Hii imekaaje wazee

Hii imekaaje wazee

Mkuu hapo kuna jambo inawezekana huyo mwanao hela hana so alishindwa kukujibu kwa kuwa wwe ni mzazi akamtumia mke wake

Au mwanao kashikwa na mkweo
 
Ampe mzaziwake pesa alitaka akamwambie nani kma sio yeye mtotowake huyo mke huko kwao huwa hachangii misiba au hebu aache utoto
 
Huna akili, mambo ya mzazi wako yanamuhusu vipi mkeo?

Yani mmetawaliwa na wanawake kiasi kwamba hakuna kitu unaweza kufanya bila kumshirikisha mke wako?

Huu ni upumbavu na ukemewe kwa nguvu zote, hakuna replacement ya mzazi, tena ficha ujinga wako huu utachekwa, wewe unaweza kumjibu mzazi wake hivyo?
 
Hellow african

Wewe tuchukulie ni mzazi una muomba mwanao hela kuna ndugu yenu kafariki unamuuomba hela ya kuchangia kwenye msiba umeongea na mwanao wakiume akakubali vizuri baada ya nusu saa mkweo anakupigia simu anakuambia kuwa hakuna hela kama hakuna ulazima wa kuchangia usichangia wewe utamchukuliaje huyu mkweo?
Dogo huna akili kwann umwambie kuhusu Hela unazowapa wazazi wako
 
Mda mwingine busara inaitajika ndio maana watu wanasema mapenzi yana nguvu angalie na wake wa kuoa ndugu wa mume walimkata huyo mwanamke kitambo sana mwanamke anavaa kikukuuu amechora tatuu mwanamke anajikoboa wazazi waliona ishara mbaya wakagoma mke akaamua amebebe mimba kwa makusudi
Umejuaje kama alibeba mimba kwa makusudi? Je unajua makubaliano yao wanapokuwa wawili?
 
Sio kupigwa vita kuna vitu watu tunaishi navyo na kuona vya kawaida ni bora tuongee watu wapate kuamka kuna wanaume wengi hata humu wapo maamuzi wanafanyiwa na wake zao
Mnaoviona vya kawaida ni ww, huyo mwanao na jamii ilowazunguka,na kwa maana hiyo bas mnahitaji ufufuo na uzima
 
Mkuu sio mimi mimi siwez kubali uho ujinga ni mshikaji wangu wa karibu sana ndio yamemkuta
Hivi kwa nini mkiletaga story zenu humu za ajabu ajabu mkishukiwa kama mwewe mnasingizia jamaa zenu? Mwanaume ambaye kila kitu anamshirikisha mkewe atakuwa anamapungufu fulani.
 
Mwanaume ukishaoa, upatapo hela tenga mafungu 3.
1. Kwa ajili ya matumizi ya familia
2. Kwa ajili ya uwekezaji na dharurA
3. Kwa ajili yako binafsi.
Kama huyo mwamba anapangiwa hadi matumizi na mkewe mwambie anunue dera tu aanze kucheza baikoko
 
Back
Top Bottom