Hii kusema kuwa Waamuzi wanazibeba timu kubwa ni kuwatwika mzigo isiyostahili

Hii kusema kuwa Waamuzi wanazibeba timu kubwa ni kuwatwika mzigo isiyostahili

May Day

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2018
Posts
6,311
Reaction score
9,027
Kumekuwa na mijadala iliyoibuka haswa kwa hizi timu zetu kongwe huku kila upande wakijaribu kutumu kuwa Refa alipendelea timu kubwa.

Mbaya zaidi ni pale hata wale wenye nafasi ya kusikilizwa au kuaminiwa kama Makocha, nao wakiingia kwenye mkumbo huo.

Inashangaza na kuhuzunisha kwa Mtu Mzima mwenye akili timamu anapopambana kupinga adhabu kwa tukio ambalo hata angekuwa yeye ndio anachezesha angelazimika kutoa kadi kwani sheria na kanuni inataka hivyo.

Tunawapa presha bure Waamuzi ili hali hakuna tukio mahsusi Mtu analoweza kulisisitizia kuwa Refa kafanya upendeleo wa makusudi...matukio mengine ni hamsini kwa hamsini na kwa uamuzi wowote ambao Refa angefanya basi lazima angelaumiwa na upande mmoja.

Mimi sio Mtaalamu wa soka lakini kwa kuona tu walau naweza kufanya tathmini ya kiwango changu.

Kwa mfano mechi ya juzi ya Simba na Namungo ilitawaliwa sana na uchezaji wa kukamia haswa kwa upande mmoja ambapo Refa alikuwa kwenye mtihani mkubwa wa kukwepa mitego ya udanganyifu iliyokuwa ikifanywa na Wachezaji ili kunufaika kirahisi... haswa wale wa Namungo..kiukweli tunatakiwa kumpongeza Muamuzi maana alikuwa kwenye wakati mgumu.

Mara kadhaa tuliona Wachezaji wakijiangusha na Refa alipowapotezea waliamua kuamka wenyewe na kuendelea na Mchezo.

Tukio kama la Morison, Manula au Boko, huenda wengi tungetamani Refa angetoa adhabu lakini sasa tukumbuke kwa aina ya uchezaji waliokuwa wanaonesha Vijana wale ni ngumu kujua kama kweli ilitumika nguvu kubwa au aliguswa tu na kujitupa chini kwa kishindo ili kumshawishi Mu/Waamuzi?.

Tukumbuke sisi tunaangalia kwa karibu kupitia Runinga ili hali Muamuzi yeye alikuwa anafuatilia kule Mpira ulipo tofauti na camera inayotuonesha sisi Watazamaji...Hivyo Waamuzi wasipokuwa makini wangejikuta wanatoa adhabu kwa faida ya aliyedanganya.

Tukio kama la Inonga kwenye mechi na Coast ambapo ilibidi aadhibiwe kwani kupeleka kichwa chake tu inatosha kuonesha nia ovu hata kama Mchezaji yule hakuguswa...na tusiwe Wanafiki hivi Mtaani kweli Mtu ataangushwa kwa kupigwa kichwa chepesi vile?...lakini kwa kuwa kuna sheria za mpira na kanuni basi ilibidi aadhibiwe na ilikuwa haki.

Kadi nyekundu ya Namungo, Ruvu shooting hivi kweli tunawataka nini Marefa?. Kwa Mechi zote hizi mbili sijaona kukosea kukubwa kwa Marefa mpaka kustahili kushutumiwa kwa nguvu na misuli ya shingo kututoka.
 
Kuna matukio yanasababisha timu ionekane Ina bebwa mfano mechi ya Simba na namungo,
John Boko kabla Kona aijapigwa amsukumiza kwa mikono miwili Defender wa namungo kama mieleka na kumtupa chini na hajapewa kadi.
Kipa Aish manula anatoka langoni mbaka nje ya 18 anamzuia mchezaji wa namungo Jacob Masawe kwa mikono na kumwangusha chini lakini hajapewa kadi.

Benard Morrison wakati Simba inafanya shambulizi kwenye Lango la Namungo ana mpiga Defender wa namungo Kiwiko na kumwangusha lakini refa hajatoa kadi, iyo ndio maana halisi ya timu kubebwa.
 
Mbona nimetoa maelezo kwa hayo matukio.

Nimesema Wachezaji wengi walikuwa wanajitupa chini hovyo hivyo ni mtihani kwa Muamuzi kujiridhisha kama kweli kulikuwa na nguvu kiasi hicho mpaka Mtu kuanguka au alijilegeza tu?...vipi kama Morison alirusha tu mkono Mchezaji akajitupa kama kapigwa na gobore? Muamuzi nae anakwepa kudanganyika kijingajinga.

Na mbona hukutaja tukio la Kibu kupigwa kichwani na Refa hakutoa adhabu, si ni kwamba tu alishindwa kujiridhisha ingawa sisi tunaotazama kwa Runinga tulijiridhisha tukaona ile ni faulo iliyohitaji adhabu kwa Mchezaji...tukitanguliza ushabiki tutajikuta tunawaonea sana Marefa.
 
