Hayati Dkt. Magufuli anapohukumiwa kwa kifo chake

Hayati Dkt. Magufuli anapohukumiwa kwa kifo chake

Magufuli asafishiki hata iweje kaua watu mno yule mzee..na ndo kitu kinachofuta mazuri yake
 
1.All in all, mtu huyu hatetembea tena kwenye uso wa dunia.
2. History lazma iandikwe ili watoto wetu wajue yawapasa kutenda yapi wanapopata madaraka
3.Kibinadamu ni vigumu sana kutokujisikia ahueni kwa kifo cha mtu aliyetulazimisha tumwabudu
4. Mungu anisamehe kwa namna furaha inavyojaa moyoni nikikumbuka kifo cha huyu bwana,....yaan ilifikia mahala ilifikia watu wakamfananisha na YESU.
 
LoL! The man is gone. Na ameshasahaulika. Learn to live with that reality! Ameenda na hatorudi!
 
Nafura unapojenga hoja. Kaini asingeweza kuuwawa na wazazi wake. Wakati huo alikuwepo Adam na Eva, pamoja na watoto wao wawili. Hivyo bado adamu aliendelea kuzaa si kwamba hakuendelea kuzaa, hivyo kizazi kingeendelea. Swala la kutouwawa kwa Kaini lilikuja baada ya Kaini mwenyewe kumlilia Munguhuku akiomba msamaha na kusema takuwa na maisha ya namna gani kwa hilo alilolitenda. Aliona atakoswa ushirikiano k
Nashukuru kwa kile ulichoeleza, na kile ulichoniongezea ambacho sikuwa nacho.

Lakini pia nakupongeza kwa kutokuhamaki wakati wote wa michango ya kila mmoja.

Wazo muhimu, wanadamu tumeaswa kutokuhukumu tusije tukahukumiwa. Andiko jingine lasema, hata tuwe na dhambi kubwa namna gani, tukiomba toba iliyo njema, tunapata msamaha kamili wa dhambi zetu kwa kuwa bwana wetu ni mwingi wa huruma na msamaha, si mwepesi wa hasira.

Juu ya marehemu, tunaweza kusema alifanya hiki kibaya na kile kizuri, lakini hatuwezi kusema ndiyo sababu ya kifo au kuishi kwake maana waovu na wema, wote hufa na wote huishi. Na kuna wakati waovu huishi zaidi kuzidi hata watu wema.

Yu wapi huyo ndugu yetu, miongoni mwa watakatifu au la, hutegemea hekima ya Mungu na maisha yake au ya kila siku, au dakika yake ya mwisho. Tukumbuke mfano wa Yesu juu ya mshahara wa wafanyakazi, mwingine aliyeanza tangu asubuhi na mwingine dakika za mwisho, lakini wote walipata mshahara mmoja. Hata kama tukayajua yote mabaya ya marehemu (jambo ambalo si rahisi), hakuna ajuaye dakika yake ya mwisho alimwambia nini Mungu wetu aliye mwingi wa msamaha.

Kifo ni ibada kwa tuliobakia, ni ujumbe mkuu kuwa siku moja nasi tutakufa. Tutakufa namna gani, ni fumbo. Kufa kwa mateso makubwa au bila mateso, siyo uthibitisho wa maisha yetu kuwa mema au mabaya. Kuna wakati watu wema hufa kwa mateso makali kuliko waovu, ili mateso yao yawe sadaka kwaajili ya wengine. Hivyo ni kosa kufikiria kuwa kila afaaye kwa mateso makali, basi alikuwa mdhambi mkubwa - nje kidogo ya mada.

Wale ambao maisha yao yalikuwa katika hatari ya kifo, mateso na dhuluma, na wengine wakamlilia Mungu, wana kila sababu ya kumshukuru Mungu pale anapowaondolea hatari hizo kwa namna yoyote iwayo. Hawa hawamhukumu mtu bali wanamshukuru Mungu kwa wema na ulinzi wake na kwa kuwa amewapa nafasi ya kuishi kwa amani na matumaini yaliyo hai.
 
