuma, Itigi mpaka Tabora.
Kariua mpaka Uvinza.
Sikonge mpaka Mlele.
Hata kabla hatujafikiria kilichomo chini ya ardhi hiyo, kilimo tu kinaweza kubadilisha maisha ya watu wetu.
Wangapi wametajirika kupitia hizo fursa, mbona kila awamu watu wanarudi nyuma kua masikini acheni propaganda watanzania sie nimasikini wakutupwa gusa hizo aridhi kama utafungwa kwa kuvamia hifidhi za kiba za taifa........
 
Wangapi wametajirika kupitia hizo fursa, mbona kila awamu watu wanarudi nyuma kua masikini acheni propaganda watanzania sie nimasikini wakutupwa gusa hizo aridhi kama utafungwa kwa kuvamia hifidhi za kiba za taifa........
Nenda Njombe, Mafinga, Madibira, Makete, Wanging'ombe, Kapunga, ukaone vijana walivyowekeza kwenye kilimo cha parachichi, mpunga, Vitunguu nk.
Nenda Namtumbo, Madaba, Mbinga, Ukaone vijana wanavypiga pesa kwenye kilimo cha Nafaka kama Mahindi na Maharage.
Nenda Ifakara, Kisaki, Mbingu, Mang'ula, Mbigili nk ukajionee vijana waliojitoa wanavyopiga pesa kwenye kilimo cha mpunga.
Wewe kazi yako kuzurula na bahasha yako ya kaki mjini kutafuta ajira huwezi kuziona fursa hizo.
Endelea kulala, miaka 10 ijayo utaenda Njombe kuomba kazi kwa mkulima wa Parachichi
 
Naunga mkono hoja yako.
Angalau Tanzania kuna fursa kwa kada mbalimbali kutajirika tofauti na ilivyo Kenya.
Kenya ardhi yote imetwaliwa na watu wachache wenye uwezo, ni ngumu kwa jamii nyingine kupata chochote kupitia ardhi hiyo.
Tanzania ni jitihada zako ndizo zitakufanya uwe lofa milele au usogee hatua kadhaa mbele.
Kuna ardhi ipo ipo tu kuanzia Lindi mpaka Ruvuma, Itigi mpaka Tabora.
Kariua mpaka Uvinza.
Sikonge mpaka Mlele.
Hata kabla hatujafikiria kilichomo chini ya ardhi hiyo, kilimo tu kinaweza kubadilisha maisha ya watu wetu.
Umeliweka vizuri sana Mkuu. Watu wanasubiri kuwekewa hela mfukoni na Serikali. Hapo ndipo wanapotea
 
Kenya mpaka uwe na hali ya ahueni aisee lazima umepigika mno, Kenya kukuta vijana ni matajiri au viongozi wa ngazi za juu serikalini au kwenye organizations ni ngumu sana, Tanzania ukienda maeneo ya Iringa kule matajiri wengi sana ni vijana wadogo from early 20s wamepata pesa kwenye miti, avocado's etc

Ukienda kanda ya ziwa vijana wengi sana ni matajiri wamepata pesa kwenye madini, uvuvi, wtc

Ukienda kaskazini utakutana na vijana wengi wanamiliki expedition companies na tour operators wametajirika ni vijana wadogo yaani kila eneo Tanzania kuna fursa ya mtu yeyote kufamikiwa tofauti na monopolised Kenya, waliofanikiwa ndio wataendelea kufanikiwa na maskini wanazidi kua fukara.
Hii ni kweli , Tz vijana wadogo wanapiga pesa kuliko huko kenya kumiliki ardhi ni ishu ....Kenya pesa ipo ila inatajirisha wanasiasa na wageni .
 
#Mama Samia mitano tena
Tanzania maisha ni mazuri sana
Wengi wanaona Watanzania ni legelege au hawatambui haki zao ndiyo maana hawachukui hatua dhidi ya maamuzi ya wanasiasa. Wanatamani vijana wetu wangekuwa kama vijana wa Gen Z wa Kenya ambao kwa siku mbili wameteketeza mali zenye thamani ya mamilioni kwa hasira za financial bill 2024.

Matajiri wanne nchini Kenya, utajiri wao unazidi karibu nusu ya wakenya wote(40%) wakichanganywa kwa pamoja. Matajiri hao wana utajiri unaofikia Ksh. bilioni 333( Tsh. trilioni 6.26).

Utafiti unaonesha ukuaji wa tofauti kati ya walio nacho na wasio nacho ambapo wakenya 130 matajiri zaidi wanamiliki mali sawa na 70% bajeti ya Kenya kwa mwaka. Matajiri watano zaidi nchini Kenya ni Merali, Shah, Bedi, Kenyatta na Mahendra wakiwa na utajiri wa jumla ya dola za kimarekani 3.2.
View attachment 3027359

Baada ya hapo ongeza na Manu Chandaria, Moi family, William Ruto & Associates

Wakenya wengi wanaishi chini ya dolla moja, pesa yao kuipata ni kazi. Karibu na Nairobi CBD kuna makazi ya slums 3 Kibera, Mathare na Makuru kwa Njenga ambazo zinaishi watu zaidi 2.5 Milioni.

View attachment 3027353
Umaskini huu na tofauti ya kipato ndiyo unatia hasira kwa vijana mpaka hawafikiri mara 2 whether wachome bunge au magari ya Seikali.
View attachment 3027354
 
Umeliweka vizuri sana Mkuu. Watu wanasubiri kuwekewa hela mfukoni na Serikali. Hapo ndipo wanapotea
Wanaota ndoto, hakuna serikali itakuwekea pesa mfukoni kirahisi hivyo
Serikali inawezesha vijana wenye nia na malengo ya kuzalisha Mali.
Mwaka jana serikali kupitia Wizara ya Kilimo imetoa fungu la pesa kwa vijana furani wa Makete ili walime ngano.
Hivi sasa vijana wapo kazini wanazalisha.
Hawa wengine wanataka kwanza waone shamba, trekta, nyumba nzuri na wapewe pesa mkononi ndiyo waende shamba.
Watasubiri sana.
 
Kama ni umasikini Tanzania ndo ingekua ya kwanza kuandamana, wewe angalia wadamanaji vijana wameva vizuri hata kupita waalimu wa Tanzania,
Hapana mkuu umasikini unakwenda mbali zaidi.

Wewe unafikiri maandamano ya CDM au vijana wa chuo kuna mtu huwa amevaa matambala ya deki??

Ukitafiti ni wasomi wangapi kila mwaka wanazaliwa kenya bila tumaini la maisha bora ndio ungejua kwanini juzi kiliwaka,tz bado bado wengi tuna katumaini dhaifu kamebakia.
Tunaendelea kuchochea kuni tutafika tu sehemu ambayo mtu akiongeza bei ya sukari kwa shiliki 100,moto unawaka,kwa saa hizi bado.
 
Back
Top Bottom