Hidden cancer cures

..Kuhusu cancer nimetumia miaka saba kusoma hayo makitu kaka Na hata navyoandika ujumbe huu namalizia zamu yangu wodi ya watoto wenye kansa...so hamna jipya la Zaidi utakalonieleza kuhusu hilo...

Sloan Kettering wana uzoefu wa miaka 130,itakuwa wewe miaka 7 tu.Unatakiwa uje na hoja za kupinga ninachosema.Sio kuleta uzoefu wako wa upofu.

..Natumia simu ila nikipata muda tutajadili tu kwa faida ya wote hata Na mimi pia...elimu ni pana sana na kubali hufahamu kila kitu ndio utajifunza...

Kati ya yote uliyosema hapa ndio umeongea kama mtu mwenye ubongo wa kufikiri.Na mimi nakusubiri kwa hamu kubwa.Kwenye HIV/AIDS nilipata madaktari waliopinga,hivyo najisikia faraja pia hapa kupata madaktari wapingaji.

..Nini kutibu Kansa kaka...babu wa kikombe alitibu mpaka na ukimwi...

Hapa kwenye ukimwi ndugu daktari nilishaongelea,labda wewe bado uko gizani,lakini kwa kifupi ukimwi unatibika vizuri tu na hautishi,hata malaria ni hatari zaidi ya ukimwi,ukimwi ni ugonjwa rahisi sana kuutibu na hauambukizwi kwa njia ya ngono kama unavyodhani au ulivyoambiwa,inaonekana wewe doctor utakuwa gizani sana.

..Hivi unajua kuna some sort of cancer huwa zinapotea tu bila tiba ?

kwa kuwa uko gizani hivyo unadhani umeongea kitu kigeni.Sasa angalia quote yangu mwenyewe hapo chini.

...Our bodies reverse different types of cancers everyday in our lives without our knowledge due to strong immune system. Those with weak immune systems will find out this battle in the hospitals....


.....hizo hizo alternative medicine zina hadi degree marekani tena doctorate kabisa kama MD ila hujiulizi mbona hospitalini watu hawapungui ? Nitarudi kaka

Hapa unahitaji nikupige shule nzito sana.
 

Mkuu Deception, HESHIMA KWAKO KWA UZI HUU WENYE MANUFAA.
Mkuu mimi ninaomba msaada wa
(1)Dosage za mihogo na aina gani inayofaa kutumika wakati wa hayo matibabu (mibichi au iliyochemshwa) hasa kwakuzingatia kwamba mkuu RGforever hapa juu alivyobainisha kwamba ina high concentration za Vitamin B17.
(2)Dosage ya Sodium bicarbonate na je nihii hii inayotumika majumbani kwetu na wakina mama? pia inatumikaje wakati wa matibabu maana kwa ninavyojua mimi inapatikana(kama nihii ya majumbani) katika form ya powder, mf labda unachanganya na kimiminika chochote(naomba vipimo) au unaibwia ikiwa kwenye form yake ya powder (pia naomba kipimo chake).
natanguliza shukrani kwa elimu hii maridhawa, ubarikiwe sana
 
Deception
Bob Marley yasemekana alikufa kutokana na kansa ya ngozi(Melanoma) kusambaa mwilini, naye ni alikuwa mtumizi wa bangi (kuvuta). Je unasemaje kuhusu hilo.
 
Last edited by a moderator:

Mkuu ukifuatilia vizuri reply zangu taratibu toka mwanzoni kabisa utajua yote hayo kasoro hilo la sodium bicarbonate pekee ambalo sijalizungumzia kwa undani.Ninakwambia hivyo kwa kuwa nataka uelewe kwa undani cancer ni nini,sayansi yake ikoje,inasababishwa na nini na sayansi ya matibabu yake ikoje,utajua mambo mengi zaidi ya hayo kama utanifuatilia vizuri toka mwanzo.