Haya ayanihusu, naongelea binadamu kuhukumu. Sijaja hapa kuongelea Lisu au sijui Ben Sanane, kama unahitaji kuwaongelea toa mada zinazowahusu. Nachofahamu Mungu uona kwa jicho la tofauti! Mungu wetu ndiye anae hukumu na kusamehe, mimi ni nani nichukue mamlaka ya Mungu? Kaini aliuwa bado mungu akampa ulinzi. Soma mada vizuri.
Mkuu usiminyane Magufuli amekufa
Full stop
 
Nyie mnachuki pum.vu aliwanyoosha kwa wizi wenu shangilieni maana Sasa hayupo wa kuwazuia kuiba

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Furahi nafsini mwako maana umeweza kutukana.

Sisumbuliwi wala kuteseka kufikiria namna ya kumjibu anayetukana. Nateseka na kulazimika sana kutafakari mtu anapotoa hoja.

Anayetukana ni dhahiri, hana chochote cha kujenga moyoni na akilini, ni wa kuonewa huruma kuliko kumchukia.

Ujaliwe hekima, japo ndogo sana, ili uwepo wako Duniani uache hata kitu kidogo cha kuwajenga.
 
Haya ayanihusu, naongelea binadamu kuhukumu. Sijaja hapa kuongelea Lisu au sijui Ben Sanane, kama unahitaji kuwaongelea toa mada zinazowahusu. Nachofahamu Mungu uona kwa jicho la tofauti! Mungu wetu ndiye anae hukumu na kusamehe, mimi ni nani nichukue mamlaka ya Mungu? Kaini aliuwa bado mungu akampa ulinzi. Soma mada vizuri.
Usiangaike nao hao, maneno yamewachoma. Kwa hiyo wanajibaraguza!
 
Kifo ni tukio la kiasili. Katika imani kadhaa za kidini zina elezea kifo kilitokea baada ya Adamu na Hawa (Eva) kwenda kinyume na mapenzi ya muumba wao (MUNGU). Ndipo Mungu alitamka kuwa tutakufa, au kurejea katika mavumbi.
Binadamu wa kwanza kufa alikuwa Abeli. Ambaye aliuliwa na kakaye aitwae Kaini. Kaini japo alimuuwa Abeli, bado Mungu alimlinda Kaini na hata
Itoshe kusema tu, wew ni sukuma gang. Jiwe alishakufa kutokana na ujuaji uchwara wake.
 
Mada yangu haiongelei hao watu, naongelea mtu kuhukumiwa, je sisi binadamu tuna mamlaka ya kuhukumu? Hata kama mtu alifanya makosa? Soma uelewe mada usikurupuke. Ndo maana nikasema hata Kaini aliuwa kwanini Mungu bado alimlinda Kaini? Watu wengi ukurupuka wajui mada inachosema. Lakini pia hao unao wataja unaushahidi kuwa Magufuli aliwauwa? Mbona kumekuwa na tuhuma za Ben Sanane kuuwawa na Boss wake, Kumekuwa na tuhuma alie kuwa Makamu mwenyekiti wa Chadema kuuwawa na Mwenyekiti?
Lakini watu wangapi wamepoteza maisha nyakati za uongozi tofauti? Hii haiwezi kukufanya uhukumu. Anae hukumu ni Mungu pekee!
Alikuwa na mamlaka ya kuunda tume ya kijaji kufuatilia matukio haya ambayo yalikuwa na public interest, he never did that, now will you tell us the motive behind! Makosa yapo ya kutenda na kutokutenda yote yaweza kuwa makosa.
 
Yeye mwenyewe alijisababishia hayo matokeo kwahiyo kama ni lawama ni zake mwenyewe hivyo mleta uzi usitafute wa kumlaumu,
Kama alivyosema Mzee Mwinyi kuwa "maisha ya duniani ni sawa na hadithi tu hivyo kuwa hadithi nzuri kwa hao watakaosimuliwa" hii maana yake utakavyoishi ndivyo utakavyosimuliwa kwa watu wakati wewe haupo umeshatangulia mbele ya haki.
Maisha ya bongo wakati mwingine yamejaa unafiki watu wapo tayari wakusifie kwa sifa za uongo ili mradi wapate wanachokitaka kutoka kwako hivyo mtu akili kichwani mwako.
 
