Hii imekaaje kuhusu huu mtaala mpya wadau

Hii imekaaje kuhusu huu mtaala mpya wadau

Kati ya watu ambao walitani situ moja tuondokane na ile mitaala yenye mafungamano na elimu ya kikoloni (Colonial Education), basi na mimi nimo!
Na kwa hiyo katika hili, kwa kweli naipongeza sana serikali kwa kufanya mabadiliko ya mitaala ya elimu ili iendane na dunia ya sasa, lakini pia mahitaji ya nchi na watu wake.

NB: Sasa hivi mashambulizi yote yataelekezwa kwenye kuyavunja majeshi yetu mawili (Jeshi la polisi na magereza) ili na yenyewe yawe huru na ya kisasa! Kuliko ilivyo sasa ambapo hayana tofauti na majeshi ya Kikoloni tuliyo yasoma kwenye somo la Historia kule sekondari.


Lakini pia kuirejesha ile Rasimu ya Katiba ya Jaji Warioba ili nchi nayo isonge mbele kwenye nyanja za kiuchumi na kisiasa.
 
Curriculum inaweza kuwa ni nzuri sana Kwa kuangalia, ila uzuri wake utatokana na utelezaji wake Kwa ufanisi...!!

Je, mazingira wezeshi na vifaa vya kufundishia vipo? ....Au ndio tunarudi kule kule TU darasa Lina watoto 45 wanaosoma computer science ila shule Ina computer mbili TU na tena moja ni ya mwalimu kuu, muda wote imefungiwa ofisini.🙂‍↔️
Hicho ndio kitakachofuata,wanaanza kuwachorea watoto picha za computer ubaoni
 
Somo la dini limewekwa ili liwasaidie nini wanafunzi?

Mtoto anasoma dini ili iweje?
Elimu ya DINI ingetoka kwenye list maana inaongoza kwa kuchezea bongo zetu kwa kuamini vitu vinapatikana kwa sababu ya kumtumaini MUNGU ambae hatuna uhakika nae kama ana huruma na sisi.ASANTE
Hapa Serikali imejichanganya. Maana nchi yetu inatambulika kama ni secular state!! Sasa mambo ya masomo ya dini kwenye mitaala yanafuata nini, tena kwenye hii karne ya 21?

Elimu ya dini haikutakiwa kuingizwa kwenye mitaala. Na badala yake utaratibu ungetumika kama ule wa zamani. Kila mwanafunzi anakuwa huru kushiriki kwenye imani yake.
 
Curriculum inaweza kuwa ni nzuri sana Kwa kuangalia, ila uzuri wake utatokana na utelezaji wake Kwa ufanisi...!!

Je, mazingira wezeshi na vifaa vya kufundishia vipo? ....Au ndio tunarudi kule kule TU darasa Lina watoto 45 wanaosoma computer science ila shule Ina computer mbili TU na tena moja ni ya mwalimu kuu, muda wote imefungiwa ofisini.🙂‍↔️
Atakuwa aliyeandaa hii ana akili kama za LIKUD ...Yaani wenyewe hawafikiri nje ya box.,Wanajua mtoto kazaliwa kigoma so lazima asome fani ya uvuvi,yaanj hawafikiri kuna maisha nje ya kigoma,kuna maisha nje ya Tanzania,hawaoni maisha ya sasa tunakimbizana na globalisation,Dah Tanzania bado tuna safari sana
 
Hapa Serikali imejichanganya. Maana nchi yetu inatambulika kama ni secular state!! Sasa mambo ya masomo ya dini kwenye mitaala yanafuata nini, tena kwenye hii karne ya 21?

Elimu ya dini haikutakiwa kuingizwa kwenye mitaala. Na badala yake utaratibu ungetumika kama ule wa zamani. Kila mwanafunzi anakuwa huru kushiriki kwenye imani yake.
Mambo yanaanzaga taratibu kaka,mwishowe utasikia yaliyomo yamo...
 
