The Phylosopher
JF-Expert Member
- Mar 11, 2015
- 1,968
- 2,957
Ukweli ni kwamba hali ya kisiasa ya sasa hapa nchini inakatisha tamaa sana.
Ukisoma maandiko mengi humu ndani ya wenye mrengo wa upinzani, wanailaumu ccm kuwadhoofisha huku wakisahau kwamba hakuna chama siasa chenye jukumu la kuruhusu chama pinzani kisitawi.
Ukiwa kama mpinzani unalazimika kutumia njia yoyote kuhakikisha chama chako kinavutia raia wa kawaida Kwa wingi, kikishaungwa mkono kiwango hicho hata mkiibiwa kura hao watu hawatakubali.
Hali tuliyonayo Kwa sasa hapa nchini tuna wapinzani dhaifu sana wanaonunulika wabinafsi wababe na wengi wao wako pale Kwa maslahi yao binafsi.
Katika mazingira ya namna hii hakuna mwamko mkubwa sana huku mtaani unaoleta kashkash kama za mwaka 2010 ambapo hata ccm wenyewe walikuwa wamejikatia tamaa.
Kwa sasa taifa linazungumzia kupanda Kwa gharama za maisha, ila wapinzani wamekomaa na tume huru mara uchaguzi huru mara katiba mpya nk.
Katika muktadha kama huo akija kinana akasema tunduma njia nne Bashe akaja na mbolea nusu bei Samia akaja na elimu bure hadi form six nk itakuwa ngumu sana raia kukuelewa mpinzani kuwa unapambana Kwa Kwa niaba ya mwananchi wa kawaida.
Naomba wapinzani tubadili namna ya kufanya siasa tufanye siasa zenye ushawishi kwa watu ili tuungwe mkono na ccm istaafishwe siasa.
Ukisoma maandiko mengi humu ndani ya wenye mrengo wa upinzani, wanailaumu ccm kuwadhoofisha huku wakisahau kwamba hakuna chama siasa chenye jukumu la kuruhusu chama pinzani kisitawi.
Ukiwa kama mpinzani unalazimika kutumia njia yoyote kuhakikisha chama chako kinavutia raia wa kawaida Kwa wingi, kikishaungwa mkono kiwango hicho hata mkiibiwa kura hao watu hawatakubali.
Hali tuliyonayo Kwa sasa hapa nchini tuna wapinzani dhaifu sana wanaonunulika wabinafsi wababe na wengi wao wako pale Kwa maslahi yao binafsi.
Katika mazingira ya namna hii hakuna mwamko mkubwa sana huku mtaani unaoleta kashkash kama za mwaka 2010 ambapo hata ccm wenyewe walikuwa wamejikatia tamaa.
Kwa sasa taifa linazungumzia kupanda Kwa gharama za maisha, ila wapinzani wamekomaa na tume huru mara uchaguzi huru mara katiba mpya nk.
Katika muktadha kama huo akija kinana akasema tunduma njia nne Bashe akaja na mbolea nusu bei Samia akaja na elimu bure hadi form six nk itakuwa ngumu sana raia kukuelewa mpinzani kuwa unapambana Kwa Kwa niaba ya mwananchi wa kawaida.
Naomba wapinzani tubadili namna ya kufanya siasa tufanye siasa zenye ushawishi kwa watu ili tuungwe mkono na ccm istaafishwe siasa.