Pre GE2025 Hawa ‘Wakimbizi walioteuliwa kwenye nafasi za maamuzi’ ni kina nani?

Pre GE2025 Hawa ‘Wakimbizi walioteuliwa kwenye nafasi za maamuzi’ ni kina nani?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kutokuwa na hofu kwa kutoambiwa kuna tatizo hakupunguzi ukubwa wa tatizo. CDF amefanya vizuri sana kulifanya Taifa zima kujua ukubwa wa tatizo. Hii itasaidia watu kutokuwa na maswali mengi Rais atakapochukua dhidi ya wahamiaji haramu ambao wamepewa madaraka, au pia kuuona wazi uzembe wa Rais kama hatachukua hatua.

Fikiria nchi inafikia kuwa na naibu waziri mkuu ambaye ni mhamiaji haramu ambaye hajawahi kuukana uraia wa wazazi wake. Alipokuwa waziri wa madini alifanya jitihada kubwa kuwapokonya leseni Watanzania kwa njia chafu na kuwapa wanyarwanda wenzake. Sasa ni naibu waziri mkuu na waziri wa nishati, je, tunafahamu atafanya nini?
Hii tafsiri yake ni kuwa Rais aliambiwa ila aligoma kusikiliza. na alichofanya CDF ni kumshitaki Rais kwa wananchi.
 
Jeshi halijaingilia siasa. Wahamiaji haramu ni suala la kiulinzi na usalama.

Ukiwa na wahamiaji haramu ambao umewaweka mpaka maeneo nyeti, siku kukitokea kutoelewana na mataifa mengine, wanaweza kutumika dhidi yako.
Mhamiaji haramu anaingiaje kwenye maeneo nyeti na kushika nafasi za maamuzi kama sio kupitia michakato ya kisiasa ambayo Jeshi halihusiki zaidi ya kuwa na taarifa?
 
Usikute nae anajihami Tanzania hatuna majina ya mkunda hapa upatikana Congo na Burundi atuambie asili yake wapi.
 
Sijapata kuona CDF poyoyo kama huyo.

Alishindwa kukaa na Amiri jeshi Mkuu akampa hizo habari za Kiintelijensia peke yake?

Nimemuona ni fala tu.
Kwa mara yakl kwanza Mrembo Faiza nakubaliana na wewe. Labda kama Rais ameamua kulitumia jeshi kisiasa kuwatisha watu wanaompa changamoto kwenye nafasi yake. Vinginevyo ni upoyoyo wa kiwango Cha juu kabisa
 
Bila ya shaka watakuwa wamepata somo la kupunguza kuropoka. Yaani watanzania walivyo na chuki na mafanikio ya wenzao huku ni kutoa sababu tu za kutaka kuona watu wa aina wafulani waonekane ni raia daraja la pili hawastahili kushika nafasi za uongozi.

Very irresponsible statement nchi zilizoendelea kwa kauli yenye kugawa jamii kama ivyo kwa nafasi yake kesho magazeti yanaanzisha harakati za kumtaka astaafu.

Jamani failures zetu za maisha katika uwanja ambao changamoto zetu zinafanana, mwingine akitoboa ni maarifa yake au baraka zake kutoka kwa muumba; sio tena kuwatafutia sababu hawastahili.

Huko Mtwara ni wamakonde wa Tanzania ndio waliokuwa wakiwaficha wenzao wa msumbiji; sasa tuitimishe wamakonde hawastahili kushika nafasi Tanzania, wakati tushakuwa na raisi wa kabila hilo.

Kwenye ili kamanda kapotoka, ile sio kauli ya kujenga nchi; isipokuwa ni ya kubomoa mshikamano wa nchi.
Sio kwamba anatumika kisiasa dhidi ya Samia?
 
Hii tafsiri yake ni kuwa Rais aliambiwa ila aligoma kusikiliza. na alichofanya CDF ni kumshitaki Rais kwa wananchi.

