HezibuLlaah hawana tena woga kupigana na Israel.Warusha maroketi wanapotaka.Netanyahu aitisha kikao kujadili hali isiyokawaida.

HezibuLlaah hawana tena woga kupigana na Israel.Warusha maroketi wanapotaka.Netanyahu aitisha kikao kujadili hali isiyokawaida.

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Maroketi ya Hezbollah hapo jana yamerushwa maeneo nyeti sana ya Israel hasa kaskazini.Hali hiyo imemfanya Netanyahu aitishe kikao cha dharura kujadili mabadiliko ambayo yamezidisha hofu kote kote nchini humo.
Ving'ora vimewashwa kote kuwafanya watu kuingia kwenye mahandaki yao.Uwanja wa bengurion umefungwa kwa muda.
Kwa upande mwengine HizbuLlaah wamekanusha madai ya Netanyahu kwamba walifanikiwa kuipiga mitambo yote ya kurushia maroketi wakati yakiandaliwa kufanya mashambulizi.
Baada ya mvua hiyo ya makombora HizbuLlaa wamesema hatua ya mwanzo kulipiza kisasi cha kifo cha kamanda wake Fuad Shukr imemalizika.Katika ujumbe huo wamesema mashambulio yao dhidi ya Israel yatasimama mara tu vita vya Gaza navyo vikisimamishwa.

Israel stages heavy airstrikes on Lebanon as Hezbollah launches attack over slain top commander

 
Hesbullah mbona kama wao ndio wanaooumizwa zaidi. Wao wanatia hofu, israel ikijibu inaua kabisa kuanzia watoto hadi makamanda wakuu.
20240825_085125.jpg

Hapa inaonyesha wananchi wanataharuki, pia vyuo vikuu vimefungwa. Mbinu yao inaweza kuwa na faida maana inafanya pasikalike huko kaskazini. Israel ifike wakati ijitanue iteke kabisa Lebanoni yote.
 
Hesbullah mbona kama wao ndio wanaooumizwa zaidi. Wao wanatia hofu, israel ikijibu inaua kabisa kuanzia watoto hadi makamanda wakuu.
View attachment 3078558
Hapa inaonyesha wananchi wanataharuki, pia vyuo vikuu vimefungwa. Mbinu yao inaweza kuwa na faida maana inafanya pasikalike huko kaskazini. Israel ifike wakati ijitanue iteke kabisa Lebanoni yote.
Umechanganya mambo na picha.
Ambako hakukaliki kwa sasa ni kaskazini ya Israel na hao unaowaona ni mayahudi wakikimbizana kuingia mashimoni mwao.
 
Issue sio kurusha hayo mafashi fashi tunataka kusikia yameleta madhara gani? Kama kurusha mbona Toka Oct 7 wanarusha tu?
Wao kila siku wanarusha bila mafanikio.
Naona kama wanaumia wenyewe zaidi maana majibu ya israel huwa yanagonga moyoni kabisa
 
Issue sio kurusha hayo mafashi fashi tunataka kusikia yameleta madhara gani? Kama kurusha mbona Toka Oct 7 wanarusha tu?
Askari kadhaa na waisrael wameshakuja kutokana na hayo unayoyaita mafashifashi na watu wamekimbia majumba yao.Yote hayo huoni kuwa ni madhara.
Kubwa zaidi tunalozungumza hapa ni kile kiwango cha kutokuoga kupigan na taifa kubwa kisilaha linaloungwa mkono na Marekani.
 
Kama hayagongongi moyoni mwa Israel basi wasingeitisha vikao na wala wasingewasha vingora kuwashtua watu wao.
Mafanikio yao ni terror au kuwaweka watu kwenye taharuki. Hilo wamefanikiwa na hicho ndicho wanakishughulikia wazayuni.
 
Kwahiyo webabu,Mimi nikimuuwa baba yako.wewe unakuja kulusha mawe juu ya paa la nyumba yangu Kisha unajipongeza kuwa umelipa kisasi?
 
Askari kadhaa na waisrael wameshakuja kutokana na hayo unayoyaita mafashifashi na watu wamekimbia majumba yao.Yote hayo huoni kuwa ni madhara.
Kubwa zaidi tunalozungumza hapa ni kile kiwango cha kutokuoga kupigan na taifa kubwa kisilaha linaloungwa mkono na Marekani.
Lete hiyo habari inayoonyesha askari kadhaa wa IDF wamefariki kutokana na hayo mafashi fashi hatutaku mawaidha.
 
Umechanganya mambo na picha.
Ambako hakukaliki kwa sasa ni kaskazini ya Israel na hao unaowaona ni mayahudi wakikimbizana kuingia mashimoni mwao.
Kwan kusin mwa Lebanon kunakalika sheikh
 
Israel atajikuta miaka na miaka nchi iko katika state of war huku war yenyewe haipo ndio mtego alioingizwa na iran. Wanajifanya wana akili lakini muajemi kawazidi mbali sana na hapo tatizo ni mmarekani tu ndio anamuumiza kichwa muajemi ila sio hao mgambo wa kizayuni
 
Back
Top Bottom