Hawa ndio wana JamiiForums niliokutana nao

Hawa ndio wana JamiiForums niliokutana nao

Japokuwa Kwenye suala la Pesa ni kwl tunadanganyana mno ila kwakweli kwa usomi watu ni wasomi humu ndani wengi elimu yao aghalabu ni ya ngazi ya chuo....ukikuta mdada huku naye anajielewa msomi, huwezi fananisha jamii forums na Facebook au insta....Wasomi hapa wako......
 
1. Wote wana magari
2. Wote wana majumba yenye majina ya kizungu ie contemporary house, bungalow, crib, mansion na kadhalika.
3. Magari waliyo nayo ni ya gharama kubwa, hamna mwenye vits wala IST.
4. Elimu zao ni kubwa kama nyumba zao na magari yao.
5. Wote ni maboss
6. Wote ni wafanyabiashara wakubwa.
7. Wote ni watu wa safari sana, zile safari za nje ya bara letu.
8. Wote walizipeleka familia zao vacation
9. Wote wamesoma shule nzuri za kimataifa
10. Wote walikuwa wakali sana darasani.
11. Wote wana wenza wenye hela nyingi na wazuri sana.
12. Wote familia zao ni bora sana na zina upendo wa hali ya juu sana.
13. Wote wanatumia simu kali na za juu. Techno na infinix wanawapa walinzi wao
Wote wana access na mkuu wa nchi muda wowote watakao.

Usiwaamini mtu hapa jukwaani, watu wamechoka balaa.
Watu hawana ajira, wanapost kuwa wao ndio wana uwezo wa kuajiri.

Watu hawana mitaji lakini hapa wanajiita wafanyabiashara wakubwa.

Hawana pesa ya kulipa pango la nyumba, wanaishi kama digidigi kwa kuwakimbia wenye nyumba walizopanga, lakini wakiwa hapa jukwaani wanajiita Land lord.

Kuwa macho ndugu yako
giphy.gif
 
Sidhani kama ni haki sana kumrushia mawe na kumsimanga Bujibuji Simba Nyamaume , katoa yake ya moyoni kwa namna alivyochambua jinsi tunavyoji-mwambafy hapa JF. Thread zetu nyngi zimejaa majigambo na majisifu, matokeo yake tunakosa hata dili kwa sababu ya kujinyanyua sana kuliko tulivyo. Na hizi pseudonyms tunazotumia humu ndio zinaficha mengi. Yanaandikwa mengi ya ukweli na uongo, ni juhudi zetu kuchagua lipi ni lipi. Binafsi natoa ushuhuda huu kwa wana JF niliokutana nao!
  1. Nimepata marafiki wazuri na wabaya. Wazuri ninaendelea nao mpaka leo na wabaya tumepotezeana.
  2. Nimefanya biashara na wana JF kadhaa kunako 2015-2022, wengine bila kuonana sura, ni kuaminiana tu, mambo yameenda vizuri sana, nawashukuru wao kwa kuniunga mkono.
  3. Kupitia majukwaa mbalimbali, nimechota ujuzi mwingi sana, hasa lile jukwaa la ujasiriamali, kuna elimu nyingi sana mle. Nimewafuata wahusika PM mara kadhaa kuomba ufafanuzi na wamenisaidia sana.
  4. Nimalizie kwa kusema kwamba sometimes tunakosa mambo mengi ya manufaa kwa kuandika mambo feki na kuweka sifa zetu feki. Kama huna kazi sema huna kazi usaidiwe, kama huna kipato sema huna kipato upewe ideas za kutengeneza kipato nk. Otherwise JF ni jukwaa la muhimu sana kwa upande wangu najifunza mengi mno.
 
Kudai kwamba wote wako hivi au wote wako vile ni uongo. Ni uzushi.

Je, kati ya hao wanaJF ‘wote’ nawe umo?

Sijawahi kuona popote pale hapa JF ambapo kila mtu alisema ana gari au yeye ni bosi au sijui kasoma shule bora.

Hiyo ‘wote’ ni projection yako tu.

Acheni uzushi na uongo.
Mwambie huyo [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom