Ewaaaah! touch your kids emotionally
Wala sio kwa kulipa ada.
wlaa sio kwa kupeleka mchele.
Awe na nyakati na watoto ambazo watabaki kumtafsiri yeye kama baba hata kama anakaa nao mbali!
Ilinipa wakat mgumu sana kukubaki ukweli na uhalisia. Sikua nimetarajia. Ikanipa tabu
Yahp, alifikiri hivyo, na nili notice hilo kwenye session
Sijui kwann huwa hawafikirii kuwa wanatazamwaje na wanaodhan wanawahitaji. Kama umeweza mfanyia mwanaume mwenzake hiv , ataanzaje kukukuamini kuwa huwez mfanyia na yeye??
Shukran mkuu. Ila kuhusu wao kunitafuta sidhani. Wale ni viburi mnoo. Wana ego za hatari. Kilichotufkkisha hapa na wife n ego yake tu, nilikua tayar kumsamehe nkkawa nambembeleza
ah kabisa.
Hii thread leo nina uzoefu wa binafsi kabisa.
nimepita hapo mwaka juzi, so najua hii.
Ni kipindi kinavuruga sana, inampasa utulivu wa hali ya juu!
Talaka haina mwamba bana, unakaa chini unanyoosha miguu unakunywa maji zako lita tano tano kwa mfululizo mana kuna likitu unalisikia linaunguza hapa kwenye koo!
Alooh!
EHEHEHEHHEHEE watu waache kuchezea maisha ya wengine kwa starehe zao aiseee!
Na ukiona mtu yuko radhi apoteze kila kitu wewe upate na ilhali unajua kabisa mkosaji na anayesababisha hiyo ndoa ivunjike ni nani, hata kwa watu ukijikosha na kujisafisha Huwa vinalipwa kwa kiasi kikubwa sana.
Wakuu heshima kwenu. Poleni na majukumu. Ndugu yenu numerudi tena kuwajuza yale yanayoendelea kunisibu, maana najua hapa wamejaa watu wenye upeo wa kushauri, kutia moyo ,kuonya, kukufungua jicho upate alert na wengine weeengi sana. Wiki kadhaa zimepita toka nilete mikasa yangu na mazonge ya...
www.jamiiforums.com
"Samansi" ya mahakama ilielekeza nifike mahamani siku ya leo tarehe 12 Feb 025 nami nikafanya hivyo.
Katika kesi hii mimi kama mdaiwa na aliyekua mke wangu kama mdai.
Niseme tu kitu, katika mfumo wa serikali na personally katika suala hili, nimekuja kugundua, wanawake wame occupy sana nafasi nyingi serikalini, sasa sijui sababu ni nini?
Maana ;
- nilipoitwa dawati, incharge pale alikuwa mwanamke.
nilipoitwa baraza, kikao chote kilijawa na wazee wa baraza wanawake
Kama ambavyo nilikua nimeamua kuwa natamani hili suala liishe tu, na pia kwa kuzingatia ushauri wa baadhi yenu ndugu zangu wana JF, sikupemda kesi iwe na mambo mengi.
Tulipoitwa chamber na hakimu, alianza kwa kusema "hii kesi leo mmeitwa ili iweze kutajwa tu na kipangiwa siku nyingine, hivyo, mdaiwa utasomewa tu charges zako kisha kama una neno utatamka"
Akasoma,kama ilivyo ainishwa kwenye "samansi" niliopokea ,kuwa mdai anataka
1. Talaka
2. Mgawanyo wa mali
3. Kuishi na watoto
4. Matunzo ya watoto
Akauliza "unasemaje?"
Nikamjibu, "nimesikia na sina pingamizi juu ya lolote katika hayo, na kwasababu sina pingamizi naomba mahakama kama inaweza, hili suala tulimalize hapa hapa na leo leo mheshimiwa hakimu"
Akauliza "umekubaliana na haya yote?"
Nikamjibu "ndiyo, nakubaliana na dai lake la talaka, pia nakubaliana na dai la mgawanyo wa mali, japo nitaomba kujua muongozo wa mahakama unasemaje kuhusu hilo , pia muongozo wa mahakama unasema nini kuhusu matunzo ya watoto na kuishi ma watoto, maana yote niko tayari ku comply"
Akasema "kama ni hivyo, basi hii kesi ni nyepesi na itakwenda vizuri, kuhusu mgawanyo wa mali, mahakama ina suggest 50% 50%, unless kama kama mmoja wenu hajaridhika na mtahitaji tuingie katika ushahidi wa kuthibitisha mchango wa kila mmoja kwa vithibitisho.
