Hii ipoje kuhusu mwanaume kuwa na kipato ndio aoe??

Hii ipoje kuhusu mwanaume kuwa na kipato ndio aoe??

Kelams

Member
Joined
Jan 9, 2024
Posts
12
Reaction score
25
Kumekuwa na mijadala mingi kuhusu suala la "Wakati gani wa Mwanaume kuoa". Wengi wameenda mbali zaidi na kusema, "Suala la mwanaume kuoa sio umri, bali ni kipato na uwezo wa kuilea familia"

Swali: Mwanaume huyo atagundua vipi kuwa kipato chake alichonacho sasa kinamwezesha yeye kuoa?? Ni kipato cha aina gani akiwa nacho Mwanaume ana uwezo wa kuhudumia mke na mtoto/watoto?
 
Dunia ya leo mtu akisikia kauli kipato kichwani anajiwa na mawazo ya mtu anayeingiza kwa siku 50K,mwenye nyumba nzuri kazi nzuri etc.

Kipato kinachozungumzwa ni kule wewe mwenyewe ulipokuwa bachelor hukuwahi kulala njaa,japo una kipato limit kwamba kwa siku ni 10/20K ila kuna siku inafunguka unapiga hata 40K mtu wa hivi hashindwi kuishi na familia kama kuoa ingezingatiwa kuwa na kipato kikubwa kama wengi wanavyodhani basi kuoa wangeoa wachache sana.
 
Kelams Swali zuri,

Kwanza sijajua umri wako lakini mathalani kwa kijana wa makamo (25-35) ni vema kabla hajaingia kwenye swala la ndoa atambue anataka nini kwenye maisha yake (vipaumbele).

Wapo watu ambao familia ni kipaumbele cha kwanza kwenye maisha yao, wapo wengine wanahitaji kutimiza malengo mengine tofauti ya kimaisha kabla ya ndoa, yote kwa yote hakuna umri maalum ulioahinishwa kuoa, cha kuzingatia ni viupaumbele vyako ulivyojiwekea.

Kukujibu swali lako la kuhusu kipato na ni kwa namna gani atagundua kuwa amefikia kiwango kitachomuwezesha kuoa.

Kwanza pesa haijawahi kutosha maishani, mathalani hata matajiri kila siku wanapambana kuongeza vipato vyao, kwahiyo hakuna muda utafika na kusema pesa imetosha kuingia kwenye ndoa ila cha msingi ni pale ambapo utaona unaweza kujikimu wewe na huyo mtarajiwa wako pamoja na familia, hii pia itategemea na mtu utakaetaka kuwa nae na maisha (lifestyle) mnayoishi, kama utataka kuingia kwenye ndoa na "madunga embe" (slay queens) hapo ni lazima ujipange haswaaa, lakini kwa maisha yetu ya kitanzania hakikisha una kuwa na mtu utakae mmudu kwa kipato chako lakini pia jitahidi uongeze vyanzo vyako vya mapato kwasababu unapoingia kwenye ndoa tegemea baada ya muda familia itaongezeka (watoto), watahitaji kula, kuvaa,kusoma n.k.

Kupanga ni kuchagua.
 
Ni dhana ya vijana wa kisasa tu zamani mambo hayo hayakuwep
Kelams Swali zuri,

Kwanza sijajua umri wako lakini mathalani kwa kijana wa makamo (25-35) ni vema kabla hajaingia kwenye swala la ndoa atambue anataka nini kwenye maisha yake (vipaumbele).

Wapo watu ambao familia ni kipaumbele cha kwanza kwenye maisha yao, wapo wengine wanahitaji kutimiza malengo mengine tofauti ya kimaisha kabla ya ndoa, yote kwa yote hakuna umri maalum ulioahinishwa kuoa, cha kuzingatia ni viupaumbele vyako ulivyojiwekea.

Kukujibu swali lako la kuhusu kipato na ni kwa namna gani atagundua kuwa amefikia kiwango kitachomuwezesha kuoa.

Kwanza pesa haijawahi kutosha maishani, mathalani hata matajiri kila siku wanapambana kuongeza vipato vyao, kwahiyo hakuna muda utafika na kusema pesa imetosha kuingia kwenye ndoa ila cha msingi ni pale ambapo utaona unaweza kujikimu wewe na huyo mtarajiwa wako pamoja na familia, hii pia itategemea na mtu utakaetaka kuwa nae na maisha (lifestyle) mnayoishi, kama utataka kuingia kwenye ndoa na "madunga embe" (slay queens) hapo ni lazima ujipange haswaaa, lakini kwa maisha yetu ya kitanzania hakikisha una kuwa na mtu utakae mmudu kwa kipato chako lakini pia jitahidi uongeze vyanzo vyako vya mapato kwasababu unapoingia kwenye ndoa tegemea baada ya muda familia itaongezeka (watoto), watahitaji kula, kuvaa,kusoma n.k.

Kupanga ni kuchagua.
Hakika ni kuchagua
 
Wazazi ndio chanzo, anataka afaidi zawadi ya mtoto wake wa kike... So lazima uwe na kipato cha kuweza kutoa M30 na Moo 30 ili uoe
 
Kwa zama hizi nadhani suala la ndoa lime kuwa complex kinyama, sio wanandoa wenyewe hadi hiyo ndoa yenyewe ni kisanga.

ndoa ni muungano wa watu wawili, mki elewana vyema hiyo ndio nguzo kuu maana mta jua namna bora ya kupangilia maisha yenu.

Hiyo 10k Kwa siku Kwa baadhi ya familia ni kipato kikubwa sana, ikiwa kita fika sehemu sahihi.

Sio mna kutana kwa mkapa halafu ghafla ndoa, kinacho fata ni kugomeana tu.
 
mbna simple tu, uwe na kipato cha kumudu basic needs zako wewe na familia i mean mke na watoto basi
 
Ishu sio kipato kwa maana ya kiwango cha fedha ulichonacho. Kila mtu ana namba yake. Ishu ni je, Ukarimu unao?? Unaweza kutoa 10 yako ya mwisho ukaacha kodi ya meza wewe ukatembea au kujikaza kiume?
 
Back
Top Bottom