Hidden cancer cures

Hidden cancer cures

Ila Mkuu Deception nina Maswali mawili ya Kuanzia..

1. Je mtu atumie mda gani Dozi ya Kuweka Mwili Katika Hali ya Alkaline. Mfano Kutumia Juisi ya Malimao

2. Na Muda Gani pia Mtu atumie kuondoa Sumu mwilini..
 
Nimefarijika sana na elimu hii mimi kidogo nina ushuhudi wa tiba asilinza mimea:

Baba yangu mzazi tokea nimekuwa sasa zaid ya miaka 25 iliyopita sijawahi mshuhudia akienda hospitali kutibiwa kwa homa wala tumbo, mara moja ambayo naikumbuka baba yangu alienda hospitali ni ajali kwenye jicho ambayo ilisababisha jicho lake kuondolewa,

Ni mtumiaji mzuri wa aloevera juice ile ya asili yani anakatakata anachemsha anakunywa, sikumbuki ni mara ngapi kwa wiki au mwezi ila nilikuwa naishuhudia mara kadhaa, sikuwa naelewa au nahisi ilikuwa hainihusu ila ni mara nyingi,

Sikuwahi kumuona baba yangu akinywa soda toka nimezaliwa na kuwa na akili ya kuitambua soda, siwezi kusema hajawahi kunywa ila sijawah muona,

His favourate food ni mboga za majani, ugali wa dona, maziwa, mihongo kuna viazi vikuu na magimbi.

Sijui wala sitaamini mtu akiniambia baba yangu amekula chips sijawahi kuhisi kama hata kuwaza ashawahi kuwaza, chumvi iliyozidi kwenye chakula itamfanya asile chakula, yeye husema ni bora ale chakula kisicho na chumvi kuliko kula chakula kilichozidi chumvi,

Nataka kusema nini hapa!?

Umri wake ni zaid ya miaka 70 ila ana nguvu za kutosha nadiriki kusema akisimama na mwanae wa 2, na 3 wanaonekana wazee au wamelingana kwa uimara wa mwil, anafanya sana mazoezi so anauwezo mkubwa sana wa nguvu na uimara,

Mkuu Deception, tunashukuru sana kwa hii elimu ya bure naamini itatusaidia na kubadilisha uelekeo na utaratibu wa maisha yetu kuelekea ule unaofaa
 
Nimejaribu Kutafuta Source Za Vitamin B17 nimepata hizi hapa hope zitasaidia

Zinazopatikana kwa Urahisi zaidi na Zina High amount

1. Mihogo (cassava)
2. Mbegu za Mapeazi
3. Mbegu za Apple/Tufee


Zingine unaweza Pata hapa
Foods Containing B17 (Nitrilosides)

Mkuu RGforever ahsante,nimeangalia hiyo website ulioiweka hapo ,nimekuta vitu vyingi ndugu zanguni tuleni Mihogo,viazi vitamu, magimbi, Maharage .
 
Mkuu RGforever ahsante,nimeangalia hiyo website ulioiweka hapo ,nimekuta vitu vyingi ndugu zanguni tuleni Mihogo,viazi vitamu, magimbi, Maharage .

Shida ya magimbi zinatoka kwa msimu, ingekuwa ni kila siku aaaa ningekula sana, yaani jamii za mihogo ndo zinatokaga kwa misimu sana!
 
Shida ya magimbi zinatoka kwa msimu, ingekuwa ni kila siku aaaa ningekula sana, yaani jamii za mihogo ndo zinatokaga kwa misimu sana!

Si mbaya ,mbona hata matunda mengi ni ya msimu.Ukitumia wakati wa msimu wake ,hivyo virutubisho vyake vinakuwa mwilini.
 
Watu ambao hawajaelimika, sanasana Waafrika wanakufa kwa speed sana sababu ya vitu kama hivi, ulichoandika hapo juu hakina ukweli wowote! kusema pharmaceutical industries zinafaidika sana ndo sababu wanaziba ukweli kuhusu treatments ni uongo mtupu.

