Hii imekaaje kuhusu huu mtaala mpya wadau

Hii imekaaje kuhusu huu mtaala mpya wadau

Kuhusu namba 5
Hivi kwanini tunang'ang'ania kufundisha watoto elimu ya primary kwa kiswahili.
Wakati kijana akifika sekondari au chuoni au kwenye udahili au ofisini katika kuandaa ripoti lugha inayotumika ni kingereza..!
Hivi hawa wapuuzi hawalioni hili gapu...?
Kwanini tusiweke msingi wa hii lugha kwa watoto toka primary..?

Halafu namba 29
Hiyo Historia na Historia ya Tz na maadili yaani sijaelewa.
 
Wala haijulikani si unaona hata hakuna TV ya Kilimo, somo la Kilimo sio ishu, ila masomo ya dini yamepenya
Noma sana, SUA sijui wanafundisha nini siku hizi?! Kilimo kimekua kama mafanikio, hata ukisoma sio lazima ufanikiwe, kwahiyo hata kilimo ni hivyo hivyo, unaweza usisome kilimo na ukalima na ukafanikiwa. Tunabahatisha bahatisha tu, kama mafanikio ya doto magari
 
No. 30 Kwahiyo Form four leavers hawataweza kusoma Astashahada ya Ualimu means ili mtu apate diploma lazima aende Advance🤔🤔,.
Au mie ndio sijaelewa
Ndio hivyo hakutakuwa na astashahada ya ualimu nk elimu ya sekondari kidato cha nne ni kazma kwa kila mwanafunz ila tu watakao faulu kidato cha 4 kwenda 6 hao ndoo watatupatia professionalisms wakutosha
 
📌 POINT #4 Nimekuwa naipigia chapuo sana bora wameiweka iwe lazima maana sasahivi GRADUATES wengi wamekimbilia kuwa MAWINGA😬😬😬 wakati kuna fursa kibao kwenye UFUNDI!!!

#Vijana nendeni VETA mkasome ufundi huko siku za usoni hakuna ujanjaujanja watu wenye ujuzi ndo watakuwa na hela sana.

KOZI AMBAZO HAZIMTUPI MTU;
1. UFUNDI WA UMEME WA MAGARI
2.UFUNDI UMEME WA MAJUMBANI NA VIWANDANI.
3.UFUNDI UASHI
4.UFUNDI SEREMALA
5.UFUNDI MAKENIKA
5.UFUNDI WA VIFAA VYA UMEME.
6.UFUNDI SIMU,COMPUTER NA VIFAA VYA MAWASILIANO.
7.UFUNDI BOMBA,N.K.

📌BILA KUSAHAU KUJUA KUENDESHA GARI NA KUWA NA LESENI NA PASSPORT💪💪💪SIO MCHONGO UNATOKEA NJE YA NCHI UNAMAVYETI YOTE PLUS UJUZI ILA HUNA PASSPORT HUU NAO NI UJINGA,VIJANA FANYENI MMILIKI PASSPORT,ACHENI KUZUBAAA!!!
 
Waziri wa Elimu ni Prof. Adolf Mkenda ambaye kwa sasa ana miaka takribani 62! Watoto wake hawasomi shule hizi saint kayumba! Na wala hana fikra za kumpeleka mtoto wake au mjukuu wake Muungano Shule ya Msingi au Uhuru Shule ya Msingi.
Miaka mitano mbeleni 2030 wanaifuta haya madudu na kuweka madudu mengi! Watoto wetu wanalishwa ujinga na watu ambao watoto wao hawalishiwi ujinga huu.
 
MABADILIKO MAPYA YA MITAALA YA ELIMU SHULE ZA MSINGI, SEKONDARI NA VYUO 2025

MABORESHO YA MITAALA AMBAYO YANAENDA KUBADILISHA MFUMO WETU WA ELIMU:

1.Mtihani wa darasa la Saba utafutwa.


2.Mwanafunzi akianza darasa la kwanza lazima amalize Kidato cha nne.

3.Kutakuwa Mtihani wa Upimaji wa Kitaifa wa darasa la sita (STANDARD SIX NATIONAL ASSESSMENT).

