#COVID19 Hayati Magufuli alificha taarifa ya Vifo vya Corona at our Risk

#COVID19 Hayati Magufuli alificha taarifa ya Vifo vya Corona at our Risk

Chadema hamna pa kushikilia!

Tumepashika penyewe. Tunajua mchawi siyo CCM bali kuna agenda mpya tokea awamu 5 inaitwa urais ni taasisi.

Haijulikani hii taasisi mpya ni kwa mujibu wa kifungu kipi cha katiba. Haijulikani ilikampeni wapi kuwa yenyewe. Haijulikani wajumbe wake ni nani.

Hii bila shaka ni taasisi ya watu wasiojulikana.

Hii ina majibu yetu ya nani nyuma ya kesi ya mwamba. Nani nyuma ya kupotea Lijenje, Ben, Azory na hata nani walikuwa kwenye viroba. Nani nyuma ya shambulizi la Lissu. Hii inajua nani wapo nyuma ya SABAYA.

Hawa ndiyo wenye kesi na hukumu zao pale law school.

Hao ndiyo wenye uhusika ukuu na wahanga wa Corona.

Hawa ndiyo wanaotuharibia nchi.

Hao ndiyo wanaotugombanisha.

"Hawa ni ama zao ama zetu!"
 
Lockdown ndiyo utetezi pekee kwa huyo Mhutu. Hakuna jipya wala ubunifu kwenye lockdown zaidi sana jiwe alijificha nyumbani kwake huku akiwaasa watu wasijifungie ndani.

Lile boya la mzizima nalo likawa linawakusanya watu mikutanoni halafu anawaasa wasikusanyike
Na wewe ulijificha wapi? Ulitaka ufungiwe kama kuku wa kizungu au? Magufuli is a hero!!
 
Salim Ahmed Salim foundation imetoa mchango wa 100m/- MUHAS kuunga mkono jitihada dhidi ya UVIKO-19.

Hatua ya kupongezwa kabisa yenye kustahili kuungwa mkono bila kujali nani haoni umuhimu huo.

Hata hivyo wakfu huo wamesema walisukumwa kutoa pesa hizo katika kuyaenzi maisha ya marehemu mke wa Waziri Mkuu mstaafu huyu, ambaye alifariki 20 Oct 2020 kwa ugonjwa hatari wa UVIKO.




Hayati Magufuli kwa wakati huo Rais wa JMT kumbe alijua akamuombea ila akaendelea kudai hakukuwa na Corona nchini.


Roho ngumu kabisa za binadamu zenye kustahili kuangaliwa vinasaba vyake.

Mama Amne alikuwa mgonjwa wa Covid19 halafu hapo JPM yupo karibu yake na hana mask ya aina yoyote ile!.

Namuona Kiongozi huyu kama alishakubaliana na hali halisi ya kiafya aliyokuwa nayo.
 
Magufuli na wale wasaidizi wake wote waliondoka kwasababu ya nini vile? ugonjwa wa moyo!.

Watu mna kumbukumbu ndogo sana, wenzenu wamezika ndugu zao sababu ya Corona, nyie mnasema simple tu; "hakuna Corona, ni uongo wa wazungu"
 
Unadhani Madam Salim alikufa au alivunga kufa tu?

Wanasema waswahili asiyejua kufa aangalie kaburi.

Kufa kila mtu atakufa ni swala la mda tu mimi ninachoongelea ni corona
 
Kufa kila mtu atakufa ni swala la mda tu mimi ninachoongelea ni corona

Kufa kila mtu atakufa ila wengine watauawa na watu labda kama huyu hapa:

IMG_20211015_144814_546.jpg


Wengine wamesokomezwa huko na wapumbavu kama kina Bolsonaro na shujaa wenu kwa UVIKO.

Natural deaths tutashukuru Mungu. Umeua au kusokomeza wenzio huko. Kwa hakika hatukuwachi.
 
Wamekufa kibudu wangapi? Kwani shujaa wako kafaje? Ijekuwa miye kidampa [emoji16][emoji16]?
Shujaa wangu amekufa kishujaa haswa, hakutetereka, amekufa na misimamo yake.
Na amezikwa kishujaa pia, na ataenziwa mpaka mwisho wa dunia hii.