Hakuna sehemu aliyosafishwa, na siko kusafisha, bali naongea wazi hakuna chuki ya marehemu duniani. Kujenga chuki kwa mtu alokufa nadhani ni kutokuwa na akili za kufikiri. Nimeongelea kifo chake na yasemwayo kwa hicho kifo. Sasa nimsafishe kwa nani?
Nyie ndo mtakao kufa vifo vya ajabu na vibaya! Wewe si Mungu kuhukumu!
Sasa nimtetee Magufuli kwani anagombea uRais. Soma uelewe mada chuki zako usikimbie na kuandika tofauti ya mada.
Napenda kukukumbusha utakufa pia, je umetafakari maisha yako?
Sasa mbona wew ndiye mwenye chuki, unasema tusihukumu ili hali unasema jamaa atakufa kifo cha ajabu. Wasukuma bhan, hata mkizeeka bado mnakuwa vile, mkipewa madaraka mnakuwa kama Jiwe.
 
Kifo ni tukio la kiasili. Katika imani kadhaa za kidini zina elezea kifo kilitokea baada ya Adamu na Hawa (Eva) kwenda kinyume na mapenzi ya muumba wao (MUNGU). Ndipo Mungu alitamka kuwa tutakufa, au kurejea katika mavumbi.

Binadamu wa kwanza kufa alikuwa Abeli. Ambaye aliuliwa na kakaye aitwae Kaini. Kaini japo alimuuwa Abeli, bado Mungu alimlinda Kaini na hata akasema atakae muuwa kaini basi atalaaniwa. Hivyo Mungu alimpeleka Kaini nchi ya mbali. Hii yote kumuepusha na kumlinda na mabaya. Mungu alifanya haya yote japo Kaini alikuwa na dhambi ya kumuuwa nduguye.

Mungu utazama tofauti, na macho ya binadamu. Na Mungu ndiye mwenye uweza wa kuhukumu. Siku hizi Tanzania hii kumezuka, tabia ambayo inaonesha watu kufurahia kifo au vifo vya watu wengine. Na kama walikuwa hawampendi huyo mtu au watu; ndo watazusha mengi. Wabaya wake watajifanya wao ni mungu (Mungu), watahukumu, watasema huyu alifanya mabaya ndo maana kafa.

Watajiona wao waliobaki ndo wajanja, hawana makosa au dhambi mbele ya Mungu. Najiuliza hivi kuna mahala popote pale iwe katika misaafu au maandiko yoyote ya kidini na imani zinginezo, pana sema mtu anae kufa mapema au kabla ya wenzie ana dhambi na Mungu kaamua kumkomoa?

Nachojua Mungu alisema tutakufa, hakuna atakaeishi milele hapa duniani. Ndo maana watu ufa wakiwa watoto wachanga, wakiwa vijana, wakiwa wazee, na hata watoto wengine ufia tumboni mwa mama zao kabla ya kuzaliwa.

Tukidai kufa mapema ni kukomolewa na Mungu, ebu tuangalie, hawa mitume wetu, walikufa bado wakiwa vijana, na walikuwa na maadui wengi, hawakupendwa. Yesu kristo aliishi miaka isiyozidi thelathini na tatu. Na alianza kazi ya kuhubiri akiwa na miaka thelathini tu. Vile vile kwa mtume Muhamad S.W.A alikufa mapema. Si hao tu ni wengi!

Hivyo kifo ni asili. Nachoamini kila mtu anakusudi la kuwepo duniani. Na pia ana muda wake wa kuishi. Haijalishi ni miaka mingapi. Muda ukifika Mungu ndo mwamuzi wa yote, uondoke au aseme bado ubaki.

Katika kila jambo Mungu anamakusudi yake. Laweza kuwa baya au zuri, lakini Mungu anatazama tofauti na tunavyotazama sisi wanadamu.

Kikubwa tusijipe kazi ya Mungu ikawa kazi yetu. Tusijipe kuhukumu kwani hukumu ya maisha yetu utolewa na Mungu. Usihukumu usije hukumiwa.

Nimeongea haya yote ni kutokana na watu wengi, wapinzani na wana CCM kuonekana kumhukumu alie kuwa Rais wa Tanzania, J.P. Magufuli na hata kumzodoa kuwa kafa mapema, yako wapi, kuonesha tu Mungu ati kamuondoa kwa mabaya yake. Nilishangaa hata Mchungaji mmoja anajiita mzee wa upako kuongea kama vile nae anaonesha kufa kwa magufuli ni kama adhabu, eti kisa Lowasa hakuchaguliwa Urais na kuwataka watu wakamuombe Msamaha Lowasa.

