Pre GE2025 Heche: Posho siku moja tu Bungeni tulikuwa tunalipwa laki nne, halafu Mwalimu kwa mwezi unamlipa laki 4!

Pre GE2025 Heche: Posho siku moja tu Bungeni tulikuwa tunalipwa laki nne, halafu Mwalimu kwa mwezi unamlipa laki 4!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Ukisikia hazina za taifa ,, ndiyo watu kama hawa ,, mimi sina cha kuongezea zaidi ya kumuombea kwa mungu amzidishie rehema na baraka tele katika kizazi chake chote kwa kuwa muwazi,,, kwakuwa mtu asiyepindisha pindisha mambo
Mimi hapa napata wasiwasi! Kumbe hata yeye aliwahi kulipwa hizo posho lakini hakuzikataa na wala hakuwahi kuongea haya wakati huo! Sasa ndio kukumbuka au kuna nini nyuma ya pazia?
 
Mliambiwa hawa ni wanaharakasti hamuelewi..

Kwenye office , Head of Sales analipwa Mil 18, na dereva analipwa laki 3 , hapo kuna unyonyaji mmoja ampunguzie mwingine?

Nilifikiri kwa mtu mwenye hadhi yake angeongelea Muundo wa Bunge na namna gani wanaweza punguza vikao na safari zisizo na tija yeye analinganisha mishahara?

Duniani kote watu wanalipwa kutokana na Value na Impact anayoweza sababisha kwenye jamii..

Kalangabhao
We nae ni mpumbavu kabisa!!, Hebu tutajie impact ya wabunge wa ccm kulipwa pesa hizo?
 
Mimi hapa napata wasiwasi! Kumbe hata yeye aliwahi kulipwa hizo posho lakini hakuzikataa na wala hakuwahi kuongea haya wakati huo! Sasa ndio kukumbuka au kuna nini nyuma ya pazia?
Punguza kutoelewa mambo!!, Amekwambia akiukata ndio utashuka?, Wabunge wa ccm wapo wangapi bungeni waliikubali hoja yake?.
 
Punguza kutoelewa mambo!!, Amekwambia akiukata ndio utashuka?, Wabunge wa ccm wapo wangapi bungeni waliikubali hoja yake?.
Hata kama wabunge wa CCM wasingemuunga mkono, basi angalau angesema hiyo hoja wakati huo!
 
We nae ni mpumbavu kabisa!!, Hebu tutajie impact ya wabunge wa ccm kulipwa pesa hizo?
Sasa upumbavu wangu ni kitu gani?

Maisha yako yakiwa duni unanipa hasira mimi?

Wabunge wote Impact yao inafanana?

Umewahi kwenda Ruangwa, Chalinze, Dodoma, hivi karibuni?

Ushabiki wa vijana unawaharibu hamuwez chambua mambo kwa logic
 
Jitahidi kutumia ubongo wako vizur.je kaongea ukweli au ni uongo??kunufaika kwake na fedha za mazombii hakuwezi kuondoa ukweli aliousema tumia akili kidogo ondoa adui ujinga.
Embu twende taratibu,
Unataka wafanyakaz wote wafanane mishahara?

Ni bunge la wapi umewahi sikia mbunge analipwa hela ndogo?

Tumieni akili, haya matusi mtaendelea kulazwa jela kila mara na wengine kupotea kabisa, shaur yenu.
 
Back
Top Bottom