Hayati Magufuli aliweza kuwatisha waovu, mifumo iliamka kufanya kazi

Hayati Magufuli aliweza kuwatisha waovu, mifumo iliamka kufanya kazi

Kumbuka kama ni uovu yeye alikuwa mwovu wa waovu!
Na UOVU wake ni mzuri,
Sababu alimsaidia mama mjamzito kijijini kujifungua bila matusi ya manesi,

UOVU wake ulisababisha kutisha wakata umeme na wauza generators,

Makali ya umeme yalipungua,

UOVU wa aina hii wa kusaidia wananchi maskini ni UOVU mzuri.

Magu Abarikiwe.
 
Mbegu aliyoipanda jpm ipo siku itamea tu.

Ipo siku haya majizi yatalia na kisaga meno
Ni sisi Hawa Hawa tutasababisha imee,

Kwa Mfano, sasa hakuna Mtanzania utamdanganya kuwa Nchi Ina upungufu wa umeme kusababisha mgao,

Tunajua fika, kundi dogo lipo kufanya hayo Ili kutimiza maslah Yao binafsi.

Siku yaja.
 
Salaam, Shalom.

Ili pawe na Amani, huna budi kuwatisha waovu, KAZI hii ya kuhakikisha waovu hawachezei Sharubu za Serikali, Mungu alimsaidia Hayati Magufuli kuifanya kazi hiyo kwa ufasaha.

Maeneo yafuatayo, alidhibiti kwelikweli;

1. MTANDAO WA WIZI WA PESA ZA UMMA

Tumesikia Rais Samia analalamika Badala ya kuamrisha mifumo, asema kuwa umerudi mtandao wa kuiba pesa za umma, yaani pesa inatoka hazina kuja halmashauri, wanatokea watu, wanachepusha pesa hizo zinaingia katika account zao, na pesa hizo ni za mikopo tuliyokopa!

Miradi aliyeanzisha Magu, ilienda kwa kasi sababu ya ufuatiliaji wa karibu na wezi walidhibitiwa hasa.Usingeweza kukwiba pesa ya umma ukabaki salama.

2. UJAMBAZI WA KUTUMIA SILAHA.

Katika kipindi chake, majambazi walienda likizo, hilo litoshe kutupa kujua kazi kubwa aliyoifanya hasa katika kuifanya mifumo ya ulinzi na Usalama kutenda kazi Kwa viwango vya juu.

3. KUDHIBITI MTANDAO WA DAWA ZA KULEVYA

Kabla ya Magufuli kuingia madarakani, Nchi yetu ilikithiri kwa kutapakaa kwa dawa za kulevya, lakini baada ya miaka kadhaa, mateja wengi walijisalimisha katika sobber houses, sababu kuu ikiwa ni kuadimika Kwa dawa za kulevya mtaani. Hilo litoshe kutuonyesha jinsi ambavyo palifanyika kazi kubwa underground.

4. UTAKATISHAJI FEDHA

Pesa haramu, chafu zilizotokana na biashara ovu ya kuiba pesa za umma, uuzaji dawa za kulevya, biashara chafu za ukwepaji kodi, zilidhibitiwa kwa kiasi kikubwa, jambo hilo lilileta mtikisiko kwenye Uchumi kwa kuwa Kwa namna moja au ingine, pesa hizo zilisaidia kutengeneza ajira sekta binafsi.

5. MFUMO WA EFD ULIFANYA KAZI

Vituo vya mafuta kwa Mfano, vyenye kuingiza pesa nyingi, hazikuwa zikitoa EFD, na walipobanwa kutoa risiti, walitishia kugoma.

Ujasiri wa Magufuli, ulisaidia wafanyabiashara hao kurudi mezani na kukubali kutoa EFD bila masharti.

6. UFANISI KATIKA MIFUMO YA UTOAJI MIZIGO BANDARINI

Ni katika uongozi wa Hayati Magufuli, document za kutoa Mzigo bandarini zilipungua, mwanzoni palikuwa na utitiri wa karatasi na mizunguko iliyochelewesha ufaulishaji mizigo bandarini.

Scana ya ukaguzi wa vitu vinavyopita bandarini ULIFANYA KAZI utawala wa Magufuli, alipambana kweli kweli na ufanisi ulionekana.

