Etugrul Bey
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 6,514
- 15,247
Alhamdulillah ijumaa imeingia tayar na ningependa tukumbushane mawili matatu ili tujiweke tayari kukutana na hiyo siku ya Mwisho tukiwa tumeridhiwa na Mwenyezi Mungu.
Firdaus ndio pepo ya juu zaidi kuliko zote Kwa maana nyingine hii ndio pepo ambayo ni first class,na hii watairithi Mitume na Wacha Mungu.
Kwa taarifa yako Tu inasemekana zipo takribani daraja Mia Moja za pepo (100) na mkubwa wao ni huyo Firdaus.
Lakini cha kusikitisha zaidi pamoja na kuwepo hizo pepo zenye daraja takribani Mia Moja bado kuna watu hawatofanikiwa kuingia na matokeo yake wataingia motoni, Ewe Mwenyezi Mungu utujaalie tusiwe miongoni mwao Amiin.
Je watu wenye sifa gani ambao watairithi au kuingia katika hii pepo?
Kwa mujibu wa Qur'an watu wenye sifa hizi ndio ambao watairithi pepo hiyo;
WA Kwanza ni waumini ambao ni wanyenyekevu katika sala zao,hawa ni Wale ambao wanapokuwa ndani ya sala basi mawazo Yao na fikra zao zote zinakuwa ndani ya ibada ya swala,hawa hakika wamefanikiwa,
lakini kuna baadhi yetu wawapo ndani ya swala basi wanajikuta wanawaza hiki na kile na mambo kibao yanatawala swala yake,ingawa ni vigumu Kwa asilimia Mia moja kutotoka kimawazo,lakini hata ukitoka basi iwe kidogo na mara moja ujikumbushe kuwa upo ndani ya swala na ujue unawasiliana moja Kwa moja na Mola wako.
Sifa ya pili ni ambao wanajiepusha na mambo ya kipuuzi
Sifa ya tatu,na ambao wanatoa zaka,hapa inaingia na sadaka pia,maana zaka ni sehemu ya sadaka. Kwahiyo hakika kutoa sadaka ni Jambo muhimu Sana na ni ibada ambayo ina faida kubwa Sana,kuna maradhi mengine unapona Kwa kutoa sadaka Tu,
Na sadaka ndio ibada ambayo mja ataikumbuka mara Tu atakapoanza kutokwa na roho, ataomba Ewe Mwenyezi Mungu naomba walau unipe nafasi kidogo niweze kutoa sadaka. Sasa usisubir mpaka wakati huo ufike huenda usipate huo Mda wa kutoa sadaka.
Sifa ya nne, ni ambao wanazilinda tupu zao, hapa ndio wale wanachama WA jukwaa la MMU wajitafakari vizuri Sana,maana Yale mambo ya kulana kimasihara basi ujue nawe utaikosa pepo kimasihara,wazee wa Michepuko hapa kazi kwenu,hapa inakatazwa Zinaa Kwa nguvu zote,kwahiyo tujitathimini Sana.
Sifa ya tano,ni Kwa wale ambao wanazitimiza Amana zao na ahadi zao,kuna watu Jambo la kuahidi wanalichukulia kimchezo mchezo Tu,tena hawa wanasiasa hawa mjue Mungu anawaona! Maana nyie Kwa kutupiga sound hamjambo basi endeleeni Tu kutupiga sound halafu muone huko kwa Mungu kama mtafanikiwa.
Hapa Napo Jambo la Amana limeingia pia,mtu amekupa Amana yake umuhifadhie basi fanya hivyo usiingie tamaa ya kuitumia Bila ridhaa au idhini yake.
Na sifa ya sita ni Wale ambao wanazihifadhi swala zao,inamaana ambao wanadumisha swala zao siku zote,maana kuna watu huwa wanaswali ijumaa mpaka ijumaa Tu,au idi mpaka idi Tu,au akiwa na shida basi yeye ndio utamuona anaswali na mambo yake yakiwa fresh Tu basi ndio nitolee na kuswali bye bye.
