Haya ni makampuni makubwa miongoni mwa 400 yanayowekeza mabilioni ya dola nchini Israel kwajili ya Utafiti na Ubunifu (Research and Design)

Haya ni makampuni makubwa miongoni mwa 400 yanayowekeza mabilioni ya dola nchini Israel kwajili ya Utafiti na Ubunifu (Research and Design)

Jifunze kuangalia positive side punguza sumu ya negative thoughts, vitu vingi unavyotumia kuanzia simu, laptop, google, whatsapp, facebook, n.k. vinafinyiwa utafiti na maboresho Israel. ukiumwa ukienda hospitali kubwa kufanyiwa vipimo vya kisasa utapimwa kwenye mashine zinazoboreshwa Israel.
UONGO HUO KABISA, Makampuni 400 yapo kijiji gani, Israel ni u aguzi mtupu ndio alete mkorea mjapani, nina jamaa yangu yupo Chimendeli Dodoma ananiambia hao watu ni kilimo cha umwagiliaji, na madawa tu
ubunifu ni Misri na Iran wanacheza na nyuclia atom nk
 
Tatizo la madogo wa miaka ya 2000s hampendi kabisa kusoma kutafuta ukweli. Unafaham faham english hata Kidogo?
PAta hizi DATA hapa. Mwambie mtu ambaye angalau anajua kiingereza akusaidie.
Mimi sio muhumini wa data za design za namna hii. Mlituaminisha na da za namna hii na mkasema Russia hatatoboa katika vita ndani ya miezi mitatu.

Mambo ya kijeshi yana siri mno, sio ya kukuta kwenye makaratasi ya namna hii
 
Mimi sio muhumini wa data za design za namna hii. Mlituaminisha na da za namna hii na mkasema Russia hatatoboa katika vita ndani ya miezi mitatu.

Mambo ya kijeshi yana siri mno, sio ya kukuta kwenye makaratasi ya namna hii
Basi dogo kweli hujui kitu. Russia alisema HII OPERATION ANAMALIZA NDANI YA WEEK. AU NIKUPE REFERENCE?NA ALISEMA SIYO VITA NI OPERATION. HEBU ULIZA SASA NI MUDA GANI. YAANI ASITOBOE MIEZI MITATU KWA KANCHI KAMA UKRAIN? HAKO SI NI SIKU 5 TU ANAMALIZA? UNGEKUWA UNAJUA KIINGEREZA au unakaa na watu wenye akili ungejifunza. Hapa tena unaleta Russia vs Ukraine ambayo nayo huijui. 😁
 
Mimi sio muhumini wa data za design za namna hii. Mlituaminisha na da za namna hii na mkasema Russia hatatoboa katika vita ndani ya miezi mitatu.

Mambo ya kijeshi yana siri mno, sio ya kukuta kwenye makaratasi ya namna hii
PUtin alisema ni threed day special operation. Una elimu gani? Mwambie mtu akutafsirie hapo. Leo ni muda gani?😁
 
Historia ya wana israel ni wabunifu sana na wazuri ktk sayansi,teknolojia ndio mana mataifa makubwa mengi wana watu wao israel kwa ajoli ya ubunifu, yani hmaambiwa hz satellite hzbkila nchi inaweza tengeneza lkn ili iruke juu kule lazima umuone muisrael kama vike gari utatengeza lkn lazima uweke mafuta ili litembee sasa hati miliki ya chip anayo muisrael hawa jamaa achana nao wako vzuri sana tafuteni taarifa sio kubisha bisha bila sababu.
Kwamba chip ni za isreali kha mbona kali ya mwaka hicho kiwanda kinaitwaaje sasa
 
Update: Nimeleta habari za kisomi nashangaa kuna watu wameanza kuingiza mihemko ya kidini, Tatizo nini ?