Mkuu unajua kweli hata process ya cancer ilivyo? tatizo moja la mtanzania akiambiwa tu kua achana na hizo dawa za wazungu zina madhara, tumia hii ya asili anarukia fasta, tena kudanganywa zaidi anaambiwa watu wengi wametumia wakapona, anakomaa nayo mwisho wa siku anakufa..

Kama una cancer, pitia tu hizo options ambazo ni bei kubwa, huna option nyingine hadi pale cure itakapopatikana, yaweza kua kesho, ama kesho kutwa ila itabidi usubiri tu. Njia nyingine zote endelea kupoteza muda mwisho wa siku uifanye iwe worse tukuage, cancer kwenye first stages inatibika kirahisi tu, ila mnavoendekeza njia za asili inakua inafika stage inakua haiwezi kua controlled tena..

Ningekua admin wa jf post kama hizi ningefuta sababu ni za uongo mtupu, zitaua watanzania maana wao ni mstari wa mbele kuamini kila wanachosoma kwenye internet.
 
watu ambao hawajaelimika, sanasana waafrika wanakufa kwa speed sana sababu ya vitu kama hivi, ulichoandika hapo juu hakina ukweli wowote! kusema pharmaceutical industries zinafaidika sana ndo sababu wanaziba ukweli kuhusu treatments ni uongo mtupu.

Mkuu unajua kweli hata process ya cancer ilivyo? tatizo moja la mtanzania akiambiwa tu kua achana na hizo dawa za wazungu zina madhara, tumia hii ya asili anarukia fasta, tena kudanganywa zaidi anaambiwa watu wengi wametumia wakapona, anakomaa nayo mwisho wa siku anakufa..

Kama una cancer, pitia tu hizo options ambazo ni bei kubwa, huna option nyingine hadi pale cure itakapopatikana, yaweza kua kesho, ama kesho kutwa ila itabidi usubiri tu. Njia nyingine zote endelea kupoteza muda mwisho wa siku uifanye iwe worse tukuage, cancer kwenye first stages inatibika kirahisi tu, ila mnavoendekeza njia za asili inakua inafika stage inakua haiwezi kua controlled tena..

Ningekua admin wa jf post kama hizi ningefuta sababu ni za uongo mtupu, zitaua watanzania maana wao ni mstari wa mbele kuamini kila wanachosoma kwenye internet

Suala siyo kufa, suala ni kulinda afya zetu kwa kujenga afya zetu kwa kutumia vitu alivyotupa Mungu, kwanini mungu kaumba hivi vyakula vya asili? na baadhi yake vingine vinatumika kama dawa!

Ni afadhali kujenga miili bora kwa kutumia vyakula vya asili kuliko kushinda kwenye mionzi na kuharibu kwa kiwango chochote kwa kutumia vitu visivyo salama!

Wachina wanajali sana vitu vya asili na ndo maana afya zao ziko bora sana, kwanini tusijenge tabia ya kujali vitu vya asili?
 
Suala siyo kufa, suala ni kulinda afya zetu kwa kujenga afya zetu kwa kutumia vitu alivyotupa Mungu, kwanini mungu kaumba hivi vyakula vya asili? na baadhi yake vingine vinatumika kama dawa!

Ni afadhali kujenga miili bora kwa kutumia vyakula vya asili kuliko kushinda kwenye mionzi na kuharibu kwa kiwango chochote kwa kutumia vitu visivyo salama!

Wachina wanajali sana vitu vya asili na ndo maana afya zao ziko bora sana, kwanini tusijenge tabia ya kujali vitu vya asili?

Mkuu, huyu jamaa anaongelea 'cure' for cancer sio prevention, mtu ukiishi healthy siku zote unakula vizuri na unafanya mazoezi utaishi vizuri na vitu kama cancer au magonjwa mengi hutogusa...

Sema tukija kwenye swala la cure, mtu ambaye cancer ishakua, kusema kuna njia za asili kutibu ni kudanganya watu tu ambao wana uhitaji mwisho wa siku wanapoteza muda kua na false hopes na vitu ambavyo havifanyi kazi au mbaya zaidi kupoteza maisha..

