Haya ndio Mapinduzi ya Zanzibar, yamerikodiwa live na waitaliano 1964

Haya ndio Mapinduzi ya Zanzibar, yamerikodiwa live na waitaliano 1964


Bin Faza,

Salaam.

Mimi nimezaliwa Unguja,tena ni Stone Town/Baghani...na nikifia pale Unguja abadan sitazikiwa Kwerekwe!...na wala sina asili/sitokei ng'ambo,je una jingine!?

Nafikiri ushanifahamu uzuri kama kweli wewe ni Muunguja!?

Unaponambia ati nitofautishe baina ya Mtumwa na House Boy...mie najua uzuri tafauti iliyopo,sijui wewe mwenzangu!?

Ndo maana,kwenye ile post/s yangu kwa ndugu yetu Chabuso, pia nikanena yakuwa wakti mwingine yatulazim kuangalia majambo kwa utuvu wa kina na kitaaluma.

Kwa mtazamo wako wewe Sheikh Bin Faza,Mzanzibary khasa ni nani!?

Na mtu yupi khasa ana-qualify kuitwa Mtumwa tangia zama hizo pale Unguja!?

Lakini penye nilijualo tazungumza japo kiduchu.

Nakufuatilia bayana zako leo takriban wiki kadhaa. Wallahi,wafanza uzuri mno kutufumbua macho wenzio.

Nafikiri unachoharibu kiduchu,ni vile unapojaribu kila mara kuonyesha yakuwa wale Waarabu/ma-Sultan walikua ni kama vile Malaika wakti wa utawala wao pale Zanzibar!?

Usinifanze nikashindwa kukutafautisha na hao jamaa zako wa ki-bara/Watanganyika humu Jf...maana na wao wanawaona Wazungu kama vile ni nusu Miungu na kuwaabudu mno huku wakichukia Waarabu bila ya sababu zozote za msingi!?


Ahsanta
kwa kunisikiza.
Mkuu nakusoma kwa miwani ya 3D ha ha haa waereze waerewe.
ahsanta.
Cc Ritz
 
Yericko Yohana Msambila a.k.a "Yericko Nyerere".

Nakuona upo hapo chini...

Tafadhali nakusihi nenda ukanijibu yale masuali yangu nilikuoachia tangia jana kwenye ile thread yako.

Kama huna uwezo wa kujibu masuali ya Wanajamvi wenzio kwa kina,basi si uzuri kufungua thread/s na kujaza server/s humu Jf!?

Ahsanta sana.
Hata mimi nimemuona jf raha kila kitu hadharani napata ilm kutoka kwa Al akh Gombesugu:clap2::clap2::clap2: najua Yericko itamuuma !
 
Ritz huyu jamaa asikusumbue ana ugonjwa wa yule mjinga mwenzake Yericko unaitwa "amnesia" hasa kipindi hiki cha baridi ndio unawasumbua sana!

Mkuu wangu Boko haram, nimeishamwambia sioongei na mbwa naongea na mwenywe mbwa, mabwana zake hawapo kabakia huyo Yericko tu, Nguruvi3, Mag3, wameishamtosa, kama anayaweza aingie... analeta dharau eti uzi wetu umefungwa sababu yake yeye eti alihoji atukujiaandaa, teh teh, sisi kila siku uzi zetu zinafungwa tu wala kwetu siyo tatizo, kuandika uzi humu kunaitaji maandalizi gani uzi zimejaa kila kona, uzi zetu huwa ni hatari zinafunkika uzi zingine mpaka wao wanakuja.
 
gombesugu

gombesugu

Mkuu

hii yako ya leo kali kidogo, tumewasikia watanganyika wakimapaka matapo sulatan wa zanzibar kwa kila aina lakini hii nadhani unastahiki nobel prize mzee

inavojulikana kimataifa ni kwamba utumwa ulifutwa zanzibar rasmi katika 1886 -1896

sasa hao watumwa unawajuwa wewe waliokuwa zanzibar enzi za sultan iyupi tabidi tukuulize vyema yafuatayo

1. wewe umewahi kufika zanzibar, au uliogopa kwenda huko usije ukafanywa mtumwa?

Bin Faza,

Najua wewe ni msomi mkubwa mno tena ulobobea. Lakini menitia simanzi kiduchu,kuona zile propaganda za makhanatha ya Wazungu ati Utumwa ulifutika duniani/Zanzibar pale tu ati wao Wazungu walipokataza/walipoufuta...si kweli asilan!

