Darlin
JF-Expert Member
- Aug 9, 2020
- 4,796
- 10,646
Good morning future millionares 😀 😀Umewasahau wazee wa Qnet a.k.a GOOD MORNING
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Good morning future millionares 😀 😀Umewasahau wazee wa Qnet a.k.a GOOD MORNING
Pole sana brother. Kwakweli vijana wengi wa Forex ni matapeli, wengi wanaojinadi mjini kuwa na maisha mazuri sababu ya Forex sio kweli, wengi hupata hayo maisha mazuri kwa kutapeli watu! Hebu fikiria amekusanya hizo pesa zote ulizomtumia kutoka kwa watu wangapi? Maana roughly ni kama TZS 4.2M dah!Katika miaka ya hivi karibuni, biashara ya Forex imekuwa kivutio kikubwa kwa vijana wa Kitanzania wanaotafuta njia mbadala za kujiongezea kipato. Wakati Forex ni fursa halali kwa wale wenye uelewa na utaalamu wa masoko ya kifedha, inasikitisha kuona jinsi baadhi ya watu wameigeuza kuwa mtandao wa ulaghai, wakitumia ahadi za uongo kuwahadaa watu waliotayari kujitolea kila kitu kwa matumaini ya maisha bora.
Katika uchunguzi huu, tunamchunguza mtu anayejulikana kama Erick John (Instagram: pips_crusher), ambaye anatuhumiwa kwa kuwahadaa watu kwa kutumia biashara ya Forex, na kusababisha hasara kubwa kwa wahanga wake.
Mfumo wa Utapeli wa "PIPS_CRUSHER"
Kesi ya Erick ni mfano wa jinsi matapeli wa Forex wanavyofanya kazi. Mimi kama mhanga wa utapeli hau nimeona iwe ni darasa kwa wengine kwasababu mimi nimeshalipa hiyo gharama.
- Ununuzi wa Trading Bots au Expert Advisors (EA) Isiyofanya Kazi
Mnamo tarehe 11 Desemba 2024, nilinunua mfumo wa biashara ya kiotomatiki (EA) kwa gharama ya Shilingi milioni 3.5 za Kitanzania ili uweze kutrade wakati niko busy na shughuki zingine na pia kuhakikisha kama hizi trading bots zinazotangazwa sana hivi sasa zinafanya kazi kweli. Hii sio bot ya kwanza ninanunua - ni ya 4 hivyo nimekusanya taarifa za kutosha kuhusu ufanyaji kazi wa hizi trading bots ambazo huwa ni ghali sana. Sasa turudi kwa Erick anayejinadi na trading bot yake aliyoipa jina "PIPGHOST EA" Bei yake elekezi ni dola za kimarekani 1400 (sawa na 3,553,270 TZS kwa rate ya siku ya chapisho). Baada ya kulipia (risiti ipo hapa chini) nilipokea file kwenye email yangu na nikaunganisha na account yangu. Tulipigiana simu hadi video call mpaka nikaweza kuiset vizuri. Account yangu ilikuwa na mtaji wa dola za kimarekani 1000 (sawa na 2,538,050 TZS kwa rate ya siku ya chapisho). Niligundua kuwa bot iko slow sana kuchukua faida na mara nyingi kama sio zote trade iliishia njiani na kugeukia hasara ambayo kikomo (Stop Loss) iko mbali. Nafurahi kuwa alithibitisha baadaye kuwa mfumo huo haukuwa ukifanya kazi kama alivyoahidi. Hivyo akaahidi kuleta toleo jipya Januari 2025.
![]()
- Kulipia Huduma ya VPS Isiyokidhi Viwango
Katika siku hiyo hiyo, nililipa Dola za Marekani 125 kwa huduma ya VPS moja kwa moja kwake, ambayo ilisemekana ingeendelea kwa miezi miwili. Hii imechangiwa na mimi mwenyewe kutokujua wapi pa kuipata VPS sahihi. Hivyo tuseme nimelipa gharama ya kutokuwa na hiyo taarifa kwasababu sidhani kama VPS inafika bei hiyo kwa miezi 2 tu. Hata hivyo, sikuweza kuendelea kutumia huduma baada ya siku kumi, huku maombi ya msaada kutoka kwa Erick yakipuuzwa.
![]()
- Ulaghai wa Huduma ya "Account Management"
Baada ya kutoa malalamiko yangu alishauri kuwa nilipie huduma yake ya kusimamia akaunti yangu ili kurudisha hizo hasara. Bei za huduma hiyo nimeweka hapo chini. Gharama ya kuhudumia akaunti ni kubwa mno hivyo nikamsihi nimpee ada baada ya kupata faida ila akatoa wazo tuweke fedha kwenye akaunti ya pamoja ili afanye biashara mpaka mwisho wa wiki ili niwe na fedha ya kulipia huduma wiki inayofuata. Mnamo tarehe 15 Januari 2025, nlituma Shilingi 795,000 kwa Erick kwa ajili ya uwekezaji katika akaunti ya faida ya pamoja. Erick aliahidi kunishirikisha maelezo ya akaunti na kuripoti faida kufikia tarehe 17 Januari. Ahadi hizo hazikutekelezwa, na mawasiliano yote yalikatwa.![]()
![]()
![]()
![]()
![]()
![]()
![]()
Njia Zinazotumiwa na Matapeli
Kama ilivyo kwa matapeli wengine wa Forex, Erick alitumia mbinu zifuatazo:
- Ahadi za Faida Kubwa na za Haraka: Matapeli huonyesha biashara ya Forex kama njia ya haraka ya kutajirika bila kuhitaji maarifa ya kina.