Hope sauti yangu imetosha na kusikika vizuri kabisa.
Ijumaa Mubaraka!
Ni hayo Tu!
Firdaus ndio pepo ya juu zaidi kuliko zote Kwa maana nyingine hii ndio pepo ambayo ni first class,na hii watairithi Mitume na Wacha Mungu.
Kwa taarifa yako Tu inasemekana zipo takribani daraja Mia Moja za pepo (100) na mkubwa wao ni huyo Firdaus.
Lakini cha kusikitisha zaidi pamoja na kuwepo hizo pepo zenye daraja takribani Mia Moja bado kuna watu hawatofanikiwa kuingia na matokeo yake wataingia motoni, Ewe Mwenyezi Mungu utujaalie tusiwe miongoni mwao Amiin.
Je watu wenye sifa gani ambao watairithi au kuingia katika hii pepo?
Kwa mujibu wa Qur'an watu wenye sifa hizi ndio ambao watairithi pepo hiyo;
WA Kwanza ni waumini ambao ni wanyenyekevu katika sala zao,hawa ni Wale ambao wanapokuwa ndani ya sala basi mawazo Yao na fikra zao zote zinakuwa ndani ya ibada ya swala,hawa hakika wamefanikiwa,
lakini kuna baadhi yetu wawapo ndani ya swala basi wanajikuta wanawaza hiki na kile na mambo kibao yanatawala swala yake,ingawa ni vigumu Kwa asilimia Mia moja kutotoka kimawazo,lakini hata ukitoka basi iwe kidogo na mara moja ujikumbushe kuwa upo ndani ya swala na ujue unawasiliana moja Kwa moja na Mola wako.
Sifa ya pili ni ambao wanajiepusha na mambo ya kipuuzi
Sifa ya tatu,na ambao wanatoa zaka,hapa inaingia na sadaka pia,maana zaka ni sehemu ya sadaka. Kwahiyo hakika kutoa sadaka ni Jambo muhimu Sana na ni ibada ambayo ina faida kubwa Sana,kuna maradhi mengine unapona Kwa kutoa sadaka Tu,
Na sadaka ndio ibada ambayo mja ataikumbuka mara Tu atakapoanza kutokwa na roho, ataomba Ewe Mwenyezi Mungu naomba walau unipe nafasi kidogo niweze kutoa sadaka. Sasa usisubir mpaka wakati huo ufike huenda usipate huo Mda wa kutoa sadaka.
Sifa ya nne, ni ambao wanazilinda tupu zao, hapa ndio wale wanachama WA jukwaa la MMU wajitafakari vizuri Sana,maana Yale mambo ya kulana kimasihara basi ujue nawe utaikosa pepo kimasihara,wazee wa Michepuko hapa kazi kwenu,hapa inakatazwa Zinaa Kwa nguvu zote,kwahiyo tujitathimini Sana.
Sifa ya tano,ni Kwa wale ambao wanazitimiza Amana zao na ahadi zao,kuna watu Jambo la kuahidi wanalichukulia kimchezo mchezo Tu,tena hawa wanasiasa hawa mjue Mungu anawaona! Maana nyie Kwa kutupiga sound hamjambo basi endeleeni Tu kutupiga sound halafu muone huko kwa Mungu kama mtafanikiwa.
Hapa Napo Jambo la Amana limeingia pia,mtu amekupa Amana yake umuhifadhie basi fanya hivyo usiingie tamaa ya kuitumia Bila ridhaa au idhini yake.
Na sifa ya sita ni Wale ambao wanazihifadhi swala zao,inamaana ambao wanadumisha swala zao siku zote,maana kuna watu huwa wanaswali ijumaa mpaka ijumaa Tu,au idi mpaka idi Tu,au akiwa na shida basi yeye ndio utamuona anaswali na mambo yake yakiwa fresh Tu basi ndio nitolee na kuswali bye bye.
Hope sauti yangu imetosha na kusikika vizuri kabisa.
Ijumaa Mubaraka!
Ni hayo Tu!