Hii ni Yanga sio Simba, maana ya Kikosi kipana ndio hii! Hakuna Pacome, Aucho na Yao, unatoa sare na Mamelodi iliyokamilika kila idara

Hii ni Yanga sio Simba, maana ya Kikosi kipana ndio hii! Hakuna Pacome, Aucho na Yao, unatoa sare na Mamelodi iliyokamilika kila idara

Akiba gani wakati tangu droo ya robo fainali itolewe makolo walishobokea Sana mamelody wakaacha kujiandaa na mchezo wao na Alahyl sasa ndo timu pekee iliyokandwa nyumbani.
Narudia tena weka akiba ya maneno. Sote tumeangalia mechi zote, droo yenu Yanga isiwape jeuri kiivyo ni bad game plan ya Mamelod tu ingawa bado ukiniambia kati ya Mamelod na Al Ahly kwenye michuano hii, Al Ahly wako juu.
 
Ndio ball possession iwe 75 kwa 25 kweli?
Mkuu mpira unakusumbua possession waliyoipata mamelodi ni kipa kumpa pass nyingi beki Kekana mara unaenda kwa Moosa Lebusa unarudi kwa kipa Williams ulitaka hapo Yanga wafanyeje watu wanamiliki mpira ndani ya zone yao wakitegemea pass za kupenyeza ambazo nyingi waliblock wakina Bacca...Yanga wamejituma sana jana wacha waende wakapambane tena huko SA...
 
Mtu kafungwa nyumbani, anamcheka aliyetoa sare, tena bila nyota wake watatu.

Mrchi za mtoano ni technical, ball possession ya MSFC haionyeshi ukweli kuwa walikuwa na 2shots on target as compared na YNFC ambayo ilikuwa na 4shots on target, actually wilikuwa na chances kubwa ya ushindi kwa nafasi hizo nne.
 
Possession ya Mamelod ilikuwa ni mipira ya nyuma walihold sana mpira nyuma na kwasababu hatukufanya pressing ya kutosha. Hatukufanya pressing kwasababu Mamelod ni wakubwa wenzetu huwezi kuwaendea kwa papara. Lakini sio kwamba walipossess labda kwa kuupiga mwingi kila kona.
 
Mkuu mpira unakusumbua possession waliyoipata mamelodi ni kipa kumpa pass nyingi beki Kekana mara unaenda kwa Moosa Lebusa unarudi kwa kipa Williams ulitaka hapo Yanga wafanyeje watu wanamiliki mpira ndani ya zone yao wakitegemea pass za kupenyeza ambazo nyingi waliblock wakina Bacca...Yanga wamejituma sana jana wacha waende wakapambane tena huko SA...
Ahsante umeongea nilichoongea. Hawawezi kuelewa hawa kenge walioko kwenye msafara wa mamba.
 
Baada ya kikosi kinachoanza kutoka Leo Kuna mbumbumbu wengi walianza kushangilia na kupiga miluzi kwenye vibanda umiza wakisema yanga anachakazwa goli za kutosha Leo!

Baada ya kutomuona pacome, yao yao na aucho, lakini wakashindwa kujua ya kwamba yanga inacheza kitimu zaidi na sio kutegemea mchezaji mmoja mmoja, na pia wakashindwa kujua mechi za mtoano zinachezwa kimbinu zaidi ili kuvuka hatua inayofata!

Mechi ya Leo ilichezwa kimbinu na kocha GAMOND alijua key players wake muhimu awapo ivyo alikuja na mpango mkakati wa kuvunja mbinu zote za Mamelod wanazotumia kupata mabao anastahili pongezi sana!

Ufanisi tu kwenye umaliziaji ndio umeiangusha yanga lakini wamefanikiwa kucheza kimbinu na timu kubwa Kama MAMELODI iliyokuwa imesheheni nyota wake wote!

Mechi ya Pretoria ni mpya na yanga sio mwepesi kwenye mechi za ugenini Mamelod wajiandae tu wasidhani watapata mteremko Ngoma itapigwa mpaka kieleweke!

N;B wale wazee wa kuchoma viwanja Kama ndio wangewakosa wachezaji wao muhimu 3 basi ilikuwa ni kiama(kauka nikuvae) wangejuta!
Kwa hiyo wangekuwepo mngeshinda
 
Back
Top Bottom