4.Mwanafunzi atatakiwa asome fani fulani kabla hajamaliza Kidato cha nne ili aweze kujiajiri au kuajiriwa baada ya kumaliza.

5.Lugha ya kufundishia na kujifunzia itakuwa kiswahili, Kiingereza kitakuwa kama somo kwa Shule za Kiswahili Medium na lugha ya kufundishia English, kiswahili kitakuwa Kama somo kwa Shule za English Medium.

6.Elimu ya Msingi itakuwa miaka 6. Mwanafunzi ataanza darasa la kwanza akiwa na miaka 6 tofauti na ya sasa miaka 7.

8.Elimu ya Awali mwanafunzi ataanza akiwa na miaka 5.

9.Masomo ya Elimu ya Msingi yatakuwa ni KKK, Jiografia,kiswahili, Sanaa na Michezo, Hisabati,Sayansi, historia ya TANZANIA na Maadili,Dini na kiingereza na Stadi za Kazi itachomekwa.

10.Kiingereza kitafundishwa kuanzia darasa la kwanza kwa shule za Kiswahili na kiswahili kitafundishwa kuanzia darasa la kwanza kwanza kwa shule za kiingereza.

11.Shule zenye uwezo zitafundisha angalau somo moja la lugha za kigeni kama Kichina au Kifaransa.

12.Sekondari kutakuwa na mikondo 2, mkondo wa jumla na Amali (Ufundi).
Mwanafunzi atachagua kutokana na uwezo,matakwa na malengo yake ya baadaye.

13.Mkondo wa amali (ufundi) utakuwa na fani zifuatazo:-
Kilimo na Ufugaji.
Umakenika.
Biashara na Ujasiriamali.
Sanaa na Ubunifu.
Elimu ya Michezo.
Ufugaji wa Nyuki.
Uchimbaji wa Madini.
Urembo.

14.Mwanafunzi wa Mkondo wa Amali atatakiwa kuchukua Masomo manne (4) ya jumla na moja la fani.

15.Masomo ya jumla ya wanafunzi wa Amali ni:-
Hisabati.
Elimu ya Biashara.
Kiingereza.
Historia ya Tanzania na Maadili.

16.Wahitimu wa Amali watapata vyeti viwili yaani:-
Cheti cha ujumla cha Elimu ya Sekondari (NECTA) na Cheti cha Amali ( NACTIVET).

17.Kila shule itakuwa na Wakala wa VETA ili kusimamia masuala ya Ufundi.

18.Kila shule haitakuwa na Mikondo zaidi ya miwili ya Ufundi,hii ni kwa ajili ya Ufanisi na fani ziwe zinaendana na fursa za eneo husika.

19.Kutaanzishwa somo jipya la Mawasiliano ya Kitaaluma (ACADEMIC COMMUNICATION) katika A-level na Ualimu.

20.CODING itafundishwa Shule za Msingi.

21.INFORMATION and COMPUTER STUDIES (ICS) itabadilishwa na kuitwa COMPUTER SCIENCE.Somo limesukwa upya.

22.CIVICS itaunganishwa na Historia ya TANZANIA na Maadili kwa O-level.

23.O-level Masomo ya lazima yatakuwa 6 badala 7 ya Sasa.

24.Katika O-level Masomo ya Biology na Geography yatakuwa Masomo ya kuchagua pia kwa sababu Maudhui yake yamekuwa kwenye Masomo ya Jiografia na Sayansi ya Shule ya Msingi kwa mfano Afya ya Jamii,Afya ya Uzazi, Magonjwa ambukizi nk.

25.Civics, Maarifa ya Jamii,Uraia na Maadili yamefutwa, Maudhui yake yameingia katika somo la Historia ya TANZANIA na Maadili.

26.General Studies (GS) katika A-level itafutwa na Maudhui yake yatawekwa katika Somo la Historia ya TANZANIA na Maadili na Mawasiliano ya Kitaaluma.

27.Kufuta baadhi ya Masomo kumefanyika ili kuondoa tatizo la kujirudiarudia kwa Maudhui.

28.Michepuo katika Elimu ya O-level imeongezeka kutoka minne (4) hadi tisa (9).

