Fanton Mahal
JF-Expert Member
- Mar 22, 2024
- 1,597
- 4,661
- Thread starter
- #281
Ahahahah..dahh..mimi nin D moja na C moja ila hii concept sikuielewa πππKumbato na liwazo kutoka kwa pisi Kali ππ unakosaje D mbili π
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ahahahah..dahh..mimi nin D moja na C moja ila hii concept sikuielewa πππKumbato na liwazo kutoka kwa pisi Kali ππ unakosaje D mbili π
Kwanini asiliwe wakati wewe mwenyewe huko unakula wengine.Hivi nikisafiri MWEZI mmoja wajanja wanamla mke wangu??? SASA HUO SIYO UMALAYA??? Umeandika UJINGA sana
Ndio ili aoneshe kama Bado anampendaIlitakiwa abishe bishe kidogo sio?
Sasa ya nini yoote kupenda kumuweka mwenzio kwenye majaribu??Ndio ili aoneshe kama Bado anampenda
Huwa wanatishia kuona upepo ,ukiwa stable wanashangaa sana!Kuna mmoja aliitisha kikao Cha ghafula mbele ya watoto na house girl eti "nakutakia maisha mema baba ..."!!?Daah Leo umeonyesha uwanaume kamili nimefurahi kuona upo stable Kias hicho
Ayo yamemstaajabisha kwakuwa mategemeo yake yameenda tofauti
Ila ningekuwa ni mimi ningepinga talaka kama Mwanamke wa shoka bila aibu π ila mali tungegawanaSasa ya nini yoote kupenda kumuweka mwenzio kwenye majaribu??
Ahahahah..pole. haiiko hivyo.Ila ningekuwa ni mimi ningepinga talaka kama Mwanamke wa shoka bila aibu π ila mali tungegawana
Mkuu pole sana kwa changamoto uliyopitia na hongera sana kwa maamuzi uliyofikia.Wakuu heshma kwenu.
Habari za jioni.
Nimeona ni vyema kuwa update kuhusu mwenendo wa suala ambalo nilileta hapa jukwaani siku ya jumatatu katika uzi huu ππππ
Baada ya Wife kuniweka Lockup naona kama natengenezewa mazingira ya ku react nichukue hatua kali
Wakuu heshima kwenu. Poleni na majukumu. Ndugu yenu numerudi tena kuwajuza yale yanayoendelea kunisibu, maana najua hapa wamejaa watu wenye upeo wa kushauri, kutia moyo ,kuonya, kukufungua jicho upate alert na wengine weeengi sana. Wiki kadhaa zimepita toka nilete mikasa yangu na mazonge ya...www.jamiiforums.com
"Samansi" ya mahakama ilielekeza nifike mahamani siku ya leo tarehe 12 Feb 025 nami nikafanya hivyo.
Katika kesi hii mimi kama mdaiwa na aliyekua mke wangu kama mdai.
Niseme tu kitu, katika mfumo wa serikali na personally katika suala hili, nimekuja kugundua, wanawake wame occupy sana nafasi nyingi serikalini, sasa sijui sababu ni nini?
Maana ;
- nilipoitwa dawati, incharge pale alikuwa mwanamke.
Hakika wanawake wametaradadi everywhere, tukiendelea kwa mwendo huu, wanaume twafaaa
- nilipoitwa baraza, kikao chote kilijawa na wazee wa baraza wanawake
- leo hii mahakamani, hakimu alikua mwanamke.
πππππ.
Anyway,.
Kama ambavyo nilikua nimeamua kuwa natamani hili suala liishe tu, na pia kwa kuzingatia ushauri wa baadhi yenu ndugu zangu wana JF, sikupemda kesi iwe na mambo mengi.
Tulipoitwa chamber na hakimu, alianza kwa kusema "hii kesi leo mmeitwa ili iweze kutajwa tu na kipangiwa siku nyingine, hivyo, mdaiwa utasomewa tu charges zako kisha kama una neno utatamka"
Akasoma,kama ilivyo ainishwa kwenye "samansi" niliopokea ,kuwa mdai anataka
1. Talaka
2. Mgawanyo wa mali
3. Kuishi na watoto
4. Matunzo ya watoto
Akauliza "unasemaje?"