ANGALIZO:
Kuhusu tiba nilisema kwamba,kwa mtu ambaye tayari ni mgonjwa anatakiwa atumie concentrates za hivi vyakula au supplements zake ili kuharakisha kupona na si vyakula vya kawaida kama ulivyovi quote.Vyakula hivyo kweli vina vimelea vya kutibu cancer lakini si kwa kiwango kinachotakiwa kuua cancer cells,hivyo inatakiwa utumie concentrates za hivyo vyakula.Lakini kwa mtu ambaye si mgonjwa anaweza tu kula hivyo vyakula ili kujikinga na cancer.Vitu hivi inatakiwa viwe vibichi,mfano mihogo mibichi.Kuna concentrate ya vitamin B17 ambayo mimi ninayo,ni very effective kuua cancer cells na kuondoa uvimbe/tumors wa cancer yoyote,lakini ili ujue taratibu zote za tiba hii inabidi unifuatilie toka mwanzo.
Mimi nimeshatumia tiba hii ya vitamin B17 kumtibu mtu mwenye cancer.
 
Deception
Bob Marley yasemekana alikufa kutokana na kansa ya ngozi(Melanoma) kusambaa mwilini, naye ni alikuwa mtumizi wa bangi (kuvuta). Je unasemaje kuhusu hilo.

Unajua mkuu,hizi ndizo habari zinazowafanya watu wachanganyikiwe na wasielewe ukweli ni upi.Ili kufahamu ukweli wa habari kama hizi lazima watu wawe na smart brain kwanza halafu pili, wawe tayari kusikia mambo mapya ambayo hawajawahi kuyasikia,vinginevyo itakuwa ni sawa na kupaka rangi upepo.Kwanza inabidi ufahamu kwamba Bob alikuwa adui wa CIA,sasa sitaki kwenda huko sana,kama unaelewa vizuri siasa za dunia hii unaweza kupata kitu hapo.Fuatilia vizuri habari za kifo chake utapata mambo mengi sana tofauti.

Kuhusu bangi;bangi haiwezi kutibu cancer kwa kuivuta.Nimeeleza vizuri jinsi bangi inavyoweza kutumika kama tiba ya cancer.Extract kutoka kwenye bangi inayobeba THC na/au CBD ndiyo inaa uwezo wa kuondoa cancer,kwa jinsi extract hii ilivyo na nguvu unatakiwa ule kidogo sana kwa mara moja,yaani kidogo kama ukubwa wa tone la maji halafu mara mbili au tatu kwa siku.Sasa kiwango hicho huwezi kukipata kwa kuvuta,kuivuta bangi kama tiba ya cancer ni sawa na kulamba kwa ulimi dawa mseto mara moja tu bila kumeza huku ukitegemea kutibu malaria.
 
Hongera sana mkuu deception,binafsi niliandika post moja humu nikasema kila mtanzania aliyepitia shule na hata wasioenda shule wanajua kuwa magonjwa sugu uliyoyatolea ufafanuzi mkuu deception hayana tiba ila kwa mujibu wa elimu rasmi,kwahiyo hata hao madaktari wanafundishwa kupitia hiyo elimu rasmi na wanafundishwa kuwa magonjwa hayo hayana tiba na mafundisho yao yataegemea huko huko kwamba hayana tiba.Hata kisa cha huyo bob marley juu ya kifo chake ukisoma source tofauti kina utata mwingi.hao madaktari wanapinga inabidi wakubali kupokea elimu kutoka upande mwingine wa shilingi na sio kubisha tu pasipo kuwa na strong facts zaidi ya sijui kikombe cha babu.Basi hao madaktari wajiulize swali moja kwa nini huyo babu wa kikombe hajachukuliwa hatua yoyote ya kisheria?kuna nini hapo au ulikuwa ni mpango tu wa kuaminisha watu kuwa huo ugonjwa hauna dawa? Tunavyopata elimu kama hizi si vibaya tukafungua fahamu zetu ambazo zimeaminishwa kuwa magonjwa flani hayana dawa na kutoa reference za kikombe cha babu pasipo kutafakari zaidi.kitu cha muhimu hapa ni kunote hatua zote alizozielezea deception kwani nyuzi kama hizi huwa hazikai muda mrefu.
 

Ahsante mkuu kwa majibu yako, Ninawezaje nami kupata concentrated B17 sababu nina tumors sehemu mbalimbali za mwili wangu, tafadhali naomba msaada wako ndugu kabla mambo hayajazidi kuwa mabaya kwangu, jibu vyovyote vile hapa au kwenye PM.
Natanguliza shukrani mkuu Mungu akujalie
 

Mkuu kuna daktari amesema atarudi tena hapa,ninakuhakikishia kama kweli atarudi utajionea wewe mwenyewe vichekesho hapa kama wale wa kwenye ule uzi wa HIV/AIDS.Yaani hawa jamaa wanachukulia vitu kama hivi kirahisi sana eti kwa kuwa wamepewa dhamana ya udaktari.Huwa wana underestimate karibu kila kitu ambacho hakiendani na jinsi walivyofundishwa.Sasa wewe subiri ujionee mwenyewe atakaporudi.
 

