Hii tabia imekuwa sugu; mtu anaamua tu aje Dar kukusalimia na afikie kwako

Hii tabia imekuwa sugu; mtu anaamua tu aje Dar kukusalimia na afikie kwako

Tafuta hela ndugu ili utamani kula na ndugu zako wakati wote... haya malalamiko yako ni ishara ya umaskini
Nikisoma na kuangalia sura yako ilivyokauka kama goti la kiwete... Sikuoni ukiwa na lolote pako pakavu utiliwe mchuzi. Unajipapatua lakini unanuka jasho tu na kikwapa. Na midomo yako imekauka utandani mikono ya mchoma mkaa.
 
Hii tabia imekuwa sugu. Yaani mtu anakaa tu na halmashauri ya kichwa chake anaamua kuwa nimpigie jamaa yangu yupo Dar nikafikie kwake.

Mi nipo zangu home jana inaingia simu ya Abouu. Ananiuliza maisha vipi namwambia safi tunalisongesha. Maneno maneno mengi mwisho anasema nipo Dar nataka nije kwako nielekeze. Nikamuuliza wakati unapanga kuja ulinishirikisha? Unaamua tu kuja kwangu hata hujanitaarifu.

Jamaa ame mind kawaambia watu nimemkataa. Ninyi wa Mikoani mnadhani huku ni kama kwenu huko ambako hamna ratiba maalum. Mnajiamulia tu.

Mwaka juzi nlimwacha mtu stand kwa upuuzi kama huo. Kakaa zake Mbwinde mwisho kaamua kuja town a anipigia simu kuwa yupo Dar anataka aje home. Nlimwambia tu kuwa sipo home na familia tumesafiri.

Akaanza kuomba basi nimpatie pesa ya sehemu ya kulala anisubiri. Nilimwambia mwezi mzima sitokuwa home. Akataka nimtumie nauli. Nlizima na simu kabisa. Huu ni wendawazimu.

Halafu tukiwaakaribisha mnaenda kutusema kijijini kuwa huku tunaishi maisha mazuri sana hatuwajali watu wa vijijini. Mnaenda kutuponda sana kijijini kuwa tunatumia pesa vibaya.




Mimi walienda kusema nafuja sana pesa badala ya kuwasomesha watoto wao. Mtu kazaa watoto 13 anataka nimsomeshee... Mimi nina 3 tu. Bado wanaenda kusema nakuaje na watoto wachache ... Mwanaume gani. Mke amenikalia kichwani anarudi jioni kama mwanaume. Wanataka wife awafulie nguo zao. Na wanakuwa wakali akirudi awapatie chakula n.k sina hamu na ndugu kabisa.

Mmoja tumekaa naye mwaka mmoja amekuja nimsomeshe diploma. Akirudi toka chuo anaangalia TV mpaka saa 4 akipewa kazi basi za home siku yupo asaidie... Anasema anateswa sana hawezi soma. Nikasubiri likizo. Akaenda kwao kusalimia. Nikamwambia atafute chuo aendelee kusoma huko, nitamlipia ada.

Alilia sana anataka arudi Dar. Nilimwambia huku wifi yako atakutesa hutapata muda wa kusoma. Akabembeleza sana nilimkatalia coz alishanipakaza sana kijijini na kumchafua sana wife. Na mtu mwenyewe ni ndugu wa mbali kabisa..

HAWA WAGENI WENGINE NDO HUNAJISI WATOTO NA UNDUGU UNAISHIA HAPO HAPO. MNAHARIBIANA FUTURE. KILA MTU AKAE KWAKE. DUNIA YA SASA IMANI IMEKWISHA. TUSAIDIANE KATIKA SHIDA LAKINI SI KUVAMIANA TU NYUMBANI KWA KISINGIZIO CHA UKARIMU. NDUGU WENYEWE IMANI IMEWATOKA. ANGALIA WANAOBAKWA, NAJISIWA AU LAWITIWA. MHUSIKA UTAKUTA BABA, BAMDOGO, MJOMBA, COUSIN NA JIRANI KWA MBALI KIDOGO.

Wewe uchoyo na roho mbaya tu vinakusumbua badilika.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Daslama tamuu bhana.
Siyo lazima wote tuende DSM [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Nakumbuka way back 2007/8 nikiwa nimemaliza std 7,nilikuja DSM Kwa mara ya kwanza ..ilikuwa mahafali ya sister hapo jalalani kwenu[emoji23]

Aisee nilishangaa magorofa...nilikuwa nahesabu simalizi[emoji1787]

Tulikaa wiki tunazunguka tu feri,Kariakoo,yaani nikasema nikirudi kijijini watanikoma..
Ukifika unajidai umebadilika kabisa hadi ongea[emoji23][emoji23][emoji23]

Wenzio wanakutamani umetoka Dar.



