Hayati Magufuli alikosea kwenye mambo mengi mno. Kubwa mojawapo ni kumchagua huyu mtu

Inasikitisha zaidi, kuwa hao wanaoitwa "chawa," wanapojulikana uchawa wao siyo kwa kupenda afanyayo huyo wanayemshabikia, bali kwa kutegemea fadhira kutoka kwake.
 
Sikieni,suala la Bandari ni katika Ilani ya CCM.Hakuna kitakacho badilika.
Wrong!

Mkataba/Makubaliano yasipobadilika, na CCM/Samia wakaendelea kama hakuna kilichotokea, ni WAO CCM na Samia watabadilika. Usifikiri kuna mchezo hapa safari hii.
 
Uchawa ni dhana ya kufikirika tu, tena mwenye kuwa nayo ni yule anayeumizwa na hoja anazosoma.

Kikwete kafanya mengi pia, huwezi kuyaona kwa sababu akili yako imejiweka kuongelea mambo hasi tu.
Siamini tena kuwa huyu ni 'Steven Joel Ntamusana' yule yule wa mwanzo aliyechangia mchango wake wa kwanza mada ya "Mkataba/Makubaliano" ilipoanza kujadiliwa humu JF!

Ni kama umevua nguo zote na kubaki uchi wa mnyama.
Kikwete kafanya mengi pia, huwezi kuyaona kwa sababu akili yako imejiweka kuongelea mambo hasi tu.
Umenisoma wapi nilipoandika kuwa Kikwete hakufanya (meng)?

Sasa unataka hadi nihoji uwezo wako wa kuelewa unachosoma?
; ambao unazidi kujitambulisha kwamba udhaifu huo unao?
 
Kasome Ilani ya CCM alafu uone kama suala la kuleta wawekezaji halipo.
Sasa yeye kama anatekeleza Ilani ya chama chake,unataka chama kimuone hafai vipi?.
Asante sana King Kigoda kwa ushauri wako, nina matumaini nitapata darasa na ufunuo kwenye ilani ya Chama cha Mapinduzi , hatahivyo
KK, naomba tukubaliane kwamba sijasema kuwa Raisi Samia Suluhu, hafai, na kwa mlolongo huo huo niwaombe radhi wengine walio kwazika, kwani, halikuwa lengo langu kufanya hivyo.

KK, nimesema nipo nyuma ya Raisi Samia Suluhu na hilo halibadiliki kwa sasa.

Vilevile, sijasema kuwa suala la uwekezaji halifai, isitoshe hata hao wageni niliokutana nao hawakusema Uwekezaji haufai, amini usiamini mmoja wao wa Zambia alinidokeza mengi tu kuhusu yaliyowatokea Wazambia na Wachina, sinto enda huko, ila alitahadharisha kuhusu Mkataba wetu kwani wa kwao uliwahujumu, hivyo nasi tuwe makini yasije kututokea. Nakuomba usinilishe maneno.

Mkuu, ukinisoma vizuri nimesema Raisi Samia Suluhu hapaswi kutafuta ngwe nyingine, because Chama chake kitaanguka vibaya. Nikiwa na maanisha anaweza subiri ngwe nyingine kwa sababu sakati hili linafoka rushwa na hivyo kuiweka CCM katika hali ngumu kichaguzi.
 
Kwakweli hapo JEMBE huyu aliteleza, ila alikuwa na nia njema kabisa, tatizo huwezi kumjua kirahisi mzuri au mbaya wako 😡
 
Hata huyu JPM kupata huo uraisi ilikua bahati nasibu tu using kua ugomvi kati ya Lowassa na marehemu Membe JPM angekufa kama Msukuma wa kawaida.
Kila jambo lina sababu yake ndugu!
 
Wote ni wale wale tu, kule visiwani jamaa anabinafsisha visiwa kwa kasi ya ajabu. Mchezo huo huo wa hatari umeikumba bandari ya Dar es salaam....So Sad!.😢
Mkuu, tupe info visiwa vingapi vimebinafshishwa kwa muda gani, kwa masharti gani, faida zipi?
 
Kalamu una mikwara miiingi.
 
Kalamu una mikwara miiingi.
Mi nasema ukweli mtupu mkuu 'stevie', kila ninapouona huo ukweli.
Tumekutana humu JF muda mrefu wa kutosha sasa, kuweza kutambua mambo muhimu yanayotuhusu; au siyo?

Mkuu, tusipoteze lengo juu ya Tanzania yetu hii kwa sababu yoyote ile. Angalau tuwe wakweli juu ya hilo, basi, itatosha kutuweka pamoja.
 
Rais Samia kawa muungwana sana, licha ya mashambulizi mabaya dhidi ya dini yake kwa mgongo wa DP World.

Anavyotendewa sio haki hata kidogo. Kawa muungwana sana, lakini baadhi ya ndugu zetu wakristo wenzangu tumemlipa ushenzi Mama huyu.

TICTS wamekaa TPA miaka 22 lakini kwa kuwa ni wakristo wenzetu ni poa tu yaani. Kuja DPW kwa sababu ni mwarabu anayejulikana kuwa ni muislam zinaanza nongwa na sababu nyingi za kumkataa ambazo haziingi akilini hata kidogo.

Mungu ni mwema na atatupitisha mbali na huu ubaguzi unaoanza kuota mizizi kwa kigezo cha uwekezaji.
 
Hebu taja mmiliki wa TICTS, We kweli una matatizo au mnadhani mkipitia kwenye dini ndio mtashinda hii vita.
 
Kuna video au audio ya yeye akisema hivyo?
Ni kweli alisema hivyo na ndio maana akasema alikuwa anamwini sana hussein mwinyi na ndio maana kwenye awamu yake ya kwanza akamfanya kuwa waziri wa ulinzi. Ilikuwa kwenye mkutano wa ccm.
 