- Kuficha Habari Muhimu: Erick alificha taarifa muhimu, kama ukosefu wa ufanisi wa EA na VPS, hadi baada ya kupokea malipo.
- Kuzuia Mawasiliano: Ili kuepuka majibu, Erick aliwazuia wahanga wake kwenye mitandao ya kijamii na kutangaza habari kupitia akaunti nyingine ambazo hawakuziona.
Athari kwa Wahanga
Wahanga wa utapeli huu si tu wanapoteza fedha zao bali pia wanapoteza muda, matumaini, na imani yao kwa biashara halali kama Forex.
Wito kwa Vyombo vya Sheria na Jamii
Vitendo vya matapeli kama Erick vinapaswa kuchukuliwa kwa uzito. Tunatoa wito kwa:
- Vyombo vya Sheria: Kufuatilia matapeli hawa kwa kutumia ushahidi unaotolewa na wahanga.
- Jamii: Kuwaelimisha watu kuhusu mbinu za utapeli katika Forex ili waweze kuchukua tahadhari.
- Wahanga: Kupaza sauti na kushirikiana na vyombo vya sheria kufanikisha haki.
Zingatia
- Kaa mbali na mtu anayeahidi faida za haraka na zisizo za kawaida.
- Kumbuka hakuna anayeruhusiwa kufanya biashara ya uwekezaji bila ya kuwa na leseni.
- Hakikisha unapata taarifa zote muhimu kuhusu huduma au bidhaa kabla ya kufanya malipo.
- Uliza vyeti vya uthibitisho na historia ya mtu au kampuni anayejihusisha na biashara yoyote ya uwekezaji nchini kutoka CMSA.
Hitimisho
Ulaghai wa Forex ni tatizo linaloongezeka, na ni jukumu letu kama jamii kulinda watu wasio na hatia dhidi ya matapeli kama Erick. Kupitia uandishi huu, tunatumaini kuwa hatua za haraka zitachukuliwa dhidi yake na wengine wanaofanya vitendo vya aina hii.
Kama una ushahidi au unataka kushiriki hadithi yako, tafadhali wasiliana nasi kupitia barua pepe au simu. Sote tuna jukumu la kuhakikisha kuwa biashara inakuwa ya uwazi na halali.
Mmesahau LBL wakuu hhUmewasahau wazee wa Qnet a.k.a GOOD MORNING
Mkuu unaweza kunielekeza kidogo kuhusu spot trading nimejaribu kupitia youtube tuotorials ila bado sijapata uelewaPole sana brother. Kwakweli vijana wengi wa Forex ni matapeli, wengi wanaojinadi mjini kuwa na maisha mazuri sababu ya Forex sio kweli, wengi hupata hayo maisha mazuri kwa kutapeli watu! Hebu fikiria amekusanya hizo pesa zote ulizomtumia kutoka kwa watu wangapi? Maana roughly ni kama TZS 4.2M dah!
Mimi nimeshangaa kwasababu unaonekana upo ready kutake risks za kutumia bots tena kwa pesa mingi tu, na nimeona katika miamala yako umewithdraw USDT kutoka Binance. Sasa kama una elimu kuhusu USDT + any other digital currency si ni afadhali ukafanya copy trading ya futures au spot hapo hapo Binance tena for FREEEEE!!! Maana copy trading ya futures kwenye Binance hata kwa $500 tu ambayo haifiki hata TZS 1.5M ingekupa return nzuri weekly kuliko hata ahadi hewa za huyo jamaa.
Anyways bro, Mungu akusaidie upate namna ya kurecover angalau 50% ya ulichopoteza!
Mi siijui lakini pia siwezi ingia kitu nisichokijua, tamaa ndo inasababisha wengi wapigweNimegundua ni mgeni, hakuna mwana JF mwenye zaidi ya miaka miwili humu anaweza akajiingiza kwenye huo utapeli wa Ontario
Kwa muda gani na biashara ganiHio hela ungefungua biashara usingekosa faida ya laki
Spot trading ni rahisi sana, unachotakiwa kujifunza zaidi ni namna ya kufanya uchambuzi wa currencies ili kuwa na uelewa japo kidogo wa kujua kuwa sarafu fulani kwa ilipofikia ina dalili ya kupanda au kushuka na ndio ufanye maamuzi.Mkuu unaweza kunielekeza kidogo kuhusu spot trading nimejaribu kupitia youtube tuotorials ila bado sijapata uelewa
Nitakuja na thread yake pia. Ni mission yangu ilikuwa kutest kila mtu anaesemekana ni tapeli na nimefanikiwa sana 2024 kuchunguzaa kwa data.Kuna mshenzi mmoja anaitwa Ibrahim inano nae tapeli kama huyu tu
Kenge yule kasepa na hela yangu 2150$Nitakuja na thread yake pia. Ni mission yangu ilikuwa kutest kila mtu anaesemekana ni tapeli na nimefanikiwa sana 2024 kuchunguzaa kwa data.