Hayati Magufuli aliweza kuwatisha waovu, mifumo iliamka kufanya kazi

Hayati Magufuli aliweza kuwatisha waovu, mifumo iliamka kufanya kazi

KAZI za Magufuli zinaonekana Kwa macho.

Magu hakuwa Mwizi, asingefanya makubwa yanayoonekana.
Kwani Ukiwa mwizi huwezi fanya makubwa?

Kwani saizi makubwa hayafanyiki yanayoonekana Kwa macho?

Huu wizi hapa alikuwa anafanya nani?👇👇
Screenshot_20221119-094007.png
Screenshot_20221119-093841.png


Kadanganye wake zako
 
Siku Inakuja,

Chain ya wizi iliyo ndani ya mfumo inayoshirikiana na mapandikizi yaliyoko upinzani kukwamisha wazalendo kunyoosha waovu,

Chain hiyo itakatwa tu.

Magufuli ametuachia Roho ya UZALENDO juu ya nchi yetu, na hayupo wa kutuzuia.

Mungu atubariki.
Mkuu..chanzo cha chain hiyo ni chama tawala.
 
Kwani Ukiwa mwizi huwezi fanya makubwa?

Kwani saizi makubwa hayafanyiki yanayoonekana Kwa macho?

Huu wizi hapa alikuwa anafanya nani?👇👇View attachment 2936057View attachment 2936058

Kadanganye wake zako
Shabiby anafanya nini bungeni,

Inawezekana vipi aache biashara ya mabasi yake Kisha kuja bungeni kutetea wananchi?

Nauli zimepanda akiwa bungeni, kwanini hakutoka kutetea Maslahi ya wananchi?

Cartel ya wabunge matajiri, kamwe haijawahi kusimamia maslah ya Wananchi.

Magu alikuwa mzalendo.
 
Mkuu..chanzo cha chain hiyo ni chama tawala.
Kumbuka kuwa Magu pia alikuwa chama tawala,

Mfumo huo umeteka chama, na unafanya KAZI Kwa karibu na wanasiasa wa Upinzani Maslahi,

Wizi Hauna chama, hivyo tuungane kuua kundi Hilo.

Ndomana, tunadai Katiba mpya na Tume huru ya Uchaguzi kabla ya Uchaguzi wowote.
 
Shabiby anafanya nini bungeni,

Inawezekana vipi aache biashara ya mabasi yake Kisha kuja bungeni kutetea wananchi?

Nauli zimepanda akiwa bungeni, kwanini hakutoka kutetea Maslahi ya wananchi?

Cartel ya wabunge matajiri, kamwe haijawahi kusimamia maslah ya Wananchi.

Magu alikuwa mzalendo.
Hujajibu hoja,wizi huo alikuwa anafanya Samia? 😁😁😁

Muwe mnawadanganya wapumbavu.Pamoja na kubana taarifa,Wapinzani,vyombo vya habari,wanaharakati nk lakini hakuna mwaka CAG aliwahi sema Ufisadi umepungua awamu ya 5 yaani licha ya kufanya uhariri wa taarifa.

Mojawapo ya sekta amabzo wizi mkubwa ulifanyaikani mamiradi hayo Makubwa na pesa za Halmashauri ndio maana Samia ameamua kizirudisha zitolewe na Banks,alisimamisha ule wizi kanuni Mpya zinakuja 🤪🤪🤪
 
Hujajibu hoja,wizi huo alikuwa anafanya Samia? 😁😁😁

Muwe mnawadanganya wapumbavu.Pamoja na kubana taarifa,Wapinzani,vyombo vya habari,wanaharakati nk lakini hakuna mwaka CAG aliwahi sema Ufisadi umepungua awamu ya 5 yaani licha ya kufanya uhariri wa taarifa.

Mojawapo ya sekta amabzo wizi mkubwa ulifanyaikani mamiradi hayo Makubwa na pesa za Halmashauri ndio maana Samia ameamua kizirudisha zitolewe na Banks,alisimamisha ule wizi kanuni Mpya zinakuja 🤪🤪🤪
Kama Magu alikuwa anaiba pesa Kisha anakwenda kujengea Flyovers, mabarabara, Mji wa Magufuli Dodoma na IKULU, Masoko ya kisasa na Bus terminals,SGR,daraja la Busisi, ununuzi wa ndege Kwa pesa alizoiba,

Basi kiongozi Mwizi wa aina hiyo ndiye tumtakaye.
 