Michepuo iliyoongezeka ni:-
Sanaa.
Lugha.
Muziki.
Michezo.
Tehama.

29.Masomo ya O-level yatakuwa:-
Biology.
Physics.
Chemistry.
History.
Geography.
Historia ya TANZANIA na Maadili.
Hisabati.
Kiswahili.
English.
Elimu ya Biashara.
Utunzaji wa _Taarifa za Fedha.
Computer Science.
Bible Knowledge.
Elimu ya Dini ya kiislamu etc.

30.Astashahada ya Ualimu itafutwa kisha itaanzishwa Stashahada (DIPLOMA) ya Elimu ya Awali, Ualimu wa Msingi na Ualimu wa Elimu Maalumu.

Watakaosoma Stashahada watakuwa waliomaliza Kidato cha Sita na itasomwa kwa miaka miwili.

31.Walimu wa Sekondari wote watakuwa na Shahada (DEGREE). kwa sababu nchi nyingi zinaenda na mwelekeo huu.

32.Vyuo vilivyokuwa vinatoa Stashahada (DIPLOMA) ya Ualimu wa Sekondari vitatumika kutoa continuous Professional Development.
Seen
 
Mtoto wangu ataenda soma Great Britain.. elimu ya Tanzania kama homa za majira

MABADILIKO MAPYA YA MITAALA YA ELIMU SHULE ZA MSINGI, SEKONDARI NA VYUO 2025

MABORESHO YA MITAALA AMBAYO YANAENDA KUBADILISHA MFUMO WETU WA ELIMU:

1.Mtihani wa darasa la Saba utafutwa.


2.Mwanafunzi akianza darasa la kwanza lazima amalize Kidato cha nne.

3.Kutakuwa Mtihani wa Upimaji wa Kitaifa wa darasa la sita (STANDARD SIX NATIONAL ASSESSMENT).

4.Mwanafunzi atatakiwa asome fani fulani kabla hajamaliza Kidato cha nne ili aweze kujiajiri au kuajiriwa baada ya kumaliza.

5.Lugha ya kufundishia na kujifunzia itakuwa kiswahili, Kiingereza kitakuwa kama somo kwa Shule za Kiswahili Medium na lugha ya kufundishia English, kiswahili kitakuwa Kama somo kwa Shule za English Medium.

6.Elimu ya Msingi itakuwa miaka 6. Mwanafunzi ataanza darasa la kwanza akiwa na miaka 6 tofauti na ya sasa miaka 7.

8.Elimu ya Awali mwanafunzi ataanza akiwa na miaka 5.

9.Masomo ya Elimu ya Msingi yatakuwa ni KKK, Jiografia,kiswahili, Sanaa na Michezo, Hisabati,Sayansi, historia ya TANZANIA na Maadili,Dini na kiingereza na Stadi za Kazi itachomekwa.

10.Kiingereza kitafundishwa kuanzia darasa la kwanza kwa shule za Kiswahili na kiswahili kitafundishwa kuanzia darasa la kwanza kwanza kwa shule za kiingereza.

11.Shule zenye uwezo zitafundisha angalau somo moja la lugha za kigeni kama Kichina au Kifaransa.

12.Sekondari kutakuwa na mikondo 2, mkondo wa jumla na Amali (Ufundi).
Mwanafunzi atachagua kutokana na uwezo,matakwa na malengo yake ya baadaye.

13.Mkondo wa amali (ufundi) utakuwa na fani zifuatazo:-
Kilimo na Ufugaji.
Umakenika.
Biashara na Ujasiriamali.
Sanaa na Ubunifu.
Elimu ya Michezo.
Ufugaji wa Nyuki.
Uchimbaji wa Madini.
Urembo.

14.Mwanafunzi wa Mkondo wa Amali atatakiwa kuchukua Masomo manne (4) ya jumla na moja la fani.

15.Masomo ya jumla ya wanafunzi wa Amali ni:-
Hisabati.
Elimu ya Biashara.
Kiingereza.
Historia ya Tanzania na Maadili.

16.Wahitimu wa Amali watapata vyeti viwili yaani:-
Cheti cha ujumla cha Elimu ya Sekondari (NECTA) na Cheti cha Amali ( NACTIVET).