Elimu ndio imekufa rasmi ,ni mtaala wa hovyo kuwahi kutoka,kwanza hatuwezi kuwa implemented kwa kuwa shule nyingi hazina hyo miundombinu
 
Atakuwa aliyeandaa hii ana akili kama za LIKUD ...Yaani wenyewe hawafikiri nje ya box.,Wanajua mtoto kazaliwa kigoma so lazima asome fani ya uvuvi,yaanj hawafikiri kuna maisha nje ya kigoma,kuna maisha nje ya Tanzania,hawaoni maisha ya sasa tunakimbizana na globalisation,Dah Tanzania bado tuna safari sana

Unajuaje kama Sio Likud mwenyewe ndio kaandaa hiyo programme?

🤣🤣🤣🤣🤣

Anyways ?


A. Is Likud a prophet or

B. Likud yupo kwenye system anawaambia watu wawatoe watoto Wao shule za EM Kwa sababu anajua what is going on behind the scene?


Only God knows.
But what?

Listen to Likud so that your days shall be many and Merry.


Thanks me later 🙏🙏🙏🙏🙏
 
MABADILIKO MAPYA YA MITAALA YA ELIMU SHULE ZA MSINGI, SEKONDARI NA VYUO 2025

MABORESHO YA MITAALA AMBAYO YANAENDA KUBADILISHA MFUMO WETU WA ELIMU:

1.Mtihani wa darasa la Saba utafutwa.


2.Mwanafunzi akianza darasa la kwanza lazima amalize Kidato cha nne.

3.Kutakuwa Mtihani wa Upimaji wa Kitaifa wa darasa la sita (STANDARD SIX NATIONAL ASSESSMENT).

4.Mwanafunzi atatakiwa asome fani fulani kabla hajamaliza Kidato cha nne ili aweze kujiajiri au kuajiriwa baada ya kumaliza.

5.Lugha ya kufundishia na kujifunzia itakuwa kiswahili, Kiingereza kitakuwa kama somo kwa Shule za Kiswahili Medium na lugha ya kufundishia English, kiswahili kitakuwa Kama somo kwa Shule za English Medium.

6.Elimu ya Msingi itakuwa miaka 6. Mwanafunzi ataanza darasa la kwanza akiwa na miaka 6 tofauti na ya sasa miaka 7.

8.Elimu ya Awali mwanafunzi ataanza akiwa na miaka 5.

9.Masomo ya Elimu ya Msingi yatakuwa ni KKK, Jiografia,kiswahili, Sanaa na Michezo, Hisabati,Sayansi, historia ya TANZANIA na Maadili,Dini na kiingereza na Stadi za Kazi itachomekwa.

10.Kiingereza kitafundishwa kuanzia darasa la kwanza kwa shule za Kiswahili na kiswahili kitafundishwa kuanzia darasa la kwanza kwanza kwa shule za kiingereza.

11.Shule zenye uwezo zitafundisha angalau somo moja la lugha za kigeni kama Kichina au Kifaransa.

12.Sekondari kutakuwa na mikondo 2, mkondo wa jumla na Amali (Ufundi).
Mwanafunzi atachagua kutokana na uwezo,matakwa na malengo yake ya baadaye.

13.Mkondo wa amali (ufundi) utakuwa na fani zifuatazo:-
Kilimo na Ufugaji.
Umakenika.
Biashara na Ujasiriamali.
Sanaa na Ubunifu.
Elimu ya Michezo.
Ufugaji wa Nyuki.
Uchimbaji wa Madini.
Urembo.

14.Mwanafunzi wa Mkondo wa Amali atatakiwa kuchukua Masomo manne (4) ya jumla na moja la fani.

15.Masomo ya jumla ya wanafunzi wa Amali ni:-
Hisabati.
Elimu ya Biashara.
Kiingereza.
Historia ya Tanzania na Maadili.

16.Wahitimu wa Amali watapata vyeti viwili yaani:-
Cheti cha ujumla cha Elimu ya Sekondari (NECTA) na Cheti cha Amali ( NACTIVET).

17.Kila shule itakuwa na Wakala wa VETA ili kusimamia masuala ya Ufundi.