So unataka kusema nini Sasa kwamba Raisi akifia madarakani uchaguzi urudiwe
Yap! Katiba mpya italiweka hili sawa. Mimi nadhani makamu wa raisi atakuwa raisi kwa siku 90 tu na latika muda huo uchaguzi ufanyike watu wapate chaguo lao. Samia ni chaguo la katiba; si chaguo la wananchi.
 
Kwangu mimi Kosa kubwa la JPM hakuangalia kuwa mbinu yake ya uongozi itasababisha maafa gani baadae. Uongozi wa JPM ulionesha kuwa rais anaweza kujaza watu wa kabila lake katika serikali yake mpaka kwenye Usalama wa Taifa. Pia aliweza kuonyesha ukiwa Rais unaweza ukafanya upendeleo wa wazi wazi katika maendeleo ya kijijini kwenu. Ishu ya bandari isingefika mbali kama JPM asingebana upinzani na Bunge lingekuwa na upinzani. JPM alianzisha kitu cha kuwa Rais akiamua imepita haina mjadala hakuna spika, jaji au nani wa kupinga. Haya ndo tunayoyaona katika uongozi wa sasa. Katika uongozi matendo yatarudiwa kwa miaka endelevu ijayo. Kwa hio mimi sishangai ya Samia .Yatakuja makubwa zaidi ya haya kwa sababu Magufuli ndo alionesha nini maana ya Umungu mtu, ambao Katiba yetu inampa Rais. Yaani kuhusu suala la biongozi wetu hatuna maono ya muda mrefu. Hata JPM angekuwa bado hai, je una uhakika Rais anayemfatia ansingefanya yale mabaya ya JPM. Kinachoturudisha nyuma Tanzania ni hatuna malengo ya muda mrefu. Hata ukiangalia ishu ya Bandari mtu anasign mkataba apate chake anamuachia msala Rais ajaye. Kuna tafiti ilifanywa wakati wa Mkapa kwa ajili ya kuondoa umasikini Tanzania Rais aliyefuata hakuifanyia maamuzi. Serikali ikae chini iwe na mikakati ya muda mrefu tuwe na malengo ya miaka kuanzia 25 kwenda juu.
 
Rais Samia kawa muungwana sana, licha ya mashambulizi mabaya dhidi ya dini yake kwa mgongo wa DP World.
Dah!

Sasa nijieleze vipi kwako ndipo upate kunielewa vizuri wewe mtu, hivi akili zenu huwa zinawekwa sumu ya namna gani hiyo inayoondoa kujiona mtu mwenye uwezo wa kuona jambo na kulielewa lilivyo, bila ya kuegemea upande ulioteka akili hiyo?

Samia hajawa na uungwana wowote, kama anadiriki kuingiza taifa kwenye janga kama hili analotafuta kutuingiza
TICTS wamekaa TPA miaka 22 lakini kwa kuwa ni wakristo wenzetu ni poa tu yaani. Kuja DPW kwa sababu ni mwarabu anayejulikana kuwa ni muislam zinaanza nongwa na sababu nyingi za kumkataa ambazo haziingi akilini hata kidogo
Ungekuwa ni mtu mwenye akili huru, wala usingethubutu hata mara moja kuutumia huo mfano wa TICTS. Hakuna mfanano wa aina yoyote kati ya "Makubaliano/Mkataba" alioingia nao TICTS na huu mnaolazimisha nyinyi, na kwa bahati mbaya kabisa mnaingiza na udini humo humo.
Hivi taifa kuwa la kiarab, ni lazima litangulizwe na Uislam (dini) kabla ya uarab wao?
Mwarab hawezi kufanya mambo kinyume na dini ya kiislam?
Mungu ni mwema na atatupitisha mbali na huu ubaguzi unaoanza kuota mizizi kwa kigezo cha uwekezaji.
Huyu Mungu unayemlilia hapa, siyo mali ya mtu yeyote, wala wa dini maalum.
Mungu aliyeiweka hii nchi hapa ilipo, anaipenda sana, bila kujali hizo dini mbalimbali zilizopo hapa. Hilo kwangu linatosha, na ninaamini ni Mungu huyo ndiye atakayetuondolea ujambazi huu mliotaka kuuleta hapa.
 
Mkuu kwani hujamsikia borntown akitamba kuwa yeye ndie alimuibua huko chini kabisa na kumpa uwaziri na baadae akamshauri mwendazake amchague kama msaidizi wake mkuu,ndivyo alivosema hivi majuzi kwenye mkutano mmoja wa kikanda, na akaenda mbali kuwa kasoro ni kuwa ana hasira sana, pumbafu stupid.
 
Kwenye mkutano mkuu wa ccm 2020 Magufuli alisema wazi kabisa kwamba yeye chaguo lake namba moja la mgombea mwenza alikuwa Hussein Mwinyi ila wazee wakamchagua Samia yeye hakumpenda kabisa ila chama kiliamua
Sio kweli, hakuna aliposema wazee walichagua Samia. Yeye alisema "ukishindanishwa na mwanamke huwezi kushinda". But it's obvious Mwinyi alikua reserved amrithi Shein that's all ila hakuna popote alisema hayo maneno unayomlisha.
 
Mkuu naona unasahau mapema upinzani upo muda mrefu bungeni,je ni kipi ulizuia ambacho walio kwenye madaraka walinuia kukifanya na wakashindwa kukifanya sababu ya kelele kutoka upinzani? je maoni ya Warioba kuhusu katiba yalipita? je wakati ule hakukuwa na upinzani? upinzani wa TZ ni sawa tu na joka la bibisa wapo kwa ajili ya kunetwork tu mjengoni, upinzani upo Kenya,Malawi,Zambia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…