Hii ni ajabu ya Dunia. Wana CCM wenyewe hawajui ni kwa nini chama chao kinaitwa Chama cha Mapinduzi!

Hii ni ajabu ya Dunia. Wana CCM wenyewe hawajui ni kwa nini chama chao kinaitwa Chama cha Mapinduzi!

Nadharia yako nzuri na Bora Sana... Lakini haihusiani na CCM kuitwa chama Cha Mapinduzi. Nina HAKIKA na hilo kwa asilimia mia.
Ukisikia mtu anasema ana hakika na jambo kwa asilimia mia ujue huyo anabumbabumba.

Weka uthibitisho wa asilimia mia hapa.
 
Ukisikia mtu anasema ana hakika na jambo kwa asilimia mia ujue huyo anabumbabumba.

Weka uthibitisho wa asilimia mia hapa.
Wala sibumbi bumbi. Mimi niko "Verified" kwa ivo siwezi kusema nina HAKIKA asilimia mia wakati Sina hakika hiyo.

Ninajua kwa kuwa mimi ni miongoni mwa wanaojua ni kwa nini CCM inaitwa chama Cha mapinduzi.
 
Wala sibumbi bumbi. Mimi niko "Verified" kwa ivo siwezi kusema nina HAKIKA asilimia mia wakati Sina hakika hiyo.

Ninajua kwa kuwa mimi ni miongoni mwa wanaojua ni kwa nini CCM inaitwa chama Cha mapinduzi.
Mpaka hapa bado unabumbabumba tu kwa sababu hujatoa uthibitisho.

Nilitegemea uniwekee video hiki hapa kikao kilitoa jina kikataja sababu, au uweke waraka wa kukipa chama kipya jina unaoelezea jina limepatikana vipi.

Lakini unakuja na essentially habari za "trust me bro, mimi najua" 😂😂😂
 
Sawa kabisa... Lakini TANU na ASP haitoi jina mapinduzi!

Sasa ilikuwaje muunganiko wa TANU na ASP ulizaa Chama Cha Mapinduzi?

CCM wenyewe hawana jibu 😃😀😄😄

Sijui kama hata chawa wao johnthebaptist na Lucas Mwashambwa kama wanajua ni kwa nini chama chao kinaitwa mapinduzi.
TANU na ASP vilikuwa Vyama vya kupigania Uhuru

Vikafanyiwa Mapinduzi ya " kifikra" na kuunganishwa kuwa Chama Cha kuwaletea Maendeleo Wananchi

Tarehe 5/2/1977 nilisherehekea pale Shule ya Msingi Mirongo Mwanza na ndipo tulifahamiana na Shujaa Magufuli tukiwa Vijana Wadogo kabisa 😂😂🔥
 
TANU na ASP vilikuwa Vyama vya kupigania Uhuru

Vikafanyiwa Mapinduzi ya " kifikra" na kuunganishwa kuwa Chama Cha kuwaletea Maendeleo Wananchi

Tarehe 5/2/1977 nilisherehekea pale Shule ya Msingi Mirongo Mwanza na ndipo tulifahamiana na Shujaa Magufuli tukiwa Vijana Wadogo kabisa 😂😂🔥
Wewe kwa Magu ni kibabu... Wewe wenzako ni kina Mkuchika😀😆😃
 
Mpaka hapa bado unabumbabumba tu kwa sababu hujatoa uthibitisho.

Nilitegemea uniwekee video hiki hapa kikao kilitoa jina kikataja sababu, au uweke waraka wa kukipa chama kipya jina unaoelezea jina limepatikana vipi.

Lakini unakuja na essentially habari za "trust me bro, mimi najua" 😂😂😂
Lengo la bandiko litafanikiwa kama nikiweka ithibati sasa hivi?

Ninachotaka ni wana CCM wenyewe waseme ni kwa nini chama chao kinaitwa *mapinduzi"?
 
Leo hapa Iringa kwenye yale mabishano ya mitaani kuhusu siasa nimeshangazwa Sana na wana CCM.

Zaidi ya wana CCM 50 niliokutana nao na kuwauliza ni kwa nini chama chao kinaitwa "Chama Cha Mapinduzi" hakuna hata mmoja aliyekuwa na jibu.