Kama Magu alikuwa anaiba pesa Kisha anakwenda kujengea Flyovers, mabarabara, Mji wa Magufuli Dodoma na IKULU, Masikio ya kisiasa,SGR,daraja la Busisi, ununuzi wa ndege Kwa pesa alizoiba,

Basi kiongozi Mwizi wa aina hiyo ndiye tumtakaye.
😂😂😂😂

Mumewe aligalagala pale Kijazi darajani kwa furaha
 
Kama Magu alikuwa anaiba pesa Kisha anakwenda kujengea Flyovers, mabarabara, Mji wa Magufuli Dodoma na IKULU, Masikio ya kisiasa,SGR,daraja la Busisi, ununuzi wa ndege Kwa pesa alizoiba,

Basi kiongozi Mwizi wa aina hiyo ndiye tumtakaye.
Sasa hapo ndio unadhihirisha upunguani wako,kujenga hivyo ndio kunazuia mtu kuwa mwizi au Kuna justify wizi?

Nimekuuliza hayo ma flaiova sijui Madara and such blaa blaa hayajengwi? Au kabla yake hayakuwahi kujengwa? Nataka majibu
 
Betting ipo tangu enzi za Nyerere 😂
Itakuwa nawe unabet Mzee,

Mara ya kwanza kuona ofisi za betting nilishangazwa sana.

Watu wako makini watulivu wameshika kalamu utadhani wanafanya ya maana,

Kumbe ni Ujinga Ujinga tu.
 
Sasa hapo ndio unadhihirisha upunguani wako,kujenga hivyo ndio kunazuia mtu kuwa mwizi au Kuna justify wizi?

Nimekuuliza hayo ma flaiova sijui Madara and such blaa blaa hayajengwi? Au kabla yake hayakuwahi kujengwa? Nataka majibu
Ndo nasemaje,

Ikiwa KAZI ya Magu Kwa Miaka mitano inayoonekana ya ujenzi wa mabarabara Nchi nzima, umeme kutokatika, flyovers, hospitals , ndege, ujenzi viwanja vya ndege, SGR, madaraka, nknk ikiwa KAZI hizo zinatokana na wizi,

Basi wizi wa Magufuli ndio tuutakao.
 
Ndo nasemaje,

Ikiwa KAZI ya Magu Kwa Miaka mitano imayoonekana ya ujenzi wa mabarabara Nchi nzima, umeme kutokatika, flyovers, hospitals nknk ikiwa KAZI hizo zinatokana na wizi,

Basi wizi wa Magufuli ndio tuutakao.
Mabarabara Nchi nzima yapi hayo 😁😁
Magu alijenga Barabara Dar tuu tena za mradi wa wafadhili wa DMDP I,Samia ndio anajenga Barabara Nchi nzima.

Mwendazake alikuta Mikoa haijaunganishwa na lami baada ya miaka 5 ikiwa na mavumbi ,Samia ndio analinganisha Sasa hivi.

View: https://www.youtube.com/live/vGWDByHCFYc?si=0nKFhmuM8X1iCazq

Umeme utakatokaje wakati wafanyabiashara na wawekezaji wamekimbiza? 🤪🤪

Kazi ya Samia sio ya kitoto 👇👇

View: https://twitter.com/mamayukokazini/status/1768923114304389344?t=wFEtVoRe-dpkXk2maNXQtQ&s=19

Niongeze bakora?
 
Salaam, Shalom.

Ili pawe na Amani, huna budi kuwatisha waovu, KAZI hii ya kuhakikisha waovu hawachezei Sharubu za Serikali, Mungu alimsaidia Hayati Magufuli kuifanya kazi hiyo kwa ufasaha.

Maeneo yafuatayo, alidhibiti kwelikweli;

1. MTANDAO WA WIZI WA PESA ZA UMMA

Tumesikia Rais Samia analalamika Badala ya kuamrisha mifumo, asema kuwa umerudi mtandao wa kuiba pesa za umma, yaani pesa inatoka hazina kuja halmashauri, wanatokea watu, wanachepusha pesa hizo zinaingia katika account zao, na pesa hizo ni za mikopo tuliyokopa!

Miradi aliyeanzisha Magu, ilienda kwa kasi sababu ya ufuatiliaji wa karibu na wezi walidhibitiwa hasa.Usingeweza kukwiba pesa ya umma ukabaki salama.

2. UJAMBAZI WA KUTUMIA SILAHA.

Katika kipindi chake, majambazi walienda likizo, hilo litoshe kutupa kujua kazi kubwa aliyoifanya hasa katika kuifanya mifumo ya ulinzi na Usalama kutenda kazi Kwa viwango vya juu.

3. KUDHIBITI MTANDAO WA DAWA ZA KULEVYA

Kabla ya Magufuli kuingia madarakani, Nchi yetu ilikithiri kwa kutapakaa kwa dawa za kulevya, lakini baada ya miaka kadhaa, mateja wengi walijisalimisha katika sobber houses, sababu kuu ikiwa ni kuadimika Kwa dawa za kulevya mtaani. Hilo litoshe kutuonyesha jinsi ambavyo palifanyika kazi kubwa underground.

