Hii tabia imekuwa sugu; mtu anaamua tu aje Dar kukusalimia na afikie kwako

Hii tabia imekuwa sugu; mtu anaamua tu aje Dar kukusalimia na afikie kwako

Nyie ndo watu JF huwa mnadai mna maisha mazuri sana humu....

Swali la kuwa na maisha mazuri au mabaya hakuna aliyelisema popote, nachosema sisi tunathamini ndugu zetu hata waje na magaga au bila viatu mjini.

Vyote tulivyonavyo ni Mungu ametupa tu kwa Rehema zake, tunaweza kuwa hao wa vijijini na hao wakawa wa mjini.
 
Duuuh! nilirudi kijijini kwetu,nikakuta stori ya bibi mmoja,alienda kwa mwanae mjini,alinyanyasika Sana,hadi akaomba arudi kijijini kwenye maisha ya shida.Watu wa mjini msiwadharau watu wa kwenu,chakula tu au malazi ni nongwa...?
Anyway mnasubiriwa,mkifa mkazikwe huko vijijini,ambako wachimba kaburi mtawakuta haohao mnaowajandia,wasije makwenu.

Siku zote hua namwomba mungu nimudu shida zangu, hua sitaki kumsumbua mtu na maisha yake na yeye asinisumbue.

Shida ya watu wakija kwenye nyumba wanakuja na mazoea ya walipotoka na akifika akakuta utaratibu fulani tofauti na alivyozoea anaona anaonewa japo kuonewa kweli kupo ila ni kwa uchache wengi wanasumbuliwa na huelewa mdogo.

Unakuta mtu keshazoea kula milo mitano kwa siku akija kwako akakuta milo mi3 nyama chache anaanza kujudge mbona mnaendesha magari ila chakula ndani hakuna mara mwanamke anaroho mbaya hatak tule..! na n.k.

Mi siwezi kukaa kwa ndugu, na ndugu wakija kwangu wafate utaratibu wangu hutaki left, binafsi ni bora nilale stand kwa ndugu ntapita kusalimia tu.
 
Ukweli kabisaa, ndugu wa mke huwa hawapatagii tabuuu.

Sitasahau mie nilichofanyiwa, niliondoka mie mdogo wa mke wa Kaka alibakiii. Baadae nilijua kuwa yule ndo ubavu wa Kaka na pale ni kwake ana mamlaka ya nani akae nani asikae.

Mwaka wa 11 huu sijawahi kanyaga tena kwao.
Magufuli hostel si zipo Coca[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Ila kuna watu wana roho ngumu sana kuhusiana na hawa ndugu wanaokuja pasi na kutoa taarifa. Jamaa anawauliza " Je, mlisikia mimi naumwa?" "Hapana tumekukumbuka sana ndo maana tumekuja kukusalimia". "Ok, kwa vile sasa mmekuja na mmeniona nipo mzima, basi kesho asubuhi na mapema mjiandae kurudi mlikotoka".

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Ila kuna watu wana roho ngumu sana kuhusiana na hawa ndugu wanaokuja pasi na kutoa taarifa. Jamaa anawauliza " Je, mlisikia mimi naumwa?" "Hapana tumekukumbuka sana ndo maana tumekuja kukusalimia". "Ok, kwa vile sasa mmekuja na mmeniona nipo mzima, basi kesho asubuhi na mapema mjiandae kurudi mlikotoka".
Hii kubwa kuliko,hawapeleki hata daraja la Mfugale wakashangae kidogo ndio awarudishe.....?
 
Ila kuna watu wana roho ngumu sana kuhusiana na hawa ndugu wanaokuja pasi na kutoa taarifa. Jamaa anawauliza " Je, mlisikia mimi naumwa?" "Hapana tumekukumbuka sana ndo maana tumekuja kukusalimia". "Ok, kwa vile sasa mmekuja na mmeniona nipo mzima, basi kesho asubuhi na mapema mjiandae kurudi mlikotoka".
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siku zote hua namwomba mungu nimudu shida zangu, hua sitaki kumsumbua mtu na maisha yake na yeye asinisumbue.

Shida ya watu wakija kwenye nyumba wanakuja na mazoea ya walipotoka na akifika akakuta utaratibu fulani tofauti na alivyozoea anaona anaonewa japo kuonewa kweli kupo ila ni kwa uchache wengi wanasumbuliwa na huelewa mdogo.

Unakuta mtu keshazoea kula milo mitano kwa siku akija kwako akakuta milo mi3 nyama chache anaanza kujudge mbona mnaendesha magari ila chakula ndani hakuna mara mwanamke anaroho mbaya hatak tule..! na n.k.