Pia matunzo ya watoto yamejikita katika chakula, malazi, afya, na ada. Jukumu hili ni la baba kikawaida, lakini mahakama inaangalia kama mama naye anajiweza, basi jukumu hili wote mtagawana.
Na mwisho kuhusu kuishi na watoto, maadam wako chini ya miaka 18, wataishi na mama, ila baba una ruhusa ya kuwaona . Kama unahama mkoa, maana yake watoto watakuja kwako likizo ambapo, mama atagharamia nauli za kwenda likizo na baba atagharamia nauli za kurudi.
Hivyo basi , ndugu mdai nitakuuliza na utajibu hoja moja baada ya nyingine.
1. Talaka.
Hapa nikawaambia sina pingamizi, niko tayari mke wangu apewe haki yale kama anavyo hitaji. Hapo, wife nikaona kashusha pumzi ndedu nzito. Na muda mwingi alikua anajifuta jasho ingawa ndani pana feni. Katika session yote honestly, sikumtazama usoni. Na hatukusalimiana.
2. Mgawanyo wa mali.
Nikasema, kwakua kesi hii imeshanigharimu suala la muda , nakubaliana na pendekezo la mahakama la fifty fifty, kama mwenzagu, mdai anaona amebanwa naomba apewe uhuru wa kuchagua ratio itayompa comfort. Akasema mimi nataka 60%. Hakimu akauliza, mdaiwa (mimi yani) uko tayari, nikasema SINA PINGAMIZI, mahakama impe hiyo 60% anayotaka.
3. Matunzo ya watoto
Hapa nikasema, always nimekua nalipa ada miaka yote, hivyo hili nitae delea nalo, na pia nitawahudumia gharama ya chakula isiyozidi 150,000/= kwa mwezi kwa kuanzia kwasababu, suala hili limeniathiri biashara zangu pia nahitaji ku settle na kuanza upya maisha, hivyo nikitulia nita adjust.
4. Kuishi na watoto.
Nikasema, nakubaliana na pendekezo la mahakama hapo juu.
Hakimu akasema, aisee, hii kesi imeemda vizuri sana.
Wife akaomba "mheshimiwa naomba kidogo niongee na baba .... pembeni, kuhusu suala la mgawanyo wa mali"
Nikajibu "hakimu, sihitaji kuzungumza private , maana sioni kama kuna suala lolote ambalo kwasasa naweza ongea nae tukaelewana, kama ana jambo lolote aliseme hapa mbele yako"
Wife muda woote alikua anafuta jasho sijui maana yake ni nini, lakini katika vitu naamini, ni kwamba alitegemea confrontation na mimi labda nimuwekee kauzibe na vikwazo vya kukubali ombi la talaka, lakini akaona kila kitu nimekubaliana nae kama alivyotaka. Na kila alipotaka kuibua malalamiko, hakimu akawa anasema, naomba tusiguse sababu za mgogoro wenu kwakua sio sehemu ya madai yako mdai, yote uliyodai, tujikite hapo.
Hakim, akayasoma maandishi aliyoandika kisha akaita kila mtu asaini, nikasaini na yeye akasaini, lakini anaposaini akawa anajilalamisha chini chini, hata sijui anaongea nini.
Basi baada ya hapo tukaambiwa , baada ya siku 45 hati ya talaka itatoka na taratibu za utathmini zitaanza, hivyo tutakiwa kufika.
PIa nikatumia fursa hiyo kueleza kuhusu uharibu wa wa wizi uliotokea nyumbani kuonyesha RB ili ifahamike kuwa mali imeharibiwa na wezi.
Pia , ikafamika pale katika shauri kuwa mimi nilishahama nyumbani, na hii nikaona imem suprise mdai wangu, na sijui sababu ni nini!.
Baada ya yote, hakimu, akasema tumemaliza.
Nikanyanyuka na kutoka, japo niliona yf anaaga huku amekaa ana delay kutoka, like she was exhausted with the proceeding that ended.
Sijajua sasa kama walikua wanayapanga yao mengine au lah!!
Ikaisha hivyo.
Sasa baada ya siku ya 45 days ndio mengine yatafuata.
Kifupi nimefurahi hili suala halijawa extended, ngoma imeitwa leo na imetamatika leo, maana wengi walikua wanasema hii kitu inaweza ikaenda 2 months.
