Hii misafara ya viongozi imekuwa kero sasa

Hii misafara ya viongozi imekuwa kero sasa

Shida ipo hapa nowadays huwa respond yao imekua ndogo sana wanasingizia wingi wa comments hivyo wanashindwa kuzisoma kwa wakati..
Hata humu jf tuanzishiwe Jukwaa la kuwa tunaambiana na kupashana habari za Barabarani.

Kuna siku nakuja Dar nimepita Gairo ilikuwa ni usiku wa sasa nne hivi niko mdogo mdogo mara ghafla naona Gari tatu zimegongana Barabara zimefunga Barabara na hakuna alama yoyote.

Hakuna cha Traffiki wala nini ikanibidi niweke Reflector yangu na nikachukua Oanga langu na kuanza kukata majani kwa umbali wa kama mita mia pande zote

Majeruhi na Maiti tukazisomba kuzipeleka Gairo ndio kujua chanzo cha ajali Fuso ilianguka pale Jamaa walikufa wote Gari nyingine zikaja kuigonga ile Fuso na moja kutumbukia korongoni ikaja IT gari dogo Sienta nayo ikaingia chini ya Tela.

Nchi za wenzetu kila gari kubwa ina Radio call na mnapewa frequency moja kama kuna ajali amnayo imefunga Barabara na ni sehemu hatari mnaambiana.
 
Hata humu jf tuanzishiwe Jukwaa la kuwa tunaambiana na kupashana habari za Barabarani.

Kuna siku nakuja Dar nimepita Gairo ilikuwa ni usiku wa nne hivi niko mdogo mdogo mara ghafla naona Gari tatu zimegongana Barabara zimefunga Barabara.

Hakuna cha Traffiki wala nini ikanibidi niweke Reflector yangu na nikachukua Oanga langu na kuanza kukata majani kwa umbali wa kama mita mia pande zote

Majeruhi na Maiti tukazisomba kuzipeleka Gairo ndio kujua chanzo cha ajali Fuso ilianguka pale Jamaa walikufa wote Gari nyingine zikaja kuigonga ile Fuso na moja kutumbukia korongoni ikaja IT gari dogo Sienta nayo ikaingia chini ya Tela.

Nchi za wenzetu kila gari kubwa ina Radio call na mnapewa frequency moja kama kuna ajali amnayo imefunga Barabara na ni sehemu hatari mnaambiana.
Humu watu wanaendekeza habari za ngono tu. Hata ukianzisha thread/jukwaa la traffic updates watatokea wapuuzi na kuuharibu uzi wenyewe wote.
 
Kuna haja serikali itafute njia mbadala ya kusafirisha viongozi maana ishakuwa adhabu kwa raia wengine hasa kwa Dar.

Leo kwa watumiaji wa Pugu Road kuanzia Vingunguti mpaka Airport watakuwa mashuhuda wa hili.

Barabara za Vingunguti kwenda kwa Mnyamani na ya Majumba Sita kwenda Kinyerezi zote zimefungwa sababu ya ujenzi. Mbadala pekee ni mchepuko wa mataa ya Airport.

Sasa leo bila taarifa maalum traffic wamejazana kwenye mataa ya Airport na kwa ubabe kabisa wanaforce watu waende moja kwa moja wasiingie barabara inayokwenda kulia kuelekea majumba sita.

Baada ya takriban lisaa limoja ndio misafara inaanza kutoka Airport. Sasa kwa starehe ya viongozi wachache nusu ya mji ulisimama ama kutaabisha watu kwenda masafa marefu kufika makwao. Kuna baadhi ya watu makazi yao yapo mita chache tu toka petrol station ya Airport lakini walilazimishwa kwenda mpaka mataa ya majumba sita ambapo napo kumefungwa kulazimisha kugeuza tena na kurudi nyuma.