Mi siwezi kukaa kwa ndugu, na ndugu wakija kwangu wafate utaratibu wangu hutaki left, binafsi ni bora nilale stand kwa ndugu ntapita kusalimia tu.
Haina shida,ila mahusiano na watu wa kwenu,yawe mazuri na ujitahidi kuwatriti kama walivyo na labda kwa kuwavumilia baadhi ya tabia zinazovumilika.Yule dingi mtoto wa yule bibi,inasemekana alikua hana shida,ila mkewe ndo alionekana ana shida,matokeo yake yule dingi,akikuja kapata shida ya figo,na uwezekano wa kupewa na ndugu,ulikuwepo,lakini ndugu walikwepa hilo jukumu,dingi alifariki.Inasikitisha sana.Dingi yule anapigania afya yake,ndugu wanaongea yao,alifariki yule dingi.R.I.P niliwahi kwenda kwake,kumtembelea,pale Sinza,he was a good man indeed,nilipofika tumekaa tunaongea,kwasababu alijua mimi natokea kijijini kwake na anajua utamaduni wa kule,zililetwa ndizi za kupikwa,akamwambia mkewe,huyu hawezi kula hicho chakula,akafurahia,msongeeni ugali,nikasongewa ugali,nikala nikainjoi,jioni nikasepa zangu,kipindi hicho alikua anafanya dialysis.He was a a good man kwakweli.
 
Wacheni roho mbaya, hao wanakuja na kheri zao.

Wapokeeni bila masimango wala chuki, kwa bashasha na furaha. Siku tatu za mwanzo ni wageni, baada ya hapo waishi kama wenyeji.

Uislam mi mwema sana, haujaacha kitu. Uislam una miongozo mema kabisa ya maisha ya kila siku. Ukiifata huharibikiwi.
 
Hii tabia imekuwa sugu. Yaani mtu anakaa tu na halmashauri ya kichwa chake anaamua kuwa nimpigie jamaa yangu yupo Dar nikafikie kwake.

Mi nipo zangu home jana inaingia simu ya Abouu. Ananiuliza maisha vipi namwambia safi tunalisongesha. Maneno maneno mengi mwisho anasema nipo Dar nataka nije kwako nielekeze. Nikamuuliza wakati unapanga kuja ulinishirikisha? Unaamua tu kuja kwangu hata hujanitaarifu.

Jamaa ame mind kawaambia watu nimemkataa. Ninyi wa Mikoani mnadhani huku ni kama kwenu huko ambako hamna ratiba maalum. Mnajiamulia tu.

Mwaka juzi nlimwacha mtu stand kwa upuuzi kama huo. Kakaa zake Mbwinde mwisho kaamua kuja town a anipigia simu kuwa yupo Dar anataka aje home. Nlimwambia tu kuwa sipo home na familia tumesafiri.

Akaanza kuomba basi nimpatie pesa ya sehemu ya kulala anisubiri. Nilimwambia mwezi mzima sitokuwa home. Akataka nimtumie nauli. Nlizima na simu kabisa. Huu ni wendawazimu.

Halafu tukiwaakaribisha mnaenda kutusema kijijini kuwa huku tunaishi maisha mazuri sana hatuwajali watu wa vijijini. Mnaenda kutuponda sana kijijini kuwa tunatumia pesa vibaya.




Mimi walienda kusema nafuja sana pesa badala ya kuwasomesha watoto wao. Mtu kazaa watoto 13 anataka nimsomeshee... Mimi nina 3 tu. Bado wanaenda kusema nakuaje na watoto wachache ... Mwanaume gani. Mke amenikalia kichwani anarudi jioni kama mwanamke. Wanataka wife awafulie nguo zao. Na wanakuwa wakali akirudi awapatie chakula n.k sina hamu na ndugu kabisa.

Mmoja tumekaa naye mwaka mmoja amekuja nimsomeshe diploma. Akirudi toka chuo anaangalia TV mpaka saa 4 akipewa kazi basi za home siku yupo asaidie... Anasema anateswa sana hawezi soma. Nikasubiri likizo. Akaenda kwao kusalimia. Nikamwambia atafute chuo aendelee kusoma huko, nitamlipia ada.

Alilia sana anataka arudi Dar. Nilimwambia huku wifi yako atakutesa hutapata muda wa kusoma. Akabembeleza sana nilimkatalia coz alishanipakaza sana kijijini na kumchafua sana wife. Na mtu mwenyewe ni ndugu wa mbali kabisa..
izo mambo kwa wachagga hamna iyo ki2!!!
 
Kiukweli kwa maisha tuliyo nayo sasa inapendeza mgeni akija aje kwa taarifa.

Ni asiyeelewa tu namna dunia imefikia wapi kwa sasa ndo ataona ye mgeni akija tu kwake bila taarifa ni sawa.

Hawa hawa tunaowaamini wengi wamekuwa mwiba kwa baadhi ya familia hasa baada ya kuja bila kuwa na vya msingi vilivyowaleta.
Hata wewe 😅😅😅
 
Back
Top Bottom