Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Very very true. Kuna namna nilikua nimeandaa kisasi juu ya huyu mtu ila nikaghairi baada ya kufikiri kwa kina
Achana kabisa na hayo mawazo.Very very true. Kuna namna nilikua nimeandaa kisasi juu ya huyu mtu ila nikaghairi baada ya kufikiri kwa kina
Ha ha haTaarifa anayo, kutwa kumpigia simu eti aongee na watoto wskati mtoto mkubwa ana simu.
SI kaileta baada ya kuisusiaDuuuh hiyo ni hatar tupu
HahahahaSI kaileta baada ya kuisusia
Duh ukala makombo na ukoko kabisa na sahani ukalamba bila kujali ukoko uliungua.🤣🤣🤣🤣🤣🤣Tulizaa tena kabinti, na alipojifungua alikuja kukaleta...aliporudi kwake,usiku mtoto akilia sana ananipiga simu nikamsaidie kumbembeleza nae alale kidogo anachoka
Ha ha ha haNaona unampa ujuzi kaka angu. Mkiwa mnaongea huko pm au whatsApp utamfundisha vitu vingi zaidi na atapona haraka sana.
So sad. Lakini wewe ni shujaa. Wewe ni mshindi. MUNGU atakupa amani ya kweli. Hawa wadudu mashetani waitwao wanawake wanatunyima amani halisi.Wakuu heshma kwenu.
Habari za jioni.
Nimeona ni vyema kuwa update kuhusu mwenendo wa suala ambalo nilileta hapa jukwaani siku ya jumatatu katika uzi huu 👇👇👇👇
Baada ya Wife kuniweka Lockup naona kama natengenezewa mazingira ya ku react nichukue hatua kali
Wakuu heshima kwenu. Poleni na majukumu. Ndugu yenu numerudi tena kuwajuza yale yanayoendelea kunisibu, maana najua hapa wamejaa watu wenye upeo wa kushauri, kutia moyo ,kuonya, kukufungua jicho upate alert na wengine weeengi sana. Wiki kadhaa zimepita toka nilete mikasa yangu na mazonge ya...www.jamiiforums.com
"Samansi" ya mahakama ilielekeza nifike mahamani siku ya leo tarehe 12 Feb 025 nami nikafanya hivyo.
Katika kesi hii mimi kama mdaiwa na aliyekua mke wangu kama mdai.
Niseme tu kitu, katika mfumo wa serikali na personally katika suala hili, nimekuja kugundua, wanawake wame occupy sana nafasi nyingi serikalini, sasa sijui sababu ni nini?
Maana ;
- nilipoitwa dawati, incharge pale alikuwa mwanamke.
Hakika wanawake wametaradadi everywhere, tukiendelea kwa mwendo huu, wanaume twafaaa
- nilipoitwa baraza, kikao chote kilijawa na wazee wa baraza wanawake
- leo hii mahakamani, hakimu alikua mwanamke.
😁😁😁😁😁.
Anyway,.
Kama ambavyo nilikua nimeamua kuwa natamani hili suala liishe tu, na pia kwa kuzingatia ushauri wa baadhi yenu ndugu zangu wana JF, sikupemda kesi iwe na mambo mengi.
Tulipoitwa chamber na hakimu, alianza kwa kusema "hii kesi leo mmeitwa ili iweze kutajwa tu na kipangiwa siku nyingine, hivyo, mdaiwa utasomewa tu charges zako kisha kama una neno utatamka"
Akasoma,kama ilivyo ainishwa kwenye "samansi" niliopokea ,kuwa mdai anataka
1. Talaka
2. Mgawanyo wa mali
3. Kuishi na watoto
4. Matunzo ya watoto
Akauliza "unasemaje?"
Nikamjibu, "nimesikia na sina pingamizi juu ya lolote katika hayo, na kwasababu sina pingamizi naomba mahakama kama inaweza, hili suala tulimalize hapa hapa na leo leo mheshimiwa hakimu"
Akauliza "umekubaliana na haya yote?"
