Hii ndio Orodha ya makundi ya watu wanaohitaji Katiba Mpya na wasiohitaji

Kwakuwa wana CCM ni wengi. Kwakuwa vijana chini ya miaka 40 na wenye kipato duni ni wengi. Kwakuwa wazee wa miaka zaidi ya 60 ni wengi na kwakuwa akina mama ni wengi, basi mjumuisho wao inaonesha wasiotaka Katiba Mpya ni WENGI SANA! Hivyo basi, wanaodai Katiba Mpya ni wahuni wachache ambao hawatakiwi kuyumbusha mawazo ya wengi!
 

Na Kwa kuwa wenye elimu ni wachache

Wenye uwezo kiuchumi ni wachache
Wenye Ari na nia ya kutimiza ndoto za maisha yao ni wachache

Wenye kupenda haki ni wachache

Hili unamzungumziaje?
 
3. Wana CCM
Kundi hili lipo lipo, hili ni Kama bendera, Inategemea serikali itakapoegemea. Serikali ikisema Katiba mpya ndio, nalo linasema Katiba mpya ndio, serikali ikisema hapana, nalo linasema hapana.
Nimecheka kama mazuri vile… CCM watuaribia sana hiki kizazi kinachoitwa watoto wa TEUZI.
 

Elimu na umasikini hapo ni kigingi
 
Tungepata walau msimamzi wa katiba hii iliyopo naamin tungefika tupatakapo.
 
Tanzania haina wazee 60+ kwa uwingi uliousema,CCM imeua wazee wetu kwa kuwapa umasikini.
Takwimu zinaonyesha vijana ndio asilimia 80 Tanzania . Na hawa vijana kwa uwingi wao wakielimishwa umuhimu wa katiba mpya.
 

Umenena iliyokweli
 
Tanzania haina wazee 60+ kwa uwingi uliousema,CCM imeua wazee wetu kwa kuwapa umasikini.
Takwimu zinaonyesha vijana ndio asilimia 80 Tanzania . Na hawa vijana kwa uwingi wao wakielimishwa umuhimu wa katiba mpya.

πŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜ƒ

Ati imeua Wazee wetu
 

Mkuu ahsante Kwa kushiriki mjadala
 
Na Kwa kuwa wenye elimu ni wachache

Wenye uwezo kiuchumi ni wachache
Wenye Ari na nia ya kutimiza ndoto za maisha yao ni wachache

Wenye kupenda haki ni wachache

Hili unamzungumziaje?

..kuna makosa ktk uwasilishaji au uchambuzi wa makundi kuhusu katiba.

..mchambuzi amefanya kosa la kuchanganya kundi linalopinga katiba mpya, na kundi lisilokuwa na uelewa wa katiba.

..mchambuzi au mtoa mada alitakiwa ayabainishe makundi yafuatayo.

1. Kundi linalodai katiba mpya.

2. Kundi linalopenda katiba ya zamani.

3. Kundi lisilokuwa na uelewa wa katiba.

..makundi # 1 na # 2 yanatakiwa kuwaelimisha na kuwashawishi walioko ktk kundi # 3.

..vilevile kuna umuhimu wa KUJIFUNZA toka ktk kundi # 3. Kutokuielewa katiba haimaanishi kutokuihitaji katiba.
 
Mengi uliyoyaandika ni ya kweli kabisa.
Ifike mahali tukubaliane kwamba:
1.Katiba mpya ni hitaji mhimu kwa Watanzania
2.Katiba mpya iliyo bora haiwezi kuletwa na wanufaika na Katiba iliyopo.
3.Katiba mpya na iliyobora kwa nchi nyingi za Africa, huwa inapatikana kwa njia mbili tu
a)Kwa utashi wa wenye nguvu ya kimamlaka,na/au

b) Kwa ushindi wa wenye mamlaka ya nguvu.(Hapa tofautisha wenye nguvu ya kimamlaka na wenye mamlaka ya nguvu)
4.Watanzania walio wengi ni mbumbumbu wa kisiasa, hivyo hawajitambui na kimsingi hawawezi kushiriki katika vuguvugu la kudai Katiba mpya japo ina manufaa makubwa kwao.
5.Kutokana na hoja hizo hapo juu, ni wazi kwamba upatikanaji wa katiba iliyo bora kwa Watanzania inategemea tu utashi wa mwenye nguvu ya kimamlaka ambaye, kwa hali ilivyo kwa sasa, ni Rais tu.(Rejea ujio wa Demokrasia ya vyama vingi Tanzania)
Vinginevyo, wenye mamlaka ya nguvu,( jambo ambalo sisi wananchi hatuombei litokee katika nchi yetu na Mungu aepushie mbali) wataleta hiyo katiba mpya.


Sent from my SM-G965U using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…