Tunajua yakuwa Utumwa uliendelea kwa decades nyingi mbele ya lile tamko.

Mifano ni palepale Uk penyewe palikua na utumwa mwingi ukiendelezwa dhidi hata ya watoto under ages na families zao khasa kule Wales na Ireland.

Sasa kipi wewe kikuthibitishie yakuwa ati utumwa ulikwisha,pale tu Mwingereza/Wazungu walipotangaza au kusitisha!?

Kama wao Waingereza/Wazungu walishindwa kuzima huo utumwa na udhalimu ndani ya nyumba/Taifa lao,kipi kinakufanza wewe uone yakuwa their implemetation was so effective to that extent!?

Takupa mfano mwingine kiduchu;

Sehemu na pahala pengi mno khasa;some parts of Afrika,Indian sub-Continent,middle east, Carribean Islands utumwa uliendelea as early as 1950's...tena huku serikali ya Uingereza ikijua kwa yakini na kufumbia macho. Sababu wengi ya wale waliokua wanamiliki watumwa wale walikua ni familes very powerful/Aristocracies with inherited strong political connections and influences within the Uk and Amerika.

Ahsanta.

Historia ina utamu wake,

haya uloyaeleza humu si zaidi ya ukweli mtupu.

lakini pia ni ufahamu wangu kwamba wewe unajuwa jamaa wakisemea utumwa wanakuwa wanazungumzia stori za kunta kinte, yaani mtu kafungwa minyororo na kubebeshwa gogo mgongoni

utumwa wa aina hii ninahakika haukuwepo znz baada ya 1873 baada ya soko la watumwa kufungwa rasmi.

Pili nitakuomba ujuwe history ndogo tu ya znz inayohusiana na suala la utumwa.

katika mwaka wa 1896, kadhi mkuu wa zanizbar alikuwa ni Shiekh Ali Bin abdullah Al mendhiri. Kadhi huyu alikhitilafiana na Sultan Hamad Bin Thuwaini al saeed juu ya suala la watumwa, hatimae sulatan akaamua kufunga jela kadhi huyu kwa umri wake yeye sultan ilikuwa tarehe 22/08/1896, kwa bahati mbaya asultan alifariki baada ya siku ya tatu tu tarehe 25/08/1896. wazungu wakamtaka Hamud BinMuhammad Al Saeed awe sultan kinyume cha Khalid Bin Barghash alokuwa ndie mwenye haki. Khalid akachukuwa kiti kwa nguvu na znz ikaingia vita na Uk vita hivo vilidumu kwa muda wa dakika 45. ndio vita vya kijeshi vidogo zaidi duniani.

point yangu hapa ni kwamba ikiwa sultan alidiriki kumpeleka jela kadhi wake, ijuwe suala la utumwa lilichukuliwa very serious hapo znz.

sasa ninataka utuambie hao watumwa unaowajuwa wewe kwamba walikuwepo ndnai ya serikali ya kisultan hapo znz. Sifikiri kwamab wewe umezaliwa na kukulia ndani ya 1900s

ahsante
 
Chabuso,

Haina neno ndugu yangu. Natanguliza shukran zangu za dhati

Nakusoma kwa utuvu,pia nafuatilia bayana zako kwa utuvu.

Hiyo khabar ya wingi wa watu/sensa hapo Zanzibar...kuna khabar za kuthibitisha zaidi yakuwa Zanzibar wakti ilipokua himaya kubwa zaidi centuries nyingi zilizopita pia ndo ilipokua na watu wengi/population kubwa zaidi.

Population ya Zanzibar ilianza kuporomoka zaidi pale ile himaya ya Sultan ilipoanza kudhofu kwa fitna za Wazungu khasa Waingereza.

Nafikiri hatuna haja ya kuleta malumbano mengi,nami nakubaliana nawe yakuwa tumo hapa kujifunza soote kwa pamoja.

Naomba kukuuliza suali kiduchu,kama hutojali...je wewe watokea ndugu yangu Unguja/Zanzibar!?

Mimi nina watu/Wazanzibary nilowahi kuwaona kwa macho yangu binafsi ambao waliwahi kuwa Watumwa pale Unguja enzi za Sultan!?