Sasa wewe Kidampa hata maiti yako haitapatikana ili nduguzo wakufukie kwa mila na desturi zenu za kishenzi.
 
Pamoja na udhaifu wote wa J.P.M kwenye hili suala la covid 19 alijitahid sana.Hapo hata kama huyo mama yetu alifariki kwa huu ugonjwa bado kitendo cha magufuri kusimama na msimamo wake kulikuwa na faida zaidi kuliko hiyo misimamo wa maraisi wengine

Cc brazaj
 
Mama Amne alikuwa mgonjwa wa Covid19 halafu hapo JPM yupo karibu yake na hana mask ya aina yoyote ile!.

Namuona Kiongozi huyu kama alishakubaliana na hali halisi ya kiafya aliyokuwa nayo.

Kwamba yeye alikubaliana na hali? Hata Bolnasaro ni hivyo hivyo na hata suicide bomber naye ni hivyo hivyo.

Kwamba yeye alikwenda kushika Simba mkia? Inatuhusu nini sisi, yeye hata kama angeamua kujitundika kabisa na kamba mtini?

Kinachogomba hapa, yeye akiwa kwenye dhamana alitumia nafasi yake kuupotosha umma kuhusu ugonjwa huu. Matokeo yake yakawa maelfu kwa malaki ya watu wamekufa na ugonjwa huu hapa nchini akiwamo yeye mwenyewe.

#COVID19 - Kwa mujibu wa Zitto Kabwe, Tunapoteza watu kwa kiwango kikubwa kutokana na Corona

Kwa hilo yeye na taasisi yake ya wasiojulikana hatutawaacha.
 
Kwamba yeye alikubaliana na hali? Hata Bolnasaro ni hivyo hivyo na hata suicide bomber naye ni hivyo hivyo.

Kwamba yeye alikwenda kushika Simba mkia? Inatuhusu nini sisi, yeye hata kama angeamua kujitundika kabisa na kamba mtini?

Kinachogomba hapa, yeye akiwa kwenye dhamana alitumia nafasi yake kuupotosha umma kuhusu ugonjwa huu. Matokeo yake yakawa maelfu kwa malaki ya watu wamekufa na ugonjwa huu hapa nchini akiwamo yeye mwenyewe.

#COVID19 - Kwa mujibu wa Zitto Kabwe, Tunapoteza watu kwa kiwango kikubwa kutokana na Corona

Kwa hilo yeye na taasisi yake ya wasiojulikana hatutawaacha.
Kiburi kitu kibaya sana mkuu brazaj.
 

Kuna wapumbavu wa kudumu kwenye ignore lists zetu.

IMG_20211022_100600_708.jpg


Wote wale wasiopata majibu yetu nadhani wanajua vipaji vyao vilitambulika zamani.

Hivi bado huwa wana "poke" nje pua zao bado?

Hiiiiii bagosha!
 
Kiburi kitu kibaya sana mkuu brazaj.

Kuliko kiburi cha aliye tutelekezea gonjwa akidai atakuwa malaika kiongozi?

Hivi unajua tumepoteza watu wangapi na ugonjwa huu na kadhia nzima ya watu wasiojulikana?

Au ile kula na vyeo yenu tu ndiyo vilivyo vya muhimu zaidi kuliko haki za akina Adamoo au Moses Lijenje au maelfu kwa malaki walio angamia kwa kushupaza shingo zenu?
 
Pamoja na udhaifu wote wa J.P.M kwenye hili suala la covid 19 alijitahid sana.Hapo hata kama huyo mama yetu alifariki kwa huu ugonjwa bado kitendo cha magufuri kusimama na msimamo wake kulikuwa na faida zaidi kuliko hiyo misimamo wa maraisi wengine

Faida hizo unazoziongelea ni zipi?

Hapa chini kuna malaki kwa maelfu waliokufa.

#COVID19 - Kwa mujibu wa Zitto Kabwe, Tunapoteza watu kwa kiwango kikubwa kutokana na Corona

Bado WHO wanasema cases 6 out of 7 hazitambuliwi leo Afrika. Sembuse wakati huo na takwimu kutokulewa rasmi?
 
Back
Top Bottom