4. UTAKATISHAJI FEDHA

Pesa haramu, chafu zilizotokana na biashara ovu ya kuiba pesa za umma, uuzaji dawa za kulevya, biashara chafu za ukwepaji kodi, zilidhibitiwa kwa kiasi kikubwa, jambo hilo lilileta mtikisiko kwenye Uchumi kwa kuwa Kwa namna moja au ingine, pesa hizo zilisaidia kutengeneza ajira sekta binafsi.

5. MFUMO WA EFD ULIFANYA KAZI

Vituo vya mafuta kwa Mfano, vyenye kuingiza pesa nyingi, hazikuwa zikitoa EFD, na walipobanwa kutoa risiti, walitishia kugoma.

Ujasiri wa Magufuli, ulisaidia wafanyabiashara hao kurudi mezani na kukubali kutoa EFD bila masharti.

6. UFANISI KATIKA MIFUMO YA UTOAJI MIZIGO BANDARINI

Ni katika uongozi wa Hayati Magufuli, document za kutoa Mzigo bandarini zilipungua, mwanzoni palikuwa na utitiri wa karatasi na mizunguko iliyochelewesha ufaulishaji mizigo bandarini.

Scana ya ukaguzi wa vitu vinavyopita bandarini ULIFANYA KAZI utawala wa Magufuli, alipambana kweli kweli na ufanisi ulionekana.

HITIMISHO

Pamoja na mapungufu wa kibinadamu na makosa kadhaa aliyoifanya Hayati Magufuli, itoshe kusema, Mungu alimwezesha kukaa katika KITI cha maamuzi sawasawa na kuhakikisha mifumo inafanya KAZI. Magufuli hakulalamika, alichukua hatua.

OMBI: Wananchi tunaomba atokee kiongozi atakayefuta BETTING nchini, hivi sasa, vijana wa CCM+ CDM na wasio na vyama wametekwa na jinamizi hili, HAYATI Magu hakuliweza hili. Maisha hayajawahi kuwa Bahati nasibu.

Tunamshukuru Mungu kwa zawadi ya Rais Magufuli.

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo Tanzania🇹🇿.

Amen.
Jiwe alikuwa mfalme mwenye kutumia guvu nyingi pasipo maarifa
 
Mimi kama raia mwema na mtumishi wa umma wa zama za mwendazake, hakika hakuna asiyekumbuka matukio ya huyo mtu hususani suala la kutopandisha madaraja, nyongeza ya mishahara, posho za kazi na vitisho visivyo na kifani kwa watumishi.

Ukija kwenye biashara ndo usiseme, taasisi binafsi nyingi zilikufa au kubadilishiwa matumizi.


Watu wengi hata watoto tulilazimika kuwapeleka shule za kata maana fedha ya kuwapeleka private ilikuwa changamoto na shule nyingi za private ukiondoa zile zinazomilikiwa na taasisi kama Kanisa la RC au Misikiti zilishindwa kujiendesha zikafungwa.

Kwangu mimi siipendi CCM ila huyu mama Mungu ampe miaka mitano mingine ana nafuu hata mitandaoni tunaandika mengi ya kukosoa Serikali na hatutishiwi kuwekwa kwenye viroba, pia kila mtu anaishi bila hofu, amani ipo, biashara zinafanyika na maofosini tunachapa kazi kwa furaha.

Heri utafune mhogo mkavu na maji kwa amani na uhuru kuliko nyama choma kwenye vita.


cc Rabbon

ChoiceVariable
 
Mimi kama raia mwema na mtumishi wa umma wa zama za mwendazake, hakika hakuna asiyekumbuka matukio ya huyo mtu hususani suala la kutopandisha madaraja, nyongeza ya mishahara, posho za kazi na vitisho visivyo na kifani kwa watumishi.

Ukija kwenye biashara ndo usiseme, taasisi binafsi nyingi zilikufa au kubadilishiwa matumizi.


Watu wengi hata watoto tulilazimika kuwapeleka shule za kata maana fedha ya kuwapeleka private ilikuwa changamoto na shule nyingi za private ukiondoa zile zinazomilikiwa na taasisi kama Kanisa la RC au Misikiti zilishindwa kujiendesha zikafungwa.

Kwangu mimi siipendi CCM ila huyu mama Mungu ampe miaka mitano mingine ana nafuu hata mitandaoni tunaandika mengi ya kukosoa Serikali na hatutishiwi kuwekwa kwenye viroba, pia kila mtu anaishi bila hofu, amani ipo, biashara zinafanyika na maofosini tunachapa kazi kwa furaha.

Heri utafune mhogo mkavu na maji kwa amani na uhuru kuliko nyama choma kwenye vita.


cc Rabbon

ChoiceVariable
Umesema wewe ni mtumishi wa umma,

Kabla ya Magufuli, ulikuwa unafanya deal Gani Ukiwa Ofisini zilizokuwezesha kusomesha watoto international schools?
 
Back
Top Bottom