Nikamjibu "ndiyo, nakubaliana na dai lake la talaka, pia nakubaliana na dai la mgawanyo wa mali, japo nitaomba kujua muongozo wa mahakama unasemaje kuhusu hilo , pia muongozo wa mahakama unasema nini kuhusu matunzo ya watoto na kuishi ma watoto, maana yote niko tayari ku comply"
Akasema "kama ni hivyo, basi hii kesi ni nyepesi na itakwenda vizuri, kuhusu mgawanyo wa mali, mahakama ina suggest 50% 50%, unless kama kama mmoja wenu hajaridhika na mtahitaji tuingie katika ushahidi wa kuthibitisha mchango wa kila mmoja kwa vithibitisho.
Pia matunzo ya watoto yamejikita katika chakula, malazi, afya, na ada. Jukumu hili ni la baba kikawaida, lakini mahakama inaangalia kama mama naye anajiweza, basi jukumu hili wote mtagawana.
Na mwisho kuhusu kuishi na watoto, maadam wako chini ya miaka 18, wataishi na mama, ila baba una ruhusa ya kuwaona . Kama unahama mkoa, maana yake watoto watakuja kwako likizo ambapo, mama atagharamia nauli za kwenda likizo na baba atagharamia nauli za kurudi.
Hivyo basi , ndugu mdai nitakuuliza na utajibu hoja moja baada ya nyingine.
1. Talaka.
Hapa nikawaambia sina pingamizi, niko tayari mke wangu apewe haki yale kama anavyo hitaji. Hapo, wife nikaona kashusha pumzi ndedu nzito. Na muda mwingi alikua anajifuta jasho ingawa ndani pana feni. Katika session yote honestly, sikumtazama usoni. Na hatukusalimiana.
2. Mgawanyo wa mali.
Nikasema, kwakua kesi hii imeshanigharimu suala la muda , nakubaliana na pendekezo la mahakama la fifty fifty, kama mwenzagu, mdai anaona amebanwa naomba apewe uhuru wa kuchagua ratio itayompa comfort. Akasema mimi nataka 60%. Hakimu akauliza, mdaiwa (mimi yani) uko tayari, nikasema SINA PINGAMIZI, mahakama impe hiyo 60% anayotaka.
3. Matunzo ya watoto
Hapa nikasema, always nimekua nalipa ada miaka yote, hivyo hili nitae delea nalo, na pia nitawahudumia gharama ya chakula isiyozidi 150,000/= kwa mwezi kwa kuanzia kwasababu, suala hili limeniathiri biashara zangu pia nahitaji ku settle na kuanza upya maisha, hivyo nikitulia nita adjust.
4. Kuishi na watoto.
Nikasema, nakubaliana na pendekezo la mahakama hapo juu.
Hakimu akasema, aisee, hii kesi imeemda vizuri sana.
Wife akaomba "mheshimiwa naomba kidogo niongee na baba .... pembeni, kuhusu suala la mgawanyo wa mali"
Nikajibu "hakimu, sihitaji kuzungumza private , maana sioni kama kuna suala lolote ambalo kwasasa naweza ongea nae tukaelewana, kama ana jambo lolote aliseme hapa mbele yako"
Wife muda woote alikua anafuta jasho sijui maana yake ni nini, lakini katika vitu naamini, ni kwamba alitegemea confrontation na mimi labda nimuwekee kauzibe na vikwazo vya kukubali ombi la talaka, lakini akaona kila kitu nimekubaliana nae kama alivyotaka. Na kila alipotaka kuibua malalamiko, hakimu akawa anasema, naomba tusiguse sababu za mgogoro wenu kwakua sio sehemu ya madai yako mdai, yote uliyodai, tujikite hapo.
Hakim, akayasoma maandishi aliyoandika kisha akaita kila mtu asaini, nikasaini na yeye akasaini, lakini anaposaini akawa anajilalamisha chini chini, hata sijui anaongea nini.