Mkuu sijui undani wa tatizo lako,ninakushauri uende hospitali kwa vipimo zaidi ili kupata uhakika kama hizo tumors zimesababishwa na nini,sio kila tumor ni cancer,pengine una upungufu wa madini fulani.Mimi sio daktari ila ninaheshimu fani ya udaktari kwa mambo mengi sana,ila kwenye magonjwa haya sugu ukweli uko palepale kwamba tumedanganywa.Sasa ili uwe na uhakika wa chanzo cha tatizo lako,ninakushauri ukafanye vipimo,ukishajua mapungufu uliyonayo ndio utakuwa na uhakika wa tiba utakayoifuata,hata mimi naweza kukushauri endapo tu nitajua kiini cha tatizo lako.

Si vibaya pia ukajua jinsi ya kuipata vitamin B17 kwa kuwa umeniuliza,lakini kumbuka kwenda hospitali ukapime vipimo vyote muhimu ili uwe na uhakika na kiini cha tatizo lako.Hapa Tanzania sijawahi kusikia mahali wanapouza hii vitamin,lakini kuna website nyingi za nje unaweza kupata hii vitamin B17 katika tablet form,powder form au IV form.

Kwa mfano,nenda kwenye web hiyo hapo chini na uandike vitamin B17 kwenye nafasi ya wazi na zitakuja option nyingi tu.Unaweza kutumiwa kwa njia ya DHL au vinginevyo.Kama utapata powder form huwa ina bei iliyoshiba kidogo kwa kuwa inauzwa kuanzia 1kg kwenye plastic bag,hii 1kg ya powder form ni nyingi sana na inaweza kutosha kwa dozi ya watu hata 3,kama utafanikiwa kupata tablet au IV bei yake ni ndogo sana kutegemea na idadi na ukubwa wa container yake,jaribu wewe mwenyewe kufuatilia utajua mengi tu zaidi haya.Natoa link hii ili kuwasaidia na wengine ambao hata kama hawaamini suala hili lakini wanaweza kukumbwa na tatizo hili wao au ndugu zao halafu wakashindwa kujua pa kukimbilia baada ya kupoteza matumaini kwa tiba za hospitali.

Alibaba.com andika vitamin B17 katika nafasi ya wazi.
 
Mkuu deception naomba nijue tu dalili za breast cancer for men pls msaadaa
 

Thanks Sir
 

Mkuu Deception: Nakupa like na hongera sana. Nimewahi kuchangia kwenye hoja moja ya HIV na Matumizi ya ARV na kwa nini watu wanakufa kwa kunywa sumu (Dawa). Ni kweli njia kuu na ya kwanza kwa kufight any carcinoma cells, low white cells , immunity imbalance ni kuwa na lishe sahihi . Ukiweza kucheza na lishe tu hospitali utaisahau.
Naomba wanajamvi walio curios wasome kitabu kinaitwa "Deadly Medicine and Organized Crime- How Big pharma has corrupted healthcare" utaona mwandishi alivyoanisha jinsi makampuni makubwa yalivyo na mikakati madhubuti ya kukamata serikali zetu na wakati mwingine kupindisha research ili dawa ziuzike.
Pia watu wanaotaka kujifunza zaidi kuhusu cancer and cures wanaweza kusaka kitabu kinachoitwa "Edgar Cayce on healing foods: Body , Mind and Soul" humo anaeleza umuhimu wa kuwa na alkaline state katika lishe na damu .
Nina shuhuda wa watu wawili waliokuwa na HIV in very chronic stages katika nchi ya ulaya na baada ya kulazwa alishauriwa aache ARV ... Na hadi leo ni 9 years since that incidence hao watu wanaishi vizuri kwa kuhakikisha afya zao ni zina uwiano sawia wa lishe.