Mimi niseme kwa maandiko viongozi wote wakuu wa nchi uwekwa na Mungu. Mungu angeamua Lowasa kuwa Rais angekuwa tu. Mchungaji kasahau maandiko anatumia akili za kibinadamu. Kufa kwa Magufuli si kwamba Mungu hakutaka Magufuli awe Rais, la asha. Mungu hutenda kwa wakati wake.

Jiulize katika maandiko tunaambiwa kuwa Yusufu aliuzwa utumwani na nduguze, bado huyo Yusufu akafungwa gerezani. Lakini cha ajabu akaja kuwa ndiye waziri mkuu wa nchi. Hata nduguze walipojihisi atalipiza kisasi kwa kuwafanyia mabaya, aliwaambia. Mlikusudia mabaya kwangu, lakini katika hayo mabaya Mungu alikusudia mema ili nije niwaokoe katika baa la njaa.

Mungu uona mbali zaid ya binadamu. hatujui ni kwanini Mungu aliepusha Lowasa asiwe Rais japo ilitumika njia mbaya au nzuri, lakini Mungu anakuwa na makusudi yake. Mchungaji katafakari neno la Mungu ndo utoe tamko. Hakuna lifanyikalo duniani bila Mungu kuridhia. Mungu huyo aliruhusu Ayubu apate mateso, akaruhusu watoto wake Ayubu kufa na hata mali kuharibika na kupotea lakini alikuwa na kusudi. Kifo cha Magufuli kinakusudi liwe baya au zuri ila watanzania tutajifunza kutokana na hicho kifo siku moja. Kikubwa tusijichukulie mamlaka ya kuhukumu na kusema kafa kwa sababu alikuwa katiri na kadharika. Mbona Mungu alimlinda Kaini japo alikuwa muuwaji?

Hivi kazi yetu ni kuhukumu, kwani tuliobaki hatutakufa? wangapi tumefiwa na ndugu na wazazi, je kutangulia kwao ni kwamba walitenda mabaya Mungu kawahukumu? Kwa uzoefu wa haraka tu mara nyingi watu wema hawadumu? Iwapo hadi sasa unaishi lazima ujiulize, unatakiwa kulifanyia nini Taifa lako la Tanzania, na familia yako. Si kushambulia marehemu, na kujifanya wewe ni mungu unahukumu. Leo hata viongozi wetu utasikia, oooh! Magufuli hakutenda haki, alikuwa kiongozi mbaya, alikuwa muuwaji, alitisha, hakuwa na demokrasia!

Hivi ninyi viongozi mnao sema haya si mlikuwa nae ktk uongozi wa serikali? Kwanini amkumwambia wakati huo akiwa hai kuwa ni kiongozi mbaya.

Nacho jua Magufuli alikubali kukosolewa. Naibu Waziri wa afya kipindi hicho alimkosoa kuhusu matumizi ya kujifukiza. Akamwondoa katika nafasi. Lakini baadae alimrejesha ktk wizara tofauti.

Leo wanao mkosoa magufuli haohao, wanapinga Mhe. Rais Samia kukosolewa. Wakati Rais alidai kuwepo uhuru wa kukosoa. Lakini chama chake na Bunge Wanataka asikosolewe, tumsifie hata kwa yale yasio sifiwa. Wakati wanadai wao ni wanademokrasia. Ukikosoa unahesabika msaliti, Bunge litakuita kwenye Kamati. Chama kitakaa kukuita kikuhoji kwa nini huko kinyume na Rais. Chama kinachoongozwa na mwenyekiti ambae ni Rais alie ruhusu kokosolewa.

Mungu hapendi wafitini na watu waongo, wenye roho za usaliti. Viongozi mjitafakari. Na msijione ninyi hamta kufa. Kifo kipo akijali madaraka yako. Hakuna atakae ishi milele. Kuwepo kwako pengine Mungu anataka utimize mambo fulani. Ghazabu ya Mungu ni kubwa tusihukumu tukaja hukumiwa. Magufuli kaondoka kamaliza yake. Alifanya kwa nafasi yake na kwa staili yake. Watu wote hatufanani.