Basi baada ya hapo tukaambiwa , baada ya siku 45 hati ya talaka itatoka na taratibu za utathmini zitaanza, hivyo tutakiwa kufika.
PIa nikatumia fursa hiyo kueleza kuhusu uharibu wa wa wizi uliotokea nyumbani kuonyesha RB ili ifahamike kuwa mali imeharibiwa na wezi.
Pia , ikafamika pale katika shauri kuwa mimi nilishahama nyumbani, na hii nikaona imem suprise mdai wangu, na sijui sababu ni nini!.
Baada ya yote, hakimu, akasema tumemaliza.
Nikanyanyuka na kutoka, japo niliona yf anaaga huku amekaa ana delay kutoka, like she was exhausted with the proceeding that ended.
Sijajua sasa kama walikua wanayapanga yao mengine au lah!!
Ikaisha hivyo.
Sasa baada ya siku ya 45 days ndio mengine yatafuata.
Kifupi nimefurahi hili suala halijawa extended, ngoma imeitwa leo na imetamatika leo, maana wengi walikua wanasema hii kitu inaweza ikaenda 2 months.
ADDITION:
Wakuu, kesi za kuvunjika ndoa ni nyingi sanaa nimekuatana nazo leo mahakamani. Hali sio nzuri kwenye hii taasisi ya kwanza kuanzishwa duniani
SHUKRANI WAKUU.
Usiku mwema
Ni kinyume chake. Kama huna moyo wa kukubaliana na kuacha au kuachwa usioe. Sababu siku ikitokea ama utachizika, utaua, au pressure.This is for those who cares. Mimi huwa ninawaambia ndg zangu kuwa kama huna utayari wa kuoa au kuolewa usiingie ktk ndoa. Full stop
Wewe shujaa mwingine wa kike.mimi ni Ke,
a divorcee mwaka wa 3 huu.
Mtalaka wangu aliniletea hizi hizi za kiwehu, aseeee nilimnyoosha!
Unajua watu hudhani maisha yanaishia kwenye kuoa/kuolewa.
Hapana , far as i love to be loved and to love, i love myself too.
Huwezi kufanya ujinga wote in the life, nikireact unanitishia SHAURI LA MAHAKAMA, ehehehhehee
Mpaka kesho sidhani ile scenario ataisahau.
Naulizwa na hakimu unataka talaka, namjibu yes
mimi aliniwekea kosa la cheating, ilhali yeye ndo anaishi na mwanamke (shauri la talaka lazima liwe na kosa)ahahahahaha nyau yule aliweka na kosa la namtishia uhai(nikamwambia hakimu na mkimuacha msimpe talaka anayotaka siku mtanihukumu kesi ya murder, nilichukia sana kiukweli)
Yani unashtakiwa makosa ambayo yeye ndo anayafanya, afa anakuwahi Baraza la Kata.
AH NILIMFURAHISHA!
Mi nikamwambia hakimu ndio ,(mwanasehria alishanitonya ukitaka hjii kesi iishe fasta kubali kila kosa analoshatki)
So nikakubali kila alichotaka, nyumba sijui nini nini, nikasema na yenyewe siitaki!
Mtoto oh nikitakiwa kulea basi nikae nae , akikaa nae yeye mimi baba nisihusike
Nikamwambia hakimu no worries mi mamake nipewe nitalea mwanangu na sitauliza mia ya mtu.
Ustawi wananiuliza mara mbili mbili, we mama , nawambia jamani mi nisipewe matunzo, naombeni tu mtoto wangu kwa 100%custody.
Jambo likaenda chap kwa haraka.
