Hii ndio orodha ya majiji mazuri zaidi Tanzania

G Tank

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2023
Posts
2,297
Reaction score
8,760
1. DAR - ES - SALAAM

Majiji Mengine ....

2. MWANZA - Ni jiji tangu enzi za Tanzania yenye majiji mawili
3. MBEYA - ni likijiji likubwa lakini kuna fursa nyingi, vyakula, unafuu wa huduma ya maji, utitiri wa vyuo, hospitali bora na huduma nyingine za jamii, n.k.
4. ARUSHA - Ni jiji zuri kwa watalii na matajiri wachache wenye kampuni za utalii na migodi nje ya mkoa, si kwa wananchi wa kawaida
5. DODOMA
6. TANGA

Uzuri wa jiji sio majengo tu ya mjini, ni mnyumbuiko wa mambo mengi sana kama:

  • Upatakanaji na unafuu wa Vyakula
  • Mzunguko wa Pesa ndani ya jiji
  • Hali nzuri ya hewa.
  • Huduma ya maji
  • Shule na vyuo
  • Ajira-wingi wa Makampuni na Viwanda
  • Stendi za Mabasi
  • Viwanja vya ndege
  • Hospitali
  • Barabara
  • Hoteli na Lodges
  • Timu za mpira - Ligi kuu
  • Kumbi za Starehe
  • Uzuri wa makazi ya watu
  • Usalama
  • Masoko makubwa Mall na Supermarkets
 
toa tanga😂😂😂tanga hata iringa inaizidi
 
MWANZA 😭...hili jiji wakazi wake ni kama watumwa...ogopa jiji linalosifika kwa gharama nafuu za maisha jua hapo mzunguko wa hela uko chini mnoo...kampuni nyingi na viwanda vingi wanalipa mishahara kiduchuu sana, usiombe uajiriwe na wahindi au wachina sahau hata kujenga, nilishuhudia mtu analipwa ujira wa kibarua wa elfu 40 kwa mwezi kiwanda cha soda maarufu hapo Mwanza...kisa eti wanapewa chakula bure...bado ukisema ujiajiri biashara zao za kibaguzi sana, kama huongei kisukuma au kikurya na kijaluo utapata tabu sana 😢 na mgeni ukitoboa bado watataka wakuloge, wao kila kitu ni ushirikina tu, ni bora ukatesekee manzese utatoboa ila sio Mwanza utarudi ukiwa na shipa kisa ulikua umepatia channel....maeneo mengi mazuri Mwanza ukuchunguza source yake ni madini Geita au Foreigners.
 
Ukifanya kazi kwa Wahindi na wachina tegemea manyanyaso hata uwe Lindi.

nchi yetu kuna ukabila wa kiwango kidogo, Usichanganye ukabila na wingi wa watu kwenye mkoa flani, Ukienda sehemu ina wenyeji na majirani wengi, kuna uwezekano mkubwa wao ndio wakajumuisha idadi kubwa za waajiriwa kwenye makampuni na viwanda
 
hiyo ipo majiji yote hata Dar ukiwa na lafudhi ya mkoani unabambikwa bei
 
Dar iplsipopangiliwa vizuri itakuwa ni sehemu ya kuparangana hapo badae
 
Ukisikia bangi ndo hizi! Unaweka slums kama mwanza na mbeya juu ya Arusha halaf unaweka allegations za kijinga kabsa kusupport hizi bang zako.
Arusha stendi ya mabasi ya mikoani mpaka leo ni ndogo ile ya mjini, Ni jiji zuri kwa watalii na matajiri wanaotumia ndege wanatua Uwanja wa Kia, Mbeya kuna stendi za maana kwa watu wa kawaida na uwanja wa Ndege upo kwa wenye uwezo.

Arusha kielimu ipo nyuma kuna chuo kikubwa kimoja tu cha uhasibu (IAA) hata shule ya english za serikali sidhani kama ipo, Ukienda Mbeya kuna utitiri wa vyuo kama 12 hivi, Shule za kiingereza zipo nne za serikali, Private ndio usiseme ni utititiri, Arusha inawafaa wenye pesa zao wanasomesha zile shule za Braeburn milioni 30 kwa mwaka

Arusha kuna uhalifu wa hali ya juu, Huwezi linganisha na Mbeya

Arusha kuna mzunguko mdogo wa pesa, Matajiri ni wengi lakini vyanzo vyao vya pesa ni migodi ya nje ya mkoa. sio ndani ya Arusha.

Naishia hapo ila kuna mengi zaidi
 
Tanga na Mbeya zitoe hapo hayo sio majiji ni manispaa zilizopiga hatua, majiji Tanzania ni 2 tu;

Dar es Salaam

Mwanza
 
Tanga na Mbeya zitoe hapo hayo sio majiji ni manispaa zilizopiga hatua, majiji Tanzania ni 2 tu;

Dar es Salaam

Mwanza
Mbeya ni jiji la pili kwa vyuo vingi, Jiji lenye unafuu wa vyakula, Jiji linalojitahidi kwenye huduma ya maji, Jiji la pili kwa kwenye mpira, n.k.

Ni kweli Mwanza ipo mbele kwa vingi ila Mbeya si ya kuipuuza labda uwe unaangalia majengo tu
 
NCHI ZA ULIMWENGU WA TATU.
 
Upo sawa jemedari, hiyo list ipo makini, tatizo wavimba macho watakuja kukupopoa kuhusu Mbeya na hawajui vibrant city zinakuwaje.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…