Mm kwa mashabiki sishangai sana maana ndio kazi yao na ndio maana ya ushabiki ni pamoja na kupenda kilichochako,ila nashangazwa na makocha ambao wamesoma mpra wengine walikua wachezaji bado wanakua wanafiki ili kidogo ndio linaniuzi makocha weng wa tz ni wagumu kukubali matokeo mara nying wanashusha lawam kwa refa mfano simba na namungo yule kocha ana haki gan kumuona refa amekosea nazan na wao sijui wana ushabik dunia gan ambayo mpira wa miguu dk 90 zote refa atakua sawa kwa kila maamuz yan mengine ni makosa ya kibinadam au kimpra lkn sisi tunataka kuhukumu uko ulaya pamoja na wao kuwa mbele zaid na kuruhusiwa kuangalia ad marudio ili watoe maamuz bado kuna makosa meng ya wazi na uzur wa makosa ya mpira hayabak kwa timu moja tu hakuna timu ambayo haijawai kunufaika kwa makosa ya waamuz
 
Ivi lile tukio alilofanya Aishi manula kumwangusha Jacob Masawe linaitaji Nini ili uelewe Marefa Wana hongwa? Tukio liko wazi kabisa na adhabu iko wazi ni kadi ya Njano alafu refa ana pepesa.
 
Mm kwa mashabiki sishangai sana maana ndio kazi yao na ndio maana ya ushabiki ni pamoja na kupenda kilichochako,ila nashangazwa na makocha ambao wamesoma mpra wengine walikua wachezaji bado wanakua wanafiki ili kidogo ndio linaniuzi makocha weng wa tz ni wagumu kukubali matokeo mara nying wanashusha lawam kwa refa mfano simba na namungo yule kocha ana haki gan kumuona refa amekosea nazan na wao sijui wana ushabik dunia gan ambayo mpira wa miguu dk 90 zote refa atakua sawa kwa kila maamuz yan mengine ni makosa ya kibinadam au kimpra lkn sisi tunataka kuhukumu uko ulaya pamoja na wao kuwa mbele zaid na kuruhusiwa kuangalia ad marudio ili watoe maamuz bado kuna makosa meng ya wazi na uzur wa makosa ya mpira hayabak kwa timu moja tu hakuna timu ambayo haijawai kunufaika kwa makosa ya waamuz
Ni ajabu Mtu anaikataa hata ile kadi nyekundu ya Makame, mpaka unajiuliza kama yeye angekuwa refa angefanyeje?.

Maana pale hata kama asingemgusa Kapombe kanuni ya vile tu alivyocheza Makame ni red card.
 
Ivi lile tukio alilofanya Aishi manula kumwangusha Jacob Masawe linaitaji Nini ili uelewe Marefa Wana hongwa? Tukio liko wazi kabisa na adhabu iko wazi ni kadi ya Njano alafu refa ana pepesa.
Unachotaka ww ni kigumu ata kama inakua kwel unavyotaka ww et kahongwa ili mpra wa miguu una makosa meng ambayo tukianza kuyasema dk zote zitaisha kuesabu makosa tu ndio maana yupo refa yule kazi yake kufuata sheria lkn yeye binadam sio yote hatafanya kwa usahihi kwa ilo tukio unalosema haliwez kuwa sababu ya kusema kahongwa angetoa kad ya njano sawa na ata alivyoacha sawa sio kusema wale namungo kila faulo au tukio walihukumiwa kwa kad huo mpra dunian haupo yan kwamba kila ktu kiwe sahihi ,lkn kuna matukio ata kama uwe ww utatoa tu kadi au faulo ,ebu fikiria dk 45 za kwanza kwanza zilikua na faulo nyng pamoja na muda kupotea apo apo kukawa ma waterbrake alaf bado ikaonyeshwa dk 1 ya nyongeza ni sawa apo,tukianza kuesabu makosa ktk mpr wa miguu hayaish na hayasababishwi na kuhongwa au vp ila yapo mengine ya kibinadam mengine ya uzembe au kutokujua sheria sikatai ,tunaweza kusema apa kwetu marefa wanahongwa je makosa ya waamuz yapo tz tu ,mambo ya kupanga matokeo au marefa kuarbu mchezo kwa sababu zao yapo dunian nzima sasa je ukisema marefa wanahongwa ina maana apa tz marefa wanakosea mechi za simba tu na je kwa msimu ambao kumbukumbu hazijaondoka vzur mechi gan ambayo timu pinzan ilipata kadi ya kuonewa iwe nyekundu au njano
 
Hizi kelele tu cha muhimu ligi inaendelea na hakuna timu imegoma kuleta timu uwanjani.
 
Kosa Kama la Manula kumuangusha Jacob Masawe Tena nje ya 18 Dunia nzima ya soka wanakushangaa refa, atakama umepitiwa vip refa ambaye haja hongwa awezi kuacha kutoa Yellow eti umepitiwa. Kwa wenzetu yale ni matukio Muhimu next metch wanakua demote ukachezeshe daraja la chini uko.
 
Back
Top Bottom