Hii nchi haina usawa: Mbunge miaka mitano, mafao zaidi ya Tshs. 200M, mwalimu miaka 32 kazini, mafao Tshs. 70M, miezi sita hajalipwa

Hii nchi haina usawa: Mbunge miaka mitano, mafao zaidi ya Tshs. 200M, mwalimu miaka 32 kazini, mafao Tshs. 70M, miezi sita hajalipwa

Aanze kwanza kushusha mshahara wake au kutoa slip salary yake Kama alivyowadanganya wanyonge
Unataka kusema aliposema ameshusha mshahara wake ilikuwa danganya toto?
 
Sheria za mafao wanapitisha wao. Hakuna mwanadamu asiyejipendelea yeye kwanza, though hii ni too much. 5 years 230M kwa kazi ya kusifia na kupiga makofi???
Mbaya zaidi ni hao hao wabunge ndio waliipitisha hii sheria ya mafao, upuuzi tuu. Natamani kila watakapopanda kwenye majukwaa ya kampeni washushwe na fimbo za kutosha. Tumechoka viongozi wanafiki. Halafu ni hao hao walimu wanapewaga nafasi ya usimamizi kwenye chaguzi nyingi na walivyo mambulula huwa wanafata maelekezo ya kijingaaa badala ya kusimamia sheria za uchaguzi. Wacha wateseke mpaka akili ziwarudi.
 
Hii nchi haina usawa. Hii nchi haijapata kiongozi wa kuleta usawa ingalau kwa nusu tu miongoni mwa wananchi.

Tumesikia wimbo huu wa kinafiki kuwa, Rais John Pombe Magufuli ni Rais na kiongozi wa wanyonge, wananchi wa hali ya chini.

Si kweli, no uongo na ni propaganda za kisiasa tu kwa ajili ya wapambe na wanafiki wachache wanaomzunguka huku uhalisia wa mambo ukiwa tofauti.

Mfano wa kuthibitisha hili ni huu;

Bunge limevunjwa juzi tarehe 16/6/2020. Hawa wabunge lililovunjwa juzi wameingia kazini mwaka 2015. Wamefanya kazi yao miaka mitano (5) tu toka mwaka 2015 hadi mwaka huu 2020.

Inasemekana mafao ya kiinua mgongo kwa miaka mitano tu kila mmoja ni zaidi ya Tshs. 250,000,000.

Na inasemekana wakati Rais Magufuli (eti Rais wa wanyonge) anahutubia ndani hiyo juzi kulivunja bunge hilo, tayari mzigo wa fedha wa kila mbunge ulishaingia kwenye Bank Account yake.

Hebu tazama upande wa pili wa wanyonge halisi kinachotokea.

Huko Sengerema (na naamini kwingine kote Tanzania nzima), yupo mwalimu aliyefanya kazi miaka 32 (1988 - 2020) kwa taabu na shida nyingi. Amestaafu tangu mwezi Januari, 2020. Baada ya kukokotolewa kwa mafao yake ya mkupuo atapata kama Tshs. 75,000,0000 hivi.

Kinacholeta shida ni kuwa, tangu huyu mwalimu masikini astaafu kwa mujibu wa sheria mwezi january hadi Juni hii mwaka huu, 2020 (miezi 6 sasa) bado anasotea mafao yake haya kidogo, hajalipwa.

Sasa swali la kujiuliza ni hili;

Kati ya wabunge hawa ambao bunge linavunjwa leo huku mafao yao yakiwa yaneshalipwa jana na huyu mwalimu ambaye kastaafu miezi sita (6) iliyopita na bado hajalipwa vijisenti vyake vya mafao, ni nani hasa mnyonge?

Na huu usawa katika nchi hii uko wapi? Iweje mbunge aliyefanya kazi miaka mitano tu alipwe mafao ya kiinua mgongo kikubwa hivyo kwa takribani mara tano ya mwalimu ama nesi ama daktari aliyefanya kazi kwa miaka 35?

Huyu mtetezi wa wanyonge (Bwana Magufuli) anatetea wanyonge na unyonge upi hasa?

Mimi nasema Tanzania haina kiongozi Rais mtetezi wa wanyonge. Haijapata na hakuna kizuri wala kiongozi mzuri atakayetokana na CCM ili kubadilisha hali hii na kuleta tofauti na usawa.
Mkuu, haya marupurupu ya juu kwa wabunge ndiyo hasa kivutio cha wao kuwa wabunge. Endapo wangalikuwa wanalipwa kama watu wa kada zingine walio wengi wao wala wasingekubali kuifanya kazi hiyo.
 
Mbaya zaidi ni hao hao wabunge ndio waliipitisha hii sheria ya mafao, upuuzi tuu. Natamani kila watakapopanda kwenye majukwaa ya kampeni washushwe na fimbo za kutosha. Tumechoka viongozi wanafiki. Halafu ni hao hao walimu wanapewaga nafasi ya usimamizi kwenye chaguzi nyingi na walivyo mambulula huwa wanafata maelekezo ya kijingaaa badala ya kusimamia sheria za uchaguzi. Wacha wateseke mpaka akili ziwarudi.

Nina dada yangu Mwalimu amestaafu toka mwezi wa sita mwaka 2018. Mpaka leo anafuatilia mafao yake na hajalipwa. Mbaya zaidi kwa sasa anaumwa na hana msaada wowote wa kifedha.

Hapo ndipo ninapowaona wale wafanyakazi wanaoiba na kuchukua rushwa wakiwa kazini ni mashujaa. Kwa nchi hii hali ilipofikia kufanya kazi kwa uaminifu kwa kutegemea utakuja kulipwa mafao ni ujinga wa hali ya juu!!!
 
Wajinga ni sisi wananchi kukubali kudanganywa na hawa wanasiasa, inatakiwa nchi iwe chini ya wananchi na sio wanasiasa wasiojali.
Tumekuwa taifa la waoga, wanafiki na watu wa kujipendekeza kwa watawala baadala watawala wajipendekeze kwetu.
Hakuna taifa hata moja duniani lililo chini ya wananchi bali mataifa yote yako chini ya wanasiasa. Huu mfumo unaboa sana na mwisho wa siku tunajikuta tunawafanyia wao kazi na wanajineemesha
 
Kimsingi neno 'kutunga sheria' imekaa kisiasa mnoo. Kiuhalisia ni kwamba wabunge wao 'hupitisha' sheria tu. Wizara ya sheria na katiba pamoja na mamlaka zake ndo hutunga sheria. Ambao hao 'watungaji' huishia kupata 70m baada ya miaka 30.
Kwahiyo huo mchakato wa kupitisha sheria uwe unafanywa na nani ?
 
Back
Top Bottom