Watu walio kwenye matatizo hua wako desperate sana, wako easily deceivable, nadhani unakumbuka babu wa lolliondo kama mfano mzuri, sasa mtu akiwa na cancer anaweza akaona hii kitu akaachana na njia sahihi akaenda kula mihogo sijui madude gani mwisho wa siku tatizo likazidi
 
Mkuu huyu jamaa anaongelea 'cure' for cancer sio prevention, mtu ukiishi healthy siku zote unakula vizuri na unafanya mazoezi utaishi vizuri na vitu kama cancer au magonjwa mengi hutogusa...

Sema tukija kwenye swala la cure, mtu ambaye cancer ishakua, kusema kuna njia za asili kutibu ni kudanganya watu tu ambao wana uhitaji mwisho wa siku wanapoteza muda kua na false hopes na vitu ambavyo havifanyi kazi au mbaya zaidi kupoteza maisha..

Watu walio kwenye matatizo hua wako desperate sana, wako easily deceivable, nadhani unakumbuka babu wa lolliondo kama mfano mzuri, sasa mtu akiwa na cancer anaweza akaona hii kitu akaachana na njia sahihi akaenda kula mihogo sijui madude gani mwisho wa siku tatizo likazidi

Naona kama unamshambulia mleta hoja bila ya hata kujadili hoja yenyewe,uzuri ameweka links za wapi alikotoa anachokizungumzia lakini hata hutaki kugusia huko na wala hujathibitisha sehemu yoyote kuwa jamaa ni muongo.

Nahisi una wivu
 
Naona kama unamshambulia mleta hoja bila ya hata kujadili hoja yenyewe,uzuri ameweka links za wapi alikotoa anachokizungumzia lakini hata hutaki kugusia huko na wala hujathibitisha sehemu yoyote kuwa jamaa ni muongo.

Nahisi una wivu

Nadhani hujasoma kua nimepinga alichosema jamaa, ndio kudiscuss hoja kwenyewe huko, hujasoma post zangu uanzia pale juu umesoma reply niliyomjibu mtu alafu unakuja na conclusion.. Hehehe! wivu wa nini? wivu wa kuanzisha thread JF?? hilo si ni swala la bure au? Nimeipinga hoja kama umesoma post zangu hapo juu, na nimeeleza wazi kabisa kua it won't work. Wabongo kwa kuamini conspiracy theories mmejaliwa, mtabaki nyuma hadi siku jua lilipuke.

Wewe leta discussion yako sasa, umechangia nini kwenye hoja ya jamaa kuliko mimi niliyempinga??
 
Nadhani hujasoma kua nimepinga alichosema jamaa, ndio kudiscuss hoja kwenyewe huko, hujasoma post zangu uanzia pale juu umesoma reply niliyomjibu mtu alafu unakuja na conclusion.. Hehehe! wivu wa nini? wivu wa kuanzisha thread JF?? hilo si ni swala la bure au? Nimeipinga hoja kama umesoma post zangu hapo juu, na nimeeleza wazi kabisa kua it won't work. Wabongo kwa kuamini conspiracy theories mmejaliwa, mtabaki nyuma hadi siku jua lilipuke.

Wewe leta discussion yako sasa, umechangia nini kwenye hoja ya jamaa kuliko mimi niliyempinga??

Unasema it wont work umejaribu lini na mara ngapi???

Pia hii sidhani kama ilikuwa ni discussion,jamaa katoa hoja ukielewa unashukuru ama una kaa kimya,hujaelewa unauliza na kama unapinga unapinga kwa hoja.

Lete hoja zako sasa
 
Ila Mkuu Deception nina Maswali mawili ya Kuanzia..

1. Je mtu atumie mda gani Dozi ya Kuweka Mwili Katika Hali ya Alkaline. Mfano Kutumia Juisi ya Malimao

2. Na Muda Gani pia Mtu atumie kuondoa Sumu mwilini..

Therapy ya kuweka damu alkaline na kuondoa sumu kwenye damu haina muda wa ukomo,ni kama wewe unavyokula kila siku,sasa inabidi ubadili kidogo utaratibu wa kula,mazoea ndio yaliyotufanya tuone kwamba therapy ya kuondoa sumu na kuweka damu alkaline ni kama dozi,la hasha, hivi ndivyo binadamu tulitakiwa tule.
Damu yako ikiwa safi leo haimaanishi kwamba baadaye haitachafuka tena,hivyo huu ndio unatakiwa uwe utaratibu wa kila mtu kwenye mlo wake,ukiuzoea utauona ni wa kawaida sana,hautakusumbua.
 
watu ambao hawajaelimika, sanasana waafrika wanakufa kwa speed sana sababu ya vitu kama hivi, ulichoandika hapo juu hakina ukweli wowote! kusema pharmaceutical industries zinafaidika sana ndo sababu wanaziba ukweli kuhusu treatments ni uongo mtupu....

