Hiki kizazi mnaharibu sana Kiswahili "KUHEMEA" ndio maana yake nini?

Hiki kizazi mnaharibu sana Kiswahili "KUHEMEA" ndio maana yake nini?

Kujumua
nimekutana nayo iringa ikiwa na maana amenunu kwa bei ndogo bei ya jumla kwa ajili ya kwenda kuuza kwa bei kubwa kidogo apate faida.(Kuchuuza/mchuuzi)KUJUMUA KWA maana ya mfanya biashara
Neno moja linaweza likawa na maana zaidi ya moja .
 
Yaani nakutana na mfanyakazi wangu mmoja leo namuuliza ulikuwa wapi time niliyokuwa nakutafuta ananiambia boss nilitoka kuhemea nikamuuliza kuhemea ndio maana yake nini maana tayari kichwani nilishawaza mambo ya hovyo akaniambia kuhemea ni kwenda kununua mahitaji ya nyumbani yaani sikumuelewa hivi neno kuhemea ni kununua mahitaji ya nyumbani?
Mkuu Hyrax , naona leo umeamua kulipingana neno sahihi kabisa la Kiswahili.

NB: Halafu hii sentensi yako imekaaje? Mbona ni ndeeeefu na wala haionekani wapi umeweka japo kituo kimoja au mkato? Yaani ni mwendo wa vurugu mechi! Nadhani ugonjwa unao wewe. Inasikitisha kwamba huuoni.
 
USHAURI WANGU KWA BAKITA
Maneno kama haya yanayotumiwa sana na jamii ambayo yamezuka yenyewe na jamii inayakubali na sehemu kubwa ya jamii inayatumia katika kuwasiliana iyaingize katika lugha ya kiswahili iyarasmishe.
Tuchukulie mfano
BODA BODA-piki piki ya abiria
BODA WANGU, au yule BODA-dereva wa boda
Hii ndio lugha inayotumiwa mtaani.
Ungekuwa unazungumza kwa mayakini (facts), kamwe usingeweka huo mfano. Naweza kusema kisahihi kwamba wewe ndiye uko nyuma ya wakati.
 
Duu kumbe bora hata umeuliza labda tutapata majibu,
Nimejiuliza sana hili neno. Je ni rasmi?

Lakini pia nikajiuliza kwa niniwasema kuhemea?
Nikawaza labda kile kitendo cha kwenda kununua vitu vilivyosambazwa chini, unaviinamia hivyo ni kama vile unavihemea/pumulia, Maana hii hutumika hasa kwenye manunuzi ya sokoni specifically vitu vya kula mf matunda, mboga, viungo n.k mostly vinatandazwa chini hasa huko kwa hao wenzetu.

BTW ni neno ambalo silipendi kabisa, maana hata unayemuuliza kwa nini mnaita kuhemea hana jibu, Kuna haja gani ya kuleta msamiati complicated, bora hata ingekua neno la kilunga, neno sokoni mbona lipo wazi tuu kwa kila mtu,
Kuna maneno mawili unachanganya: kuemea na kuhemea. Haya mawili ni sahihi, yenye maana tofauti kabisa.
 
Ungekuwa unazungumza kwa mayakini (facts), kamwe usingeweka huo mfano. Naweza kusema kisahihi kwamba wewe ndiye uko
Ungekuwa unazungumza kwa mayakini (facts), kamwe usingeweka huo mfano. Naweza kusema kisahihi kwamba wewe ndiye uko nyuma ya wakati.
ni kweli sijaweka mifano halisi ya maneno ya kiswahili yaliyotungwa na BAKITA .
kwakuwa ni maneno magumu ambayo siyakumbuki ambayo ni tofauti na maneno yanayotumika na jamii mtaani katika mawasiliano.
Nikiyakumbuka nita yashare hapa.
 
ni kweli sijaweka mifano halisi ya maneno ya kiswahili yaliyotungwa na BAKITA .
kwakuwa ni maneno magumu ambayo siyakumbuki ambayo ni tofauti na maneno yanayotumika na jamii mtaani katika mawasiliano.
Nikiyakumbuka nita yashare hapa.
Una hakika neno bodaboda halijasanifiwa na kuingizwa kwenye lugha rasmi ya Kiswahili? Hilo ndilo swali langu.
 
