Uchaguzi 2020 Hedaru: Dkt. Magufuli amuagiza katibu mkuu TAMISEMI apeleke milioni 100 kukarabati kituo cha afya

Utakuta watu kama nyie kodi hamlipi ila mnataka kodi ziwanufaishe nyie.
Kama hupandi ndege ni wewe
 
Ahadi kama hizi zinapotolewa kwenye kampeni ni rushwa,tume ya uchaguzi ya ccm ndiyo hivyo tena.

Mbwa hamng'ati mmiliki wake.

Fedha zinatoka bila utaratibu,Makofuli ndiye rais,bunge na mahakama...uongozi wa hivyo kwelikweli
 
Hizo ndege zimeenda Nchi zipi prime zinazoleta watalii wengi hapa Nchini?

Sent from my TA-1024 using JamiiForums mobile app
Dah asee kweli upinzani upo ,yani ununue ndege leo then kesho zianze safari unadhani hizo ni sawa na Hice ,usafiri wa anga unataratibu zake nadhani utakuwa shahidi kuna mikoa hata hizo ndege za ATCL zilikuwa hazifiki ila sasa zinafika na usiseme tu kuwa zinaenda wapi utakuwa ni muongo.
Hizo ndege zinaenda India na baadae China,kwa sasa zinaenda soko la bara hili la Afrika kama South Africa ,Entebe,Comoro ,Kenya kwani hizo nchi zipo bongo .
Unadhani ndege hizo zinatosha kwenda ulaya na Marekani ndio mana zinatakiwa walau kubwa kubwa ziwe hata Sita unataka twende bila Stategic Planning kama vile mlevi kaona Barmed hii ni biashara ya kimataifa mzee haihitaji kukurupuka utaharibu soko lako unatikwa ukianza hakuna kufaulisha ni mwendo wa hii inapaa hii inatua Wazungu hawapendi Kucancell route kisa ndege imechelewa.
Tulia mambo yanakuja mazuri Bullet Train kutoka Korea zinafanana na kichwa cha ndege mbona mwaka huu mtakonda.
 
Pamoja na umuhimu wa mradi lakini timing ya kutoa hela inaashiria rushwa ya dhahiri kabisa. Ila Vibogoyo TAKUKURU hawatafanya lolote
 
Hii ni rushwa ktk uchaguzi, na si mara moja katoa. Hajakemewa hata mara moja. Ingekuwa ni hoja ya kwa nini hazijaletwa wakati zilipangwa, si kosa. Kitabu kinacho andikwa rafu za Magufuli kwenye kampeni, cha kwanza kimejaa na kufungwa.
 
Akili fupi unashindwa kuelewa kwamba hizo 490 B ndani ya miaka miwili zinaweza kusababisha 1Trilioni? Kupitia ndege tunaweza kupata watalii ambao watalipa tozo za utalii, watalipa nauli ya ndege, hoteli zitafanya biashara na kutoa kodi. Achilia mbali ajira kwa tour guide, ajira kwa wafanyakazi wa ndege ajira kwenye hoteli.
Akili za nyumba zinaangalia leo haziangalii kesho na kesho kutwa.
Magufuli tumemwelewa sana mitano mingine inamhusu.


Sent from my Infinix X655 using JamiiForums mobile app
 
Huku mikoani kwa mpango wa 'force account's darasa moja linajengwa kwa sh 7m. Hiyo 490b ni madarasa 70e! Itapunguza sana uhaba wa madarasa.
 
Bunge limeidhinisha lini na wapi
Mkulu unachanganya mambo
Hizi ni dakika za kuzungumza haya kweli mbona hujifunzi?!
Toeni hiyo millioni 100 mzitafune
Kwani in five yrs hukujua hakuna kituo cha Afya
Hizi ahadi zipo tangu 1949 bado tu
 
Sheria,kanuni na taratibu wazitunge na kuzipitisha kibabe wenyewe lakini hawawezi kuzifuata. Hii ni rushwa par se.
 
Hivi ukiacha Mahera, huyu mwenyekiti wa hiyo tume mbona hasikiki hata kukohoa?
 
28/10 pigachini mtu
 
Milioni 100 ikamalizie majengo, ijenge sehemu ya kuhifadhia maiti, Ikanunue Xray si ndio baadae utakuja kumtumbua mtu useme amejenga chini ya kiwango na kununua mashine mbovu!

Let us be serious guys!

Haya maigizo yataisha lini!

Takukuru!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…