Wana jamvi-- Dawa ziwe ni very last resort ila dawa in general ni sumu , zinalenga kufight bacteria , je zinachagua waue bacteria gani while our bodies have natural bacterias as well: Tuchukue muda , tusome , tujifunze kuuliza . Kweli madaktari wamesoma ila tuulize inapobidi. Inasikitisha sana kila ukiandikiwa dawa ni mara chache sana madktari anajali kukushauri what to eat , how and when. Kwa kuwa miili yetu ndio hazina zetu basi tuwe na majukumu ya kuitunza kwa lishe sahihi.
 
Hayasemayo Deception si ya kuzusha wala ya kubuni ila kwa vile waliowengi wameweka dharau na kutojali kwa vile wameathiriwa sana na umagharibi, walitegemea waje wazungu kutuambia kinaga ubaga ili waamini, ingia HAPA
 
Last edited by a moderator:
Hayasemayo Deception si ya kuzusha wala ya kubuni ila kwa vile waliowengi wameweka dharau na kutojali kwa vile wameathiriwa sana na umagharibi, walitegemea waje wazungu kutuambia kinaga ubaga ili waamini, ingia HAPA

ndugu achana na wazushi hao...jifunze kuchuja habari zinazopatikana online....hata hayo anayoleta deception ni umagharibi pia. Mtapoteza muda bure mwisho wa siku mnakuja hospitali mko terminal stage....kuna mzee mtoto wake ana Ewing's sarcoma alikataa mtoto wake asitibiwe na chemo sasa leo kaja mtoto mguu umeoza inabidi amputation...acha kabisa haya mambo yasome tu online wengine tunayaishi
 
Kutokana na kutingwa na mihangaiko nimechelewa kumjibu bwana deception ila sasa nitajaribu kadri nitakavyoweza natumai watu wengi watajifunza…

Kwanza kabisa nitaeleza kwa ufupi kuhusu kansa maana hapo ndio tumetofautiana na bwana deception, na itakuwa kwa faida ya wengi maana pamoja na yeye kuielezea vizuri, ameiandika kwa lugha ya kiingereza kwa hiyo mimi nitaelezea kwa Kiswahili.

Miili yetu imejengwa na viini hai (cells). Tabia ya cells ni kujigawanya mara mbili (cell division) mpaka itakapochoka na kufa. Kujigawanya huku husimamiwa na genes. Kila cell inapojigawanya kuna makosa hufanyika ila genes inayosimamia ugawanyo huu utafuta makosa hayo na kujaribu kuyarekekebisha.

Wakati mwingine makosa hayo hushindwa kurekebishwa na kusababisha cells kujigawanya bila utaratibu na kwa kasi zaidi ya kawaida na kutengeneza cells zisizo za kawaida….hii husababisha tumors ! Tumors hutengeneza mishipa ya damu ili kuizunguka ili kuhakikisha haifi(angiogenesis)…Kupitia mfumo wa damu cells za tumors usafiri kuelekea sehemu nyingine za mwili na kusababisha KANSA.

Nini husababisha tumors ambazo hupelekea kufanya kansa ndani ya mwili? Kwa ufupi hakuna sababu moja inayosababisha kansa. Ni mjumuiko wa vinasaba tunavyorithi (genetic), mazingira yanayotuzunguka (air pollution etc), aina ya maisha tunayoishi (uvutaji wa sigara nk) maambukizi ya virusi na kadhalika.

Njia bora Zaidi ya kupigana na tatizo la kansa ni uzuiaji (prevention)...kansa nyingi zinaweza kuepukwa kwa kubadili aina ya maisha kwa kula vizuri, kupunguza uchafuzi wa mazingira, kupunguza matumizi ya sigara na pombe, kujenga tabia ya kupima afya na kadhalika..

Tiba ya kansa imegawanyika katika aina tatu….upasuaji, tiba ya mionzi (radiotherapy) na tiba ya kemikali (chemotherapy). Kama zilivyo tiba nyingi za magonjwa mengine…tiba za kansa zina madhara na mapungufu yake pia mfano chemotherapy haiwezi tibu kansa ya ubongo pia sio mara zote hufanya kazi. Pamoja na mapungufu hayo bado zimeonyesha mafanikio makubwa kwa wagonjwa.

