Uchaguzi 2020 Hii inakatisha tamaa kwa Dkt. Magufuli

Tuchague kuuza nchi yetu kwa Amsterdam Mzungu mrafi na mroho.
Mlitengeneza fomu moja ya mgombea na watanzania waliojiandikisha ni 29 million hamshangai? NEC ya ccm yangu uchaguliwe mwaka 2017 aliwadharau hakuhangaika nao Wala kuwatumia kumshauri ,akasema hajawajua Hadi leo. Aliwadharau wanec Sana.
 
Watabadirisha kila kitu, watajenga na kufanya mambo mengi lakini hayatawapa ushindi kwenye mioyo ya watu, walichokosea ni kimoja tu ni kwamba wamepora uhuru na haki za msingi za raia wa Tanzania kwani walizuiwa na nani kutenda haki huku wakileta maendeleo?
 
[emoji706][emoji706][emoji706]
 
Kwa huyo mnaemtaka atakuja kufanya nini?
Kuweka rehani madini ili waweze kupewa msaada? Au kumililisha Mali za Taifa kwa hao mabeberu kama wanavyojieleza kwenye ilani yao.
Magufuli aliwekeza zaidi kwenye propoganda,barabara nyingi bado zipo pale pale alipoishia kikwete,na ujenzi wa reli ndo kwanza umeanza,kwa kifupi he has done nothing
 
Nitajie nchi ambayo Rais anayetetea nafasi yake huwa anaachana na majukumu yake ya Urais pale inapofikia kipindi cha Uchaguzi mkuu.
Ndio maana panahitajika tume huru,maana yake watendaji wote wa tume kuanzia ngazi ya taifa hadi chini waajiriwe na tume na wawe wanawajibika kwa tume ya uchaguzi peke yake,sasa unakuta DED mwajiri wake nani? si ni huyo rais ambaye pia ni mgombe unamtajiaje atende haki? kule tume kaajiriwa kwa muda lakini anabaki na uajiriwa wake serikalini kuna haki hapo.
yote hayo yanatokana na uoga wa CCM pakiwa na haki haitadumu madarakani.
 
Kwa huyo mnae mtaka atakuja kufanya nini ?
Kuweka rehani madini ili waweze kupewa msaada ? Au kumililisha Mali za Taifa kwa hao mabeberu kama wanavyojieleza kwenye ilani yao
Mimi sijui Sana kiswahili je kuna mtu anaeweza niambia mabeberu ni Akina nani?
Nchi wahisani ni zipi
Tafadhali zitaje nchi wahisani na nchi mabeberu
 
.
Ni vema ukaandika haya baada ya 28. 10 .2020, maana unayoandika Nia sawa na usiku was Giza.
Kwa mihemko yako wadhani watu wote wanamchukia JPM.
Subiri, time will tell.
unataka kutuambia kuwa
> mgombe wenu ataripa visasi endapo tutamchagua
> mgombea wenu hatafuata sheria na haki za raia za uhuru wa mawazo
> ataendelea tena kuwa Mungu mtu kama alivyofanya safari hii
> atatunyanyasa zaidi ya kipindi kilichipita,kama mateso yatazidi kipindi kilichopita kuna sababu gani ya kumchagua
CCM mmerogwa na nani kwa nn mnawatisha wapiga kura huku mnatarajia ushindi wa kishindo how?
 
Je CCM endapo ikaanguka wataendelea kuitetea Katiba hii iliyopo??
 
Fikra ndogo hii mdogo wangu ni kweli Mimi ni kaka yako lakini, sina hata chembe moja ya akili iliyolala kama ninavyoona wapinzani wanavyohaha huku wakiwa hawajui wanapinga nini, na siwezi kukulaumu wewe maana najua ni wakati tu unaokufanya ukahisi unachokiwaza kwa Sasa uko sahihi.
 
Kwa huyo mnae mtaka atakuja kufanya nini ?
Kuweka rehani madini ili waweze kupewa msaada ? Au kumililisha Mali za Taifa kwa hao mabeberu kama wanavyojieleza kwenye ilani yao
Hilo tutalijadiri 2025.kwa sasa tunajua for sure magu hajafanya lolote zaidi ya propaganda, hilo la Lissu acha tumpe kura tu then 2025 tutajua
 
Muacheni adanganywe na kina Polepole ili siku akistuka Wananchi wamemgomea asijue wapi pa kuazia.
Rais Magufuli angekuwa Rais bora kama angeamua kufungua masikio yake. Haisikilizi, haoni wala hahisi chochote kile kutoka kwa binadamu wenzake. Rais wetu anahisi amaongoza watoto wake wa kuzaa kiasi kwamba katika mila zetu za Kitanzania baba hakosei na yupo sahihi. Amejiaminisha kuwa yupo sahihi dhidi ya watu zaid Milioni 50 wa nchi hii.
Kujenga majengo wakati watoto wako wanalala njaa na kukosa huduma muhimu ni ujinga wa kiwango cha juu zaidi.
Hakuna Mtanzania atalamika ukosefu wa ndege dhidi ya chakula.
Rais Magufuli aelimishwe kuchagua vipaumbele kutokana na muda tulionao.
 
Si jukumu la serikali kumpa pesa mtu, si jukumu la serikali kumjengea mtu nyumba yake, si jukumu la serikali kukutaftia ww chakula ule, si jukumu la serikali kukununulia ww nguo uvae upendeze bali vitu hivi ni juhudi zako binafsi mwenyewe na akili zako kuvitafta, jukumu la serikali ni kushughulika na vitu vya umma/vyenye faida kwa wote na si kwa mmoja mmoja, kama ww ni mkulima lima uza mazao yako pata pesa jenga,kula, vaa, kam ww n mfanyabiashara uza bidhaa zako pata pesa tumia kwenye mambo yako, kam we umeajiriwa fanya kazi lipwa mshahara fanyia mambo yako, kama umeshindwa kufanya kazi ukapata pesa kuendesha maisha yako basi utasubir sana na kuitupia lawama serikali wakati haihusiki moja kwa moja na maisha yako
 
Maendeleo ya Nchi na watu kuna ufisadi mkubwa kwenye miradi yote mikubwa, kuna 10% ununuzi wa Ndege kuna ufujaji wa pesa za umma kujenga chato Airport kienyeji pasipo idhini ya bunge huku CAG alitolewa kafara kuficha Aibu
 
Nitajie nchi ambayo Rais anayetetea nafasi yake huwa anaachana na majukumu yake ya Urais pale inapofikia kipindi cha Uchaguzi mkuu.
Nchi zote kasoro Tanzania pekee ndipo kuna Ujinga huo kinyume cha haki za demokrasia, bunge lilivunjwa lakini mpaka leo mawaziri wapo kazini , wanawania ubunge wakiwa na magari ya wizara zao, katiba imekiukwa kwa kiwango cha kutisha sana.
 
Watu walikuja kushangaa kinyago walicho chonga wazungu, hawajazoea maana vinyago vingi vinatengenezwa na wamakonde.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…