Hii ndio orodha ya majiji mazuri zaidi Tanzania

Hii ndio orodha ya majiji mazuri zaidi Tanzania

1. DAR - ES - SALAAM
2. MWANZA
3. MBEYA
4. ARUSHA - Ni jiji zuri kwa watalii na matajiri, si kwa wananchi wa kawaida
5. DODOMA
6. TANGA

Uzuri sio majengo tu ya mjini, ni mnyumbuiko wa mambo mengi sana kama

  • Upatakanaji na unafuu wa Vyakula
  • Mzunguko wa Pesa ndani ya jiji
  • Hali nzuri ya hewa.
  • wingi wa Makampuni na Viwanda vikubwa
  • Stendi za Mabasi
  • Viwanja vya ndege
  • Vyuo vikuu
  • Hospitali
  • Barabara nzuri
  • Hoteli za kisasa
  • Timu za mpira - Ligi kuu
  • Kumbi za Starehe
  • Uzuri wa majengo mjini
  • Uzuri wa makazi
  • Huduma ya maji ya bomba
  • Usalama
  • Masoko makubwa Mall na Supermarkets
Dar haina uzuri wowote sema ni mji mkubwa tu! Kwa hiyo watu wanalazima kukaa maana hakuna namna!
 
Mwanza ipo kimakosa...hili jiji wakazi wake ni kama watumwa...kampuni nyingi na viwanda vingi wanalipa mishahara kidogo sana, usiombe uajiriwe na wahindi au wachina sahau hata kujenga, bado ukisema ujiajiri biashara zao za kibaguzi sana, kama huongei kisukuma au kikurya na kijaluo utapata tabu sana 😢
Kafungue kiwanda chako uwalipe mamilioni ya pesa, kwanza wa wanoajiriwa viwandani ni nyinyi wakuja, watu wa Mwanza wanawaza mambo ya uvuvi, madini, biashara na mambo ya uwekezaji wenye tija.
 
Wahindi na wachina wananyanyasana hata wao kwa wao, Wahindi wana kitu kinaitwa "castes", kuna castes tano wanaamini wahindi weusi na watu weusi ni daraja la mwisho kabisa hawana tofauti na watumwa, hawaruhusiwi kupanda farasi, hawaruhusiwi kuingia kwenye mahekalu ya dini za kihindi, n.k.

Kuhusu ukabila kwenye biashara binafsi tushukuru nchi yetu ina ukabila wa chini, Kwenye biashara binafsi maboss hupenda kuwaweka watu wa karibu wanaowajua na kuwaamini ambao mara nyingi huwa ni ndugu, watoto wa shangazi, binamu, n.k. kama ni kampuni kubwa kuna nafasi kwa wengine bila kujali sana kabila.
Kingine msukuma sio mkabila ni kama vile wahehe hawana undugu na mazoea kwenye kazi kama huna sifa na vigezo eti kwa vile wewe ni msukuma mwenzangu utaangukia pua.
 
Kingine msukuma sio mkabila ni kama vile wahehe hawana undugu na mazoea kwenye kazi kama huna sifa na vigezo eti kwa vile wewe ni msukuma mwenzangu utaangukia pua.
Ukabila wasukuma hawana tena ukileta ujinga wa kujuana kazi huwezi Msukuma hawezi kukubeba hii pia inasababishwa na ukubwa wa kabila jamii za watu wachache ndo zinatabia ya kujuanajuana!
 
Ukisikia bangi ndo hizi! Unaweka slums kama mwanza na mbeya juu ya Arusha halaf unaweka allegations za kijinga kabsa kusupport hizi bang zako.
Kuna jiji la ovyo na la ajabu kama arusha nyinyi hata kwenye uchumi Singida anawapumulia nyuma, mlishabakiza kujitapa kwenye hali ya hewa na mapori ya maonesho utadhani mnaishi kwenye mapori ya hifadhi.
 
Ilo jiji la Arusha sio jiji la watafuji kama unaenda kutalii hapo sawa kwa wapambanaji miji pendwa ni Dar, Mwanza na Mbeya tu kwingine utachechemea kama sio mkulima au mwajiriwa.
Ni kweli, Arusha ina matajiri wengi ambao ni wafanya biashara wenye migodi nje ya Arusha na wageni wa nchi za nje wanaofanya kazi UN.

ndani ya jiji mzunguko wa pesa ni mdogo sana
 
Arusha stendi ya mabasi ya mikoani mpaka leo ni ndogo ile ya mjini, Ni jiji zuri kwa watalii na matajiri wanaotumia ndege wanatua Uwanja wa Kia, Mbeya kuna stendi za maana kwa watu wa kawaida na uwanja wa Ndege upo kwa wenye uwezo.

Arusha kielimu ipo nyuma kuna chuo kikubwa kimoja tu cha uhasibu (IAA) hata shule ya english za serikali sidhani kama ipo, Ukienda Mbeya kuna utitiri wa vyuo kama 12 hivi, Shule za kiingereza zipo nne za serikali, Private ndio usiseme ni utititiri, Arusha inawafaa wenye pesa zao wanasomesha zile shule za Braeburn milioni 30 kwa mwaka

Arusha kuna uhalifu wa hali ya juu, Huwezi linganisha na Mbeya

Arusha kuna mzunguko mdogo wa pesa, Matajiri ni wengi lakini vyanzo vyao vya pesa ni migodi ya nje ya mkoa. sio ndani ya Arusha.

Naishia hapo ila kuna mengi zaidi
Ukweli mtupu watu walishakarieishwa eti Geniva ya nyoko.
 
Mbeya ni jiji la pili kwa vyuo vingi, Jiji lenye unafuu wa vyakula, Jiji linalojitahidi kwenye huduma ya maji, Jiji la pili kwa kwenye mpira, n.k.

Ni kweli Mwanza ipo mbele kwa vingi ila Mbeya si ya kuipuuza labda uwe unaangalia majengo tu
Vijana wakibongo ni ushamba na ujinga ndio wanachoringia, wanapima uzuri wa miji kwa wingi wa maghorofa.
 
Mmeanza kupigania visivyowapa faida,, ni kama mko stressed na personal life zenu mnakuja kupumzikia kubeza mikoa msiyoishi.
Deborah Paul unaweza kuweka list yako ya majiji pendwa, japo najua ulitaka Arusha iwe namba moja lakini huo mji wenu hauna fursa umejikita kwenye utalii tu na madini.
 
Back
Top Bottom