Majina yao ninayo kibindoni mpaka kesho,na mpaka makaburi yao walipozikwa pale Unguja nayajua!

Labda tukubaliane yakuwa,tuna tafsiri tafauti yakuwa Mzanzibary khasa ni nani,na je Utumwa nao khasa ni nini!?

Au matendo gani/yepi yenye kuhalalisha mtu a-qualify kuitwa Mtumwa!?

Nafikiri hizi ni hoja zenye kuhitaji uchambuzi wa kina na unyambulisho wa kitaaluma!?

Ahsanta.

kaka wapi mimi natako haina umuhimu sana,lakini nitakwambia kuwa umejijibu mwenywe katika hapo nilipoweka red,na hicho ndicho kitu ninachojaribu kuongelea hapa

haya ninayoyaongea hapa nimesoma kwenye vitabu,nimefanya utafiti wangu mwenyewe,lakini namshukuru sana bibi yangu ukoo wake ulikuwa unatokea kisiwa kimoja kinaitwa Tumbatu pale Unguja kutoka na hadith zake alizozisikia kwa bibi zake na kutuhadidhia sisi wajukuu zake ndio nimepata picha kamili ya zanzibar na wazanzibari

kama umesoma vizuri hizi comments zangu nimeandika sehemu nyingi tu wako baadhi ya wazanzibar walikuwa wanamiliki watumwa lakini hakuna mzanzibari aliekuwa mtumwa,kwaufupi kama walikuwa watumwa basi wameletwa hao kutoka nje ya zanzibar,kama unawajua watumwa na unajua sehemu walipozikwa tayari nimeshajbu swala lako,kumbuka zanzibar lilikuwa soko kubwa la kuuza watumwa, watumwa walikuwa wakiletwa kutoka sehemu mbali za bara Afrika,sehemu kama kongo nk,mmoja kati ya wafanya biashara za watumwa alikuwa mswahili mmoja anaeitwa kwa jina la Tiptip huyu jamaa alikuwa na jeshi la watu 2000 ambalo alikuwa anaingia nalo ndani ya Afrika na kuchukua watumwa!!,Notorious

Nani wazanzibari nimeshaeleza kwenye moja za commets zangu,haina haja ya mimi kurudia kuandika tena hapa,Haya yote ninayoandika sio tu kama nimesoma bali pia ni history iliopo katika ukoo wangu,wazee wanaongea watoto tunasikiliza halafu tuna weka moja na moja tunapata jibu 😉

Sio kila mtu mweusi allikuwa mzanzibar na sio kila mwarabu alikuwa mzanzibari 😉
 
gombesugu

Historia ina utamu wake,

haya uloyaeleza humu si zaidi ya ukweli mtupu.

lakini pia ni ufahamu wangu kwamba wewe unajuwa jamaa wakisemea utumwa wanakuwa wanazungumzia stori za kunta kinte, yaani mtu kafungwa minyororo na kubebeshwa gogo mgongoni

utumwa wa aina hii ninahakika haukuwepo znz baada ya 1873 baada ya soko la watumwa kufungwa rasmi.

Pili nitakuomba ujuwe history ndogo tu ya znz inayohusiana na suala la utumwa.

katika mwaka wa 1896, kadhi mkuu wa zanizbar alikuwa ni Shiekh Ali Bin abdullah Al mendhiri. Kadhi huyu alikhitilafiana na Sultan Hamad Bin Thuwaini al saeed juu ya suala la watumwa, hatimae sulatan akaamua kufunga jela kadhi huyu kwa umri wake yeye sultan ilikuwa tarehe 22/08/1896, kwa bahati mbaya asultan alifariki baada ya siku ya tatu tu tarehe 25/08/1896. wazungu wakamtaka Hamud BinMuhammad Al Saeed awe sultan kinyume cha Khalid Bin Barghash alokuwa ndie mwenye haki. Khalid akachukuwa kiti kwa nguvu na znz ikaingia vita na Uk vita hivo vilidumu kwa muda wa dakika 45. ndio vita vya kijeshi vidogo zaidi duniani.

point yangu hapa ni kwamba ikiwa sultan alidiriki kumpeleka jela kadhi wake, ijuwe suala la utumwa lilichukuliwa very serious hapo znz.

sasa ninataka utuambie hao watumwa unaowajuwa wewe kwamba walikuwepo ndnai ya serikali ya kisultan hapo znz. Sifikiri kwamab wewe umezaliwa na kukulia ndani ya 1900s

ahsante

Bin Faza,

Wallahi,nimeipenda mno hii bayana yako na imenichekesha mno!ahaha!!