18.Kila shule haitakuwa na Mikondo zaidi ya miwili ya Ufundi,hii ni kwa ajili ya Ufanisi na fani ziwe zinaendana na fursa za eneo husika.

19.Kutaanzishwa somo jipya la Mawasiliano ya Kitaaluma (ACADEMIC COMMUNICATION) katika A-level na Ualimu.

20.CODING itafundishwa Shule za Msingi.

21.INFORMATION and COMPUTER STUDIES (ICS) itabadilishwa na kuitwa COMPUTER SCIENCE.Somo limesukwa upya.

22.CIVICS itaunganishwa na Historia ya TANZANIA na Maadili kwa O-level.

23.O-level Masomo ya lazima yatakuwa 6 badala 7 ya Sasa.

24.Katika O-level Masomo ya Biology na Geography yatakuwa Masomo ya kuchagua pia kwa sababu Maudhui yake yamekuwa kwenye Masomo ya Jiografia na Sayansi ya Shule ya Msingi kwa mfano Afya ya Jamii,Afya ya Uzazi, Magonjwa ambukizi nk.

25.Civics, Maarifa ya Jamii,Uraia na Maadili yamefutwa, Maudhui yake yameingia katika somo la Historia ya TANZANIA na Maadili.

26.General Studies (GS) katika A-level itafutwa na Maudhui yake yatawekwa katika Somo la Historia ya TANZANIA na Maadili na Mawasiliano ya Kitaaluma.

27.Kufuta baadhi ya Masomo kumefanyika ili kuondoa tatizo la kujirudiarudia kwa Maudhui.

28.Michepuo katika Elimu ya O-level imeongezeka kutoka minne (4) hadi tisa (9).

Michepuo iliyoongezeka ni:-
Sanaa.
Lugha.
Muziki.
Michezo.
Tehama.

29.Masomo ya O-level yatakuwa:-
Biology.
Physics.
Chemistry.
History.
Geography.
Historia ya TANZANIA na Maadili.
Hisabati.
Kiswahili.
English.
Elimu ya Biashara.
Utunzaji wa _Taarifa za Fedha.
Computer Science.
Bible Knowledge.
Elimu ya Dini ya kiislamu etc.

30.Astashahada ya Ualimu itafutwa kisha itaanzishwa Stashahada (DIPLOMA) ya Elimu ya Awali, Ualimu wa Msingi na Ualimu wa Elimu Maalumu.

Watakaosoma Stashahada watakuwa waliomaliza Kidato cha Sita na itasomwa kwa miaka miwili.

31.Walimu wa Sekondari wote watakuwa na Shahada (DEGREE). kwa sababu nchi nyingi zinaenda na mwelekeo huu.

32.Vyuo vilivyokuwa vinatoa Stashahada (DIPLOMA) ya Ualimu wa Sekondari vitatumika kutoa continuous Professional Development.
Nchi zilizoendelea zina community college hata ambaye ajafaulu anaenda huko kujitoa kwa fani anayoitaka bado mfumo hautoi suluhisho la moja kwa moja kwa watu
 
WaTz mmezoa kulalamika tu... Ndiyo maana hamfanikiwi ktk maisha... Jambo hata liwe zuri kiasi gani mmanataka kuleta upinzani hamtaki kujadili mambo ktk upekee wake...
Halafu muwe mnajitahidi kusoma mabadiriko mbalimbali ya kisekta yanapotokea...
 
Unajuaje kama Sio Likud mwenyewe ndio kaandaa hiyo programme?

🤣🤣🤣🤣🤣

Anyways ?


A. Is Likud a prophet or

B. Likud yupo kwenye system anawaambia watu wawatoe watoto Wao shule za EM Kwa sababu anajua what is going on behind the scene?


Only God knows.
But what?

Listen to Likud so that your days shall be many and Merry.


Thanks me later 🙏🙏🙏🙏🙏
Tutapeleka Nairobi watoto wetu,mambo ya kuwang'ang'aniza watoto wetu wasome kilimo cha nyanya kisa wanakaa Ilula hatutaweza,...
 
Back
Top Bottom