Pre GE2025 Haya mabango ya Mama Samia kila kona, nani anagharimia? Yanatusadia nini kama nchi?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Ulaji huo,kama huyo bibi angekua anafanya vizuri kweli basi asingehitaji mabango nchi nzima ili kutukumbusha utendaji kazi wake .
 
Akili za watanzania, wamezoea misaada tu, hata bango anajiuliza linamsaidia nini
 
Hayana faida wala msaada wowote kwa mtanzania.

Zaidi yanadhihirisha uwezo duni wa kufikiri wa baadhi ya waafrika Tanzania ikiwa mfano.
 

Mabango ya sa100 ni mengi kuzidi hata kazi alizo fanya,ccm wanatumia nguvu nyingi sana kumnadi mana hauziki ni famba.
 
Ni bora hayo maeneo wangeruhusu wafanyabiashara waweke mabango ya biashara zao, wangeondoa gharama na kuingiza faida, alafu watambue kuna msimu wa kampeni sio kila mda ni mabango tu....hivi ni nchi gani ambayo walishawahi kuona kila sehemu kuna picha ya rais tena kwenye mambango? bongo bwana... hovyo kabisa.
 
Km yanakuudhi hamia nchi ya jirani. Huyo ndiyo Rais wetu yaliyoandikwa ndiyo ukweli wenyewe.
Kwa hiyo mnamfanyia kampeni ajulikane?🤣

Kwa hiyo yeyote anayempinga mpo tayari kumpora uraia wake
 
Waungwana husema Chema chajiuza....
Wanaojidai wamesomea propaganda eti wanadai wanamuuza ili kumfanya akubalike na kusifika kilakonaa Kwa kumjaza akilini mwa watu.

Wajinga hung'amua,wapumbafu husifu na kushangilia....
 
Maza Kama haoni kuwekwa kwenye mabango ni kumchora basi namshangaa zaidi yeye kuliko walioyaweka.
 
Kiasili mwanamke kaumbwa kudanganywa bibie hilo halijui ndo kwanza analegeza jicho!

Ukitaka kum-win mwanamke we mnadanganye na umsifie tu (mnafikie) aaah kwisha kazi!

Chawa ndo mida yao hii na watakupinga sana mleta mada bora chawa inajulikana ni njaa kuliko ccm nzima na wenye taaluma zao kusifia kasoro mpina wanamuona kama kaasi vile kisa ukweli wake!

Achana na bango omba zile za wachoraji kwa mkono ila usizicheke wanakosea makusudi!
 
nakuheshimu sana brother.
 
Simple tu kama wewe uko ktk mfumo na ni ded sehemu fulani unaangalia bajeti inasemaje una kaa kikao kazi na watu wako mnakuja na proposals ya kutumia hela kutengeneza bango la kumshukuru mama kwa kujenga hospital
 
Tunahitaji

1. Huduma bora za afya
2. Maji safi, salama ya uhakika
3. Umeme usio katikakatika
4. Miundombinu imara
5. Katiba mpya
6. Kushuka kwa mfumuko wa bei
7. Kudhibiti rushwa

[emoji625]
 
Ni kodi zetu
 
Sasa watazipigia wapi Kodi zetu zisipotumika kwenye takataka zisizo na tija kama hizi.
 
Atosheki kuanikwa kwenye maofisi ya serikali Hadi mabarabara nako.
Bango moja TU kuuzia sura si chini ya milioni moja kwa mwezi achilia gharama za kulitengeneza watu wanakufa kwa kukosa mia Tano TU ya Panadol ye anafurahia tu kuunguza Kodi zetu kuuzia sura nchini nzima sababu Kila kitu anapewa burre ajui hata Bei ya sabuni,nyanya.
Atoe za kwake mfukoni zitumike kuanikwa juani,kama maofisini hatosheki kuanikwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…