ADDITION:
Wakuu, kesi za kuvunjika ndoa ni nyingi sanaa nimekuatana nazo leo mahakamani. Hali sio nzuri kwenye hii taasisi ya kwanza kuanzishwa duniani
Shukran, it was mapito yenye mafunzo kuhusu maisha, binadamu, mapenzi, ndoa!
Leo niko na tafsiri pana sana kuhsu vyote hivyo.
Namshukuru Mungu sijabaki na bitterness, nimejifunza , ninaamini katika kukua, kubadilika, kupoteza mwelekeo wa maisha.
Wakati fulani ili usonge mbele ni lazima unaoongozana nao mbadilishane njia!
Shukran, it was mapito yenye mafunzo kuhusu maisha, binadamu, mapenzi, ndoa!
Leo niko na tafsiri pana sana kuhsu vyote hivyo.
Namshukuru Mungu sijabaki na bitterness, nimejifunza , ninaamini katika kukua, kubadilika, kupoteza mwelekeo wa maisha.
Wakati fulani ili usonge mbele ni lazima unaoongozana nao mbadilishane njia!
On top ya huu uzoefu kuna kitu kigumu sana kimejiumba kwako
.....kutokumwamini mtu mwingine kirahisi.....
Kitu nilichogundua cha muhim, ukikutana na kiumbe mpya jaribu sana kwa akili uchimbe taratibu ujue historia au maumivu alopitia kabla yako ili ikiwezekane imponye kwanza ndipo safari ianze.
Nimegundua ukikutana na mtu aliyeumizwa sana huwa kuna uwezekano mkubwa wa uhusiano kufa au kuyumba sana.
nzuri sana.
Huwa inadhaniwa watu hawawezi kuishi bila ndoa , sio kwlei aisee.
Ndoa yenye majeraha na machozi kila siku, better off kukaa mwenyewe ukisikia mgongoni kunawasha unajikuna ukutani!
aH
Of course sio kitu rahisi, na wala tukisema kuwa amefanya jambo la kishujaa maana yake haumii au haiumi, Sio kweli.
Ilikuwa ni maisha uliyotamani kupata uzee nayo pamoja ila kila siku senema, Hapana!
HATA UZEE WENYEWE HUTAFIKA , aiseeh!
Mimi huwa nina falsafa ngumu sana pengine, kuliko niendelee kuwepo kwenye situation inaniumiza kwa kuwa naipenda, bora niiistop yale maumivu ninayoumia yawe yanaenda yakifade kuliko kubaki kwenye same situation na maumivu ni yale yale na hayatastop.
Ndoa za wakristu ni mpk kifo.
iwapo nitabarikiwa miaka 70 ya kwenye biblia, basi ndo kwanza kuna mingine kama 28 hivi inanisubiri.
So nikae nasubiri kuteseka next last 28 yrs , Hapana aisee!
ACHA TU IVUNJIKE NIANZE MOJA NA ARIFU!
On top ya huu uzoefu kuna kitu kigumu sana kimejiumba kwako
.....kutokumwamini mtu mwingine kirahisi.....
Kitu nilichogundua cha muhim, ukikutana na kiumbe mpya jaribu sana kwa akili uchimbe taratibu ujue historia au maumivu alopitia kabla yako ili ikiwezekane imponye kwanza ndipo safari ianze.
Nimegundua ukikutana na mtu aliyeumizwa sana huwa kuna uwezekano mkubwa wa uhusiano kufa au kuyumba sana.
Partly yes.
Although mi nimekataa hii kuikiri kwenye mahusiano yangu next after.
Ntajikosea sana haki kuendelea kujeruhika na maisha ya awali.
Watu hawafanani.
Hata mimi had part kwenye kuvunjika ndoa hiyo so kubaki hujisamehi kila siku unaacha na kuvunja tu mahusiano kisa ex alikujeruhi hii hapana.
So yes, imenipa uzoefu na kuwafahamu binadamu zaidi na kujua when to stop and when to persue and when to keep a person.
Mapenzi bado kitu muhimu sana in life.
Ndoa bado ni kitu chema sana
inavunjika leo, unaheal, unatizama your role, your lessons ah mbna unafall tena tu.
Ila sasa , watu wa aina yetu pia as you are saying hatuogopi pia kuvunja iwapo uhusiano umezingua.
Lakini hatutavunja tu alimradi kwa kuwa tunajua gharama ya kuvunja ndoa au uhusiano unaostahili kutunzwa.
