Hii ndo top ten ya vyuo vya kata bongo,vijue kabisa usije ukadanganyika kuvichagua kwa wadogo zangi

Hii ndo top ten ya vyuo vya kata bongo,vijue kabisa usije ukadanganyika kuvichagua kwa wadogo zangi

Ni vyema ukajipeleka wewe mwenyewe pale Milembe, maana uzima wa akili yako unatia shaka!!!!!!!!!!!!:heh::heh:
 
#teamIFM ........Ifm kama man utd tu yani uipende usiipende utaiongelea tu.....Raha sana kila muda midomoni mwenu ifm tu
 
Huwezi kufananisha Kondoo na Mbuzi hata kama wote ni wanyama wanaocheua; Umejiuliza maswali ya msingi kwamba vyuo hutofautiana kwa courses. Kwa mfano SUA ni cha kilimo utalinganishaje na UDSM, MUHAS ni cha afya unalinganishaje na IFM? Acha kulinganisha aliyevaa kaputura na mwingine suti yupi amependeza bila kuangalia mazingira gani? Hujui ukivaa suti shambani kila mtu atakushangaa hata kama utakuwa mahili kwa kulima.

umesema kweli, atalinganishaje muhas(afya) na mzumbe(management na biashara), nakupa like
 
Watu hupenda kuleta mada za kipuuzi ili ajisifie kuwa na yeye ameweka mada na ikachangiwa na wengi cha msingi ni kumuona pimbi tu!!
 
Kwa jins mfumo, ulivo sasa hivi wa ajira na maisha kwa ujumla, haya mambo ya ranking ya vyuo hayana umuhimu wowote, katika ajira hata hayana nafasi issue ni competence ya mtu, kwani hizo ranking wanatumia mpaka vigezo vya majengo ya chuo.
 
nani asiyejua st augustine chuo cha kata? vyeti vyao vinaishia kanda ya ziwa tu.

thubutuuu! Nahic unaponda kwa kuwa ni private. Hata hivyo it is the largest private university in Tanzania. We nenda udsm yako na yule anaenda saut yake, kuna tatizo kuani?
 
Hizo ranking za chuo mnaangalia vigezo gani? Mbna tunashuhudia mtu ka graduate ardhi university ambacho umekiweka nafasi ya tano harafu anakwenda kuwa lecturer udsm, mwingne ame graduate BAF mzumbe ambacho kwa ranking zao hakiko hata top five then anaajiriwa kuwafundisha BCOM wa UDSM, sasa hapo vigezo ni nini ? Unaoleta hizi thread za mashndano ya vyuo unawapa presha wengne na kujiona wamepotea kuchagua vyuo kumbe hakuna lolote, suala ni kuwa competent katika kada yako, na ndio maana wanafunzi wengne wanatoa priority zaidi kwa vyuo badala ya course za kusoma. Mfano mtu anasema anataka kusoma medicine asipochaguliwa muhas akapelekwa dodoma anachukia na kuona bora angesoma kozi nyingne tofauti katika na medicine katika chuo kingne labda UDSM, professional kwanza harafu chuo kinafuata
 
Thread yako inasema top ten ya vyuo vya kata, lakini umetaja vyuo vitano ambavyo kwako ni bora na vitano vingine ambavyo wewe unaviita ni vya kata, sasa nashndwa kukuelewa mtoa maada hvi top ten viko wapi sasa?
 
tabu wengi wenu hamjui mnatafuta nini mkienda shule
kuna ubora gani wa chuo ikiwa wewe mwakilishi uliyesoma uko huwezi kutoa mchango wa maana kwa jamii kwa umaskini huu tulio nao? au huwezi kutafsi ulichosoma kwa maisha halisi?
yaani we ukiwa na kigari na umepanga upande pamoja na kimasta cha chuo fulani unaona umefika bila kujua malengo zaidi ya elimu uliyo nayo kwa mazingira yetu.
wasomi punguzeni ubinafsi angalieni elimu mlizozipata kwa upana mkubwa zikigusa jamii ndio ubora wenu utaonekana.
ikumbukwe kuwa tumesoma kwa kodi za jamii hata kama baba yako kakusomesha asingeweza kukulipia gharama hata ya tution fee kama angetakiwa alipie kihalali
ningependa kila anayejiita msomi afikirie kuajili watu wasio pungua saba yaani darasa la saba 4 form four 2 form six 1
na kila mmoja amiliki ardhi isiyopungua ekari 4 kokote kule ardhi yetu inakisha na sisi ndi walinzi tuliobaki isije ikatokea fursa ikaonekana ardhi yote wanayo wageni.
hapa mtaeleweka
 
Ama kweli utoto ni kazi, mimi nimesoma St. joseph kwenye interview moja nilikutana na wanafunzi kibao kutoka udsm ,cha ajabu walikuwa na mbwembwe kibao,mwisho wa siku nilipata hiyo kazi baada yakuwabwaga kwenye interview nasikuwa namtu yeyote aliyekuwa ananifahamu kwny kampuni kwn mimi nizaidi ya mtoto wa mkulima, nakwass napiga mpunga wakueleweka.Endeleeni na upuuzi wakujadili vyuo huku watu wanaendeleza maisha.
Note: Uwezo wa mwanafunzi kwanza ubora wa chuo baadae
 
ubora wako unaupima kwa kitu gani? je unawajua vyema graduates wa IFM?
wewe najua bado boom liko sasa jishaue kununua hutu tu vocha twa MB uishiwe mapema uone kama hukula nyasi

Graduates wa IFM ni wale waliolalamika kwa Kova kuwa wanafanyiwa mambo mabaya
 
Vip mwalimu mleta mada,hivi mkifungua pale udsm ndo unakuwa 2nd year sio? Jitahidi dogo uje upige pind la kiswahili kwa madogo kule shule za kata ambako ulponda vyuo vyake,tehe..tehe...
 
inapopaswa kuongea ukweli ni vizuri ingawa sio kila mtu anaweza kukubaliana nao kutokana na sababu zake binafsi
najua hii post itapata diss nyingi KUTOKANA NA UKWELI WAKE,What i need is ujumbe uwafikie wahusika wajue position ya vyuo vyao katika ranking ya vyuo bora bongo,OK ngoja nianze na vyuo bora bongo then ni malizie na vyuo vya kata


kwa upande wa vyuo bora
1.UDSM
2.SUA
3.MUHAS
4.HUBERT KIARUKI
5.ARDHI

kwa upande wa vyuo vya kata
1.UDOM
2.ST AGUSTIN
3.IFM
4.EKENRORD TAN5
5.CBE

Wadogo zangi??..kiswahili chenyewe tabu...
 
Thread yako inasema top ten ya vyuo vya kata, lakini umetaja vyuo vitano ambavyo kwako ni bora na vitano vingine ambavyo wewe unaviita ni vya kata, sasa nashndwa kukuelewa mtoa maada hvi top ten viko wapi sasa?

Hajielewi huyo
 
huwezi pambanisha ng'ombe na nyumba,unlike na like.huyu hajielew akajipange.utafananishaje chuo cha biashara ifm na muhimbili,sua na udsm?
 
Back
Top Bottom