Nikamjibu, "nimesikia na sina pingamizi juu ya lolote katika hayo, na kwasababu sina pingamizi naomba mahakama kama inaweza, hili suala tulimalize hapa hapa na leo leo mheshimiwa hakimu"
Akauliza "umekubaliana na haya yote?"
Nikamjibu "ndiyo, nakubaliana na dai lake la talaka, pia nakubaliana na dai la mgawanyo wa mali, japo nitaomba kujua muongozo wa mahakama unasemaje kuhusu hilo , pia muongozo wa mahakama unasema nini kuhusu matunzo ya watoto na kuishi ma watoto, maana yote niko tayari ku comply"
Akasema "kama ni hivyo, basi hii kesi ni nyepesi na itakwenda vizuri, kuhusu mgawanyo wa mali, mahakama ina suggest 50% 50%, unless kama kama mmoja wenu hajaridhika na mtahitaji tuingie katika ushahidi wa kuthibitisha mchango wa kila mmoja kwa vithibitisho.
Pia matunzo ya watoto yamejikita katika chakula, malazi, afya, na ada. Jukumu hili ni la baba kikawaida, lakini mahakama inaangalia kama mama naye anajiweza, basi jukumu hili wote mtagawana.
Na mwisho kuhusu kuishi na watoto, maadam wako chini ya miaka 18, wataishi na mama, ila baba una ruhusa ya kuwaona . Kama unahama mkoa, maana yake watoto watakuja kwako likizo ambapo, mama atagharamia nauli za kwenda likizo na baba atagharamia nauli za kurudi.
Hivyo basi , ndugu mdai nitakuuliza na utajibu hoja moja baada ya nyingine.
1. Talaka.
Hapa nikawaambia sina pingamizi, niko tayari mke wangu apewe haki yale kama anavyo hitaji. Hapo, wife nikaona kashusha pumzi ndedu nzito. Na muda mwingi alikua anajifuta jasho ingawa ndani pana feni. Katika session yote honestly, sikumtazama usoni. Na hatukusalimiana.
2. Mgawanyo wa mali.
Nikasema, kwakua kesi hii imeshanigharimu suala la muda , nakubaliana na pendekezo la mahakama la fifty fifty, kama mwenzagu, mdai anaona amebanwa naomba apewe uhuru wa kuchagua ratio itayompa comfort. Akasema mimi nataka 60%. Hakimu akauliza, mdaiwa (mimi yani) uko tayari, nikasema SINA PINGAMIZI, mahakama impe hiyo 60% anayotaka.
3. Matunzo ya watoto
Hapa nikasema, always nimekua nalipa ada miaka yote, hivyo hili nitae delea nalo, na pia nitawahudumia gharama ya chakula isiyozidi 150,000/= kwa mwezi kwa kuanzia kwasababu, suala hili limeniathiri biashara zangu pia nahitaji ku settle na kuanza upya maisha, hivyo nikitulia nita adjust.
4. Kuishi na watoto.
Nikasema, nakubaliana na pendekezo la mahakama hapo juu.
Hakimu akasema, aisee, hii kesi imeemda vizuri sana.
Wife akaomba "mheshimiwa naomba kidogo niongee na baba .... pembeni, kuhusu suala la mgawanyo wa mali"
Nikajibu "hakimu, sihitaji kuzungumza private , maana sioni kama kuna suala lolote ambalo kwasasa naweza ongea nae tukaelewana, kama ana jambo lolote aliseme hapa mbele yako"
Wife muda woote alikua anafuta jasho sijui maana yake ni nini, lakini katika vitu naamini, ni kwamba alitegemea confrontation na mimi labda nimuwekee kauzibe na vikwazo vya kukubali ombi la talaka, lakini akaona kila kitu nimekubaliana nae kama alivyotaka. Na kila alipotaka kuibua malalamiko, hakimu akawa anasema, naomba tusiguse sababu za mgogoro wenu kwakua sio sehemu ya madai yako mdai, yote uliyodai, tujikite hapo.
Hakim, akayasoma maandishi aliyoandika kisha akaita kila mtu asaini, nikasaini na yeye akasaini, lakini anaposaini akawa anajilalamisha chini chini, hata sijui anaongea nini.
Basi baada ya hapo tukaambiwa , baada ya siku 45 hati ya talaka itatoka na taratibu za utathmini zitaanza, hivyo tutakiwa kufika.
