Hatimae hukumu imetoka tayari, siku ya kwanza tu ya kesi kusikilizwa


Inasikitisha sana😭😥
 
Kuna hii comment, af kuna mmoja pia nasubiri ajibu... asipojibu nitamtafuta nimtag😅
Huwa natamani hawa kufahamu umri wao, na kama ni wakubwa natamani kufahamu kama wana watoto wa kike... kama una D2 utanielewa😂😂
Ebu mtag huyo
 
Ahahahah..kwakweli pale mwanzon hata mimi nilikua naona kabisa, nachizika. Ila namshukuru sana Mungu amenihurumia sana akanipa utulivu, ila niwe mkweli, nimelia lia sana kwenye hili sakata
Hili swala la kutengana mkiwa tayari mmezaa linaumiza mnoo. Mpk kufikia hatua yakutengana kabisa ni mengi magumu umeyapitia ya kuteseka sana.

Unaweza tembea njiani mwanaume machozi yanadondoka kwa utungu!

Maumivu yakutengana hayapoi wala kuisha ghafla itachukua miaka

Omba Mungu apoze maumivu Yako na akupe kusahau ya huyo mwanamke.

NILIPITIA HUMO, NAWAHURUMIA WANAOELEKEA KUPITIA HUMO

hichi kiumbe tulichopewa kina kasoro nyingi za kiufundi hasa kichwani
 
Mkuu kama ulivyoeleza kuwa haufahamu masuala ya kisheria sikulaumu hata kidogo.

Taratibu za kesi za ndoa/talaka zinaanzia Baraza la usuluhishi.wa ndoa ambap kunaeza kuwa Baraza la kata au Bodi chini ya taasisi ya kidini, huko mnachukua Fomu namba 3 tu.

Sasa hii Fomu namba tatu,inaelezea jambo moja tu kuwa barazalimejaribu kusuluhisha lakini limeshindwa. Baada ya hapo ndio mnaenda sasa Mahakamani moja kwa moja sasa hii maana yake ni kuwa Mahakamani hamtakuwa na habari ya usuluhishi tena bali ni kesi moja kwa moja yaani ni kutoa ushahidi na kupokea utetezi.

Sasa tukirudi kwenu, utaona mmeenda mkaanza usuluhishi tena Mahakamani, na ukiangalia Mahakama imegeuka kama sehemu ya nyie Wadaawa adala ya kuwa kimya ipokee ushahidi na utetezi wa Mdai na Mdaiwa.

Hapo ndio shida imeanzia na kuivuruga kabisa kesi nzima. Na hili lote naelekeza lawama kwa Mh. Hakimu husika sababu amefanya asiyotakiwa kufanya na kafikia hitimisho bila kupokea ushahidi rasmi na utetezi rasmi.

Yaani kaendesha hiyo kesi kama mpo ofisi ya kijiji 😂. Bado tuna safari ndefu sana kwenye huu mhimili.

Si umeona hata wewe umeamini kuwa utaratibu wa kushuhulikia kesi ya mgogoro wa ndoa unaanzia sijui dawati la jinsia na hizo ngazi zingine ulizozitaja hapo juu. Hii sio kweli na huo sio utaratibu uliowekwa na sheria. (Bado sikulaumu sababu haukua unafahamu hili)

Utaratibu wa kufungua kesi ya mgogoro wa ndoa/talaka ni hatua mbili tu;

1. Baraza la Usuluhishi wa ndoa Kata au Bodi ya usuluhshi wa ndoa chini ya taasisi za kidini
2. Mahakama.

Hizo njia nyingine zote hazipo kisheria na hazitambuliwi na sheria zinazosimamia masuala ya ndoa.
 