17.Kila shule itakuwa na Wakala wa VETA ili kusimamia masuala ya Ufundi.

18.Kila shule haitakuwa na Mikondo zaidi ya miwili ya Ufundi,hii ni kwa ajili ya Ufanisi na fani ziwe zinaendana na fursa za eneo husika.

19.Kutaanzishwa somo jipya la Mawasiliano ya Kitaaluma (ACADEMIC COMMUNICATION) katika A-level na Ualimu.

20.CODING itafundishwa Shule za Msingi.

21.INFORMATION and COMPUTER STUDIES (ICS) itabadilishwa na kuitwa COMPUTER SCIENCE.Somo limesukwa upya.

22.CIVICS itaunganishwa na Historia ya TANZANIA na Maadili kwa O-level.

23.O-level Masomo ya lazima yatakuwa 6 badala 7 ya Sasa.

24.Katika O-level Masomo ya Biology na Geography yatakuwa Masomo ya kuchagua pia kwa sababu Maudhui yake yamekuwa kwenye Masomo ya Jiografia na Sayansi ya Shule ya Msingi kwa mfano Afya ya Jamii,Afya ya Uzazi, Magonjwa ambukizi nk.

25.Civics, Maarifa ya Jamii,Uraia na Maadili yamefutwa, Maudhui yake yameingia katika somo la Historia ya TANZANIA na Maadili.

26.General Studies (GS) katika A-level itafutwa na Maudhui yake yatawekwa katika Somo la Historia ya TANZANIA na Maadili na Mawasiliano ya Kitaaluma.

27.Kufuta baadhi ya Masomo kumefanyika ili kuondoa tatizo la kujirudiarudia kwa Maudhui.

28.Michepuo katika Elimu ya O-level imeongezeka kutoka minne (4) hadi tisa (9).

Michepuo iliyoongezeka ni:-
Sanaa.
Lugha.
Muziki.
Michezo.
Tehama.

29.Masomo ya O-level yatakuwa:-
Biology.
Physics.
Chemistry.
History.
Geography.
Historia ya TANZANIA na Maadili.
Hisabati.
Kiswahili.
English.
Elimu ya Biashara.
Utunzaji wa _Taarifa za Fedha.
Computer Science.
Bible Knowledge.
Elimu ya Dini ya kiislamu etc.

30.Astashahada ya Ualimu itafutwa kisha itaanzishwa Stashahada (DIPLOMA) ya Elimu ya Awali, Ualimu wa Msingi na Ualimu wa Elimu Maalumu.

Watakaosoma Stashahada watakuwa waliomaliza Kidato cha Sita na itasomwa kwa miaka miwili.

31.Walimu wa Sekondari wote watakuwa na Shahada (DEGREE). kwa sababu nchi nyingi zinaenda na mwelekeo huu.

32.Vyuo vilivyokuwa vinatoa Stashahada (DIPLOMA) ya Ualimu wa Sekondari vitatumika kutoa continuous Professional Development.
 
WaTz mmezoa kulalamika tu... Ndiyo maana hamfanikiwi ktk maisha... Jambo hata liwe zuri kiasi gani mmanataka kuleta upinzani hamtaki kujadili mambo ktk upekee wake...
Halafu muwe mnajitahidi kusoma mabadiriko mbalimbali ya kisekta yanapotokea...
HAPANA SIO BURE MI NAHISI TUMEROGWA

Ila mambo ni mengi mno japo hoja zingine za ukosoaji zipo poa sana tu yani ila tuzingatie huu ni mwanzo na Wala si wageni tunajua serikali Huwa inalahumiwa Kwa utekelezaji m'bovu Kwa mipango mbalimbali. Ila hii nchi Kunasehemu tumevrugwa.

Watoto wanamaliza form4 wengine chuo ila hawana hili Wala lile,basi sio mbaya acha tuweka elimu ya ujuzi ngazi ya o level,povu kibao mara watoto wetu watafanywa kuwa saidia fundi tu mara hivi.

Sijui utekelezaji utakuwaje(kimazoe au kiumakini?) na uzuri Raia tushaanza kuonesha wasi wasi juu ya serikali hasa kwenye swala la utekelezaji
 
Back
Top Bottom