1.Unatumia hisia au una uthibitisho wa hicho ulichokisema hapo juu?
2.Niambie unataka uthibitisho wa aina gani ili ujue kwamba niliyosema ni kweli?

...Mkuu unajua kweli hata process ya cancer ilivyo?

Naijua.

...tatizo moja la mtanzania akiambiwa tu kua achana na hizo dawa za wazungu zina madhara, tumia hii ya asili anarukia fasta, tena kudanganywa zaidi anaambiwa watu wengi wametumia wakapona, anakomaa nayo mwisho wa siku anakufa..

1.Hoja yako ya msingi hapa ni ipi?
2.Mimi nasema kwamba dawa za cancer za hospitalini sio tu zina madhara bali zinaua.Wewe unasemaje?

..Kama una cancer, pitia tu hizo options ambazo ni bei kubwa, huna option nyingine hadi pale cure itakapopatikana, yaweza kua kesho, ama kesho kutwa ila itabidi usubiri tu...

Yaani hapa unazungumza kitu usichokielewa kabisa.Kwanza wewe mwenyewe unakubali kwamba kwenye mainstream hamna tiba ya cancer.Sasa nijibu swali langu la hapo chini;

Sloan Kettering cancer research institute ilianzishwa mwaka 1884 ili kufanya utafiti wa tiba ya cancer,miaka 130 imeshapita na bado hawajafanikiwa kupata tiba ya cancer,wewe unawaambia watu waendelee kusubiri.Je,unaweza kuniambia kwanini kwa miaka yote hiyo bado hawajapata tiba ya cancer?

..Njia nyingine zote endelea kupoteza muda mwisho wa siku uifanye iwe worse tukuage, cancer kwenye first stages inatibika kirahisi tu, ila mnavoendekeza njia za asili inakua inafika stage inakua haiwezi kua controlled tena..

Hisia tu ndio zimetawala,hii ni ishara ya ukosefu wa elimu sahihi na ganzi ya ubongo inayokufanya usiweze kufikiria nje ya mipaka uliyowekewa na elimu rasmi,kama huko tayari kuelewa mimi sina uwezo wa kukubadilisha,unaweza kuchagua hicho unachokiamini lakini waache wengine wenye akili ya kudadisi watafute ukweli.Usifikiri kwamba kila mtu humu ana akili yenye ganzi kama yako.Wewe huna uwezo wa kumwambia mtu humu asisome habari fulani.Kama kweli una hoja zenye mashiko mimi nakusubiri,usitake kuwaharibia wengine wakose mambo ya msingi.

..Ningekua admin wa jf post kama hizi ningefuta sababu ni za uongo mtupu, zitaua watanzania maana wao ni mstari wa mbele kuamini kila wanachosoma kwenye internet

Kasumba tu ndio inakupeleka vibaya,au labda nimegusa maslahi.Bado sijaona hoja yako ya msingi hata moja.Ukitaka kuona tofauti kati ya mimi na wewe kwenye nguvu ya ubongo,njoo na hoja zako tuweke ubaoni watu wajionee wenyewe,kama wewe unataka kuendelea kuwa mtumwa wa kifikra siwezi kukuzuia,lakini sitakuruhusu uchafulie wengine washindwe kujua ukweli ambao ni muhimu katika maisha yao.

Thibitisha kwamba hiki ninachosema ni uongo.
 
Bado hujanipa maelezo ya kutosha huyo binti alitibiwa hospitali gani na alipewa dawa gani.

Kwa maelezo yako inaonekana huyo binti atakuwa na ugonjwa uitwao vitiligo,ugonjwa huu mara nyingi unasababishwa na kinga ya mwili kushambulia mwili wenyewe maeneo mbalimbali kama vile tishu nk,kwa huyu biti yeye ngozi yake ndiyo hushambuliwa.