Unajifulia nguo, unanyoosha pasi mwenyewe. Mostly unapika mwenyewe, huyo mwanamke ana umuhimu gani kama sio golikipaHakuna mke unayeweza kumuita Golikipa. Anapobaki nyumbani anashinda amelala tu na kuangalia TV? Mwanamke anaamka asubuhi anaandaa watoto kwenda shule, anakuandalia kila kitu uende kwenye mihangaiko yako; anasafisha nyumba, anapika, anafua, anahakikisha kila kitu ndani ya nyumba kinakaa sawa. Unarudi nyumbani kutoka ulikokuwa anakupokea na kukuandalia chakula, una-relax na kuwa na akili ya kuendelea kutafuta mkate wa kesho na kwa watoto anafanya hivyo. Leo wewe ni wa kumuita Golikipa!!!! Hivyo vyote anavyofanya unaona SIYO kazi???? Wanaume mna matatizo sana ya uelewa na ni wabinafsi sana.
Pengine umeamua mwenyewe kufanya hizo kazi kumsaidia siyo vibaya lakini siyo golikipa.Unajifulia nguo, unanyoosha pasi mwenyewe. Mostly unapika mwenyewe, huyo mwanamke ana umuhimu gani kama sio golikipa
Unashinda kazini unakuta nguo ulizoloweka na sabuni zifuliwe bado chafu kwenye beseni, kuliko kugombana unajifulia. Anajua unawahi kazini unaamka asubuhi ndio kwanza anakoroma unanyoosha chap tunakimbia. Unarudi una njaa ndiyo kwanza anaangalia TikTok, unaingia jikoni maisha yanasonga.Pengine umeamua mwenyewe kufanya hizo kazi kumsaidia siyo vibaya lakini siyo golikipa.
Kwa kweli huyo ni zezeta. Pole sana. Ulimtoa wapi?Unashinda kazini unakuta nguo ulizoloweka na sabuni zifuliwe bado chafu kwenye beseni, kuliko kugombana unajifulia. Anajua unawahi kazini unaamka asubuhi ndio kwanza anakoroma unanyoosha chap tunakimbia. Unarudi una njaa ndiyo kwanza anaangalia TikTok, unaingia jikoni maisha yanasonga.
Huyo wala hata sifa ya ugolikipa hana ila ni zezeta. Lakini mkipishana kidogo utasikia tugawane. Hii sio story ni hali halisi ya ndoa fulani.
Aende uko sasa anapopataka, Yuko huru.Wanaume mkishamzalisha mtu tena mtoto zaidi ya 1 huwa mna vitabia vyenu ambavyo mnaviendekeza mkijua wanawake hawana pa kwenda.
Wanawake waharibifu sana.Wakuu heshma kwenu.
Habari za jioni.
Nimeona ni vyema kuwa update kuhusu mwenendo wa suala ambalo nilileta hapa jukwaani siku ya jumatatu katika uzi huu 👇👇👇👇
Baada ya Wife kuniweka Lockup naona kama natengenezewa mazingira ya ku react nichukue hatua kali
Wakuu heshima kwenu. Poleni na majukumu. Ndugu yenu numerudi tena kuwajuza yale yanayoendelea kunisibu, maana najua hapa wamejaa watu wenye upeo wa kushauri, kutia moyo ,kuonya, kukufungua jicho upate alert na wengine weeengi sana. Wiki kadhaa zimepita toka nilete mikasa yangu na mazonge ya...www.jamiiforums.com
"Samansi" ya mahakama ilielekeza nifike mahamani siku ya leo tarehe 12 Feb 025 nami nikafanya hivyo.
Katika kesi hii mimi kama mdaiwa na aliyekua mke wangu kama mdai.
Niseme tu kitu, katika mfumo wa serikali na personally katika suala hili, nimekuja kugundua, wanawake wame occupy sana nafasi nyingi serikalini, sasa sijui sababu ni nini?
Maana ;
- nilipoitwa dawati, incharge pale alikuwa mwanamke.
Hakika wanawake wametaradadi everywhere, tukiendelea kwa mwendo huu, wanaume twafaaa
- nilipoitwa baraza, kikao chote kilijawa na wazee wa baraza wanawake
- leo hii mahakamani, hakimu alikua mwanamke.
😁😁😁😁😁.
Anyway,.