Siyo lazima iwe hivyo. Kuna possibilities 2:

Possibility ya kwanza ni kwamba CDF amekwishajadiliana na Rais, na huenda Rais anataka kuchukua hatua dhidi ya watu hao, hivyo CDF ametumika kutoa taarifa kwa umma ili watu fulani watakapoanza kuondolewa Serikalini, umma ysishangae.

Possibility ya pili, Rais ameambiwa lakini hachukui hatua, CDF ameamua kuuambia umma ili kuweka records kuwa yeye alitimiza wajibu wake, lakini Rais au alipuuza au kwa sababu tusizozijua aliamua kuwaachia watu hao wajipenyeze na kujiimarusha ndani ya Serikali.
 
na cognizant nitashukuru zaidi kama tu ukishamaliza kumtajia hao pia utawaja na wakuu wote wa vikosi ( hasa vya mikoani ) ambao wanaingiza vijana jeshini kwa rushwa mbalimbali na hutomsahau pia kumtaja na cdf mstaafu mmoja ambaye kwa makusudi na upendeleo aliamua kuwaingiza jeshini ( jwtz ) vijana wote wa mkoani na kijijini kwake na kuwataka wote watumie ubini wa jina lake la ukoo huku wakitamba kuwa uwepo wao na kwa idadi yao ni kikosi jeshi tosha na godfather wao huyo akisumbuliwa tu basi hawatasita kukinukisha vile vile ili mheshimiane / tuheshimiane hapa nchini
 
Kwa mujibu wa mkuu wa majeshi Gen Jacob John Mkunda amemueleza Rais kuwa Kuna wakimbizi wapo Hadi Serikalini na wamepewa nafsi za juu kabisa za kimaamuzi

Hili inashangza na kufikirisha Sana inakuwaje Hadi mkuu wa majeshi anawajua wakimbizi na wameteuliwa na wala hajawasiliana na mamlaka za uteuzi kuzuia uteuzi wao yeye amekaa kimya Hadi leo ndio Kuja kumueleza Rais by suprise.

Mimi najiuliza hivi Rais leo atapata usingizi Kweli? Atakuwa anajiuliza ni Nani huyu nimemteua ambae Ni mkimbizi?

Lazima Rais atapitia mafail yake kwa upya mnk kwa taarifa ya leo wa kamanda wake CDF kusema wasiwasi kuwa unawateua hadi wakimbizi inamaana kwamba wasaidizi wake wanamuingiza Chaka.

Anyway Kama Kuna kiongozi au afsa tunamuhisi siyo mtanzania mwenzetu Basi tumtaje hapa hajui kuwa siyo mwenzetu.

- Mtikila: Kagame amepenyeza Wanyarwanda 35,000 Tanzania, Burigi, katika Wilaya ya Muleba

Pitieni huu uzi
kama ni kweli, na sio "spinning inafanyika" Basi, huyu CDF, na Raisi wote ni vilaza, hili halikuwa swala LA kusema hadharani, una deal nao kimya kimya, hata matokeo huwa hayasemwi,
Mkuu wa majeshi na mkuu wa uteuzi, na wao wanalalamika! Seriously! Hii ni sawa na baba kwenye familia kusema, "najua binti yangu anabakwa, na wanaombaka wanaishi humu humu ndani! "
Ni uzwazwa wa Hari ya juu!
Au kama CCM imeamua kutumia jeshi, kufanya "spinning!" Unazua jambo,ili kuifsnya jamii iame kwenye Mambo ya msingi kuanza kujadili ishu unayoitaka,
CCM wanaweza wakapandikiza story"zuchu aachwa na Mond"au, Mond akamatwa kwa kutumia madawa ya kulevya"badala, ya kuonyesha jinsi jeshi lilivyojipanga kutatua matatizo ya ugaidi, uchumi, wamekaa na wao wanasubili uteuzi, kuongezewa salary, nk,
Sasa hv wanamega ardhi ya lugalo barracks, wanafanya flemu za biashara, baa za kuuza pombe, ,"kanisa katoric wamezindua chuo cha kisasa Mbeya, kwanini jwtz,wasijenge kiwanda cha Humvee, vifaru, spare za magsri,nk, kiwe kikubwa afrika nzima, kitoe ajira kama 200000!
Mnatengeneza vifaru, Silaa za, kivita, drones, au wajenge chuo cha kisasa cha sayansi na tekinolojia, kama NASA mnatoa kozi za uhandisi vijana wanaiva.
So pathetic
 
