Hayati Magufuli ni shujaa anayepigana na walio hai

Hii kweli hadithi, mana naona unarudia rudia tuu.

Umejitahidikuandika mazuri pekee,lakin umesahau mapungufu ya utawala wake.

Maana wengi wameumia ,hasa wafanya bishara,maisha yamekuwa magumu, vyuma vimekaza mo, watu wote wamkimbilia maisha ya Kimachinga na mama ntilie ili kuweza kujiimu kimaisha.

Jumuia ya kimataifa ame funga mlango kabis ,hakupenda kutanua wigo huo.

Amejitengenezea maadui wengi, kwa kukosa kwake busara ya ku kompromise .

Unapokuwa mtawala unalazimika kubalance , Mtajiri,watu masikini, mataifa makubwa,wananchi wa kawaida.
 
Nataka nione utafikia wapi na hizi nyuzi zako za kumsifia huyo marehemu. Nakufuatilia kwa ukaribu. Walikuwepo wakina Bia yetu humu! Lakini leo hii hawapo tena! Pumzi ilishakata kitambo.
 
Ukifungua hadithi ya kaburu Pieter Botha wa Afrika kusini ni ya juu kuliko hiyo ya Magufuli kwenye miundombinu, lakini Mandela ndiye anayechukuliwa kama rais bora wa Afrika kusini bila kujenga mradi wowote.
Kama isingekuwa upendeleo wa wazungu wa Ulaya kuwapa masoko ya bure wazungu wenzao wa nchi za kusini mwa Africa, wangepata fedha za kujenga hiyo miundo mbinu?
 
Moderator kwa nini msiziunganishe nyuzi za huyu mtoa mada? Zote zinaelezea kitu kimoja tu.
 
Kama isingekuwa upendeleo wa wazungu wa zilizo endelea kuwapa masoko ya bure wazungu wenzao wa nchi za kusini mwa Africa, wangepata fedha za kujenga hiyo miundo mbinu?

Walipendelewa kwa kiwango gani? Sisi sasa hivi tuna soko la AGOA la upendeleo, tuna soko la pamoja la SADC na EA. Mbona hatuendelei kama wao?
 
We mwehu kwei kwei! Kunaweza kuwa na legacy pasipo na kazi iliyotukuka?! Jizi, jambawazi, poraji linaweza kuwa na legacy gani?! Nyau weye!
 
Fedha sasa inaingia jana nimeshika Alfu hamsini kutoka kwa jamaa yangu aliyerejea Nchini Tanzania

Ameniambia akaunti zake zimefunguliwa na ameruhusiwa kupiga mzigo

Asante Mama Bundi katuondokea furaha tele
Leo niko Arusha kibiashara, naona Parrot hoteli iliyokuwa imesimama kwa muda mrefu, nayo ukarabati umeanza.
 
Watu wengi walipotea, kuumizwa na kuuwawa, ni wajinga tu wanafikiri Magufuli alikuwa na nia njema na watanzania.
 
Atakuwa shujaa wa chato na ccm sio shujaa wa watanzania, ametuangusha sana, never again!
 
Walipendelewa kwa kiwango gani? Sisi sasa hivi tuna soko la AGOA la upendeleo, tuna soko la pamoja la SADC na EA. Mbona hatuendelei kama wao?
Nchi za SA, Namibia, South Rhodesia ambazo zimekuwa kwenye utawala wa kizungu kwa zaidi ya miaka 400, walipewa upendeleo mkubwa wa bidhaa zao kwenye masoko ya Ulaya na Marekani. Tokea nchi zimehamia kwenye utawala mtu mweusi, masoko yameanza kuyeyuka moja baada ya lingine. Matokeo yake, miundombinu inaanza kuharibika ajira zinatoweka.

AGOA ni mtego kwa nchi masikini kuwekwa kwenye himaya ya Marekani, ni mkataba wa kisiasa zaidi kuliko wa kumsaidia mkulima masikini. Wanaonufaika na AGOA kwa hivi sasa ni matajiri wanaotoka nje ya Afrika. Leo hii ukijiamulia mambo yako mwenyewe na kama hayapendezeshi Mmarekani, wanauwezi wa kukufungia usitumie soko AGOA. Tofauti na nchi zingine zenye mikataba rafiki kama Australia, au SA ya wakati wa kaburu PW Botha.
 

Nimekutajia na soko la SADC na East Afrika nalo mbona hatujaendelea?
 
Tuondolee upumbavu wako hapa!!! Mbona unahangaika kiasi hiki? Nani anakulipa kuandika huu upuuzi!? 😳😳
 
Ukifungua hadithi ya kaburu Pieter Botha wa Afrika kusini ni ya juu kuliko hiyo ya Magufuli kwenye miundombinu, lakini Mandela ndiye anayechukuliwa kama rais bora wa Afrika kusini bila kujenga mradi wowote.

title ya mandela ilikua backed up na nyerere, kuna uwezekano mkubwa pasipo nyerere basi mandela asingekuaga kwenye african politics known
 
Mie sijapata jibu kwanini walitufichwa kuwa
RAIS anauwa?

Pili hivi Marais Huwa wanatibiwa Muhimbili?

Tatu hivi marais Huwa wanatibiwa hospital ya mzena?

Nne ,hivi inawezekanaje mtu alikuwa mzima then in two weeks amekufa ? Why daktari wake hakuona ni busara Rais asiende Dar maana kwa vyovyote vile alikuwa anaumwa kiasi cha kufa ndani ya wiki mbili?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…