Kwanini artificial?
HAPANA!
Mapenzi huisha bro, yakiisha unayaacha yaende.
Unapona unapenda upya and the cycle inaendelea.
Sasa unatarajia mtu akiachana na mwenzi akae tu kiseja, sio kweli!
Wanaopata wa kuwapend after tht, wapo na wanaishi maisha mazuri tu!
Hakuna tafsiri moja kuhusu maisha.
Kwanini artificial?
HAPANA!
Mapenzi huisha bro, yakiisha unayaacha yaende.
Unapona unapenda upya and the cycle inaendelea.
Sasa unatarajia mtu akiachana na mwenzi akae tu kiseja, sio kweli!
Wanaopata wa kuwapend after tht, wapo na wanaishi maisha mazuri tu!
Hakuna tafsiri moja kuhusu maisha.
maisha yasonge mbele kwasasa, Focus your energy kwenye mambo yako,
usipoteze muda wako kutengeneza mashindano ya kuonesha maisha baada ya ndoa,
ishi maisha yako,
kwa kila nafasi unayopata ya watoto wako, itumie ipasavyo..
Mkuu Fanton Mahal kwanza pole na habari za kesi (kesi zinakula sana muda wa wadaawa) ila Mkuu nikuhakikishie jambo moja hapo hakuna mlichokifanya wala kukikwepa kwenye swala la muda. Nitakuambia kwasababu gani nasema hivyo.
Kwanza kabisa kesi zote za madai ya hamri ya talaka ni sharti la lazima zisikilizwe ushahidi hii ni ili Mahakama ijiridhishe kupitia ushahidi uliotolewa kuwa kweli hiyo ndoa imevunjika kiasi cha kushindikana kurekebishwa.
Nimesikitika sana juu ya mwenendo uliochukuliwa na Mh. Hakimu husika maana ni amefanya kituko cha aibu sana.
Tukiachana na hili la amri ya talaka embu tuangalie hapo kwenye chumo la pamoja yaani mgawanyo wa mali na mali zenyewe.
Kwanza kama imeenda hivi ulivyosimulia hapa ni dhahiri na wazi kuwa mkeo ameshindwa kuthibitisha kwanza uwepo wa hizo mali zilizotokana na ndoa, kwanini nasema hivyo ni kwasababu hizo mali ambazo bado mkapewa mgao wa 60%kwa 40% bado hata hazijatajwa hapo Mahakamani. Sasa mimi na wewe na wana JF wote tujiulize mmegawana mali gani na ipi hiyo ambayo imetajwa Mahakamani?
Tuache hili la mali na mgawanyo wake embu tuangalie hilo lingine la kuhusu watoto ambao nao mmesema wakae na mama yao, tujiulize swali tena ni watoto wapi hao?, ni nani na nani kwa majina yao?, je walitajwa hapo Mahakamani na kutambuliwa inavyopaswa kuwa?.
Hii ni aibu nyingine kwa mhimili wa Mahakama, na hapa haujatoa rushwa (sababu hujataja swala hilo) ila Mh. Hakimu kwa uzembe wa kukosa weledi amekinzana na taratibu zote na sheria zote zinazosimamia mashauri ya migogoro ya ndoa.
Nina uhakikakama utaitaja hiyo Mahakama basi hilo jalada litaitwa na Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya maana hii ni aibu na imeshakuwa mazoea sasa.
Hata kwa kuokoa muda wenu basi Mahakama ingepokea ushahidina utetezi siku hii hii moja kuliko kukanyagataratibu hivi zilivyokanyagwa. Ninaelewa kusudio lako la kuokoa muda na gharama lakini hii wiki na wewe umejifunza utaratibu usio sahihi wa namna kesi za talaka zinavyoenda.
Kesho au keshokutwa utamshauri mtu au kumpa uzoefu wako huu na akikutana na Mh. Hakimu anayejua nini kinatakiwa kufanyika ataanza kuhisi au kufikiri kuwa Hakimu husika anaweka mazingira magumu ili adai rushwa, mwisho wa yoteni kukosa imani na Mahakama na mfumo wake wote.
Walio tunga hizo sheria za ndoa walikua wanawaza nini, Yani mgawanyo wa mali ni 50 50 lkn Kulea watoto hilo ni jukumu la baba kikawaida, Kawaida gani hyo? Imetafsiriwa kisheria au ni upeo wa hakimu?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.