Hii hali inanipa upweke sana nimejitahidi kuikwepa lakini wapi

Hii hali inanipa upweke sana nimejitahidi kuikwepa lakini wapi

Jitahidi uwe unatoa msaada Kwa watu. Kwa kufanya hivi hiyo hali itaanza kupotea taratibu.

Mahusiano bora na watu ni muhimu Sana.

Unachobidi kuwa nacho ni boundary Ila sio kujitenga na watu
 
Lile tangazo naona hawakuliona, ila kwa hii mbinu jiandae kupata PM za kutosha man...😊
Hii si mbinu,nimeshiriki stories of changes misimu yote kwa ukamilifu na nimeshiriki hafla za tuzo zote ,watafute baadhi ya washindi waulize how it was kwa upande wangu hata baadhi ya mod humu wananifahamu,sio mbinu mkuu yaani mimi nipo hivyo
 
Jitahidi uwe unatoa msaada Kwa watu. Kwa kufanya hivi hiyo hali itaanza kupotea taratibu.

Mahusiano bora na watu ni muhimu Sana.

Unachobidi kuwa nacho ni boundary Ila sio kujitenga na watu
Mkuu nina utaratibu wakutembelea watoto yatima kila baada ya miezi 3 japo kuna wakati naenda kwa mwaka mara moja,nina makundi ya whatssap huwa natoa michango kwenye matatizo ama furava,nina dispensary natenga kiasi kuhudumia wanaohitaji matibabu lakini hawanafedha kila mwezi hii haitoshi?
 
Jana ulileta bandiko ukitafuta mke lakini una watoto 3, au kutokuwa na mke ndiyo kunaleta hali hiyo?..JF ya siku hizi story za kutunga zimekuwa nyingi sana.
 
Wewe ni INTROVERT, huna tatizo lolote.
Ila jitahidi kujinga na watu, bongo ni nchi ya wapiga kelele zaidi na connections.
 
Mkuu, wewe uko kama mimi kwa mambo mengi.

Ila hapo mwisho naona kama umejidanganya. Unafikiri ukioa hiyo hali ndo itaisha? Mmmmh sidhani.

Mimi kabla sijaoa nilifikiri nikioa nitaepukana na situation hii, ila wapi bwanaa. Tukitoka kazini na Mke wangu mimi huwa nakuwa busy na Jamii forums nikitembelea majukwaa yote. Muda wa kupiga story na mke wangu haujawahi kumzidi dakika 20. Wife alishanilalamikia sana, hadi nami nikaona kweli simtendei haki, lakini ndo nilishashindwa kubadilika. Hata muda huu ninapotype,sijaongea chochote na wife zaidi ya salaam tangu saa 12:42 jioni tulipokutana home.
 
Jana ulileta bandiko ukitafuta mke lakini una watoto 3, au kutokuwa na mke ndiyo kunaleta hali hiyo?..JF ya siku hizi story za kutunga zimekuwa nyingi sana.
Umesoma nilichokiandika hapo na kukielewa ama umekisoma tu,? Natafuta mke yes,ninawatoto watatu absoluto,sina marafiki naninapenda kujitenga,kati ya hayo matatu ipi inaakisi kwamba ni stori ya kutunga.Learn how to analyse things with accuracy or just precision never pretend and then criticising,haipendezi
 
Mkuu, wewe uko kama mimi kwa mambo mengi.

Ila hapo mwisho naona kama umejidanganya. Unafikiri ukioa hiyo hali ndo itaisha? Mmmmh sidhani.

Mimi kabla sijaoa nilifikiri nikioa nitaepukana na situation hii, ila wapi bwanaa. Tukitoka kazini na Mke wangu mimi huwa nakuwa busy na Jamii forums nikitembelea majukwaa yote. Muda wa kupiga story na mke wangu haujawahi kumzidi dakika 20. Wife alishanilalamikia sana, hadi nami nikaona kweli simtendei haki, lakini ndo nilishashindwa kubadilika. Hata muda huu ninapotype,sijaongea chochote na wife zaidi ya salaam tangu saa 12:42 jioni tulipokutana home.
Dah!!
 
Hapo kazi ipo mzee dates zingeenda kwenye 23 nakuendelea ningesema ni normal but hapo sio normal una tatizo la kutrust watu, kusocialize na watu tafuta what went wrong kwenye ukuaji wako malenzi and so on jibu lipo kwenye past yako
Ah! My past is full of mysteries kwa kweli,NAOMBA NIKUONE PM mkuu,nikikaa kwenye laptop hiki kishikwambi hakifungui PM
 
Katika maisha yangu yote sijawahi kuwa na marafiki,na sipendi kabisa masuala ya marafiki,hata nikipata tatizo sina rafiki wa kumwambia mtu pekee ninayeweza kumwambia ni mama tu.

Lakini pia si mtu mwepesi wakueleza hisia ama changamoto zangu kirahisi hata kwa mama,huwa namueleza nikiona kabisa hii inaniendea kombo.

Nikikaa na kundi la vijana wenzangu huwa nakuwa msikilizaji tu tena kwa muda flani tu kisha naondoka zangu.

Napenda kujitenga sana na ninaweza kukaa Siku nzima peke yangu bila taabu yoyote ile,nikitumia muda huo kufanya kazi zangu Za kiofisi au nikifanya coding ama kufanya simulation za sakiti mbalimbali kama nipo nje ya majukumu ya kitabibu.

Nikiona mtu anaanza kunizoea huwa namkwepa haraka sana maana sipendi mazoea na watu.

Sehemu ninayoishi wapangaji wenzangu inaweza pita miezi 2 hatuja onana.

Sipendi kabisa kwenda katika matukio ya sherehe na hata ikiwa ni lazima huwa nakuwa mtu wakujitenga sana maana Mara nyingi huwa siambatani na mtu kabisa.

Sipendi kupiga piga picha hovyo kabisa. Napenda sana familia hapo ndio nadhani ni marafiki pekee naweza kudumu não japo sina família.

Japo kuna wakati huwa nakuwa mpweke mno hasa nisipokuwa na na kazi ya kufanya ,hivyo huwa najitahidi kuhakikisha nakuwa na kazi Ya kufanya kila Siku.

Mimi napambana kivyangu na mambo yangu sipendi kumshirikisha mtu kabisa ,ila huwa nakuwa na hisia yakumshirikisha mke tu lakini sina.

Ninaamini kwamba kuwa na marafiki na kujichanganya sana na watu ni njia rahisi ya mimi kujiletee matatizo.

Nafikiria kuoa ili kuepukana na hali hii nadhani itanisaidia.
Kwahiyo sahivi uko wapi?
 
Back
Top Bottom