Hebu leo wakumbuke wahadhiri wa vyuo vikuu waliokufurahisha kwa jinsi ya umahiri wao wakufundisha na walivyokuwa 'fair'

Hebu leo wakumbuke wahadhiri wa vyuo vikuu waliokufurahisha kwa jinsi ya umahiri wao wakufundisha na walivyokuwa 'fair'

Jamani, ni hulka ya wanadamu kutotangaza mema ya watu lakini wepesi sana kutangaza mabaya ya watu.

Hivi karibuni kuna madaktari kadhaa walitangazwa na wanafunzi wao kwa ubaya sana! Sijui kama tuhuma walizotangazwa kwazo zilikuwa na ukweli au la!

Huu uzi naomba tufanye kinyume, tuwaseme wakufunzi wetu wa vyuo vikuu kwa majina yao kwa namna walivyo 'committed', 'fair' na mahiri katika kutoa mashule na hata walivyo fair katika kutoa na ku'mark' mitihani yenu!

Kama hukujariwa kufika chuo kikuu ww muweke mwalimu aliyekufurahisha kwa umahiri wake wa kufundisha ktk kiwango cha juu kabisa cha cha elimu ulichofikia!

Tafadhari bandugu, muelezee kidogo kivipi alikufurahisha ili kama atajua basi atiwe moyo na hayo afanyayo! Kumbuka tukitaka kuwananga huwa walimu wetu kwa ubaya huwa hatuishii kutaja majina tu bali tunaelezea kwa kirefu hata kujaza gazeti. Leo eleza hata kwa mstari mmoja tu kumjurisha alivyougusa moyo wako!

Niishie hapo
Taja nawe wako hata kama uliishiia chekechea Mkuu
 
Huyu Masenge aliwahi kugombea ubunge, alichofanywa na wajumbe ukimkumbusha ni carry over hiyo hata kama ni mtaani[emoji23][emoji23]
Masenge huwa ni wa CDM.....au alishaunga juhudi?
 
Masenge huwa ni wa CDM.....au alishaunga juhudi?

Ilikuwa mwanajuhudi enzi hizo baada ya kutoka ujeruman na degree zake, akaenda kijijini kwao wajumbe wakamfurumusha, hivi sasa hapendi kabisa kusikia siasa wala kukumbushiwa hayo makitu!
 
Ilikuwa mwanajuhudi enzi hizo baada ya kutoka ujeruman na degree zake, akaenda kijijini kwao wajumbe wakamfurumusha, hivi sasa hapendi kabisa kusikia siasa wala kukumbushiwa hayo makitu!
Bado yupo UDSM?Hajastaafu???
 
Prof. Nicholas N. T. A. Bangu
Alinifundisha Physical Chemistry SUA 1997. Ni hatari sana huyu mtaalamu. Na alishatangulia mbele za haki.
 
Prof Njabili
Prof Maghway
Dr Kiduanga
Madam Rahma
Prof Said Othman
UDSM



Mwalimu Maganga( Huyu alikua ananishushia nondo Kali za History pale Kinyala secondary kule Tukuyu Mbeya)

Caps( Hili lilikua ni jina utani akiitwa hivyo kutokana na kupenda sana kuvaa kofia. Huyu mwamba alikua pale maeneo ya Meta karibu na Meta secondary akiwa na tuition centre yake, Huyu jamaa alikua ananikamulia Language ya advance sijapata ona)
 
Late Prof.Ladislaus Lwambuka-CoET enzi hizo
Msemo wake wa siku zote "Even my mother in Bukoba will be able to identify the angle"


Sent using Jamii Forums mobile app
A similar comment was used by Prof. Mulokozi, Department of Chemistry (UDSM) in 1978. " If my mother from Bukoba gave the same answers as you did, I would have given her the same zero marks". The guy in question changed his studies from Science to Arts the same very day!
 
Dr Shika pale USSR alikuwa hatari Kwa machemical...miatisa itape deza R.I.P Dr.
 
Proff Juan Mwaikusa, Dr Mvungi mlinifunza mambo ya msingi sana, kitu kimoja cha msingi mlinifunza petience, Mungu awarehemu, sijamsahau Mwl Simwaba na Mtefu waalimu wangu wa sekondari mkae pema.

Sorry na Mwalimu Maufi wa shule ya msingi sijakusahau ukae pema peponi.

Sorry mleta mada umelenga wahadhiri but wengine we are so touched na waalimu waliotujengea misingi kabla ya kufika vyuo see you in the next life.
Mvungi yupo kwenye moyo wangu Kila nkikumbuka maisha ya chuo......alintetea kwenye point moja muhimu....naweza kusema bila yeye nsingefika apa nlipo(God is exclusive)
 
Kuna Yule wa Kule statistics kilema alikuwa anafundisha hasikiki wanafunzi wakawa wana shout "sir it is not fair" Anajibu "even God himself is not fair..... Angekuwa fair asingeniumba Mimi kiwete nyie akawaumba wazima"
 
Back
Top Bottom