Katika kampuni za teknolojia, idara ya Utafiti na Ubunifu (Research and Design) inahusika na kubuni na kuendeleza bidhaa, huduma, au teknolojia mpya kwa kutumia maarifa ya kisayansi, ubunifu, na mbinu za kisasa. Hii ni moja ya idara muhimu zaidi katika kuhakikisha kampuni inabaki kuwa na ushindani sokoni.

Why Israel - Israel wanapenda sana kusoma na kuitafiti science ndio maana watu wenye asili ya Israel wameshinda noble prizes za science nyingi kuliko kundi lolote duniani, Makampuni yamewekeza kwa watu wabunifu na wanaopenda sayansi.

Kila kinachobuniwa kinakuwa ni mali ya kampuni, wanaobuni huuza ujuzi wao kwa malipo ya pesa.

Samsung (Korea)- Kampuni hii ya Korea Kusini inafadhili miradi ya utafiti inayolenga teknolojia za simu na vifaa vya kielektroniki.

Intel (Marekani) - Kampuni ya teknolojia inayojulikana kwa utengenezaji wa microchips inayoendesha vituo vikubwa vya utafiti na maendeleo nchini Israel.

Huawei (China) - Kampuni kubwa ya teknolojia inayowekeza katika utafiti wa mawasiliano ya simu, akili bandia, na maendeleo ya teknolojia ya 5G.

Google (Marekani) - Inayo kituo cha utafiti kinachoshughulikia teknolojia za utafutaji, akili bandia, na usalama wa mtandao.

Ericsson (Sweden) - Inashiriki katika utafiti wa mitandao ya simu, teknolojia za wingu, na huduma za data za kasi ya juu.

Sony (Japan) - Inawekeza katika teknolojia za picha, sauti, na akili bandia kwa ajili ya bidhaa za kielektroniki.

Microsoft (Marekani) - Ina kituo kikubwa cha Utafiti na Ubunifu kinacholenga maendeleo ya programu na huduma za wingu (cloud services).

Siemens (Ujerumani) - Inawekeza katika teknolojia za viwandani, nishati mbadala, na mifumo ya afya yenye akili.

Apple - i phone (Marekani) - Ina kituo cha utafiti nchini Israel kinachobobea katika maendeleo ya chip za kisasa na teknolojia za vifaa vya rununu.

Nokia (Finland) - Kampuni inayojikita katika utafiti wa miundombinu ya mawasiliano ya simu, hususan 5G na IoT (Internet of Things).

Meta - Fb, Insta na Whatsapp (Marekani)- Inawekeza katika teknolojia za akili bandia, ukweli halisi (VR), na usalama wa data.

Fujitsu (Japan) - Kampuni ya teknolojia inayofanya kazi kwenye maendeleo ya supercomputers, huduma za wingu, na usalama wa mtandao.

Amazon (Marekani)- Inayo timu za utafiti nchini Israel zinazojikita katika teknolojia za wingu, biashara mtandaoni, na usalama wa mtandao.

NVIDIA (Marekani)- Kampuni inayoongoza katika utengenezaji wa GPU na akili bandia, ikiwa na kituo cha maendeleo nchini Israel.

Philips (Netherlands) - Inalenga maendeleo ya teknolojia za afya, vifaa vya uchunguzi wa matibabu, na suluhisho za taa za kisasa.

Cisco Systems (Marekani)- Inawekeza katika teknolojia za mitandao na usalama wa mtandao kupitia vituo vyake vya utafiti nchini Israel.

IBM (Marekani)- Inashirikiana na wataalamu wa ndani nchini Israel kuendeleza teknolojia za kompyuta zenye akili bandia na uchakataji wa data kubwa.
CHawa wa mama (Tanzania) - Inashirikiana indirectly na mvaa miremba wa Tanzania kwenye kutafiti vijishughuli mbalimbali vitakavyosaidia kula pesa za wananchi wasiojitambua na kumpumbaza yule bibi ushungi.
 
Back
Top Bottom