Sababu kubwa ya ugonjwa huu ndio hiyo niliyoeleza hapo juu au kwa kifupi tunaita 'autoimmune'.Magonjwa aina hii ndio ambayo hospitali huwa hawawezi kuyatibu zaidi ya kuondoa dalili.Kutokana na sayansi ya ugonjwa huu ulivyo,hata tiba hii ya cancer niliyoeleza,yaani vitamin B17 na mtiririko wake unaweza kumtibu vizuri kabisa huyo binti.Ukimpima huyo binti pH ya damu yake,lazima atakuwa acidic zaidi,ukitaka kuamini we nenda kajaribu uone.

Nikupe faida nyingine ya vitamin B17.Bila kujali kama una cancer au la,vitamin B17 pia huweza kutumiwa kama cosmetic ya asili hasa kwa wanawake.Vitamin B17 inapotumiwa,ukiachilia mbali kukulinda dhidi ya magonjwa sugu kama cancer pia inaweka ngozi katika hali ya ubora.Na kama wanawake watagundua siri hii basi hawawezi tena kuhangaika na vipodozi vyenye kemikali chafu.Vitamin B17 ina tabia ya kuondoa mabaka,rangi nyeusi za makovu ya vidonda au vipele kwenye ngozi,mikunjo ya ngozi na kuiweka ngozi katika muonekano mzuri kama mtu atakuwa na tabia ya kuitumia mara kwa mara.Yaani vitamin B17 hutambua vitu ambavyo si vya kawaida juu ya ngozi na kuviondoa.

ni kweli sina maelezo ya kutosha juu yake kwan sina mahusiano nae ya karibu ila nilikuwa nayaona mabaka hayo sehemu za nje ya mwili na nilipofuatilia nikapata taarifa hizo chache, nitajitahidi kuwa nae karibu na kumweka sawa na akinielewa nitarudi kwa ushauri zaidi. Pongezi kwa moyo wa kujitolea
 
Huyu dokta wetu FAKE tatizo mkali na ana jazba. Sawa kansa imetafitiwa huko ma ulaya miaka 130 wamesema hakuna dawa . Kina stev job imewaua . Wewe umesema dawa ipo ya chakula. Basi itangazie dunia. Na sio kuonea watu waliokata tamaa. ......harafu nyoosha maelezo na sio kurukaruka kuna mteja wako hapo juu kakuuliza dozi ya juice ya limau anywe vipi . Baadala ya kumjibu unatoa maelezo mengi yaliyo nje ya swali . Hivi ingekuwa ndio ngonjwa kakufuata hospital yako na kapata jibu hilo si kapoteza nauli yako.
 
Mwanzoni nilisema kwamba tiba hizo nilizotaja haimaanishi kwamba mgonjwa anatakiwa azitumie zote,la hasha,ila hutegemeana.Nilizungumzia hatua tatu za kutibu cancer ambazo ni kuweka pH ya damu iwe alkaline,kuondoa sumu na kuua chembe za cancer.Sasa ukiangalia vizuri kwenye tiba tajwa hapo juu utaona kwamba hatua zote tatu unaweza kuzipatia ufumbuzi kutokana na hizo tiba.

Cha msingi kukumbuka hapa ni kwamba,hatua ya kwanza na ya pili ni lazima kuzipitia.Sasa kwenye hatua hii ya tatu ya kuua chembe za cancer tayari nimeshazungumzia vitamin B17 na utaratibu wake wa matumizi.Tiba nyingine ambazo zinaweza kutumika kwenye hatua hii ya tatu ni Cannabis oil/Hemp oil.Hii ndio mojawapo ya sababu ambayo imeifanya bangi kupigwa marufuku na watu wabinafsi wanaolinda biashara zao.

Hifadhini hizi nyaraka hapo chini kwa ajili ya kumbukumbu zenu kwa yale ambayo tumeshayaongelea tayari;

Hiyo nyaraka ya pili ya Edward Griffin kwangu imegoma kupakulika, sijui wadau wengine.
 
Back
Top Bottom