Na hao matraffic waliokuwepo hapo walikuwa wakorofi na kuwa na lugha mbovu walipoulizwa sababu za kuzuia magari. Kuna polisi mmoja bonge alikuwa na uniform za khaki alidiriki hata kutishia kupiga baadhi ya madereva.

Nadhani ni wakati sasa serikali ijitathmini upya katika swala zima la kuratibu misafara ya viongozi. Maana hii ishakuwa kero kubwa hasa mida ya asubuhi na jioni njia ya Airport.

Kuna wakati hata ndege hazijatua magari yanasimamishwa, mpaka itue na hao viongozi wajivute kutoka wakati huo wengine wamenasa kwenye foleni tu.
Wewe itakuwa old skul mwenzangu, PUGU ROAD!! port access road nk
 
Foleni la leo daraja la Kigamboni daaaah. Hii nchi takataka. Tangu saa 12 mpaka saa 4 usiku hii sijatoka Kigamboni
IMG-20221208-WA0040.jpg
 
Haya yote yanatokea sababu tushaaminishwa kuwa hatupaswi kuhoji wenye mamlaka. Mtu anaamua kukufanyq atakavyo kwa kujua tu huna utakapokwenda ama huna cha kumfanya.

Kwa itikadi hii tuliyojengewa ya kuwa mwenye madaraka daima yupo sahihi imepelekea kutoweza kutofautisha kati ya haki zetu na msaada. Imefikia wakati traffic kutokukuandikia ticket sababu kiuhalisia huna kosa basi inakuwa ni msaada na si haki yako.

Japo sheria inasema fine si lazima kulipwa hapo hapo, baadhi ya traffic wanashurtisha kulipwa hapo hapo ili tu kutengeneza mazingira ya rushwa. Na sisi kwa kupuuza haki zetu tunaona tumefanyiwa msaada kulipishwa 5000 badala ya 30,000 isiyo ya halali.
Nchi ikijengwa kwa misingi ya Dhulma Nchi yetu imedhulumu sana Nyumba za Watu imedhulumu Mashamba Viwanda vya watu

Hadi juzijuzi Awamu ya 5 Watu wamedhulumiwa sana.

Lakini Faraja kaja Samia na kasema wale waliodhulumiwa na Utawala wa Awamu ya 5 watarejeshewa Fedha zao na Mali zao

Kwahiyo ile Tiketi niliyopigwa kwa Dhulma pale Chamwimo niliamua kumfanyia "Kisomo" yule Trafiki siku hizi nikipita pale simuoni.
Jazakalah kheyr.
 
Wazungu husema 'silence means consent'.
Ukimya wetu watanzania umemaanisha kuridhia kila jambo tunalofanyiwa.
Kinachotugharimu watanzania ni waongeaji wazuri mno kuliko kutenda. Na hili limekuwa na faida kubwa kwa wana CCM.
Wepesi wa kulalama ndani ya JF huku ni waoga wa vivuli vyao,uzuzu umewakolea, wamepiga kelele kuhusu ajali ya moto kariakoo, mauaji ya Mtwara, ajali ya ndege ziwa Nyanza, milipuko ya mabomu yaliyoua watu wengi etc etc sasa kimiyaa wanalalama kuhusu hizi blue lights!!
 
Dodoma hapa kuanzia bungeni mpaka kisasa sheli kwa hizi siku mbili tumemuona mtemakuni
 
Wepesi wa kulalama ndani ya JF huku ni waoga wa vivuli vyao,uzuzu umewakolea, wamepiga kelele kuhusu ajali ya moto kariakoo, mauaji ya Mtwara, ajali ya ndege ziwa Nyanza, milipuko ya mabomu yaliyoua watu wengi etc etc sasa kimiyaa wanalalama kuhusu hizi blue lights!!
Wabongo ni watu wa kwenda na trend na udaku. Serikali ishajua hilo kiasi cha kulipa kina Diamond washikane matako hadharani kudivert attention kutoka kwenye mambo ya msingi.
 