HITIMISHO

Pamoja na mapungufu wa kibinadamu na makosa kadhaa aliyoifanya Hayati Magufuli, itoshe kusema, Mungu alimwezesha kukaa katika KITI cha maamuzi sawasawa na kuhakikisha mifumo inafanya KAZI. Magufuli hakulalamika, alichukua hatua.

OMBI: Wananchi tunaomba atokee kiongozi atakayefuta BETTING nchini, hivi sasa, vijana wa CCM+ CDM na wasio na vyama wametekwa na jinamizi hili, HAYATI Magu hakuliweza hili. Maisha hayajawahi kuwa Bahati nasibu.

Tunamshukuru Mungu kwa zawadi ya Rais Magufuli.

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo Tanzania[emoji1241].

Amen.
Ok kama kweli hebu tuambie wewe ni kiasi gali hilo shetani lenu la Chato lilikusanya kupitia vile vitambulisho vya Magufuli vya 20,000.
Tuambie zilienda wapi.

Ukweli ni kwamba alitutia hofu mpk vyombo vya habari vikawa vinaogopa kuripoti mapungufu na maovu ya utawala wake.

Prof. Asad alipothubutu alipita nae.
Lisu alipothubutu alikiona.
Ben Sa8 alipothubutu kilichomfika anakijua mwenyewe.
 
  • Thanks
Reactions: K11
Ok kama kweli hebu tuambie wewe ni kiasi gali hilo shetani lenu la Chato lilikusanya kupitia vile vitambulisho vya Magufuli vya 20,000.
Tuambie zilienda wapi.

Ukweli ni kwamba alitutia hofu mpk vyombo vya habari vikawa vinaogopa kuripoti mapungufu na maovu ya utawala wake.

Prof. Asad alipothubutu alipita nae.
Lisu alipothubutu alikiona.
Ben Sa8 alipothubutu kilichomfika anakijua mwenyewe.
KAZI za Magu zinaonekana wazi.

Pita pale kijazi flyover utaona alama yake,

Tembea Nchi nzima uone KAZI zake,

Ikiwa aliiba Kisha kwenda kujenga vinavyoonekana,

Wizi wake ni mzuri wenye TIJA.
 
Shabiby anafanya nini bungeni,

Inawezekana vipi aache biashara ya mabasi yake Kisha kuja bungeni kutetea wananchi?

Nauli zimepanda akiwa bungeni, kwanini hakutoka kutetea Maslahi ya wananchi?

Cartel ya wabunge matajiri, kamwe haijawahi kusimamia maslah ya Wananchi.

Magu alikuwa mzalendo.
Shabiby alipata Ubunge kupitia huyo huyo Magufuli wenu.
Acha umasikini wa kuchukia matajiri
 
Oops! We ran into some problems

You do not have permission to view this page or perform this action.
 
KAZI za Magu zinaonekana wazi.

Pita pale kijazi flyover utaona alama yake,

Tembea Nchi nzima uone KAZI zake,

Ikiwa aliiba Kisha kwenda kujenga vinavyoonekana,

Wizi wake ni mzuri wenye TIJA.
Hujajibu.
Alikusanya sh. ngapi ya vitambulisho.
Uliwahi ht kusikia japo kijuujuu tu kwamba Ngosha alikusanya kiasi gani kupitia vitambulisho uchwara vile?
Hata bajeti yake sijui ilikuwaje na sijui alizipeleka wapi mwizi yule
 
Hujajibu.
Alikusanya sh. ngapi ya vitambulisho.
Uliwahi ht kusikia japo kijuujuu tu kwamba Ngosha alikusanya kiasi gani kupitia vitambulisho uchwara vile?
Hata bajeti yake sijui ilikuwaje na sijui alizipeleka wapi mwizi yule
Pesa za vitambulisho ziliingia kwenye fuko kubwa,

Ndiyo maana Nchi nzima enzi zake, miradi haikusimana.

Karibu🙏
 
Umesema wewe ni mtumishi wa umma,

Kabla ya Magufuli, ulikuwa unafanya deal Gani Ukiwa Ofisini zilizokuwezesha kusomesha watoto international schools?
Nimefanya kazi kabla ya Magufuli, wakati wa Magufuli na baada yake, hivyo elewa usitawi wa jamii uliimarika zaidi enzi ya utawala wa Mh. J. Kikwete, wengi walipata maendeleo halisi ya vitu na watu.