SAwa sawa..
 
ya nini bana!
Hakuna mshtaki huyo Hakimu Mfawidhi ajisomee tu hiyo kama case study, kuna watu Mali sio miongoni mwa vitu vya kujeruhi nafsi.
Mi nimemwelewa mno!
Ni ngumu kuelewa ninachokizungumzia Mkuu, lakini hili linaweza kusababisha huyu Mkuu akapoteza muda mwingi zaidi Mahakamani na pia haya mambo hayaishii kwenye hili la talaka tu, kuna kuja kufariki pia

Sasa hapo ndipo mambo yanaanza kuvurugika zaidi, fikiria baada ya kifo cha mmoja wao mwenzake anajitokeza na kuanza kudai sehemu ya mirathi, ngoma inaanza kivingine

Haya mambo yakivurugwa huwa sio poa.
 
Hataki haki yoyote hata kama anastahili.
Mbona rahisi tuu.
Mi nilikataa mpk haki zangu na sina lolote limenikuta.

Yani mtu atanilazimisha nikagombee mali?
We hujui hivi vinavyokera kiasi mtu anasena sitaki lolote chukua mpk hili shati nimevaa.

Hakuna lolote litamsumbua.
Kwanza hata talaka yenyewe unawaachia mahakamani utachukua hata baada ya miaka 6.

Yanini kwanza unless anataka kwenda kuoa.

Hamjui nyie hii stage.
 
Nakazia hapo uliposema asije msamehe huyo mtu, awamu ya pili atakufa yeye kwa stress au hata kwa hila.
 
Mimi nilitengenezewa criminal pia.

'"LIFE THREATS "
niliumia kwa kiwango kila nikikumbuka hili shtaka naishiwa mpk nguvu ya Co parenting.

Nasema kila mmoja alee tu wanae itakqvyofaa.
Baada ya kusoma hii comment , sasa ndio nimeelewa point ya msingi ya brother mrangi , aisee usemacho ni kweli. Ni vile tu huu uzi sijataka kueleza kila kitu lakini jayo uliosema yamenipata na ndio wife kwa kushirikiana na polisi wakanitia lockup.
YF alinifungulia mashtaka yafuataya sambamba na hili:

  • kesi ya shambulio (criminal)
  • namtishia uhai wake kuwa nataka kumuua (life threat) na akatumia loophole hii kubeba watoto na kuhamisha vitu ndani baada ya mimi kutowa ndani
  • kesi ya kimtandao kwamba natiashia kusambaza kwenye mitandao picha zake nilizofuma kwenye simu yake.

Haya yoote yalichukuliwa hatua sema kama ifuatavyo

- kesi ya shambulio (yaan nilipompiga baada ya kulita picha halaf akanijibu shit) hii ndio iliniweka lockup

- kusambaza picha - simu yangu ikachukuliwa na kupekuliwa na watu wao japo hapa nikawachukulia poa sana maana walizitafuta kwenye simu na hawakuziona licha ya kwamba niezificha (kitaalam) humo humo. Haba degree ya CS ilinisaidia 😅, baada ya kuzikosa wakashindwa kufungua shauri nikawa cleared

- kumtishia maisha, hii iliambatanishwa na shambulio, hivyo nilivyotolewa lockupnkwa dhamana, kesi hawakupeleka mahamakan kwakua ilikosa kabisaaa mashiko. Walini release baada ya kuchoka ku report nikaweka presha wapeleke keai mahakaman. Wakaniacha, kesho yale ndio walafungua kesi ya talaka.
 
Kwahiyo mke bado ameanza kutaka kurudi au bado shingo ngumu? Ila kumsamehe mtu wa namna hii anaweza akakuua mbeleni.
 
Sasa broo 😅unaonaje miaka 4 baadae ukiniozesha Huyu wa 14maana atakuwa na miaka 18 Mimi ndo nitakuwa 39 years kamili
Ahahahahahahah...sasa hiyo miaka 4 yeye akiwa na 18 na mimi nitakua na hiyo hiyo miala 39 sasa hapo tutakua wakwe au washkaji??? 😂
 
Mkuu, huyo anayedai sehemu ya mirathi ya mtalaka wake atakua chizi, yan mahakaman mmeachana kwa talaka, maisha na mali ya mzazi mwenzako yana kuhusu nini????
 
Tena hapa umenikumbusha kitu, hivi baada ya siku 45 hukumu inachukuliwa na wote au inachukuliwa na mdai pekee??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…