zimenunulia noaZile mil50 kila kijiji mpaka leo tunazisubiri !!!!!
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
zimenunulia noaZile mil50 kila kijiji mpaka leo tunazisubiri !!!!!
Tangu niikose ile Noah yangu ya makinikia Sina Imani na hii nchi.
Tangu tutapeliwe michango yetu ya wahanga wa tetemeko la ardhi huko Kagera,nimeacha kuchangia kitu chochote kinachosimamiwa na mwana CCM.Serikali ya Magufuli ilitutaka tuwachangie wahanga wa tetemeko Bukoba ambao nyumba zao zimebomoka, hawana chakula Wala nguo. Tukachanga, mwisho wa siku michango yetu ikachukuliwa eti ikaboreshe Miundombinu.
Ule ulikuwa Ni zaidi ya utapeli na dhuluma
Sisi tuna flow na vibe mkuu yani ni sawa tuko kwenye dance tunaenda na flow la DJ sasa hivi tunaambiwa stiglers gorge itamaliza mahitaji ya umeme, same as tulivyoambiwa kwenye gas.Katika uongo mkubwa kupita mauongo yote nadhani huu ni mkubwa kupita kiasi, eti gasi ya Mtwara ingeinua uchumi wa bongo "drastically"!!!!🤣🤣.
leo cha ajabu hata Wapinzani wote wapo kimya kama kwamba fikra zao ni "blind folded" juu ya suala la gesi ya Mtwara.
sio Wapinzani wala Chama tawala wote hawazungumzii kabisa juu ya gesi ya Mtwara.
kama Wtz tumelogwa, tumepigwa bumbuwazi,!!!!🤣🤣
Huyu ngedere anae isema serekali vibaya wewe unaona sawa tuuKuna kima alisema atatoa 50 kila vilage hahaaa kumbe hata mshahara kanshindwa
Tutamuuliza kwenye kampeni zakeMagufuli alitudanganya kabla ya miaka yake mitano aijaisha atatuongezea wafanyakazi mshahara tunaelekea kwenye kampeni au miaka mitano bado jamani
Mkuu nasikia ndani ya miaka hii mitano deni limeongezeka mara dufu. Hii 40 Tr sijui kweli?!Kuna watanzania wanaambiwa Magu kalipa madeni yote hatudaiwi hata senti
Huu mkutano uliniacha hoi sana na ujumbe wake.Taratibu blaza.View attachment 1531097
Eti baba Seya!Mkapa hana watoto, watoto wake ni wa Mramba.
Kikwete alimfunga baba Seya kisa mama Salima.
TANZANIA YA VIWANDA.Kuna uongo mwingi tuliwahi kuongopewa na watanzania weangi wakauamini hadi watu wakubwa na tuliodhani wanajua mambonao wakaukumbatia. Mimi ninaanza na huu.
1. Kipindi cha Jakaya Mrisho Kikwete akiwa rais, nakumbuka magazeti kadhaa na redio kadhaa ziliwahi ripoti kuwa kuna mapacha wawili ni watanzania ila wamesoma Marekani mmoja ni daktari bingwa na mwingine ni mfanyakazi wa NASA.
Eti kwamba walikuwa amerudi Tanzania, kwa likizo fupi ambapo huyo daktari bingwa alikuwa kafanya operesheni wagonjwa takribani 8 na wote wanaendela vizuri hapa Tanzania, wakati huyo mwanaanga wa NASA ni kati ya wanaanga wa kwanza kutembelea sayari ya Mars. Habari hiyo nakumbuka ilishikiliwa bango PJ na Gerald Hando wakati wote wako Clouds. Wakadai hawataki hojiwa na vyombo vya habari mpaka wakutane na rais.
Mimi nilianza kuwa na shaka na hao mapacha baada ya kusikia tu kuwa eti mmoja wao kashafika Mars, wkati mpaka muda huo na mpaka leo hakuna binadamu ambaye kakanyaga sayari ya Mars zaidi ya vyombo kama Rovers. Na nadhani Kikwete alikuwa mjanja hakuwahi kuwaalika ikulu.
2. Project Kubwa ya kujenga Kigamboni. Nakumbuka kuanzia mwaka 2009 mpaka 2014 nadhani, kulikuwa na video zinazoonyesha jinsi Kigamboni itakavyojengwa na wamarekani, viwanja kigamboni vikawa havishikiki kigamboni ikawa lulu. Zile video zilikuwa zinavutia sana. Jamaa yangu aliuziwa maeneo kule kwa pesa ndefu sana lakini sijajua hii story iliishia wapi, na viwanja vikaanguka thamani hadi alipotaka kuuza hakuweza kuuza hata robo ya pesa aliyotoa.
Nitarudi kuongeza
Hiyo ya nne imenichekesha sana [emoji23],[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]1.Milioni 50 kila kijiji
2.Tanzania itakua Dona kantri
3.Acacia wakitulipa kila mtanzania atamiliki Noah
4.Magufuli ni Yesu.