Tatizo watu kama ninyi huwa hatuwataki kwenye nchi sisi tunataka vilaza tu
kama ni kweli, na sio "spinning inafanyika" Basi, huyu CDF, na Raisi wote ni vilaza, hili halikuwa swala LA kusema hadharani, una deal nao kimya kimya, hata matokeo huwa hayasemwi,
Mkuu wa majeshi na mkuu wa uteuzi, na wao wanalalamika! Seriously! Hii ni sawa na baba kwenye familia kusema, "najua binti yangu anabakwa, na wanaombaka wanaishi humu humu ndani! "
Ni uzwazwa wa Hari ya juu!
Au kama CCM imeamua kutumia jeshi, kufanya "spinning!" Unazua jambo,ili kuifsnya jamii iame kwenye Mambo ya msingi kuanza kujadili ishu unayoitaka,
CCM wanaweza wakapandikiza story"zuchu aachwa na Mond"au, Mond akamatwa kwa kutumia madawa ya kulevya"badala, ya kuonyesha jinsi jeshi lilivyojipanga kutatua matatizo ya ugaidi, uchumi, wamekaa na wao wanasubili uteuzi, kuongezewa salary, nk,
Sasa hv wanamega ardhi ya lugalo barracks, wanafanya flemu za biashara, baa za kuuza pombe, ,"kanisa katoric wamezindua chuo cha kisasa Mbeya, kwanini jwtz,wasijenge kiwanda cha Humvee, vifaru, spare za magsri,nk, kiwe kikubwa afrika nzima, kitoe ajira kama 200000!
Mnatengeneza vifaru, Silaa za, kivita, drones, au wajenge chuo cha kisasa cha sayansi na tekinolojia, kama NASA mnatoa kozi za uhandisi vijana wanaiva.
So pathetic
 
Sio kwamba anatumika kisiasa dhidi ya Samia?
Ndio wajifunze sasa kuna taasisi azitakiwi kujiingiza katika cheap politics za wanasiasa. Hasa baada ya hii unintended outcome of somewhat ‘xenophobia’ iliyoibuka ghafla kutokana na statement ya hovyo iliyotolewa jana.

Amani yetu na kuheshimiana kwetu sio kwamba Tanzania ni nchi special, ipo ivyo kwa sababu wanasiasa na vyombo vya ulinzi walikuwa wanajua kuchunga kauli zao na za wengine kutoongea mambo ambayo yanayoweza gawanya watu au kuamsha hisia za chuki dhidi ya makundi mengine kwa miaka yote.
 
Hadi mwenye chama pia anahusishwa kuwa Ni muoman [emoji23][emoji23][emoji23]


Ila tuseme ukweli watanzania halisi kwa asili Ni wagogo tu

Ila pia wanasemaga malecela nae Ni mkongomani [emoji23][emoji23]
Mipaka iliwekwa, na wakoroni, jamii moja ikajikuta IPO Nchi mbili,mfsno Jaluo,Kenya na tz,mmsai Kenya na tz, sio dhambi,ukisema kama raia yoyote anayefanana na watu wa Nchi nyingine, aondoke, huo ni ujinga na upumbavu, vice president wa USA, baba mjamaika, mama Indian, kazaliwa USA!
Obama, Mama mzungu, baba M Kenya!
Trump, Biden wana asili ya Ireland, Biden alienda mpaka kijiji alichotoka babu yake, sie mi afrika bado, tunapalulana na kuchukiana kisa mie naitwa mkama, na Uganda wapo wanaoitwa mkama, au Mimi naitwa onyango,cha cha na Kenya wapo kina onyango, ni akili za kijinga Sana,
Dunia inategnenza uwezekano wa kwenda kuishi mwezini, sie tunabaguana kwa makabila!
 
Back
Top Bottom