Hii inatokea na inawezekana tu Tanzania, hivyo acheni wenye Akili watucheke na watudharau kwani tumejitakia na tunastahili

Mkuu binafsi naelewa hoja yako,lakini nikiwa mmoja wa vichwa maji,naomba nisaidie kujua hili; kama bunge tunaliita kwa awamu, kwanini sasa hatusikii bunge la awamu ya kwanza,pili,nk bali tunasikia bunge la kwanza,la pili,la tatu,.....na sasa tunalo bunge la 12?
 
Wajinga na wanasheria wa porini mnashida sana ukiisoma katiba mwanzo hadi mwisho huwezi kutana na hicho mnacho ita AWAMU, HAKIPO

Katiba inaongelea urais na Rais sasa hayo ya awamu sijui wajinga nyie mliko yatoa na ni wajinga pekee ndio wanahangaika nalo
 
Nani ameleta habari za kumchukia?? Umelewa sio???

Upumbavu wenu na kosoa kosoa zenu zisizo na msingi hazina nafasi AWAMU hii.

Mheshimiwa rais Mama Samia hana muda wa kusikiliza kosoa kosoa za kipumbavu. Muda wake ameutenga kutumikia Watanzania
Wanao hangaika na awamu ni wale walio aminishwa kuwa kuna mtu atakuwa Rais wa milele sasa kwavile walikuwa wakinufaika sana tena kiharamu na huo urais wake kwa bahati sasa mambo yameenda tofauti kabisa na matarajio yao matokeo yake wameona dawa ni kumchukia tu huyu aliyepo.
 

Sasa Mwamba, JPM si amekula chaguzi mbili? 2015 na 2020, zilibadilisha awamu za utawala wake?

Nyerere alikaa madarakani miaka zaidi ya 10 bado ilihesabika awamu ya kwanza.

Mwinyi miaka 10 awamu ya Pili, ingetokea amekua madarakani 85-90, awamu yake ingeishia hapo, angekua ametawala muhula mmoja tu.

2020 kwa mfano Mzee wa Ubwabwa angenyanyua kombe, angekua Rais wa awamu ya sita.

Kwa mantiki hiyo, awamu haziehesabiwi kwa chaguzi bali ni anaeshika madaraka.
 
Kwa mujibu wa Katiba tuliyonayo sasa hivi Rais atadumu kwa kipindi kisichozidi miaka 10 maana yake atachaguliwa kila baada ya maika 5.
Sasa tujiulize, Je Samia anayeongoza sasa hivi ambaye kikatiba anaruhusiwa kuendelea mpaka 2030 atakoma kuitwa Rais wa awamu ya 5 mwaka 2025 na baada ya hapo ndio aitwe Rais wa awamu ya 6 ambaye kikatiba lazima akomee 2030? Maana yake kama awamu iatambulika kwa mihula ya uchaguzi basi awamu ya 5 utakuwa na mihula 2 na ya sita itakuwa na mhula mmoja tu.
Awamu inatambulika kwa kuhesabu vichwa vya Urais.
 
You're a typical sample of a Wasted Sperm.
 
Watapata tabu sana mkuu
 
Hili neno awamu linatumika kuelezea kwamba Nchi imepitia ktk uongozi wa marais wangapi.
Yaani tangu tupate uhuru Tanzania tumeongozwa na Nyerere(awamu ya kwanza)
Mwinyi(awamu ya pili)
Mkapa(awamu ya tatu)
Kikwete(awamu ya nne)
Magufuli(awamu ya tano)
Samia(awamu ya sita)
Kwahiyo neno "awamu" lipo ktk kuwakilisha "kichawa/utawala wa..." na wala si mihula ya chaguzi kuu za urais kwa mujibu wa katiba ya jmt.
Hivyo ni sahii kwa SSH kutamka yeye ni rais wa sita au awamu ya sita tangu nchi yetu ipate uhuru.

Mkuu Generalist bila shaka umeelewa vizuri.
 

Muhula upo kikatiba, awamu haipo kabisa. Ni kama ulivyoeleza, inawakilisha mtu anaeshika kiti cha Urais.

Vinginevyo waliodumu madarakani wangekua na awamu mbili mbili.
 
Ili nikuelewe naomba majibu ya haya Maswali yangu yafuatayo tafadhali...

1. Kama Samia ni Rais wa Awamu ya Sita CCM walimpitisha lini, alishindanishwa na nani, Mchakato wa kupatikana Kwake ndani ya Chama ulikuwane hadi Kugombea Urais na kuibuka Mshindi rasmi?

2. Kama Samia ni Rais wa Awamu ya Sita ni lini NEC waliitisha tena Uchaguzi Mkuu hasa baada ya Kifo cha Rais Hayati Dkt. Magufuli?