Kuna wakati taasisi ya Twaweza waliafanya utafiti wa ni aina gani ya watanzania wanaoiunga mkono CCM, Leo nimeuthibitisha utafiti wao kuwa ulikuwa ni wa kweli.

Hivi kama mtu una akili timamu unawezaje kuwa kwenye chama usichojua ni kwa nini kinaitwa Chama Cha Mapinduzi?
Chama Cha Mazezeta
 
Dhana ya mapinduzi ni dhana ikiyopo sana katika falsafa za kikomunisti kutoka kwa Georg Wilhelm Friedrich Hegel.

Zamani miaka ya kati ya 1980s nilikuwa naangalia sana Televisheni ya Zanzibar. TV zilivyoanza kuingia Tanzania bara kwa wingi, TVZ ndiyo ilikuwa televisheni pekee, kabla ya CTN, DTV na ITV.

Kuna kitu kimoja nilikuwa sielewi. Kila TV ikifungwa usiku (ilikuwa inafungwa), kulikuwa na maandishi "Mapinduzi Daima".

Mimi nikawa nafikiri wanamaanisha Mapinduzi ya mwaka 1964. Nikajiuliza, hawa watu wanataka kupinduana na kuuana daima?

Baadaye, nilivyokuja kusoma falsafa za Hegel, nikakutana na kitu kinaitwa Hegelian dialectic. Thesis -> Antithesis -> Synthesis.

Unaanza na hoja. Wanakuja watu kuikosoa hoja. Baada ya kuikisoa hoja unajenga hoja bira zaidi.

Na hiyo hoja bira zaidi inakosolewa, na unatengeneza hoja ambayo imedidisha ubora.

Katika mfumo huo, unafanya "Mapinduzi Daima". Kwa sababu, ukizembea dunia itak Ukikubali kuwa mfumo wako wa kutumiana barua kwa pista ni mfumo bora kabisa, hauhitaji mapinduzi, utashindwa kujiongeza na kuvumbua email.

Kwa hivyo, vyama vya kikomunisti na kisoshalisti vina hiyo dhana ya Hegelian dialecyic ya Mapinduzi Daima.

Ndiyo maana hata CCM kinaitwa chama cha Mapinduzi.

It's Hegelian dialectic, at least in theory.
Somo zuri. Sikumbuki chanzo changu cha elimu hii, ila wakati wa Maafikiano ya TANU na ASP kutengeneza chama kipya, watu wa ASP waliweka sharti kuwa jina jipya la Chama lazima liakisi Mapinduzi kwani kwao ni alama ya utaifa wa Zanzibar na historia. Ndio msingi wa jina hilo.
 
Somo zuri. Sikumbuki chanzo changu cha elimu hii, ila wakati wa Maafikiano ya TANU na ASP kutengeneza chama kipya, watu wa ASP waliweka sharti kuwa jina jipya la Chama lazima liakisi Mapinduzi kwani kwao ni alama ya utaifa wa Zanzibar na historia. Ndio msingi wa jina hilo.
Hili ndilo jibu. Kiranga .

Unadhani tarehe ya kuanzishwa Kwa CCM kulitokea Kwa bahati mbaya? Si ndiyo siku ya kuzaliwa kwa ASP?
 
Leo hapa Iringa kwenye yale mabishano ya mitaani kuhusu siasa nimeshangazwa Sana na wana CCM.

Zaidi ya wana CCM 50 niliokutana nao na kuwauliza ni kwa nini chama chao kinaitwa "Chama Cha Mapinduzi" hakuna hata mmoja aliyekuwa na jibu.

Kuna wakati taasisi ya Twaweza waliafanya utafiti wa ni aina gani ya watanzania wanaoiunga mkono CCM, Leo nimeuthibitisha utafiti wao kuwa ulikuwa ni wa kweli.

Hivi kama mtu una akili timamu unawezaje kuwa kwenye chama usichojua ni kwa nini kinaitwa Chama Cha Mapinduzi?
Wana IQ ndogo
 
Hili ndilo jibu. Kiranga .