Yaani umeikumbusha enzi ile ya yule Halikuniki Bin Ngozi ngumu!ahaha!!

Tutazungumza kesho Al Sahib
 
Bobwe; wenye ile documentary ya Okello ni ya BBC hata mwandishi anajulikana. Angalia kuwa ni ya Black and white. Video zote mbili zimepiga tukio la siku moja hiyo hiyo. Uwezekano wa kikundi cha kiitalia 1964 kiwe na COLOR VIDEOGRAPHY halafu BBC wawe na black and white HAUPO.

Huwezi kusanya watu 500-600 chini ya mti wa kivuli ukaanza kuwafyatulia marisasi bila kutokea patashika ya baadhi kukimbia na kuondoka walipokuwa wamekaa. Hiyo video hayo marehemu wote hakuna dalili za kukimbia toka hicho kivuli cha huo mti

Zoom down kwenye image yenyewe tafuta wenye damu za marisasi zionyeshe!!!!!


By the way, umeona mitaa ya zanzibar? Hawa si walikuwa na ndege?

Mwisho ni kuwa usije-confuse kuwa sina huruma na wale waliopoteza maisha yao katika jambo hili. Nachokwambia na wote pia ni kuwa ukiona jambo chunguza. Aliyeiweka hiyo video pia ana yake. Mi namsikia tuu akisema "barbaric africans killing ARABS AND MOSLEMS" sijui hao waarabu ni dini ipi na waislamu ni kina nani!!!!

sasa mkuu unataka tufungue vitabu tisivopenda kuvihusisha na majadala huu, lakini kwa hilo sitofanya

however, the choice is entirely urs.............to believe or not
 
waarabu bado wana ndoto ya kurudi zanzibar kutawala wanasahau kuwa zanzibar ilikuwa soko la utumwa wao kwao ni Oman wasahau kabisa kurudi zanzibar hata muungano ukivunjika ndio watateswa zaidi maana waunguja bado wana usongo nao bila tanganyika mpemba asingekuwa rais wa zanzibar
 
rodrick alexander

waarabu bado wana ndoto ya kurudi zanzibar kutawala wanasahau kuwa zanzibar ilikuwa soko la utumwa wao kwao ni Oman wasahau kabisa kurudi zanzibar hata muungano ukivunjika ndio watateswa zaidi maana waunguja bado wana usongo nao bila tanganyika mpemba asingekuwa rais wa zanzibar

hivo ndio huwa ninawasikia wanasiasa wetu wakiboboja,

nani alokwambia sisi wazanzibar tunaproblem na waarabu?

hao waunguja unaowataja ni wa zainzbara ni ndugu zenu kutoka tanganyika.

ikiwa hujui Oman iko wapi kimaisha si utizame mitandao tu, mbona viongzi wetu wanakwenda kuomba oman kila muda, kwanini wasiende itali kwa mabosi wao kuomba?

baada ya muungano ikiwa oman itataka imrejeshe jemshid niambie wewe mtanganyika utafanya nini? au munauwezo wa kushindana na petro dola?????
 
warabu wapo busy sana...fikra zao na za ponda ni sawa..wameunga vipande....na wametafsiri km sheikh yahaya..kwao uongo ni sunnah
 
rodrick alexander



hivo ndio huwa ninawasikia wanasiasa wetu wakiboboja,

nani alokwambia sisi wazanzibar tunaproblem na waarabu?

hao waunguja unaowataja ni wa zainzbara ni ndugu zenu kutoka tanganyika.

ikiwa hujui Oman iko wapi kimaisha si utizame mitandao tu, mbona viongzi wetu wanakwenda kuomba oman kila muda, kwanini wasiende itali kwa mabosi wao kuomba?

baada ya muungano ikiwa oman itataka imrejeshe jemshid niambie wewe mtanganyika utafanya nini? au munauwezo wa kushindana na petro dola?????
mimi nina hamu sana muwe nje ya muungano lakini mkishatoka hatutaki wakimbizi kwani mtoto akililia wembe mpe bado mnawaza kuwa mkishakuwa nje ya muungano waoman watawafadhili kila kitu lakini huu muungano ndio unawafanya muwe huru kwani karume si alishaanza kuwashikisha adabu kama sio Nyerere wote ama mngeteketea au mngekimbia
 