3. Kama Samia ni Rais wa Awamu ya Sita je, Katiba ya CCM inamtambua ni wa Awamu ya Tano au inamtambua ni wa Awamu ya Sita kama anavyoilazimisha Yeye kila Uchao?

4. Kama Samia ni Rais wa Awamu ya Sita je, anaruhusiwa Kurithi Baraza la Mawaziri lote la aliyekuwa Rais ( Mtangulizi ) wake na kwamba alivyoapishwa tu ( baada ya Kifo cha Rais ) hakutakiwa Kuvunja Baraza zima la Mawaziri na kwamba hata Bunge nalo lingetakiwa Kuvunjwa ili Uchaguzi ufanyike upya?

Nayasubiri upesi sana Majibu ya haya Maswali yangu Manne tu ili nijue kuwa Wewe ni 'Great Thinker' au ni wale wale 'Vichwa Maji' niliowazoea tu.
 
Me huwa nahisi wanakosea kwa bahat mbaya kumbe wako 'sirias'
 
Tunamsubiri Tundu Lisu atasema nini ju ya mama. Au ndo kisha pata woga sasa. Ama kweli asie funzwa na *****, ufunzwa na ulimwengu.
 
Ni lini muheshimiwa ataacha kututangazia jinsia yake?
Na wale ambao hawachoki kuimba "Tuna imani nae Mama" yaani ni kama vile wanalazimisha kwa kutumia nguvu sana ili watu waamini kuwa 'mwanamke' anaweza........... Ni kweli anaweza hakuna haja ya kugongomelea kila saa kama vile wanawasuta watu.
 
Hivi bado unajiona una akili! Kajipime Mirembe!
 
Kwanza fahamu, awamu si neno rasmi katika medani za kiutawala wa nchi. Ni neno la wana CCM kueleza ni hatamu ya uongozi wa nani katika chama chao.

Uchaguzi wa Tanzania hauweki awamu, unaweka idadi tu ya uchaguzi.

Huwezi kujadili jambo bila ya kufahamu misingi au taratibu ya jambo hilo. Ukifahamu haya, sasa pima wazo lako na fanya mjadala.
 
Inawezekana kweli Magufuli aligufuliwa ili kuunda awamu ya sita itakayorudisha awamu ya nne? Nilisikia kuwa alipelekwa JKI na baada ya hapo ikawa history; majuzi niliuliza ni daktari gani aliyemtibu sikupata jibu.
 



Kuna baadhi wanataka aya za bandiko lako; nimefanikiwa kuwatengenezea.
====
Hoja zako zinashawishi. Lakini Mkuu, nadhani kama nchi tumekubaliana awamu za urais ni miaka kumi endapo rais atapata ridhaa ya wananchi ya kuendelea kuongoza nchi baada ya miaka mitano kwa mujibu wa matokeo ya uchaguzi mkuu. Yaani akimaliza 45 dakika za kipindi cha kwanza na kipindi cha pili akakubali kuingiza timu uwanjani.

Hayati Dr Magufuli alimaliza dakika 45 za kipindi cha kwanza (5 miaka), akaingiza timu uwajani kipindi cha pili (wananchi wakamruhusu aendelee na awamu yake ya tano). Mungu akampenda zaidi akamchukua, bahati nzuri alikuwa na msaidizi wa kuiongoza nchi katika awamu ya tano, tena walianza wote awamu hiyo. Kwakuwa Hayati Dr Magufuli ametwaliwa, technically, msaidizi wake anapewa nguvu na katiba ya nchi kumalizia dakika 45 za kipindi cha pili cha mechi hiyo (kukamilisha awamu ya tano yao waliyoruhusiwa na wananchi mwaka jana wamalizie).

Kama awamu ya sita ilitakiwa kuanza muda huu, kwa maoni yangu, nadhani aliyepewa jukumu la kuongoza nchi kwa mujibu wa katiba alitakiwa kuvunja bunge, kisha kuitisha uchaguzi mkuu mpya. Lakini, kama msaidizi ambaye sasa ni kiongozi wa nchi kwa sasa hajisikii vyema kujitambulisha kama alishiriki kuingiza timu kipindi cha pili kwamba anamalizia ngwe ya awamu ya tano, isiwe shida. Tusimlazimishe, kwa sababu nadhani watanzania tulio wengi tunahitaji ustawi wa Tanzania katika nyanja zote hasa kiuchumi. Haya mambo ya ustawi ndiyo mambo ya kulazimisha tena kwa staha. Na sisitiza tumlazimishe rais wetu mambo ya ustawi wa nchi yetu kwa STAHA.

Yangu ni hayo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…