Unadhani tarehe ya kuanzishwa Kwa CCM kulitokea Kwa bahati mbaya? Si ndiyo siku ya kuzaliwa kwa ASP?
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kiitikadi imeongozwa na Makomredi kina Abdulrahman Babu na Kassim Hanga mwanzo kabisa. Hanga kasoma kwa wakomunisti Russia. Babu kasoma Marxism London. Ndio waliokuwa ideological strategists wa kina Karume.

Hao ndio waliomsoma Hegel na kuleta hizo habari za "Mapinduzi Daima" niliyoyataja.

Sasa huoni kuwa wewe umetaja Zanzibar na mimi nimetaja huko huko?

Wewe umeeleza neno Mapinduzi limetoka Zanzibar, mimi nimekueleza Wazanzibari wamelitoa wapi hilo neno. Hiyo dhana. Nikakueleza mpaka nilivyojiuliza kwa nini wanataka mapinduzi daima? Nikaja kuunganisha na Hegelian Dialectic ya Hegel.

Mpaka nimekuelezea habari za "Mapinduzi Daima" ambazo mtu akiyesoma Hegelian dialectic za Thesis-> Antithesis-> Syntheis, repeat again, aliyoyaandika Hegel, na Hegel alivyo influence Ukomunisti, na Wakomunisti walivyo influence Mapinduzi ya Zanzibar mpaka shuke zikaitwa Fidel Castro na Mao Tse Tung, ataelewa.

Huelewi wapi?
 
Leo hapa Iringa kwenye yale mabishano ya mitaani kuhusu siasa nimeshangazwa Sana na wana CCM.

Zaidi ya wana CCM 50 niliokutana nao na kuwauliza ni kwa nini chama chao kinaitwa "Chama Cha Mapinduzi" hakuna hata mmoja aliyekuwa na jibu.

Kuna wakati taasisi ya Twaweza waliafanya utafiti wa ni aina gani ya watanzania wanaoiunga mkono CCM, Leo nimeuthibitisha utafiti wao kuwa ulikuwa ni wa kweli.

Hivi kama mtu una akili timamu unawezaje kuwa kwenye chama usichojua ni kwa nini kinaitwa Chama Cha Mapinduzi?
Chama cha mbogamboga
 
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kiitikadi imeongozwa na Makomredi kina Abdulrahman Babu na Kassim Hanga mwanzo kabisa. Hanga kasoma kwa wakomunisti Russia. Babu kasoma Marxism London. Ndio waliokuwa ideological strategists wa kina Karume.

Hao ndio waliomsoma Hegel na kuleta hizo habari za "Mapinduzi Daima" niliyoyataja.

Sasa huoni kuwa wewe umetaja Zanzibar na mimi nimetaja huko huko?

Wewe umeeleza neno Mapinduzi limetoka Zanzibar, mimi nimekueleza Wazanzibari wamelitoa wapi hilo neno. Hiyo dhana. Nikakueleza mpaka nilivyojiuliza kwa nini wanataka mapinduzi daima? Nikaja kuunganisha na Hegelian Dialectic ya Hegel.

Mpaka nimekuelezea habari za "Mapinduzi Daima" ambazo mtu akiyesoma Hegelian dialectic za Thesis-> Antithesis-> Syntheis, repeat again, aliyoyaandika Hegel, na Hegel alivyo influence Ukomunisti, na Wakomunisti walivyo influence Mapinduzi ya Zanzibar mpaka shuke zikaitwa Fidel Castro na Mao Tse Tung, ataelewa.

Huelewi wapi?
Hizo nadharia ulizoandika hazihusiani kabisa na kauli mbiu ya "mapinduzi daima".

Na hao kina Abdulrahman Babu au Kassim Hanga hawakuwa watu wenye ushawishi ASP.
 
Hizo nadharia ulizoandika hazihusiani kabisa na kauli mbiu ya "mapinduzi daima".

Na hao kina Abdulrahman Babu au Kassim Hanga hawakuwa watu wenye ushawishi ASP.
Hujathibitisha jina la Mapinduzi limetoka wapi kwa 100%.
 
Back
Top Bottom