Enzi za utawala wa Mh JPM usitawi wa jamii upande wa watu ulisimama, mzunguko wa fedha uliminywa na serikali ikaacha matumizi yanayochochea ongezeko la fedha katika jamii, mwisho wakaona haitoshi wakaanza ujambazi wa kufunga akaunti za watu benki na kuchukua fedha zao huku wengine wakiishia kwenye viroba au korokoroni.

Katika tawala zote, hakuna utawala ambao haujajenga barabara, madaraja, shule, hospitali au kutoa ajira.
Labda niwe ninaongea na vijana wa jana ambao hawajui tulipotoka, tulipo na tunakoelekea.

Hivyo sasa, nikija kwenye swali lako, nilipata fedha za kuendeshea maisha yangu na familia kupitia biashara, ufugaji, kilimo na ajira.

Chini ya utawala wa JPM alipunguza kipato changu cha kwenye ajira kwa kuacha kunipandisha madaraja, kuweka nyongeza ya kila mwaka kwa mujibu wa sheria, kufuta posho za kazi wakati bei za vitu zinapanda kila siku na shilingi ikishuka thamani kila wakati.

Pia aliathiri biashara zangu kupitia wale watu waliokuwa wakijiita wamepokea maelekezo toka juu ili waje kukushughulikia.

Upande wa kilimo, nilikuwa ninalima mazao ya biashara ambayo alienda kuathiri bei ya mazao yangu huku mengine akisema ni mboga tule tu na mengine akikorofisha mfumo wa stakabadhi ghalani.

Kwa hoja hizo usitegemee ningebaki bila kutetereka mfukoni ili kukidhi mahitaji yangu ya kila siku.

Hapo nimezungumza kwa upande wangu lakini mtu pekee aliyefurahia utawala wa JPM ni masikini hususani wale waliokuwa wanafurahia kuitwa wanyonge na watu wasio na elimu ya kutosha.

Vijana enzi za mtangulizi wake, baadhi ya kada wakihitimu wote walikuwa wanalamba ajira, ila baada ya huyo mtu wenu wengi wanalamba miguu na njia kila siku kusaka ajira bila mafanikio.

Acha niishie hapa kwa leo.
 
Salaam, Shalom.

Ili pawe na Amani, huna budi kuwatisha waovu, KAZI hii ya kuhakikisha waovu hawachezei Sharubu za Serikali, Mungu alimsaidia Hayati Magufuli kuifanya kazi hiyo kwa ufasaha.

Maeneo yafuatayo, alidhibiti kwelikweli;

1. MTANDAO WA WIZI WA PESA ZA UMMA

Tumesikia Rais Samia analalamika Badala ya kuamrisha mifumo, asema kuwa umerudi mtandao wa kuiba pesa za umma, yaani pesa inatoka hazina kuja halmashauri, wanatokea watu, wanachepusha pesa hizo zinaingia katika account zao, na pesa hizo ni za mikopo tuliyokopa!

Miradi aliyeanzisha Magu, ilienda kwa kasi sababu ya ufuatiliaji wa karibu na wezi walidhibitiwa hasa.Usingeweza kukwiba pesa ya umma ukabaki salama.

2. UJAMBAZI WA KUTUMIA SILAHA.

Katika kipindi chake, majambazi walienda likizo, hilo litoshe kutupa kujua kazi kubwa aliyoifanya hasa katika kuifanya mifumo ya ulinzi na Usalama kutenda kazi Kwa viwango vya juu.

3. KUDHIBITI MTANDAO WA DAWA ZA KULEVYA

Kabla ya Magufuli kuingia madarakani, Nchi yetu ilikithiri kwa kutapakaa kwa dawa za kulevya, lakini baada ya miaka kadhaa, mateja wengi walijisalimisha katika sobber houses, sababu kuu ikiwa ni kuadimika Kwa dawa za kulevya mtaani. Hilo litoshe kutuonyesha jinsi ambavyo palifanyika kazi kubwa underground.

