Je unasema hakuwa mnafiki? Bwana unapenda ndoto zako! Amin alifaulu sana unafiki na uwongo. Hujui historia yake?
Hujui alikuwa mwajeshi mkali wa ukoloni aliyejipatia nyota zake kuwinda Wagikuyu pale Kenya alipotumwa pale na Waingereza wakati wa vita ya Maumau? Ila alifurahia uwenyeviti wa Umoja wa Afrika baadaye...
Aliwezaje kuwa mtu anayeaminiwa na rais Obote mpaka alimpindua? Hata hivyo, wakati bado alikuwa mkuu wa jeshi la Obote alituma watu waliojaribu kumwua rais 1969, halafu 1970 aliagiza (kwa siri yote!) mauaji ya jenerali mwenzake Okoya aliyemhofia angechukua nafasi yake. Kumpindua Obote ilikuwa baadaye.
Hujui tangazo la Amin baada ya kumpindua Obote? Soma General and Administrative Order No. 2 (GAO 2/1971) :
It has been necessary to take action to save a bad situation from getting worse. We give here below examples of matters that have left the people angry, worried, and very unhappy.
I. The unwarranted detention without trial and for long periods of a large number of people, many of whom are totally innocent of any charges.
2. The continuation of a state of emergency over the whole country for an indefinite period, which is meaningless to everybody.
3. The lack of freedom in the airing of different views on political and social matters
Si ni unafiki kabisa maana akikosoa makosa yale ya Obote hakusita kuzizidisha?
Ni kitu gani kinachofanya watu hapa kumtetea huyu???