Tusijione sisi ni bora kwakuwa tu watu wanatuchekea na kutusifia. Tukachekelea na kuota kiburi kuona tuko sahihi na hatukosei! Pamoja na yote Magufuli aliwapenda watanzania. Hakuwahi kusema waondoke wakaishi Burundi.

Leo kauli hiyo inaongewa na kiongozi aliepewa dhamana na watanzania. Viongozi wamejiona wako juu ya sheria, wanauwezo wa kusema chochote. Viongozi wamekuwa na dharau. Wanajiona nchi ni yao. Hata wananchi kulalamika hawaoni haja ya kuomba msamaha.

Hata kiongozi wa nchi hawakanyi anawaacha je naye kafurahishwa na hayo maneno? Je kawatuma?
Harafu hawa hawa ndo wanasema watakuwa wapole na kuwabembeleza wananchi kuliko JPM ambaye kapewa mabaya yote.
Tukumbuke kutangulia kufa si dhambi. Na ukibakia si ujanja wa kufanya kutukana waliotangulia. Bali chukua muda wa kujitafakari.

Mungu alimlinda Kaini japo alikuwa muuwaji wa nduguye. Mungu ndiye mwenye kuhukumu. Na ndiye ajuaye mwisho wa maisha yetu. Jiulize hapo ulipo matendo uyafanyao ktk vificho au wazi, je ni mema? Je wewe ni msafi zaidi ya waliotangulia kufa?

Je, wajua kifo chako kitakuwaje? Lini utakufa? Je utakufa ukiwa na umri gani? Je alie kutangulia kafa akiwa na miaka mingapi?
Si ujanja wala umaarufu kutukana marehemu, au kutafuta umaarufu ati unajilinganisha na marehemu. Huyo kesha maliza wakati wake hayupo tena. Tuache kashfa hatujui kesho yetu. Tanzania ya leo imekuwa na siasa za kujipendekeza, sifa za kijinga, badala ya kufikiria maendeleo ya kweli. Walio tangulia tuwaache, tujenge nchi.
Kwani ukifa ndio hauhukumiwi kama ulifanya mambo ya hovyo? Kifo sio excuse Mzee.Kwani Hitler na madikteta wengine huwa unaona wanasifiwa? .

Uliyotenda yatakufuata hata kaburini,mbona akisemwa vizuri huongei?
 
Haya ayanihusu, naongelea binadamu kuhukumu. Sijaja hapa kuongelea Lisu au sijui Ben Sanane, kama unahitaji kuwaongelea toa mada zinazowahusu. Nachofahamu Mungu uona kwa jicho la tofauti! Mungu wetu ndiye anae hukumu na kusamehe, mimi ni nani nichukue mamlaka ya Mungu? Kaini aliuwa bado mungu akampa ulinzi. Soma mada vizuri.
Kwani mwenzetu wewe unasoma maandiko yapi! Si ndio hayo yanayosema auaye kwa upanga atakufa kwa upanga! Si ndio hayo yamesema ole wake amwagae damu zisizokuwa na hatia! Si ndio hayo yaliyosema yaliyofungwa hapa duniani na mbinguni pia! Be serious.
 
Unauhakika kwamba watanzania walifunga na kuomba ili uongozi wake ukome? Ulifanya utafiti! So mtu akifa madarakani uongozi wake mbaya? Tusihukumu na kujifanya tunajua zaidi kuliko Mungu.
Sababu za Magufuli kufa azijuae ni Mungu pekee, na anakusudi lake! Tusijifanya tunaelewa juu ya uondoaji wa roho za watu!
Soma kitabu Cha Amos ujue kuwa hakika Mungu hatafanya jambo lolote bila kuwafunulia manabii wake Siri zake.
 
Isome historia ya Dunia. Kifo kilichowahi kuhudhuriwa na watu wengi kuliko cha mtu yeyote ni cha Dikteta Stallin. Huyu aliua warusi kwa maelfu.

Siku ya maziko yake, maelfu ya watu walikufa kwa kukanyagana, japo taarifa ya serikali ilisema ni watu 109 tu.
Walikuwa na kiu ya kuhakikisha kama kweli amekufa.
 
Back
Top Bottom