Bwana deception ni shabiki wa tiba asilia (naturopathy treatment) na anasimamia hasa tiba kupitia chakula..Nakubaliana nae kuwa chakula ni tiba ndio maana nimesema kula vizuri kunaweza kuzuia kansa kwa kiwango kikubwa ila sikubaliani nae kuwa baada ya kansa kutokea basi diet Fulani inaweza kutibu hiyo kansa…Ni ukweli kwamba kama mwili ungeachwa ujitibu wenyewe labda na chakula tu basi binadamu asingeweza kuishi zaidi ya miaka 45….. hii inathibitishwa na kuongezeka kwa survival rate ya wagonjwa wa kansa kwenye nchi zilizoendelea kuliko nchi masikini ambazo wagonjwa wa kansa hukosa tiba sahihi nilizotaja hapo juu. Pia tukubaliane kwamba hizo tiba asilia “natural remedies” zilikuwapo kabla ya hii mainstream medicine ila kwa sababu haina scientific facts haijawahi kuwa na mafanikio kama mainstream medicine. Natural remedies ni placebo tu hamna la Zaidi.

Pia ndugu zangu wasidanganyike na neno “natural” maana sio kila kitu natural ni safe au effective. Hawa wanaojiita naturopathy doctors hawana natural diagnostic tests zozote…hata explanation ya magonjwa wameiba kwenye mainstream medicine maana kabla ya hapo hawakuwi kuelezea jinsi ugonjwa unavyotokea (physiopathology) kwa kutumia scientific facts, yote haya yamefanywa na mainstream doctors na scientists ambao leo hii wanaitwa wasiojua ama waficha tiba/ukweli.

Kinachoumiza hawa wagonjwa baada ya kuhangaika na tiba za aina hizo hurudi hospitali wakiwa terminal stage.

Hakuna kitu chochote kilichofichwa....hizi tiba za natural remedies zipo miaka tele na mpaka leo kuna clinics ziko wazi huko magharibi kwa kila mtu anayetaka kwenda kujaribu.... Ila mafanikio yake huwezi kucompare na mainstream medicine ndio maana mahospitalini kumejaa.

Just a simple fact….nchi kama ya Tanzania ambayo wananchi wengi hawana access na tiba za mahospitalini kama marekani tungetegemea life expectancy yetu iwe juu lakini sivyo hivyo kabisa….pamoja na kutegemea hizo natural remedies bado magonjwa madogo madogo yanatushinda.

Ndugu zanguni dawa ni kuishi healthy life kwa kula vizuri, jali usafi, fanya mazoezi, jenga utaratibu wa kupima afya hata kama huna magonjwa, na mwone dakari ukihisi ugonjwa. Haya mambo ya kutibu kansa na mihogo yalishatuponza tusirudie kosa. Diet itabadili vipi gene mutation jamani.

Mwenye macho aone....nakaribisha majibizano ya kistaarabu...ukileta jazba sitajibu.
Deception RGforever kupe
 
Last edited by a moderator:

Kumbe ulishampa vidonge vyake.... Yote anayoeleza nimeyasoma miaka mingi iliyopita na n upotevu tu wa muda..
 
Kumbe ulishampa vidonge vyake.... Yote anayoeleza nimeyasoma miaka mingi iliyopita na n upotevu tu wa muda..

Je umesoma jinsi nilivyomjibu?Unajua kwa nini hakurudi tena kujibu maswali yangu?Bias itakufanya ukose mengi sana ndugu yangu.
 
Ngoja nijaribu kujibu hili la life expectancy, ya Tanzania ni fupi kwa sababu wengi wetu hatuna uwezo wa kula vizuri( umaskini ndo kikwazo)Uwezo pia wa kuwaona madaktari mara kwa mara hatuna kwa sababu mara nyingi(sio zote) kunahuitaji pia hela ndo maana tunakufa mapema.
 

Sasa wewe inabidi umueleze jinsi ya kuchuja kama kweli unataka kumsaidia.Pia ni suala la common sense tu kujua kwamba si wote wanaofanya tiba asili wana uwezo wa kutibu magonjwa kama haya,pia si madaktari wote wa tiba za magharibi wanaoweza kutibu wagonjwa kwa usahihi,hii ni common sense tu wala hukuhitaji kutuambia hayo.Kwani hata wewe hujui kwamba hata ninyi mnaua watu bila kukusudia kwa sababu ya ukosefu wa uelewa wa kutosha?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…