Ndugu zenu wakija DSM msiwafukuze..maisha ndo hayahaya.
Hata wakija bila sababu muwapokeee...wengine wanataka kupata exposure..
Kama tulivyopokewa,basina sisi tupokee wenzetu.
 
Siyo lazima wote tuende DSM [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Nakumbuka way back 2008 nikiwa nimemaliza std 7,nilikuja DSM Kwa mara ya kwanza ..ilikuwa mahafali ya sister hapo jalalani kwenu[emoji23]

Aisee nilishangaa magorofa...nilikuwa nahesabu simalizi[emoji1787]

Tulikaa wiki tunazunguka tu feri,Kariakoo,yaani nikasema nikirudi kijijini watanikoma..
Ukifika unajidai umebadilika kabisa hadi ongea[emoji23][emoji23][emoji23]

Wenzio wanakutamani umetoka Dar.



Ndugu zenu wakija DSM msiwafukuze..maisha ndo hayahaya.
Hata wakija bila sababu muwapokeee...wengine wanataka kupata exposure..
Kama tulivyopokewa,basina sisi tupokee wenzetu.
Umesema kwelii kabisaa....

Watu waliokuja dar kipind aaah walikuja dar


Kwanza wanakufanya km funny....

Mimi nilishangaa friji ukifunga linawaka, Mara kuwasha tv.... Em acheni bhn...

Siku hz unakuja dar kila kitu unacho uko mkoan
 
Umesema kwelii kabisaa....

Watu waliokuja dar kipind aaah walikuja dar


Kwanza wanakufanya km funny....

Mimi nilishangaa friji ukifunga linawaka, Mara kuwasha tv.... Em acheni bhn...

Siku hz unakuja dar kila kitu unacho uko mkoan
[emoji38][emoji38][emoji38]
Mambo ya Tv tayari yalikuwepo..nakumbuka miaka ya 2000 Baba anakuja na TV nyumbani aisee hatukulala.

Hapo ndio mziwanda unakabidhiwa rimoti,hakuna watu kushikashika hovyo,,enzi hizo tukaanza na Antena..deki za mikanda ile Mkubwa..
Tukaja kununua ungo..mambo ya kulipia hayakuwepo.


Ila Mimi maghorofa tu ndo nilishangaa Daslama aisee
Ukizingatia kule Mbeya miaka hiyo kulikuwa hakuna ghorofa refu hata moja.[emoji1787][emoji1787][emoji1787]Nilihesabu ghorofa nikawa simalizi..
Sister ananisubiri.

Akatupeleka kupanda lift[emoji23]
Ni kivumbi.

Tukaenda feri kushangaa Panton.

Hapo ukirudi kijijini Toka Dar,wenzio wanakuja kukushangaa umetoka Dar...


Nyie,hebu tuwapokee ndugu zetu jamani.
Kikubwa watoe tu taarifa ili tufix ratiba za vibarua vya kausha damu.
 
Chumba kimoja na sebule....
Bila taarifa [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji119][emoji119][emoji119][emoji119]
Oky hata ukitoa taarifa
SITAKI WAGENI
Si bora hata hiyo sebule ipo. Wengine tunakaa self... [emoji1787][emoji1787]

Mara ba demu anaweka weka kambi mara siku 3 mara siku 1 mara wiki.

Na mwingine yupo standa...

Jamani tupeane taarifa hata 1wk before
 
Mkifa mitoto yenu inarudi mikoani kunyanyaswa......ndugu mliowaita wanoko hamuwataki wanachukua Mali zote ulizochuma....mke wa marehemu akishtaki, ndugu hutumia pesa za marehemu kushinda kesi....Hapo marehemu umelala kimya kaburini. Hii ndiyo dunia mkuu
Una tabia za kimasikini we mwalimu
 
kila mtu aishi kwake kwa taratibu zake...Binafsi kwangu kwa ndugu/mtu yeyote anayenifahamu apige simu afikie kwangu muda wowote ule hata kama siku za kawaida huwa hatupigiani simu mara kwa mara ingawa wasukuma mmezidi.!!!
Hongera sana mkuu.

Kuna level ya mkuu, kuna level ya maisha ukifika you can have this freedom.
 
Back
Top Bottom