Nchi ikijengwa kwa misingi ya Dhulma Nchi yetu imedhulumu sana Nyumba za Watu imedhulumu Mashamba Viwanda vya watu

Hadi juzijuzi Awamu ya 5 Watu wamedhulumiwa sana.

Lakini Faraja Samia kasema wale waliodhulumiwa na Utawala wa Awamu ya 5 watarejeshewa Fedha zao na Mali zao

Kwahiyo ile Tiketi nilipigwa kwa Dhulma pale Chamwimo niliamua kumfanyia "Kisomo" yule Trafiki siku hizi nikipita pale simuoni.
Jazakalah kheyr.
Kama dua imetiki ukute mwamba anaendesha zake gari kwa kutumia mfuniko wa ndoo huku makazi yake yakiwa jalalani.
 
Kama dua imetiki ukute mwamba anaendesha zake gari kwa kutumia mfuniko wa ndoo huku makazi yake yakiwa jalalani.
Wacha nikupe siri ya wazi Temeke ina wataalam wa Visomo kama umedhulumiwa basi huwa vinafika na vingine kinasomwa leo kesho majibu.
 
Moja ya hotuba zake maarufu iliyoandikwa kwanza katika makala mwaka 1963 halafu ikajumlishwa katika kitabu chake kiitwacho 'Uhuru na Umoja' ilikuwa barua kali aliyowaandikia wenzake kuwaomba wamsaidie "Kufuta maradhi ya ukubwa" Nyerere aliandika hivi katika mwaka huo wa 1963. ". . . Na vivyo hivyo ndivyo ilivyo kwa vimuli muli vya polisi. Mpaka sasa, kila ninapouliza sababu ya utaratibu huu wa fahari ambao si wa kidemokrasi, nimehakikishiwa kwamba wananchi wanaupenda sana. Lakini kauli hiyo inamashaka sana. Kweli wananchi wanapenda kupigiwa makelele na kufukuzwa barabarani kwa sababu tu Raisi au Waziri au Mkuu wa mkoa amependa kutembea barabarani saa za alasiri? Lazima tuache kujidanganya. Fahari ya namna hii haina uhusiano wowote na mapenzi ya wananchi, kwa sababu ni kinyume kabisa cha demokrasi. Lazima tuikomeshe"
 
Moja ya hotuba zake maarufu iliyoandikwa kwanza katika makala mwaka 1963 halafu ikajumlishwa katika kitabu chake kiitwacho 'Uhuru na Umoja' ilikuwa barua kali aliyowaandikia wenzake kuwaomba wamsaidie "Kufuta maradhi ya ukubwa" Nyerere aliandika hivi katika mwaka huo wa 1963. ". . . Na vivyo hivyo ndivyo ilivyo kwa vimuli muli vya polisi. Mpaka sasa, kila ninapouliza sababu ya utaratibu huu wa fahari ambao si wa kidemokrasi, nimehakikishiwa kwamba wananchi wanaupenda sana. Lakini kauli hiyo inamashaka sana. Kweli wananchi wanapenda kupigiwa makelele na kufukuzwa barabarani kwa sababu tu Raisi au Waziri au Mkuu wa mkoa amependa kutembea barabarani saa za alasiri? Lazima tuache kujidanganya. Fahari ya namna hii haina uhusiano wowote na mapenzi ya wananchi, kwa sababu ni kinyume kabisa cha demokrasi. Lazima tuikomeshe"
Huyo aliyejibu kuwa wananchi wanapenda itakuwa ana walakini.

Tunakubali lazima kuwe na utofauti katika misafara ya viongozi sababu za kiusalama na kiitifaki. Tatizo linakuja katika kutekeleza utofauti huo.

Panapozuiwia magari kwa lisaa lizima kwa vile mtu mmoja anataka kupita tena kipindi cha rush hour, hapo kunakuwa sio itifaki tena bali uonevu.
 
Back
Top Bottom