Shukran sana;

1. Video ya kwanza yenye mauaji na maiti makaburini ni ya rangi. 1964 ni vigumu kikundi cha kiitalia kuwa na colored videography ya ku-shoot zenj

2. Ukiiangalia hiyo helikopta kuna mahali wanatupa kitambaa cheupe, Chanini?

3. Makaburini maiti wamepangwa na wengi wana kofia zao vichwani!!!!

4. Mtangazaji anazungumza Nyerere, Rais Tanzania wakati hakukuwa na Tanzania wakati wa Mapinduzi hayo

5. Maiti wote wameuliwa chini ya MTI wa KIVULI!!!!!!! wamelaliana bila dalili za kukurupuka kuhami maisha yao. Wamefia kivulini!!!!!!

6. Kaburi lilichimbwa siku gani? ya kupindua au kabla au baada? na ukiyaangalia yamefuatana.

7. Angalieni mengine na nyie.

Kwa taarifa yako hata kama video ilikua shot in black and white sasa hivi wataalamu wanaweza ku digitally remaster ili ziwe katika rangi. Vita kuu vyakwanza na vyapili, footage zipo in colour. Kwa hayo mengine naona niishie hapa maana naweza andika insha kukujibu.
 
mimi nina hamu sana muwe nje ya muungano lakini mkishatoka hatutaki wakimbizi kwani mtoto akililia wembe mpe bado mnawaza kuwa mkishakuwa nje ya muungano waoman watawafadhili kila kitu lakini huu muungano ndio unawafanya muwe huru kwani karume si alishaanza kuwashikisha adabu kama sio Nyerere wote ama mngeteketea au mngekimbia

hizo ni fikra za mitaani tu, ukweli huwa vyengine

and opposite is always true

wewe kaka ukija znz tutakupokea kwa mikono miwili
 
Kitoabu



Kiongozi hapa umekuja na hoja muruwa kabisa....

Lakini kumbuka Umma party sio waliofanya mapinduzi, Babu na Salim ahmed salim hata iwe vipi na wao walionekana ni waarabu katika macho ya ASP

Labda Abdullah Kassim hanga aliekuwa Prime Minister wa SMZ angepewa nafasi ya karume. Kassim Hanga alikuwa msomi mzuri sana pia. lakini badala yake alikufa katika mazingira ya kiajabu na kaburi lake halijulikani lipo wapi. wengi ndani ya ASP wanasema alifungwa mawe na kutumbukwiza chumbe.

Aboud Jumbe alikuwa msomi pia na alisoma pampja na nyerere huko makerere. Pia yeye alikuwa na uzoefu katika uongozi ndani ya serikali halali ya zannzibar alikuwa asifa mkubwa katika wizara ya elimu bado nyaraka zipo za mishahara yake. Jumbe akapewa uwaziri ndani ya SMZ hatimae raisi wapili baada kuuwawa kwa karume

mshahara wa jumbe siku za sultan
View attachment 100040

au hata mzee mwinyi alikuwa na yeye yumo ndani ya ASP msomi na alikuwa akifanya kazi na Mzee Jumbe huko huko wizara ya elimu ya sultan na yeye akaonekana hafai kwasabau ni msomi, akapewa uraisi baadae.

msharaha wa mwinyi siku za sultan
View attachment 100041

Jumbe na Mwinyi walikuwa ni wale walioitwa wazanizbara, kwahivo walikuwa na sifa ya kupewa uraisi wa serkali ya mapinduzi ya zanzibar in 1964, badala ya karume. Lakini waloyaunda mapinduzi hawakuta msomi kuwa Raisi wa znz siku hizo.

Kusema ukweli siasa ya znz baada ya mapinduzi ni chafu zaidi ya biashara ya utumwa wanayosingiziwa waarabu znz

Bin fadha uko juu tunakuhitaji zaidi na nakupa mia mia hii sentes yako ya mwisho umenena, na tunakushkuru kwa kuwaelimisha Wanafunzi wa Tanganyika historia yetu iliyosimama, yenye ukweli, bin fadha popote ulipo tunakuomba uanzishe blog,au forum tupungue kuasiriwa na historia hii iliyobuniwa baada ya mapinduzi, inashangaza sana kusema zanzibar waarabu walikua wanawatesa watu wakati hata vikundi vya Taarabu vinasherekea miaka 100 tangu vianzishwe.
 