Kama ambavyo nilikua nimeamua kuwa natamani hili suala liishe tu, na pia kwa kuzingatia ushauri wa baadhi yenu ndugu zangu wana JF, sikupemda kesi iwe na mambo mengi.
Tulipoitwa chamber na hakimu, alianza kwa kusema "hii kesi leo mmeitwa ili iweze kutajwa tu na kipangiwa siku nyingine, hivyo, mdaiwa utasomewa tu charges zako kisha kama una neno utatamka"
Akasoma,kama ilivyo ainishwa kwenye "samansi" niliopokea ,kuwa mdai anataka
1. Talaka
2. Mgawanyo wa mali
3. Kuishi na watoto
4. Matunzo ya watoto
Akauliza "unasemaje?"
Nikamjibu, "nimesikia na sina pingamizi juu ya lolote katika hayo, na kwasababu sina pingamizi naomba mahakama kama inaweza, hili suala tulimalize hapa hapa na leo leo mheshimiwa hakimu"
Akauliza "umekubaliana na haya yote?"
Nikamjibu "ndiyo, nakubaliana na dai lake la talaka, pia nakubaliana na dai la mgawanyo wa mali, japo nitaomba kujua muongozo wa mahakama unasemaje kuhusu hilo , pia muongozo wa mahakama unasema nini kuhusu matunzo ya watoto na kuishi ma watoto, maana yote niko tayari ku comply"
Akasema "kama ni hivyo, basi hii kesi ni nyepesi na itakwenda vizuri, kuhusu mgawanyo wa mali, mahakama ina suggest 50% 50%, unless kama kama mmoja wenu hajaridhika na mtahitaji tuingie katika ushahidi wa kuthibitisha mchango wa kila mmoja kwa vithibitisho.
Pia matunzo ya watoto yamejikita katika chakula, malazi, afya, na ada. Jukumu hili ni la baba kikawaida, lakini mahakama inaangalia kama mama naye anajiweza, basi jukumu hili wote mtagawana.
Na mwisho kuhusu kuishi na watoto, maadam wako chini ya miaka 18, wataishi na mama, ila baba una ruhusa ya kuwaona . Kama unahama mkoa, maana yake watoto watakuja kwako likizo ambapo, mama atagharamia nauli za kwenda likizo na baba atagharamia nauli za kurudi.
Hivyo basi , ndugu mdai nitakuuliza na utajibu hoja moja baada ya nyingine.
1. Talaka.
Hapa nikawaambia sina pingamizi, niko tayari mke wangu apewe haki yale kama anavyo hitaji. Hapo, wife nikaona kashusha pumzi ndedu nzito. Na muda mwingi alikua anajifuta jasho ingawa ndani pana feni. Katika session yote honestly, sikumtazama usoni. Na hatukusalimiana.
2. Mgawanyo wa mali.
Nikasema, kwakua kesi hii imeshanigharimu suala la muda , nakubaliana na pendekezo la mahakama la fifty fifty, kama mwenzagu, mdai anaona amebanwa naomba apewe uhuru wa kuchagua ratio itayompa comfort. Akasema mimi nataka 60%. Hakimu akauliza, mdaiwa (mimi yani) uko tayari, nikasema SINA PINGAMIZI, mahakama impe hiyo 60% anayotaka.
3. Matunzo ya watoto
Hapa nikasema, always nimekua nalipa ada miaka yote, hivyo hili nitae delea nalo, na pia nitawahudumia gharama ya chakula isiyozidi 150,000/= kwa mwezi kwa kuanzia kwasababu, suala hili limeniathiri biashara zangu pia nahitaji ku settle na kuanza upya maisha, hivyo nikitulia nita adjust.
4. Kuishi na watoto.
Nikasema, nakubaliana na pendekezo la mahakama hapo juu.
Hakimu akasema, aisee, hii kesi imeemda vizuri sana.