Una hakika neno bodaboda halijasanifiwa na kuingizwa kwenye lugha rasmi ya Kiswahili? Hilo ndilo swali langu.
nimesema sijaweka mfano halisi

Ni kweli sijaweka mfano halisi wa maneno yaliyorasimishwa na BAKITA kutumika .,ambayo kiukweli ni mageni na ni magumu na yapo tofauti na maneno yaliyozoeleka na jamii kwa maana ileile na yanayotumiwa na jamii kuwasiliana.
 
Una hakika neno bodaboda halijasanifiwa na kuingizwa kwenye lugha rasmi ya Kiswahili? Hilo ndilo swali langu.
najua neno boda boda limerasmishwa kwwnye kamusi za kiswahili na kingereza.
nimeweka kama mfano usio halisi ,kwa kuwa maneno mapya yaliyotungwa na bakita ,binafsi siyakumbuki kwa kuwa ni mageni na kwangu ni magumu kwa vile hatuyatumii katika jamii yetu kuwasiliana ni mapya.au hayajazoeleka na wengi wetu.
Kiasi kwamba ukilisikia kwa mara ya kwanza unapata linakupa ukakasi.Kana kwamba jamii nzima miaka yote mlikuwa mnakosea kutumia maneno mliyokuwa mkiyatumia na kuwasilina au hamuijui au hakuwahi kuijua lugha yenu wenyewe ya kiswahili ISIPOKUWA bakita pekee ndio wenye kujua lugha ya kiswahili.
Ndio maana nikashauri ingefaa,wanapotunga maneno ni vizuri kutumia yale yaliyozoeleka na yanayotumika na sehemu kubwa ya jamii katika kuwasiliana.
 
Yaani nakutana na mfanyakazi wangu mmoja leo namuuliza ulikuwa wapi time niliyokuwa nakutafuta ananiambia boss nilitoka kuhemea nikamuuliza kuhemea ndio maana yake nini maana tayari kichwani nilishawaza mambo ya hovyo akaniambia kuhemea ni kwenda kununua mahitaji ya nyumbani yaani sikumuelewa hivi neno kuhemea ni kununua mahitaji ya nyumbani?
Wewe ni wa kizazi kipi! Neno kuhemea si jipya ni la tangu enzi za Adamu na Hawa likiwa na maana ya kutafuta chakula cha siku kwa watu walio masikini.
Nadhani wewe umezaliwa Marekani na umekuja hapa na kuishi maisha ya mboga nne, kwa hali hii si ajabu wewe kutolijua neno "kuhemea".
 
Hilo neno si la kizazi hiki, bali la kizazi kile. Ninakaribia miaka 40 na hilo neno nimekua nalisikia likiwa na maana ya kununua mahitaji ya nyumbani. Kizazi hiki wanasema 'shopping/kununua groceries'.
"Shopping" ni neno linalotumiwa na watu wenye uwezo wa manunuzi ya kila kitu.
"Kuhemea" ni neno linalotumiwa na masikini wanapotafuta chakula cha siku, hauwezi kuhemea vitu au vifaa.
 
Yaani nakutana na mfanyakazi wangu mmoja leo namuuliza ulikuwa wapi time niliyokuwa nakutafuta ananiambia boss nilitoka kuhemea nikamuuliza kuhemea ndio maana yake nini maana tayari kichwani nilishawaza mambo ya hovyo akaniambia kuhemea ni kwenda kununua mahitaji ya nyumbani yaani sikumuelewa hivi neno kuhemea ni kununua mahitaji ya nyumbani?
Hilo neno lipo toka zamani ni nsamiati wa kusema natafuta kula, kama kuku anavyotafuta kula, anahemea.
 
Back
Top Bottom