PIa nikatumia fursa hiyo kueleza kuhusu uharibu wa wa wizi uliotokea nyumbani kuonyesha RB ili ifahamike kuwa mali imeharibiwa na wezi.
Pia , ikafamika pale katika shauri kuwa mimi nilishahama nyumbani, na hii nikaona imem suprise mdai wangu, na sijui sababu ni nini!.
Baada ya yote, hakimu, akasema tumemaliza.
Nikanyanyuka na kutoka, japo niliona yf anaaga huku amekaa ana delay kutoka, like she was exhausted with the proceeding that ended.
Sijajua sasa kama walikua wanayapanga yao mengine au lah!!
Ikaisha hivyo.
Sasa baada ya siku ya 45 days ndio mengine yatafuata.
Kifupi nimefurahi hili suala halijawa extended, ngoma imeitwa leo na imetamatika leo, maana wengi walikua wanasema hii kitu inaweza ikaenda 2 months.
ADDITION:
Wakuu, kesi za kuvunjika ndoa ni nyingi sanaa nimekuatana nazo leo mahakamani. Hali sio nzuri kwenye hii taasisi ya kwanza kuanzishwa duniani
SHUKRANI WAKUU.
Usiku mwema
Karibu mkuu, tujue upande wenu katika hili..tag me if you can.Rafiki nitachangia baadaye nikiwa na computer. Huwa sipendi kuandika maneno mengi kwa kutumia simu.
Humu sidhani japo alikua anajua kuwa mimi napenda sana JF yeye akaanza kuwa mtu wa mitandao huku mwishon sasa sijui kama kajiunga humu au lah!!.Mkuu pole sana kwa changamoto uliyopitia na hongera sana kwa maamuzi uliyofikia.
Rafiki yangu mmoja alipia haya uliyopitia mpaka kupeana talaka Mahakamani, baada ya miaka mitatu nje ya ulingo wa ndoa hatimae walirudia, sijui ni nani alimdanganya.
Sasahivi jamaa anaisoma namba, ugonjwa wa moyo na Sukari juu, anapitia njia ngumu zaidi ya awali, somtimes wanawake ni scam.
Mkuu, x wife wako hayumo humu jukwaani asome huu uzi? Atapata mawili, matatu ajifunze upya, atajutia sana upuuzi wake.
Siku njema.
πHumu sidhani japo alikua anajua kuwa mimi napenda sana JF yeye akaanza kuwa mtu wa mitandao huku mwishon sasa sijui kama kajiunga humu au lah!!.
Ahahahah..nilisha delete picha contact zake na nikazi block na hata yeye alisha delete contact hata kabla yangu. Alizifuta. Mimi nimezifuata baadae sana baada ya kukubali ukweli kwamba our thing is irrepairableSafi sana. Huyo takataka saivi huko aliko ana mawazo. Halafu nataka nikupe mbinu nyingine ila hii ni yako tu kujifurahisha nikuambie tu hongera sana mana umekua huru na utainjoi sana maisha ya kua huru na kufanya utakayo, wewe wawaze watoto wako tu...siku isiyo na jina siku Moja tu kama weekend hivi, tafuta picha Moja hivi ya mrembo ama rafiki yako yoyote wa kike mrembo , weka picha yake status...utakuja kunipa majibu [emoji23]
Kumbato na liwazo kutoka kwa pisi Kali ππ unakosaje D mbili π
Kaka utaoa tena?Ahahahah..nilisha delete picha contact zake na nikazi block na hata yeye alisha delete contact hata kabla yangu. Alizifuta. Mimi nimezifuata baadae sana baada ya kukubali ukweli kwamba our thing is irrepairable
Wangapi kwenye maisha yetu wamefanya hivyo? Hata kama kuna wasaidizi unataka kusema huyo mwanamke hafuatilii kuangalia kama kila kitu kinafanyika the way she likes? After all familia ngapi hapa Tanzania zenye wanawake wa nyumbani wameajiri wasaidizi?
Marriage is not a scam madam, mnakutana wawili msiokamilika na kuunda kitu kisicho kamili don't expect a perfect marriage wakati mnakutana wasio wakamilifu.Marriage is a scam Wala sitojali kwamba umri utaenda sijui utaenda wap ila swala la ndoa uwiii limenitoka