Wife akaomba "mheshimiwa naomba kidogo niongee na baba .... pembeni, kuhusu suala la mgawanyo wa mali"
Nikajibu "hakimu, sihitaji kuzungumza private , maana sioni kama kuna suala lolote ambalo kwasasa naweza ongea nae tukaelewana, kama ana jambo lolote aliseme hapa mbele yako"
Wife muda woote alikua anafuta jasho sijui maana yake ni nini, lakini katika vitu naamini, ni kwamba alitegemea confrontation na mimi labda nimuwekee kauzibe na vikwazo vya kukubali ombi la talaka, lakini akaona kila kitu nimekubaliana nae kama alivyotaka. Na kila alipotaka kuibua malalamiko, hakimu akawa anasema, naomba tusiguse sababu za mgogoro wenu kwakua sio sehemu ya madai yako mdai, yote uliyodai, tujikite hapo.
Hakim, akayasoma maandishi aliyoandika kisha akaita kila mtu asaini, nikasaini na yeye akasaini, lakini anaposaini akawa anajilalamisha chini chini, hata sijui anaongea nini.
Basi baada ya hapo tukaambiwa , baada ya siku 45 hati ya talaka itatoka na taratibu za utathmini zitaanza, hivyo tutakiwa kufika.
PIa nikatumia fursa hiyo kueleza kuhusu uharibu wa wa wizi uliotokea nyumbani kuonyesha RB ili ifahamike kuwa mali imeharibiwa na wezi.
Pia , ikafamika pale katika shauri kuwa mimi nilishahama nyumbani, na hii nikaona imem suprise mdai wangu, na sijui sababu ni nini!.
Baada ya yote, hakimu, akasema tumemaliza.
Nikanyanyuka na kutoka, japo niliona yf anaaga huku amekaa ana delay kutoka, like she was exhausted with the proceeding that ended.
Sijajua sasa kama walikua wanayapanga yao mengine au lah!!
Ikaisha hivyo.
Sasa baada ya siku ya 45 days ndio mengine yatafuata.
Kifupi nimefurahi hili suala halijawa extended, ngoma imeitwa leo na imetamatika leo, maana wengi walikua wanasema hii kitu inaweza ikaenda 2 months.
ADDITION:
Wakuu, kesi za kuvunjika ndoa ni nyingi sanaa nimekuatana nazo leo mahakamani. Hali sio nzuri kwenye hii taasisi ya kwanza kuanzishwa duniani
SHUKRANI WAKUU.
Usiku mwema
Makombo tena!!!? Pini ilikua yangu itakuwaje makombo tenaDuh ukala makombo na ukoko kabisa na sahani ukalamba bila kujali ukoko uliungua.🤣🤣🤣🤣🤣🤣
Usimshauri hivyo. Uking'ang'ana na mke asiyekupenda iko siku watoto hao hao watakuaga baba yao kwenye jeneza. Mama amefanya yake.Umeona sasa? Mnaenda kumfanya huyo binti aone mahusiano ya ndoa ya hovyo..!!
Mkeo itakuwa amekurupuka kudai talaka ila atajutia na itamtesa sana baadae..!!
Mkuu km kuna uwezekano wa kuahirisha maamuzi fanya hivyo kwa mustakabali wa watoto wenu..!! Mkishindwa sana gawaneni vyumba mlee mtoto.
Unajua kinachoenda kutokea? Wewe utaanzisha familia na mwanamke mwingine, na mkeo nae ataanzisha familia na mwanaume mwingine..!!
Hapo mtawaweka katikati watoto wenu, wakiwa kwa baba wanakuta mama mwingine na watoto wake, wakiwa kwa mama wanakuta baba mwingine na watoto wake..!!! Hao watoto watakuwa na huzuni miaka yote.. 😥
Duuh! Pole mkuu... ila nakuhakikishia atakutafuta tu.... ni suala la muda tu...Hatuwasiliana toka siku kaondoa mguu nyumbani mkuu. Mama huyu ni jeuri kupita maelezo. Nilipata tabu kuzoea hii hali