Hazina Haina Kitu: Wazabuni, Makandaradi, Madeni, ni taabu

Hazina Haina Kitu: Wazabuni, Makandaradi, Madeni, ni taabu

Ushauri wa bure.
Mama amtoe Mwigulu pale hazina.
Kwanza itastabilaiz uchumu lkn pia itapandisha umaarufu wake.
(Jamani Mwigulu hamudu pale labda kusimamia mabasi na vituo vya mafuta, sio hazina ya nchi)
Mwigulu ni sehemu ndogo sana ya tatizo, tatizo limeanzia kwa....mwenyewe.
 
Kwa kusema kweli Wizara ya fedha haina waziri!! Ina kibuli tuu. Na uchumi wetu hauta weza kwenda mahali kwa kuwa na waziri kama Mwigulu. Huyu muweke kwenye kuweka watu kwenye viroba.
 
Chadema ndo wanakusanya kodi na kupewa mikopo ya taifa hili? Unataka wasijenge chama chao au unatakaje? Hela ya chopa nani kawapa na ni rudhuku yao unawapangia watumieje?[emoji848]
 
Ucheleweshaji wa kulipa wazabuni ni JANJAJANJA ya wahuni kupiga pesa kwenye FAINI ambayo serikali itatozwa.
Wabongo hawashindwi kitu ili kupiga, check Sasa hivi wanapigia Dili kwenye ukamataji wakosoaji then wanawaachia gharama za ukamataji hazirudi zimeingia mifukoni
Wabongo ni sawa na mchwa kila mmoja yupo bize kutafuna nyumba yetu ya mabua hali yeye kesho ndie atakaeumia
 
Licha ya Serikali ya Tanzania kuwa na upungufu mkubwa wa Dolla ya kimarekani, haijatosha na bado serikali ya Tanzania Inaonekana kuwa na Uhaba mkubwa wa Fedha za ndani ambazo Ali maarufu wanaziita madafu yaani Tsh, Hali hii imepelekea maisha kuwa magumu mtaani Kwa minajili kwamba ajira nyingi za sekta binafsi zinategemea serikali, kwani nyingi zinapata flow ya pesa kutoka Kwa mwigulu nchemba na wizara yake kiujumla.

Hali ya Hazina ni mbaya sana, pesa hakuna, ila tujikumbushe kuwa serikali kamwe haiwezi kufeli, na hiki ni kipindi cha mpito.

Hata wote tunakumbuka serikali ya Ugiriki ilivyodondoka kiuchumi, na kuokolewa na serikali ya ujerumani Kwa kuingiza Fedha kiasi Cha Dolla bilioni 100, kama Mkopo Kwa Greece , ambapo mpaka Sasa Mkopo huo uliweza kulipwa kupitia staili ya mabeberu ya magharibi ya kutumia ukoloni mamboleo.

Hali hii pia tunashukuru tumeweza kuijua kwakuwa serikali iliyopo madarakani imeruhusu uhuru wa kuongea , kwani ingekuwa enzi zile habari hii ingekuwa ni Siri kubwa
Changamoto ni posho zimepanda kwa 130% katikati ya umasikini kama huu
 
1.Kodi komozi inaua uzalishaji
2.Kukopesha wanafunzi wasome chuo kikuu then hazirudi hawana ajira au mifumo rasmi ya kuwabana warejeshe.
3.Miradi kausha damu kwa wakati
4. Mafisadi na wapigaji wanaogopwa na mahakama
5.Elimu butu isiyochochea fikra za ukuzaji uchumi
6.Kuzuia vijana wako kwenda kufanya kazi nje wakalete pesa ndani.
7.Kuzuia export ya mazao nje,mazao Sio Mali ya serikali
8.Kutegemea misaada na mikopo


Haya maeneo yakitendewa kazi tutakuwa na ziada
 
Wabongo muwe na kiasi,,

Sio kila kitu kujitia kujua, Kwa kawaida mwez July had August mifumo ya fedha serikalin inakuwa imefungwa Kwa ajili ya ukamilishaj wa maandaliz ya bajet mpya.

Utaona kuanzia September Mambo yanabadilika.
Huu sasa ndo UJUAJI.

Mkuu, una maanisha wote humu hatujawahi kuishi kuiona hiyo July/August transition before?

Kuwa mvumilivu kidogo kwenye maoni ya wengine
 
Enzi zile sawa mlinyimwa uhuru wa habari lakini hakukuwai kuwa na mfumuko wa bei za kishenzi kama hizi za maushungi.watu hawali uhuru wa habari.
Watu wavivu kwa kulalamika hamuwezekani.Fanyeni kazi,acheni uvivu.
 
Pesa tunamalizia kuhonga Waandishi wa habari, Wanasheria nk ili DP WORLD apewe bandari. Tuna tatizo la msingi Kiuongozi Nchi hii.
Maono yangu, UBINAFSISHAJI WA TPA Utangazwe wazi Makampuni yote yapewe uwanja sawa wa kiushindani tupate mwekezaji wa zao la ushindani.
Sio kutuletea wajomba zenu....ova
Watu wavivu kwa kulalamika hawawezekani,acheni uvivu,fanyeni kazi.
 
HAKUNA MRADI ULIOSIMAMA KWA KUKOSA FEDHA,
Note this!
Haijawahi tokea Tanroad kushindwa kulipa wakandarasi lakini sasa hivi wameshindwa kulipa mama hela ya Road Funds inapeleka Bwala la Mwalimu.

Miradi ya maji mingi imesimama kuna wakandarasi zaidi ya mwaka hata Advance anapata mpaka mkataba umeisha hajapewa.

Mama anaenda kufeli pakubwa sana, wabunge wanalalama chini chini wanashindwa kwenda kwenye majimbo yao

Naongea kitu nakijua nipo sekta hiyo, na cionvasations za mbunge mmoja akilalamika anashindwa kwenda jimboni kwake kwani serekali haitoi hailipi wakandarasi wakaendelea na kazi
 
Back
Top Bottom