4. UTAKATISHAJI FEDHA

Pesa haramu, chafu zilizotokana na biashara ovu ya kuiba pesa za umma, uuzaji dawa za kulevya, biashara chafu za ukwepaji kodi, zilidhibitiwa kwa kiasi kikubwa, jambo hilo lilileta mtikisiko kwenye Uchumi kwa kuwa Kwa namna moja au ingine, pesa hizo zilisaidia kutengeneza ajira sekta binafsi.

5. MFUMO WA EFD ULIFANYA KAZI

Vituo vya mafuta kwa Mfano, vyenye kuingiza pesa nyingi, hazikuwa zikitoa EFD, na walipobanwa kutoa risiti, walitishia kugoma.

Ujasiri wa Magufuli, ulisaidia wafanyabiashara hao kurudi mezani na kukubali kutoa EFD bila masharti.

6. UFANISI KATIKA MIFUMO YA UTOAJI MIZIGO BANDARINI

Ni katika uongozi wa Hayati Magufuli, document za kutoa Mzigo bandarini zilipungua, mwanzoni palikuwa na utitiri wa karatasi na mizunguko iliyochelewesha ufaulishaji mizigo bandarini.

Scana ya ukaguzi wa vitu vinavyopita bandarini ULIFANYA KAZI utawala wa Magufuli, alipambana kweli kweli na ufanisi ulionekana.

HITIMISHO

Pamoja na mapungufu wa kibinadamu na makosa kadhaa aliyoifanya Hayati Magufuli, itoshe kusema, Mungu alimwezesha kukaa katika KITI cha maamuzi sawasawa na kuhakikisha mifumo inafanya KAZI. Magufuli hakulalamika, alichukua hatua.

OMBI: Wananchi tunaomba atokee kiongozi atakayefuta BETTING nchini, hivi sasa, vijana wa CCM+ CDM na wasio na vyama wametekwa na jinamizi hili, HAYATI Magu hakuliweza hili. Maisha hayajawahi kuwa Bahati nasibu.

Tunamshukuru Mungu kwa zawadi ya Rais Magufuli.

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo Tanzania🇹🇿.

Amen.
Mfuate alipo we kenge
 
Asingefariki lazima angelazimika kubadili mfumo, angechagua mfumo upi, hata mimi sijui.
Ingefika pahala asingeweza tena kuwatawala watu kwa hofu tena, kiasili a human being is rebel, ni vile tu watu walikuwa kwenye shock bado, kwa hiyo alitake advantage ya huo muda.

Kwa hiyo ni mbinu ya muda mfupi, watu wakijiadjust na kuanza kujitafuta na kujipata wapi palipo na udhaifu mambo hubadilika.
 
Ndo nasemaje,

Ikiwa KAZI ya Magu Kwa Miaka mitano inayoonekana ya ujenzi wa mabarabara Nchi nzima, umeme kutokatika, flyovers, hospitals , ndege, ujenzi viwanja vya ndege, SGR, madaraka, nknk ikiwa KAZI hizo zinatokana na wizi,

Basi wizi wa Magufuli ndio tuutakao.
Kwani ni vipi katika hivyo hakijawahi kufanyika nchi hii, au ambacho hakifanyiki hivi sasa, au ndio mambo ya mahaba niue?
 
Maono yake juu ya Tanzania Tajiri yenye kujitegemea, itakayosaidia Nchi maskini ulaya,


Lazima tuhakikishe yanatimia.
Kuna Nchi Ulaya ni masikini zaidi yenu?
 
Kwani ni vipi katika hivyo hakijawahi kufanyika nchi hii, au ambacho hakifanyiki hivi sasa, au ndio mambo ya mahaba niue?
Mengi yamewahi kufanyika na yanafanyika,

Kutumia miaka mitano pekee kuanzisha ujenzi SGR, Daraja la Busisi, Flyovers, Ununuzi wa ndege, barabara Nchi nzima,

Jambo Hilo linashtua,

Magu ametupa kujua kuwa nchi yetu Ina pesa nyingi sana zinazopotea Bure.

Mimi siipendi CCM, ila Magu alisababisha tuitazame Nchi yetu Kwa jicho la tofauti.

Baada ya tarehe 17, tutaendelea na spana.
 
Back
Top Bottom