Yaah! hakika ni uchambuzi mzuri, inawezekana ni CINEMA, je na hawa JOHN OKELO, ABEDI AMANI KARUME na MOHAMED BABU, PIA NI CENEMA. Je tunahoja za kuwakana hao. Wasi wasi ndio Akili. Sipingi uchambuzi huu (OBSERVATIONS). Ila tusiwe washabiki, kama ni changa la Macho, tulijadili kwa Maslahi ya Vizazi vijavyo.

Hiyo ya kina Okello na Karume na Babu ni ya BBC na hata mwandishi wake anajulikana kwa jina, sijawahi kuitilia mashaka
 
Nicholas

warabu wapo busy sana...fikra zao na za ponda ni sawa..wameunga vipande....na wametafsiri km sheikh yahaya..kwao uongo ni sunnah

Kwani sheikh yahya na yeye alikuwa mwalabu,

kwani kuna kosa mtu kuwa mwalabu?

kwani kuna kosa mtu kuwapenda waarabu?
 
Nyerere bila ya kuwagawa wazbr asingeweza kupitisha ukoloni wake z'br,kwa miaka ya hivi karibuni mbinu ya kuwaga z'br haifanyi kazi tena,watanganyika hata wafanye vipi hawawezi tena kuuficha ukweli,zanzbr kwanza porojo baadae.
 
babou

kitachosikitisha ni kitu kimoja tu nacho ni kwamba watu wasomi wanashindwa kutafautisha baina ya mapinduzi na massacre. 1964 kulifanyika mambo mawili

1. mapinduzi

2. massacre.

Tatizo la pili nanialiyefanya mapinduzi hayo.

1. Mipango yote ilitoka Ulaya na USA tunawajuwa kwa majina walioshiriki katika kupanga mapinduzi lakini siwataji humu.

2. Aloshika bunduki ni MTANGANYIKA. Hili ndio linalotukera sisi wazanizbari. Walituulia jama zetu wapatao 17,000 kwa usiku mmoja tu. Jesgi la tanganyika lilipewa mazoezi maalum huko Tanga na likapitia Bagamoyo kidogo kidogo kwenda kujipanga.

3. Ufunguo wa ghala za silaha alikuwa Kakabidhiwa Bwana Mohammed suleiman Mohammed Al Mfadhil, wiki moja hivi kabla ya mapinduzi akapokonywa na kamanda wake muingereza na kupewa mznzibara ambae alitakiwa awabidhi ufungu huo majeshi ya tanganyik amuda ukifika na alifanya hivo. Bwana huyo Mohammed ndie wakanza alouliwa

Sasa nadhani unafamu kwamba jitendo baya walilolifanya ni kuwatarget watu kwa kabila zao na rangi zao.

Nakwa hilo hatuwasamehe watanganyika maisha na musituone kimya lakini litasemewa hilo wakati wake ukifika

Daaah ! Hii kesi ya mauaji ya kimbari umewauzia Watanganyika ?
We nI nouma aiseeh !.....tafuteni sababu nyingine ya kuvunja muungano bana !
 
Kwa taarifa yako hata kama video ilikua shot in black and white sasa hivi wataalamu wanaweza ku digitally remaster ili ziwe katika rangi. Vita kuu vyakwanza na vyapili, footage zipo in colour. Kwa hayo mengine naona niishie hapa maana naweza andika insha kukujibu.

Benz; Ahsante Nakushukuru. Ninazo baadhi ya documentary zilizowekwa rangi kwa mtindo unaosema. Lakini huwa hazina "LUSTER" kama original pictures.

Zanzibar Revolution 1964 - YouTube

Ile video ya kwanza ndio hii hapa wanaanzia uwanjani. Waligundungua hawajaweka hata sound tracks ndio wakaanza tena editing na kuingiza sauti ya kiitalia nk. Benz, hizo rangi za hiyo ndege mzee wangu ni original siyo digitally remastered na 1964 hakukuwa na camera za megapixels kama za sasa. Hawa ni waitalia 1964, wao wana color video graphy BBC hawana!!!

Kule makaburini wanaranda na HELIKOPTA!!!! sio ndege tena hii sijui waliiacha wapi maana uwanjani ilkuwa zogo.
 
Back
Top Bottom